Tumbiliwaulaya
JF-Expert Member
- Nov 22, 2020
- 280
- 435
MBOLEA zinazotumika Katika kilimo ni moja ya kemikali zinazozalishwa kwa kuibadilisha GESI ASILIA kuwa MBOLEA katika nchi zilizo endelea. Hivyo kilimo cha Tanzania kinaweza kufaidika sana kama tukianzisha kiwanda kikubwa cha kubadilisha GESI ASILIA kuwa MBOLEA.
Kwa mujibu wa ripoti ya Benki ya Dunia ya mwaka 2013, uchumi wa Tanzania unategemea kilimo kwa zaidi ya robo moja ya Pato la Taifa (27-32%). Kilimo kinatoa 85% ya bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi na kinaajiri 80% ya nguvukazi nchini.
Tanzania huaagiza 90% ya MBOLEA kutoka nje ya nchi, 10% iliyobaki huzalishwa ndani. Lakini pia, MBOLEA inayozalishwa ndani inafaa kwa udongo wenye tindikali (asidi) tu.
MBOLEA YA UREA ndio mbolea inayotumika zaidi nchini ikichukua zaidi ya 33% ya jumla mbolea zote nchini. Na matumizi ya mbolea yanazidi kupanda kila mwaka.
Kama tukianzisha kiwanda cha kuzalisha tani 2300 za AMMONIA kwa siku na tani 4000 za UREA kwa siku (sawa na tani milioni 1.3 za urea kwa mwaka), kiwango hiki kitaweza kukidhi mahitaji ya soko la ndani na kiasi cha mbolea inayobaki katika masoko ya kikanda na kimataifa. Mradi wa mbolea unaweza kufanikiwa katika uwekezaji mdogo tu.
Prosesi za kuibadilisha GESI ASILIA kuwa MBOLEA.
Hatua ya kwanza kabisa gesi asilia (CH4) itabadilishwa kuwa AMMONIA hapo kuna miungano mbalimbali ya kikemikali itafanyika kwa kutumia vichocheo. AMMONIA yenyewe ni mbolea tayari.
Baada ya hapo AMMONIA itabadilishwa kuwa MBOLEA YA UREA kwa kutumia miungano ya kikekimali.
Lakini pia kutoka kwenye AMMONIA tutafanya miungano mingine ya kikemikali kupata mbolea zifuatazo; AMMONIUM NITRATE (NA), AMMONIUM SULPHATE (SA), AMMONIUM PHOSPHATE (PA).
Kutoka kwenye AMMONIUM NITRATE (NA) tutafanya miungano ya kikemikali na kutapata mbolea ya CALCIUM AMMONIUM NITRATE (CAN).
Kutoka kwenye AMMONIUM PHOSPHATE (PA) tutapata mbolea ya MONOAMMONIUM PHOSPHATE (MAP), na DIAMMONIUM PHOSPHATE (DAP).
Jedwali hili hapa chini linaonyesha matumizi ya mbolea mbalimbali Tanzania.
View attachment 1796151
Mchoro huu wa chini unaonyesha hatua za kuibadilisha GESI ASILIA kuwa MBOLEA ya AMMONIA.
View attachment 1796152
Mchoro huu wa chini unaonyesha mbolea tutakazo zipata kutoka kwenye AMMONIA baada ya kufanya miungano mingine ya kikemikali.
View attachment 1796153
Dangote anajenga kiwanda cha mbolea , kuna uwezekano atatuma gesi kama malighafi ya kuzalishia maana sasahivi anapata gesi kwa ajili ya kuzalishia nishatiKulikuwa na mwekezaji toka Ujerumani kwenye mradi huo wa mbolea na hiyo gesi, naona kampuni hiyo ilikwishajiondoa baada ya kutoonekana maendeleo yoyote kuhusu gesi yenyewe.
Sioni tatizo na hilo ili mradi tu maslahi ya nchi yetu yazingatiwe kiweledi kabisa.Dangote anajenga kiwanda cha mbolea , kuna uwezekano atatuma gesi kama malighafi ya kuzalishia maana sasahivi anapata gesi kwa ajili ya kuzalishia nishati
ndio nasikia kwako mkuuDangote anajenga kiwanda cha mbolea , kuna uwezekano atatuma gesi kama malighafi ya kuzalishia maana sasahivi anapata gesi kwa ajili ya kuzalishia nishati
Ngoja tuoneHii sahau chini ya serikali ya CCM
Muda mrefu sana dangote alipanga kujenga kiwanda cha mbolea wakati wa awamu ya nne , ilikuwa akimaliza kujenga kiwanda cha saruji ajenge cha mboleandio nasikia kwako mkuu
Tukifanikiwa vyema kuwaminya matapeli waliomo kwenye bidhaa hizo na nyingine kadhaa tutafanikiwa vyema kuijenga Tanzania yenye neema.kuanzisha kiwanda kama hiki maana yake ni kuua mrija wa watu hapo,tuache kuagiza mbolea nje? harafu wapigie wapi mbwa gizani? mambo hayahaya ndio yapo kwenye sukari na mafuta ya kula kwenye hivyo vitu vitatu ndio mahali mbwa huwa anapigiwa gizani.
Ehe halafu ikaishia wapi?Muda mrefu sana dangote alipanga kujenga kiwanda cha mbolea wakati wa awamu ya nne , ilikuwa akimaliza kujenga kiwanda cha saruji ajenge cha mbolea
Viongozi tuliowachagua wajitahidi kuyaona haya.Muda mrefu sana dangote alipanga kujenga kiwanda cha mbolea wakati wa awamu ya nne , ilikuwa akimaliza kujenga kiwanda cha saruji ajenge cha mbolea
Kweli mkuu, bila kuwa na hivi viwanda hatuwezi kufanya mapinduzi ya kilimoHili ni shamba la bibi wewe unapakua unavyoweza mengine baadae
Pamoja kamandaKweli mkuu, bila kuwa na hivi viwanda hatuwezi kufanya mapinduzi ya kilimo
Matapeli ni wengi sana na hao ndio wanao kwamisha maendeleo.Tukifanikiwa vyema kuwaminya matapeli waliomo kwenye bidhaa hizo na nyingine kadhaa tutafanikiwa vyema kuijenga Tanzania yenye neema.
Hili kundi ndilo sumbufu sana katika kuhujumu juhudi za wananchi.
Professor wa msoga alikula cha juu akawagawia wachina!Gesi tayari 'tumegawa' kwa WAHISANI hatuna chetu.
Je, wakulima wetu wa kipato cha chini wataweza kumudu bei ya mbolea zitakazozalishwa?Kiwanda kitanunua kwa haohao hakiwezi kuchukua bure.
Wataweza kumudu kwasababu zitazalishwa hapahapa nchini hivyo zitauzwa kwa bei ya chini.Professor wa msoga alikula cha juu akawagawia wachina!
Je, wakulima wetu wa kipato cha chini wataweza kumudu bei ya mbolea zitakazozalishwa?
Kwa nadharia ni wataalamu lakini vitendo ni ziro inawezekana hatukiamini tulicho jifunza tulishinda mitihani tupate vyetiMBOLEA zinazotumika Katika kilimo ni moja ya kemikali zinazozalishwa kwa kuibadilisha GESI ASILIA kuwa MBOLEA katika nchi zilizo endelea. Hivyo kilimo cha Tanzania kinaweza kufaidika sana kama tukianzisha kiwanda kikubwa cha kubadilisha GESI ASILIA kuwa MBOLEA.
Kwa mujibu wa ripoti ya Benki ya Dunia ya mwaka 2013, uchumi wa Tanzania unategemea kilimo kwa zaidi ya robo moja ya Pato la Taifa (27-32%). Kilimo kinatoa 85% ya bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi na kinaajiri 80% ya nguvukazi nchini.
Tanzania huaagiza 90% ya MBOLEA kutoka nje ya nchi, 10% iliyobaki huzalishwa ndani. Lakini pia, MBOLEA inayozalishwa ndani inafaa kwa udongo wenye tindikali (asidi) tu.
MBOLEA YA UREA ndio mbolea inayotumika zaidi nchini ikichukua zaidi ya 33% ya jumla mbolea zote nchini. Na matumizi ya mbolea yanazidi kupanda kila mwaka.
Kama tukianzisha kiwanda cha kuzalisha tani 2300 za AMMONIA kwa siku na tani 4000 za UREA kwa siku (sawa na tani milioni 1.3 za urea kwa mwaka), kiwango hiki kitaweza kukidhi mahitaji ya soko la ndani na kiasi cha mbolea inayobaki katika masoko ya kikanda na kimataifa. Mradi wa mbolea unaweza kufanikiwa katika uwekezaji mdogo tu.
Prosesi za kuibadilisha GESI ASILIA kuwa MBOLEA.
Hatua ya kwanza kabisa gesi asilia (CH4) itabadilishwa kuwa AMMONIA hapo kuna miungano mbalimbali ya kikemikali itafanyika kwa kutumia vichocheo. AMMONIA yenyewe ni mbolea tayari.
Baada ya hapo AMMONIA itabadilishwa kuwa MBOLEA YA UREA kwa kutumia miungano ya kikekimali.
Lakini pia kutoka kwenye AMMONIA tutafanya miungano mingine ya kikemikali kupata mbolea zifuatazo; AMMONIUM NITRATE (NA), AMMONIUM SULPHATE (SA), AMMONIUM PHOSPHATE (PA).
Kutoka kwenye AMMONIUM NITRATE (NA) tutafanya miungano ya kikemikali na kutapata mbolea ya CALCIUM AMMONIUM NITRATE (CAN).
Kutoka kwenye AMMONIUM PHOSPHATE (PA) tutapata mbolea ya MONOAMMONIUM PHOSPHATE (MAP), na DIAMMONIUM PHOSPHATE (DAP).
Jedwali hili hapa chini linaonyesha matumizi ya mbolea mbalimbali Tanzania.
View attachment 1796151
Mchoro huu wa chini unaonyesha hatua za kuibadilisha GESI ASILIA kuwa MBOLEA ya AMMONIA.
View attachment 1796152
Mchoro huu wa chini unaonyesha mbolea tutakazo zipata kutoka kwenye AMMONIA baada ya kufanya miungano mingine ya kikemikali.
View attachment 1796153
Inabidi kufanya analysis ya kutosha kujua kweli kama gharama za uzalishaji zitakuwa chini compared to imported fertilizers ili kuwezesha kitakachozalishwa kushindana kwenye soko.Wataweza kumudu kwasababu zitazalishwa hapahapa nchini hivyo zitauzwa kwa bei ya chini.
Ngoja tuoneInabidi kufanya analysis ya kutosha kujua kweli kama gharama za uzalishaji zitakuwa chini compared to imported fertilizers ili kuwezesha kitakachozalishwa kushindana kwenye soko.