adui namba moja ni ccm, hao wengine wanafata chini yake.Maadui wakuu wa taifa:
(1) Ujinga
(2)Umasikini na
(3)Maradhi.
Adui namba moja hapo juu ndo anamsibu Mh. Msukuma. Pia hakana staha kale kajamaa ni ka kupuuza tu.
Professor anaonekana ni 'dalali' kwenye ishu ya umeme wa gesi, akiwa waziri alitumia lugha kali na ya kuuzi kwa wawekezaji wa ndani akina mengi, aliwaita eti matajiri wenye uwezo wa kuwekeza kwenye 'pipi' na sio kwenye gesi. Unajiuliza hao matijiri Wazungu wenye uwezo walianzaje? Walizaliwa matajiri? Pasipo kuthaminiwa na kuaminiwa wangefika pale?
Ukweli ni kua wasomi wa nchi hii wengi wanaendeshwa na wanasiasa au matajiri. Wanaosoma sana ila wanaishia kwenye umasikini hivyo huamua kujiuza wenyewe
Kama umbeya basi aliuleta Hayati Magufuli maana ndio alikua Rais na ndie alietusanua kuhusu gas labda kama ulikua usikilizi hotuba zake.S
Siyo ya kwetu vipi? Mwaga data hapa, si umbeya
Hapa sipo kwa ajili ya upinzani madudu tuliyokua tunalalamikia miaka mingi Serikali ilikua ni CCM na wasomi walikuwa wa CCM haohao sishangai kuwaona wakirudi tena hii Dunia bro.View attachment 1752792
Badala ya chadema sasa kambi rasmi ya upinzani bungeni mnawaona ni kina nani??
WASOMI !
Akina Assad
Akina Muhongo
Akina Kichere
Etc
Ndio maana Spika kasema lugha za kihasibu sio kila mtu atazielewa niambie shirika la ATCL ambalo lilikufa limefufuliwa kwa shilingi ngapi ili tuweze ku compare na hiyo hasara ya billion 60.Ndo walichokueleza na ukaamini... USISAHAU HAO HAO WALIKUELEZA NDEGE ZETU MWAKA 2018 ZILITENGENEZA FAIDA NA WENGINE WAKAMWAGA NA MAGAWIO SERIKALINI...
Mabeberu mpaka Faida yao irudi ndio inakua ya Watanzania wanyonge vipi unajua mkataba ni wa mda gani?Gas ya mtwara Ni ya kina nani
Beberu yupi? Au na wewe upo lile kundi la wajinga wanaosema JK aliwapa wachina gas yote baada ya Rizwan kushikwa China na madawa ya kulevya? Really!! Mapunda yote yaliyojaa Dar yanasubiri kazi ya kubeba unga, rizwan abebe unga mwenyewe akakamatwe! Kweli Tanzania kuna mazuzu!Mabeberu mpaka Faida yao irudi ndio inakua ya Watanzania wanyonge vipi unajua mkataba ni wa mda gani?
Lugha za kihasibu ndio hizo hizo hasara ni hasara na faida ni faida asitake kutoa mpira nje kwa sababu zisizo na mashiko...Ndio maana Spika kasema lugha za kihasibu sio kila mtu atazielewa niambie shirika la ATCL ambalo lilikufa limefufuliwa kwa shilingi ngapi ili tuweze ku compare na hiyo hasara ya billion 60.
Kama profesa kingereza tatizo, kwa hiyo darasa la sana ndie kingereza kitakuwa nafuu? Mapungufu ya msomi, mafanikio(kifedha) ya mbumbumbu mmoja mmoja yasihalalishe kubeza umuhimu wa elimu. Hiyo Mike anayo itumia kupayuka hayo aelewe haikubuniwa, kuendelezwa na kufikia kiwango iliopo na mtu wa elimu kama ya msukuma.Maprofesa wengine mpaka kiingereza tatizo
Maprofesa wameingia mikataba ya kihayawani
Maprofesa maprofesa bora tukae kimya
Ila jomba Kama musukuma kakuchoma hivi ,ukiona makelele ujue limekugusa
Elimu kubwa inafundisha kuwa bilionea? au hadi uibe? Yaani unakuta mtu anajisifu kasoma sana alafu hakuna jambo lolote analoletea faida binadamu kuhusu elimu yake...Yeye kuwa tajiri asiye na elimu zaidi ya ile ya darasa la saba sio sifa kama anavyodhani. Wapo watu wengi tu wanaoshindwa kufika popote kimaisha sababu ya elimu zao ndogo.
Numbers never lie.... Yaani wewe ndo unataka kutuambia, lugha ya kihasibu inawea ikageuza ile hasara ya 150B kwa miaka mitano mfululizo iwe faida? ACHA WEHUNdio maana Spika kasema lugha za kihasibu sio kila mtu atazielewa niambie shirika la ATCL ambalo lilikufa limefufuliwa kwa shilingi ngapi ili tuweze ku compare na hiyo hasara ya billion 60.
MY POINT IS.... Kwao wao, kila anawapa mawazo mbadala wanamnyooshea vidole... kila anayesema maovu yao wanamnyooshea vidole... WAKAAMUA KUWAONDOA WOTE... sasa wamebaki kunyoosheana vidole wao wenyeweHapa sipo kwa ajili ya upinzani madudu tuliyokua tunalalamikia miaka mingi Serikali ilikua ni CCM na wasomi walikuwa wa CCM haohao sishangai kuwaona wakirudi tena hii Dunia bro.
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]Mheshimiwa Msukuma amepata umaarufu mkubwa siku za karibuni haswa kwa kumkejeli Profesa Muhongo mwenye kuamini kwamba umeme wa gesi ni suluhisho la suala zima la nishati hiyo. Ni mawazo ya Profesa Muhongo na anao uwezo wa kuyatetea kwa hoja kila anaposimama na kuongea bungeni.
Naona kama Msukuma anakwenda mbali sana anapoamua kumkejeli Profesa na akawaweka katika kundi moja maprofesa wote kwa kigezo cha kutokubaliana tu na mitazamo yake. Ujinga ni mzigo mzito sana na upo uhakika hao mabilionea na mamilionea wanaojulikana kila kona wanawategemea wasomi wenye elimu za juu.
Tutakuwa tunapotea kama Taifa tukianza kukubaliana na dhana hizi za darasa la saba kuwa na manufaa na mafanikio kiasi cha wenye elimu kubwa kuanza kuonekana hawana maana. Ni kosa kubwa sana tutakuwa tunalifanya.
Wanaokesha usiku ndani ya maabara kubwa za mataifa yaliyoendelea wakitafuta kila aina ya chanjo dhidi ya Covid19 ni wasomi wa viwango vya juu. Na matokeo ya elimu zao wameanza kuzaa matunda kwani miezi michache ijayo dunia kwa maana ya ile ya watu kuchanganyika wakifanya shughuli mbalimbali itaanza kurudi kama ilivyokuwa zamani.
Wanaoandika ilani na kuwawezesha wagombea wanaopanda majukwaani ni wataalam wa fani mbalimbali. Hivyo Msukuma kuwepo kwake mle bungeni ni matunda ya hao hao wasomi anaowakejeli kisa tu ametofautiana kimtazamo na Prof Muhongo.
Ujinga kama alivyowahi kusema Hayati Mwalimu Julius Nyerere pale Karimjee miaka ya nyuma ni sawa na uchi wa akili. Ndio sababu hata wanamichezo ambao wanafanikiwa wakiwa na elimu ndogo, wakishapata pesa za kutosha huamua kutafuta elimu ambayo waliikosa hapo kabla, lengo ni kuuvalisha nguo ubongo.
Wenye elimu ya darasa wanaoweza kufika alipofika Mheshimiwa mbunge Msukuma ni wachache sana. Na sekta zetu nyingi zimekuwa zikikwama kwa kukosa maarifa sahihi ya wakati husika. Uendeshaji wa taasisi zetu nyingi ukiuchunguza kwa undani unagundua upungufu mwingi unaotokana na elimu kuwa ni ndogo pamoja na wahusika kukosa ufahamu mpana wa kitu wanachokifanya, wanakosa exposure.
Nimemuelewa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kumkabidhi wizara ya mambo ya nje Mama Liberata Mulamula, anataka aitumie exposure yake kubwa katika kujenga taswira chanya ya Tanzania kimataifa. Inakuwa ni aibu unapomsikia mbunge anakejeli elimu wakati ndio silaha namba moja ya mataifa yaliyoendelea.
Kejeli anazokutana nazo Prof Muhongo zinawahusu pia maprofesa wengi ambao wamefanya mengi ya maana na yenye kuonekana kwa faida ya taifa. Ni mawazo fulani duni kuiponda elimu eti kwa sababu ya kutofautiana mitazamo na msomi mmoja
Kosa lake ni kuwa mkweli kwenye nchi ya watawala waongowaongo, incompetent!Niambieni kosa la Profesa Muhongo ni nini?
Profesa anataka tuwe na energy mix, yaani vyanzo vingi vya nishati ikiwemo gesi
Profesa anaeleza kuwa ili umeme wa maji uwe bei chini ni mpaka kwanza urudishe pesa yako uliyoitumia kuinvest kisha ndo mbeleni buko unaweza kuufanya cheap na it takes time
[emoji106][emoji106][emoji106]Msukuma ni mgonjwa wa akili, kutoelewa kwake hoja ya Prop Mhongo ndiko kulikosababisha personal attack zake..
Speaker naye ni wakuaumiwa kwa kuruhusu bunge kufanya personal attacks na sio kujikita kwenye hoja. Speaker ndio msimamizi wa hii mijadala sasa kama anashindwa kusimamia na kuwa mshabiki kwa maslahi yake binafsi mbeleni huko tutapata shida..
Kuruhusu elimu inakejeliwa ndani ya Bunge na bunge linashangilia maana yake ni kuiambia jamii iachane na shule maana haina umuhimu wala msaada...effect yake ni kubwa kuliko tunavyodhania.
Awamu ya tano nayo ni ya kulaumiwa kwa kulazimisha watu watumie fikra za mtu mmoja na ukipingana naye basi wewe msaliti, sio mzalendo, mpiga dili, kibaraka nk.
Prop Mhongo aliwakilisha fikra zake na kuzitetea kwa ufahamu wake bila kumkejeli mtu, Msukuma kama hakubaliana alipaswa kuweka hoja zake mezani tupime na sio kufanya personal attack.