Mkuu
majany umejibu vizuri sana, sema umetumia maneno ya kitaalam zaidi. Hoja ya
mwanawao inamaana japo wengi wetu huwa hatupendi kuuliza vitu hata kama hatujui kwa kuona aibu.
Kwa uelewa wangu ni kwamba, benki inapopewa kibali cha kuendesha biashara huduma za kibenki nchini na BoT, huwa wanatakiwa kuweka kiwango fulani cha fedha BoT, hii ni pesa ambayo hawawezi kuichukua. Na BoT hufuatilia mwenendo wa benki husika na kuitaka iongeze kiwango hicho kutokana na fedha za wateja wake.
Kwa mantiki hiyo kiwango cha hiyo akiba hutofautiana kutoka benki moja hadi nyingine kutokana na kiwango cha fedha walizonazo na ukubwa wa benki.
Na jambo la pili, benki zinakua insured, na hawatakiwi kuwa na kiwango zaidi ya kile ambacho wamekubaliana na kampuni ya insurance na vilevile BoT wanakagua kuona hivyo viwango vinazingatiwa. Ndio maana kila mara utakuta mabenki yanaenda kuweka na kutoa hela BoT. Ni kosa benki kuhifadhi fedha zaidi ya kile ilichopangiwa au kukiwekea insurance.
Hadi hapo nadhani kama benki itapatwa na majanga, wateja wao wanakuwa na uhakika wakupata fedha zao.
Nadhani imeeleweka hata kama sio kwa kiwango ambacho muuliza swali alikitarajia, nadhani wadau wengine wataongezea.
Be blessed