Tukibaki Hai, Tutasimulia

Tukibaki Hai, Tutasimulia

Jamani Tivuu ake tuwekee nyingine basi
 
TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 16


Na Steve B.S.M



Mpelelezi aliingia ndani ya ukumbi wa San Pablo Lytton Casino.

Macho yake yalitazama hapa na pale. Huku na kule.

Alitazama saa yake ya mkononi. Kweli alikuwa amechelewa.

Alikuwa anailifahamu hilo.

Kutazama kwake saa kulikuwa ni kuangalia tu ni namna gani amekawia.

Alifika kwenye kumbi kubwa, akasimama na kutazama kwa kama dakika mbili hivi.

Hakumwona mlengwa wake.

Mwanamke yule hakuwapo kwenye uwepo wa macho yake.

Waliojaa hapa walikuwa ni wacheza kamari na wala starehe wengine. Walijaa kwelikweli. Lakini si anayemtafuta.

Akashusha pumzi fupi.

Akiwa ametundika koti lake la mvua mkono wake wa kushoto, akasogea mahali pa kujipatia kinywaji.

Alihitaji kitu cha kumpoza kwa siku hii ya leo wakati akitazama kama bado ana nafasi ya kumwona mlengwa wake.

Aliagiza glasi ya whisky, akaegama akinywa taratibu.

Mara kadhaa alikunja sura yake akimeza kitu hii ngumu akiwa anatafakari yaliyotokea leo.

Huku macho yake hayakulala. Bado yaliendelea kutazamatazama kama atabahatika kumwona mtu wake..

Alijiuliza.

Kwanini mwanamke yule hakuona busara kubadilishana namba pale walipoonana kwa mara ya kwanza badala yake akasihi waonane hapa majira kama haya?

Alipoyatafakari ya mwanamke huyo, akahitimisha kwa kukiri ni mwanamke wa kipekee.

Alitabasamu.

Namna alivyocheza naye kamari na kushinda kila mchezo, hili amekuwa akiliwaza sana, kwake ilikuwa ni ajabu mno.

Akashushia na fundo moja la whisky.

Alikunja sura kwa mbali akimeza fundo hilo.

Hivi vitu vigumu huwa anakunywa mara chachechache, siku kama ya leo.

Lakini kwake haijawahi kuwa tabu kamwe.

Si mtu wa pombe sana lakini alibarikiwa kichwa cha kuhimili pombe. Ni nadra sana kumkuta amezidiwa sababu ya ulabu.

Alisafisha koo lake linaloungua alafu akaagiza tena kinywaji.

Akanywa taratibu na kumaliza.

Bado hakufanikiwa kumwona mtu wake.

Kabla hajaagiza tena, akaona aendee mchezo wake aupendao. Mchezo wa kamari.

Aliketi katika mashine moja iliyokuwa pweke, akaweka pesa, mchezo ukaanza.

Alicheza mchezo mmoja baada ya mwingine. Aliweka pesa na kuweka pesa.

Kila alipoweka pesa, ikaliwa.

Kuna muda alibamiza mashine hiyo kiasi majirani zake wakamwangalia kwa taharuki.

Aliona linamfanyia kusudi.

Lakini hilo haikumsaidia kwani alipoweka tena, pesa ikaliwa.

Alihisi kichwa kimekuwa kizito. Ufanisi wake umepungua mno.

Yote hii sababu ya pombe?

Hapana. Alikataa.

Tangu lini?

Lakini kadiri muda ulivyozidi kusonga mbele ndivyo alizidi kuhisi anazidiwa.

Kichwa kinakuwa kizito, kinazungukazunguka.

Akaminya macho yake kwanguvu.

Punde, akahisi mkono kwenye bega lake la kulia. Kutazama, ni yule mwanamke mrembo.

Alikuwa amesimama akitabasamu.

Tabasamu mwanana linalovutia.

Nywele zake leo alikuwa amezilazia bega la kushoto, amevalia gauni la kijani lililoacha mabega yake yote wazi.

Gauni hilo lilimetameta na mwanga wa hapa.

Alilioanisha na kidani cha hereni yake ndefu iliyoning'inia katika sikio lake lenye matundu mawili ya kuvalia hereni.

Tundu la pili katika masikio yake, aliyavalia hereni fupi rangi nyekundu.

Rangi ambayo aliioanisha na mkoba wake mdogo usiokuwa na mkanda.

Mkoba huo alikuwa ameushikilia na mkono wake wa kushoto.

Mpelelezi akasema,

"Aaanh ni wewe!"

Macho yake yalikuwa malegevu.

Akajifaragua kusimama awe sambamba na mgeni wake.

Mwanamke yule akatabasamu akimwangalia.

Akasema,

"Naona umekuja."

Mpelelezi akamjibu,

"Ndio, nimeitikia wito wako "

Mwanamke akamwambia,

"Lakini umechelewa. Nimekuwa hapa kwa muda mrefu sana kukungojea."

Mpelelezi akahamaki akisema,

"Hivyo ulikuwa hapa hata nusu saa iliyopita?"

Mwanamke huyo akatikisa kichwa chake kuridhia.

Akamwambia Mpelelezi kwamba alimwona akifanya yote hayo mpaka kuja kwenye mashine hii ya kamari.

Muda wote huo tangu aingie macho yake yalikuwa pamoja naye.

Alisema,

"Nilitaka kuona uvumilivu wako kama upo sawa na wangu, haswa baada ya kuniweka hapa masaa."

Aliposema hayo, akamuuliza Mpelelezi kama angetaka kucheza naye michezo kadhaa. Mpelelezi akakataa.

Tayari alishapoteza michezo kadhaa hapa, na kichwa chake hakipo sawa.

Hata aliposema hayo, akapata fahamu ya kwamba miguu yake haikuwa na nguvu. Alikuwa anatumia jitihada kubwa sana kujikaza asije akaangukia chini.

Magoti yaligongana.

Yanatetemeka.

Aliomba Mungu wake anayemjua Mwanamke huyu asitambue mapambano yake hayo ya siri lakini alikosa matumaini.

Alihisi anaelekea kushindwa

Aliachana na mazungumzo ya mwanamke huyo akizingatia zaidi mwili wake unaoenda nje ya uwezo.

Jasho jembamba linamchuruza.

Mwanamke yule akamuuliza,

"Upo sawa, bwana?"

Akatikisa kichwa kuridhia. Uso wake ameukunja.

Ghafla, akaona ukumbi unabiduka chini kuwa juu na juu kuwa chini.

Kufumba na kufumbua yuko chini. Hoi!

Anawasikia na kuwaona watu kwa mbali sana. Hamna anachohisi mwilini mwake. Si joto wala baridi. Si maumivu wala furaha.

Haelewi.

Alisikia kwa mbali mwanamke akisema,

"Mungu wangu! Msaada. Nahitaji msaada."

Aliona watu, kwa muono wake hafifu, wakiwa wamesimama wanamtazama.

Wamesimama kama mishumaa.

Wanamwangalia pasipo kufanya lolote lile.

Hakuelewa watu hao walikuwa wanafurahi ama wanasikitika juu yake kwani nyuso zao hazikuonekana vema.

Aliwaona katika ukungu mithili ya kioo kilichoathiriwa na mvuke.

Muda kidogo akasikia mwangwi wa watu wakiangua vicheko huku glasi zikigongana kang-kang, kang-kang.

Kisha hureeeeee!

Akajipotezea fahamu.

***

Brooklyn, New York.

Asubuhi ya saa mbili.

Baada ya mhudumu kuweka mezani kisahani kidogo chenye 'hot ice cream', Richie alinyanyua kijiko chake upesi akajipakulia mdomoni.

Alikuwa amevalia shati pana lenye rangi ya kutu. Masikioni ana 'earphone' zisizotoa sauti. Chini ana jeans nyeusi yenye mkanda mpana uliobana kwanguvu shati lake.

Miguuni raba nyeupe.

Alikuwa na hamu kweli na ice cream.

Uso wake ulieleza namna gani alivyofaidi ladha hii adhimu kila alipoitia mdomoni mwake.

Akiwa anaendelea kufurahia chakula hiki, 'hafla, akasikia mtu akimwita kwa jina lake.

Mtu huyo alikaa kiti kilichomkabala naye, akatabasamu na kumjulia hali.

Alikuwa ni mwanaume mweusi mwenye kunyoa nywele zake kwa mtindo wa panki.

Ana ndevu nyingi zilizochongwa vema kufunika taya na kidevu chake.

Juu amevalia koti la 'jeans', ndani tisheti nyeusi. Chini amevalia suruali ya jeans rangi ya samawati na viatu vikubwa vya kaki aina ya 'Timberland'.

Aliambatana na begi mgongoni. Begi ambalo aliliweka mezani punde alipoketi chini.

Richie akatabasamu.

Huyu ndo' ambaye alikuwa akimngojea hapa.

Alisema,

"Upo ndani ya muda, Jamal. Hiko ndo' nakupendea."

Jamal, mwanaume yule mweusi, akamwambia akiwa anaegeshea mguu wake juu ya mwingine,

"Kwa namna ulivyonisihi, ilibidi niwahi hapa kabla ya kunyookea chuo. Ebu niambie ni kazi gani hiyo?"

Hapa Richie akamshusha presha Jamal.

Alimwambia,

"Ni udadisi wangu tu unanisumbua, bwana. Sijajua kama jambo hili ni kubwa ama lah japo hisia zangu zinanambia hivyo."

Akatoa 'flash drive' rangi nyeupe na kumpatia Jamal.

Akamwambia,

"Nitazamie kazi hizi uniambie nini maana yake."

Jamal akauliza,

"Kazi gani?"

Richie akamsihi,

"Tazama uone."

Jamal akafungua begi lake na kutoa tarakilishi yake ya kisasa chapa ya HP rangi ya fedha.

Akaifungua na kuiwasha kisha akapachika 'flashdrive' alopewa.

Akiwa anangoja, akaagiza kahawa kwa mhudumu. Punde kidogo kahawa yake ikafika ikiwa inafuka moshi.

Akanywa taratibu akibofya tarakilishi yake kwa kidole kimoja cha mkono wa kuume.

Baada ya muda kidogo, akamuuliza Richie,

"Nani amekupa kazi hii?"

Richie akajibu kwa kuuliza,

"Kwani vipi?"

Jamal akaendelea kutazama kazi hiyo akifungua kurasa baada ya kurasa, upesi akirusha macho yake ya kitaalamu.

Richie akajisogeza karibu naye apate kuona.

Alitazama kioo cha tarakilishi asipate kuelewa hata kilichoandikwa.

Akauliza,

"Kuna nini?"

Jamal akamjibu,

"Kuna vitu vingi sana ndani ya data hizi. Kwa haraka hivi sitaweza kujua kila kitu. Yanipasa kuwa na muda."

Richie akauliza,

"Kwani kwa ulivyotazama hapo, hujapata hata wazo tu la juujuu?"

Jamal akatikisa kichwa akisema,

"Si hivyo kama unavyodhani, Richie. Hizi data ni complex na zimewasilishwa kwa kutumia lugha ya kitaalamu ya kemia. Unahitaji muda wa kutosha kuzipitia na kuelewa.

Muda huu wa dakika kumi na tano hautatosha. Hizi fomula za kikemia zs molecular na structural ambazo zimewekwa hapa zina taarifa nyingi za compounds.

Nahitaji kuzichambua ili kupata picha kamili ni nini kinachoongelewa hapa."

Richie akashika kiuno. Akauliza,

"Kwahiyo itachukua muda gani?"

Jamal akamjibu,

"Nipe wiki hivi, n'takujuza hatua niliyofikia."

Richie akastaajabu,

"Hatua? Sio kwamba utakuwa ushajua kila kitu?"

Jamal akaguna.

Akaifunga tarakilishi yake na kuchomoa flash ya Richie.

Akamkabidhi akimwambia,

"Kama una haraka sana, tafuta mtu mwingine. Mimi sitaweza."

Richie akapaswa kuwa mpole.

Alitabasamu akimrudishia bwana huyo flash mkononi mwake akimsihi afanye vile anavyoona bora.

Lakini akaweka neno,

"Tafadhali jitahidi iwe upesi iwezekanavyo."

Jamal akamtoa hofu. Alimwambia atafanya kila kilichopo ndani ya uwezo wake.

Kwasababu ya muda kumtupa mkono, akafungasha vitu vyake aondoke. Hakumalizia hata kahawa yake mezani.

Aliweka begi mgongoni akatokomea akimwacha Richie anamsindikiza kwa macho.

Alipotokomea, ndo' Richie akampigia simu Hilda kumweleza kuwa ameshafika mahala walipokubaliana.

Yu upande wa kaskazini wa mlango wa mgahawa.

Baada ya robo saa, Hilda akawa amewasili eneo hilo.

Alikuwa amevalia kijisweta chepesi kilichokuwa wazi, rangi yake jani la mgomba lililokauka.

Ndani yake anashati jeusi lililofika mpaka mapajani.

Chini ana taiti nyeusi iliyomkaba mpaka kwenye enka za miguu, ikapokelewa na viatu aina ya 'allstars' rangi nyeupe.

Alivutia kutazama.

Watu kadhaa hapa mgahawani walimpatia muda wao kumtazama, haswa Richie ambaye alimtazama mpaka anafika na kuketi mbele yake.

Moyo wake ulikuwa unaenda mbio.

Hakuelewa kwanini hakuwahi kumzoea Hilda.

Kila mwanamke huyo anapotokea mbele ya macho yake basi amekuwa akimkamata mazingatio mithili ya jambo la kushtukiza.

Naye Hilda, kama mtu anayefahamu hilo, akatabasamu akimtazama Richie.

Aliketi.

Akatengeneza nywele zake kwa mkono wa kuume.

"Nimefika."

Richie akatabasamu. Punde mhudumu akaja na kumsikiza mgeni. Ndani ya muda mfupi chakula chepesi cha asubuhi kikawapo mezani.

Chakula hicho kilisindikizwa na soga za hapa na pale, wakitaniana na kuongea mambo ya jumla kabla hawajafika katika mada yao kuu.

Hapa kwa hamu, Hilda akamuuliza Richie juu ya kazi ile.

Alitaka kujua wapi alipofikia katika mkakati wake.

Richie akatabasamu kisha akajikomba kwa kujiamini.

Alimwambia Hilda,

"Kazi ipo mkononi mwa mtaalamu hivi sasa tunavyoongea. Ndani ya wiki hii tutakuwa tushapata kujua haswa kinachoendelea baina ya boss Bryson na mabwana wale."

Lakini Hilda alihofia.

Alikumbuka maagano yale aliyoapa kuhusu kazi hiyo kuwa kila jambo litakuwa siri.

Akamtahadharisha Richie.

Alimwambia laiti kazi hiyo ingelikuwa bado imo mikononi mwake kwa siri, basi katu asingelimhusisha kwa kuhofia kuhatarisha usalama wake.

Lakini katika hilo Richie alipiga kifua chake. Akamtoa hofu na kumjaza matumaini.

Alimwambia,

"Hilda, utafanyaje kazi usiyojua inahusu nini? Na hujakaa ukajiuliza kama boss wako anakulipa fedha kiasi kingi hivyo yeye atakuwa anapata kiasi gani? Kwanini hiyo kazi ina pesa nyingi hivyo?

Tumia akili, Hilda. Hii kazi inaweza ikawa mlango wetu wa mafanikio. Huwezi jua tutaibuka na nini hapa. Hamna mafanikio bila kubeba risk.

Tukubali kulibeba hili. Mbeleni, naona kabisa, kuna tuzo."

Hilda akasema,

"Lakini wewe Richie ndo' ulikuwa wa kwanza kunisihi kuhusu usalama wangu kwenye hii kazi. Mbona umegeuka ghafla hivyo?"

Richie akatumia fursa hii kumweleza Hilda juu ya namna gani alitafakari usiku mzima juu ya swala hili mezani.

Katika tafakari yake hiyo, alijiona yeye pamoja na mwenziwe wanavyoweza kutumia mwanya huu katika kutamatisha uduni wa maisha yao kwa ujumla.

Aliwaza namna gani watakavyoweza kufurahia maisha yao kwa kusafiri huku na kule kuburudisha nafsi zao kwa mandhari nzuri kama zile za Maldives na Copacabana endapo watakapojenga misingi ya pesa.

Lakini zaidi, hili ndani ya nafsi yake asimwambie mtu yeyote, aliona hii inaweza ikawa nafasi ya kujiwezesha kiuchumi katika namna ambayo ataweza kumhudumia mwanamke ampendaye.

Mwanamke huyu aliyeketi mkabala naye.

Hapo alisema na kifua chake pasipo kutumia kinywa na sauti.

Alisema na macho tu Hilda asielewe kitu.

Yeye aliendelea kutafuna, kwa taratibu, akiwaza haya mambo.

Ladha ya chakula aliisikia kwa mbali sana.

Richie alimshika mkono akamsihi amwamini. Kila kitu kitakuwa sawa.

Lakini zaidi akamwomba Hilda kiasi fulani cha pesa.

Kiasi ambacho kilimfanya Hilda aache kutafuna amtazame Richie machoni.

Akamuuliza,

"Dola elfu kumi? Ya nini yote hiyo?"

Richie akamweleza mpango wake.

Laiti wakitumia pesa hiyo, basi watamshawishi bwana Jamal aifanye kazi yao kwa haraka na ufanisi.

Aliamini kufanya kazi hiyo kiridhaa huenda ikapelekea wao kuchelewa malengo.

Hilda akatilia shaka.

Aliona pesa hiyo ni kubwa sana kiasi kwamba itamshtua bwana huyo kuanza kupeleleza nini kipo nyuma yake.

Badala yake alishauri iwe dola alfu mbili.

Hapo wakaridhiana.

Richie akanyanyua simu yake na kumpigia Jamal.

Aliweka 'loudspeaker'.

Bwana huyo alipopokea, akamweleza kuhusu ofa yake.

Jamal aliposikia hiyo ofa akasema kazi hiyo itakuwa tayari ndani ya siku tatu. Lakini kama wakiongeza kidogo basi ndani ya siku moja tu atakuwa ameikamilisha.

Hapo Hilda na Richie wakatazamana.

Richie akaonyesha ishara ya vidole kumi. Hilda akatikisa kichwa kukataa.

Akaonyeshea vidole vitatu.

Basi Richie akasema kwenye simu,

"Dola alfu tatu, kazi kesho iwe tayari."

Jamal akaridhia.

Alisema,

"Tuonane kesho majira ya asubuhi, hapohapo tulipoonana leo."


**
 
TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 16


Na Steve B.S.M




Mpelelezi aliingia ndani ya ukumbi wa San Pablo Lytton Casino.

Macho yake yalitazama hapa na pale. Huku na kule.

Alitazama saa yake ya mkononi. Kweli alikuwa amechelewa.

Alikuwa anailifahamu hilo.

Kutazama kwake saa kulikuwa ni kuangalia tu ni namna gani amekawia.

Alifika kwenye kumbi kubwa, akasimama na kutazama kwa kama dakika mbili hivi.

Hakumwona mlengwa wake.

Mwanamke yule hakuwapo kwenye uwepo wa macho yake.

Waliojaa hapa walikuwa ni wacheza kamari na wala starehe wengine. Walijaa kwelikweli. Lakini si anayemtafuta.

Akashusha pumzi fupi.

Akiwa ametundika koti lake la mvua mkono wake wa kushoto, akasogea mahali pa kujipatia kinywaji.

Alihitaji kitu cha kumpoza kwa siku hii ya leo wakati akitazama kama bado ana nafasi ya kumwona mlengwa wake.

Aliagiza glasi ya whisky, akaegama akinywa taratibu.

Mara kadhaa alikunja sura yake akimeza kitu hii ngumu akiwa anatafakari yaliyotokea leo.

Huku macho yake hayakulala. Bado yaliendelea kutazamatazama kama atabahatika kumwona mtu wake..

Alijiuliza.

Kwanini mwanamke yule hakuona busara kubadilishana namba pale walipoonana kwa mara ya kwanza badala yake akasihi waonane hapa majira kama haya?

Alipoyatafakari ya mwanamke huyo, akahitimisha kwa kukiri ni mwanamke wa kipekee.

Alitabasamu.

Namna alivyocheza naye kamari na kushinda kila mchezo, hili amekuwa akiliwaza sana, kwake ilikuwa ni ajabu mno.

Akashushia na fundo moja la whisky.

Alikunja sura kwa mbali akimeza fundo hilo.

Hivi vitu vigumu huwa anakunywa mara chachechache, siku kama ya leo.

Lakini kwake haijawahi kuwa tabu kamwe.

Si mtu wa pombe sana lakini alibarikiwa kichwa cha kuhimili pombe. Ni nadra sana kumkuta amezidiwa sababu ya ulabu.

Alisafisha koo lake linaloungua alafu akaagiza tena kinywaji.

Akanywa taratibu na kumaliza.

Bado hakufanikiwa kumwona mtu wake.

Kabla hajaagiza tena, akaona aendee mchezo wake aupendao. Mchezo wa kamari.

Aliketi katika mashine moja iliyokuwa pweke, akaweka pesa, mchezo ukaanza.

Alicheza mchezo mmoja baada ya mwingine. Aliweka pesa na kuweka pesa.

Kila alipoweka pesa, ikaliwa.

Kuna muda alibamiza mashine hiyo kiasi majirani zake wakamwangalia kwa taharuki.

Aliona linamfanyia kusudi.

Lakini hilo haikumsaidia kwani alipoweka tena, pesa ikaliwa.

Alihisi kichwa kimekuwa kizito. Ufanisi wake umepungua mno.

Yote hii sababu ya pombe?

Hapana. Alikataa.

Tangu lini?

Lakini kadiri muda ulivyozidi kusonga mbele ndivyo alizidi kuhisi anazidiwa.

Kichwa kinakuwa kizito, kinazungukazunguka.

Akaminya macho yake kwanguvu.

Punde, akahisi mkono kwenye bega lake la kulia. Kutazama, ni yule mwanamke mrembo.

Alikuwa amesimama akitabasamu.

Tabasamu mwanana linalovutia.

Nywele zake leo alikuwa amezilazia bega la kushoto, amevalia gauni la kijani lililoacha mabega yake yote wazi.

Gauni hilo lilimetameta na mwanga wa hapa.

Alilioanisha na kidani cha hereni yake ndefu iliyoning'inia katika sikio lake lenye matundu mawili ya kuvalia hereni.

Tundu la pili katika masikio yake, aliyavalia hereni fupi rangi nyekundu.

Rangi ambayo aliioanisha na mkoba wake mdogo usiokuwa na mkanda.

Mkoba huo alikuwa ameushikilia na mkono wake wa kushoto.

Mpelelezi akasema,

"Aaanh ni wewe!"

Macho yake yalikuwa malegevu.

Akajifaragua kusimama awe sambamba na mgeni wake.

Mwanamke yule akatabasamu akimwangalia.

Akasema,

"Naona umekuja."

Mpelelezi akamjibu,

"Ndio, nimeitikia wito wako "

Mwanamke akamwambia,

"Lakini umechelewa. Nimekuwa hapa kwa muda mrefu sana kukungojea."

Mpelelezi akahamaki akisema,

"Hivyo ulikuwa hapa hata nusu saa iliyopita?"

Mwanamke huyo akatikisa kichwa chake kuridhia.

Akamwambia Mpelelezi kwamba alimwona akifanya yote hayo mpaka kuja kwenye mashine hii ya kamari.

Muda wote huo tangu aingie macho yake yalikuwa pamoja naye.

Alisema,

"Nilitaka kuona uvumilivu wako kama upo sawa na wangu, haswa baada ya kuniweka hapa masaa."

Aliposema hayo, akamuuliza Mpelelezi kama angetaka kucheza naye michezo kadhaa. Mpelelezi akakataa.

Tayari alishapoteza michezo kadhaa hapa, na kichwa chake hakipo sawa.

Hata aliposema hayo, akapata fahamu ya kwamba miguu yake haikuwa na nguvu. Alikuwa anatumia jitihada kubwa sana kujikaza asije akaangukia chini.

Magoti yaligongana.

Yanatetemeka.

Aliomba Mungu wake anayemjua Mwanamke huyu asitambue mapambano yake hayo ya siri lakini alikosa matumaini.

Alihisi anaelekea kushindwa

Aliachana na mazungumzo ya mwanamke huyo akizingatia zaidi mwili wake unaoenda nje ya uwezo.

Jasho jembamba linamchuruza.

Mwanamke yule akamuuliza,

"Upo sawa, bwana?"

Akatikisa kichwa kuridhia. Uso wake ameukunja.

Ghafla, akaona ukumbi unabiduka chini kuwa juu na juu kuwa chini.

Kufumba na kufumbua yuko chini. Hoi!

Anawasikia na kuwaona watu kwa mbali sana. Hamna anachohisi mwilini mwake. Si joto wala baridi. Si maumivu wala furaha.

Haelewi.

Alisikia kwa mbali mwanamke akisema,

"Mungu wangu! Msaada. Nahitaji msaada."

Aliona watu, kwa muono wake hafifu, wakiwa wamesimama wanamtazama.

Wamesimama kama mishumaa.

Wanamwangalia pasipo kufanya lolote lile.

Hakuelewa watu hao walikuwa wanafurahi ama wanasikitika juu yake kwani nyuso zao hazikuonekana vema.

Aliwaona katika ukungu mithili ya kioo kilichoathiriwa na mvuke.

Muda kidogo akasikia mwangwi wa watu wakiangua vicheko huku glasi zikigongana kang-kang, kang-kang.

Kisha hureeeeee!

Akajipotezea fahamu.

***

Brooklyn, New York.

Asubuhi ya saa mbili.


Baada ya mhudumu kuweka mezani kisahani kidogo chenye 'hot ice cream', Richie alinyanyua kijiko chake upesi akajipakulia mdomoni.

Alikuwa amevalia shati pana lenye rangi ya kutu. Masikioni ana 'earphone' zisizotoa sauti. Chini ana jeans nyeusi yenye mkanda mpana uliobana kwanguvu shati lake.

Miguuni raba nyeupe.

Alikuwa na hamu kweli na ice cream.

Uso wake ulieleza namna gani alivyofaidi ladha hii adhimu kila alipoitia mdomoni mwake.

Akiwa anaendelea kufurahia chakula hiki, 'hafla, akasikia mtu akimwita kwa jina lake.

Mtu huyo alikaa kiti kilichomkabala naye, akatabasamu na kumjulia hali.

Alikuwa ni mwanaume mweusi mwenye kunyoa nywele zake kwa mtindo wa panki.

Ana ndevu nyingi zilizochongwa vema kufunika taya na kidevu chake.

Juu amevalia koti la 'jeans', ndani tisheti nyeusi. Chini amevalia suruali ya jeans rangi ya samawati na viatu vikubwa vya kaki aina ya 'Timberland'.

Aliambatana na begi mgongoni. Begi ambalo aliliweka mezani punde alipoketi chini.

Richie akatabasamu.

Huyu ndo' ambaye alikuwa akimngojea hapa.

Alisema,

"Upo ndani ya muda, Jamal. Hiko ndo' nakupendea."

Jamal, mwanaume yule mweusi, akamwambia akiwa anaegeshea mguu wake juu ya mwingine,

"Kwa namna ulivyonisihi, ilibidi niwahi hapa kabla ya kunyookea chuo. Ebu niambie ni kazi gani hiyo?"

Hapa Richie akamshusha presha Jamal.

Alimwambia,

"Ni udadisi wangu tu unanisumbua, bwana. Sijajua kama jambo hili ni kubwa ama lah japo hisia zangu zinanambia hivyo."

Akatoa 'flash drive' rangi nyeupe na kumpatia Jamal.

Akamwambia,

"Nitazamie kazi hizi uniambie nini maana yake."

Jamal akauliza,

"Kazi gani?"

Richie akamsihi,

"Tazama uone."

Jamal akafungua begi lake na kutoa tarakilishi yake ya kisasa chapa ya HP rangi ya fedha.

Akaifungua na kuiwasha kisha akapachika 'flashdrive' alopewa.

Akiwa anangoja, akaagiza kahawa kwa mhudumu. Punde kidogo kahawa yake ikafika ikiwa inafuka moshi.

Akanywa taratibu akibofya tarakilishi yake kwa kidole kimoja cha mkono wa kuume.

Baada ya muda kidogo, akamuuliza Richie,

"Nani amekupa kazi hii?"

Richie akajibu kwa kuuliza,

"Kwani vipi?"

Jamal akaendelea kutazama kazi hiyo akifungua kurasa baada ya kurasa, upesi akirusha macho yake ya kitaalamu.

Richie akajisogeza karibu naye apate kuona.

Alitazama kioo cha tarakilishi asipate kuelewa hata kilichoandikwa.

Akauliza,

"Kuna nini?"

Jamal akamjibu,

"Kuna vitu vingi sana ndani ya data hizi. Kwa haraka hivi sitaweza kujua kila kitu. Yanipasa kuwa na muda."

Richie akauliza,

"Kwani kwa ulivyotazama hapo, hujapata hata wazo tu la juujuu?"

Jamal akatikisa kichwa akisema,

"Si hivyo kama unavyodhani, Richie. Hizi data ni complex na zimewasilishwa kwa kutumia lugha ya kitaalamu ya kemia. Unahitaji muda wa kutosha kuzipitia na kuelewa.

Muda huu wa dakika kumi na tano hautatosha. Hizi fomula za kikemia zs molecular na structural ambazo zimewekwa hapa zina taarifa nyingi za compounds.

Nahitaji kuzichambua ili kupata picha kamili ni nini kinachoongelewa hapa."

Richie akashika kiuno. Akauliza,

"Kwahiyo itachukua muda gani?"

Jamal akamjibu,

"Nipe wiki hivi, n'takujuza hatua niliyofikia."

Richie akastaajabu,

"Hatua? Sio kwamba utakuwa ushajua kila kitu?"

Jamal akaguna.

Akaifunga tarakilishi yake na kuchomoa flash ya Richie.

Akamkabidhi akimwambia,

"Kama una haraka sana, tafuta mtu mwingine. Mimi sitaweza."

Richie akapaswa kuwa mpole.

Alitabasamu akimrudishia bwana huyo flash mkononi mwake akimsihi afanye vile anavyoona bora.

Lakini akaweka neno,

"Tafadhali jitahidi iwe upesi iwezekanavyo."

Jamal akamtoa hofu. Alimwambia atafanya kila kilichopo ndani ya uwezo wake.

Kwasababu ya muda kumtupa mkono, akafungasha vitu vyake aondoke. Hakumalizia hata kahawa yake mezani.

Aliweka begi mgongoni akatokomea akimwacha Richie anamsindikiza kwa macho.

Alipotokomea, ndo' Richie akampigia simu Hilda kumweleza kuwa ameshafika mahala walipokubaliana.

Yu upande wa kaskazini wa mlango wa mgahawa.

Baada ya robo saa, Hilda akawa amewasili eneo hilo.

Alikuwa amevalia kijisweta chepesi kilichokuwa wazi, rangi yake jani la mgomba lililokauka.

Ndani yake anashati jeusi lililofika mpaka mapajani.

Chini ana taiti nyeusi iliyomkaba mpaka kwenye enka za miguu, ikapokelewa na viatu aina ya 'allstars' rangi nyeupe.

Alivutia kutazama.

Watu kadhaa hapa mgahawani walimpatia muda wao kumtazama, haswa Richie ambaye alimtazama mpaka anafika na kuketi mbele yake.

Moyo wake ulikuwa unaenda mbio.

Hakuelewa kwanini hakuwahi kumzoea Hilda.

Kila mwanamke huyo anapotokea mbele ya macho yake basi amekuwa akimkamata mazingatio mithili ya jambo la kushtukiza.

Naye Hilda, kama mtu anayefahamu hilo, akatabasamu akimtazama Richie.

Aliketi.

Akatengeneza nywele zake kwa mkono wa kuume.

"Nimefika."

Richie akatabasamu. Punde mhudumu akaja na kumsikiza mgeni. Ndani ya muda mfupi chakula chepesi cha asubuhi kikawapo mezani.

Chakula hicho kilisindikizwa na soga za hapa na pale, wakitaniana na kuongea mambo ya jumla kabla hawajafika katika mada yao kuu.

Hapa kwa hamu, Hilda akamuuliza Richie juu ya kazi ile.

Alitaka kujua wapi alipofikia katika mkakati wake.

Richie akatabasamu kisha akajikomba kwa kujiamini.

Alimwambia Hilda,

"Kazi ipo mkononi mwa mtaalamu hivi sasa tunavyoongea. Ndani ya wiki hii tutakuwa tushapata kujua haswa kinachoendelea baina ya boss Bryson na mabwana wale."

Lakini Hilda alihofia.

Alikumbuka maagano yale aliyoapa kuhusu kazi hiyo kuwa kila jambo litakuwa siri.

Akamtahadharisha Richie.

Alimwambia laiti kazi hiyo ingelikuwa bado imo mikononi mwake kwa siri, basi katu asingelimhusisha kwa kuhofia kuhatarisha usalama wake.

Lakini katika hilo Richie alipiga kifua chake. Akamtoa hofu na kumjaza matumaini.

Alimwambia,

"Hilda, utafanyaje kazi usiyojua inahusu nini? Na hujakaa ukajiuliza kama boss wako anakulipa fedha kiasi kingi hivyo yeye atakuwa anapata kiasi gani? Kwanini hiyo kazi ina pesa nyingi hivyo?

Tumia akili, Hilda. Hii kazi inaweza ikawa mlango wetu wa mafanikio. Huwezi jua tutaibuka na nini hapa. Hamna mafanikio bila kubeba risk.

Tukubali kulibeba hili. Mbeleni, naona kabisa, kuna tuzo."

Hilda akasema,

"Lakini wewe Richie ndo' ulikuwa wa kwanza kunisihi kuhusu usalama wangu kwenye hii kazi. Mbona umegeuka ghafla hivyo?"

Richie akatumia fursa hii kumweleza Hilda juu ya namna gani alitafakari usiku mzima juu ya swala hili mezani.

Katika tafakari yake hiyo, alijiona yeye pamoja na mwenziwe wanavyoweza kutumia mwanya huu katika kutamatisha uduni wa maisha yao kwa ujumla.

Aliwaza namna gani watakavyoweza kufurahia maisha yao kwa kusafiri huku na kule kuburudisha nafsi zao kwa mandhari nzuri kama zile za Maldives na Copacabana endapo watakapojenga misingi ya pesa.

Lakini zaidi, hili ndani ya nafsi yake asimwambie mtu yeyote, aliona hii inaweza ikawa nafasi ya kujiwezesha kiuchumi katika namna ambayo ataweza kumhudumia mwanamke ampendaye.

Mwanamke huyu aliyeketi mkabala naye.

Hapo alisema na kifua chake pasipo kutumia kinywa na sauti.

Alisema na macho tu Hilda asielewe kitu.

Yeye aliendelea kutafuna, kwa taratibu, akiwaza haya mambo.

Ladha ya chakula aliisikia kwa mbali sana.

Richie alimshika mkono akamsihi amwamini. Kila kitu kitakuwa sawa.

Lakini zaidi akamwomba Hilda kiasi fulani cha pesa.

Kiasi ambacho kilimfanya Hilda aache kutafuna amtazame Richie machoni.

Akamuuliza,

"Dola elfu kumi? Ya nini yote hiyo?"

Richie akamweleza mpango wake.

Laiti wakitumia pesa hiyo, basi watamshawishi bwana Jamal aifanye kazi yao kwa haraka na ufanisi.

Aliamini kufanya kazi hiyo kiridhaa huenda ikapelekea wao kuchelewa malengo.

Hilda akatilia shaka.

Aliona pesa hiyo ni kubwa sana kiasi kwamba itamshtua bwana huyo kuanza kupeleleza nini kipo nyuma yake.

Badala yake alishauri iwe dola alfu mbili.

Hapo wakaridhiana.

Richie akanyanyua simu yake na kumpigia Jamal.

Aliweka 'loudspeaker'.

Bwana huyo alipopokea, akamweleza kuhusu ofa yake.

Jamal aliposikia hiyo ofa akasema kazi hiyo itakuwa tayari ndani ya siku tatu. Lakini kama wakiongeza kidogo basi ndani ya siku moja tu atakuwa ameikamilisha.

Hapo Hilda na Richie wakatazamana.

Richie akaonyesha ishara ya vidole kumi. Hilda akatikisa kichwa kukataa.

Akaonyeshea vidole vitatu.

Basi Richie akasema kwenye simu,

"Dola alfu tatu, kazi kesho iwe tayari."

Jamal akaridhia.

Alisema,

"Tuonane kesho majira ya asubuhi, hapohapo tulipoonana leo."


**
Asnt sn @S.Mollel
 
Back
Top Bottom