wa stendi
JF-Expert Member
- Jul 7, 2016
- 25,190
- 27,434
Nakumbuka kipindi hicho redio ilikuwa inatangaza mpira wa simba na yanga sasa tukawa tunasikiliza, mimi nikamuuliza mzee mmoja sasa simba anacheza mpira na huyo yanga!!vipi huyo yanga hamwogopi simba!!!yule mzee akanijibu yanga ni mkali balaa anampiga simba!!
Mi nikamuuli huyo yanga kwani ni mnyama gani!! Yule mzee akanijibu kama unataka kuwaona pasua hiyo redio watatoka huko utawaona!!mimi nikamwambia unasema kweli?? Yule mzee akasema ni kweli ngoja niondoke alafu uipasue utaona mwenyewe!! Yule mzee akaondoka mimi nikaona ni kweli!!
Nikamwambia dogo apande juu ya mti dogo akapanda mimi nikaandaa ngazi nikaweka kwenye mti nikaenda kuchukua shoka la baba mvunguni mwa kitanda!
Asee hamuwezi amini niliikung'uta ile redio shoka nikakimbilia ile ngazi nikapanda juu ya mti kusubiri simba na yanga watoke,Kumbe yule mzee alinidanganya!
Mi nikamuuli huyo yanga kwani ni mnyama gani!! Yule mzee akanijibu kama unataka kuwaona pasua hiyo redio watatoka huko utawaona!!mimi nikamwambia unasema kweli?? Yule mzee akasema ni kweli ngoja niondoke alafu uipasue utaona mwenyewe!! Yule mzee akaondoka mimi nikaona ni kweli!!
Nikamwambia dogo apande juu ya mti dogo akapanda mimi nikaandaa ngazi nikaweka kwenye mti nikaenda kuchukua shoka la baba mvunguni mwa kitanda!
Asee hamuwezi amini niliikung'uta ile redio shoka nikakimbilia ile ngazi nikapanda juu ya mti kusubiri simba na yanga watoke,Kumbe yule mzee alinidanganya!