Tukio gani ulifanya shuleni mpaka leo haujalisahau?

Tukio gani ulifanya shuleni mpaka leo haujalisahau?

Hii yangu nahisi ndo kiboko

Kipindi tupo form 4 mwanzo sana pale tulikuwa tukiletewa test hizi wasichana walikuwa wanatunyoosha sana sisi wavulana tukaanza kudharaulika darasani tukawa tunaitwa science B hii kitu ilituuma sana

Sisi wavulana Tukaongea na Monitor tukaandika barua tuwe tunabaki shule mpaka saa 2 usiku, ikumbukwe shule ilikuwa ni ya day...basi mkuu wa shule alikuwa anatuamini akatukubalia ila sharti lilikuwa ni wavulana only ndio tutakuwa tunabaki tukasema sio kesi

Kazi ikaanza rasmi piga misuriii weee tukaanza kuvuka mipaka..tukawa tunapika mpaka ubwabwa shule[emoji23][emoji23] tunachanga tunanunua mchele wale wanaokaa karibu wanaleta sufuria tunapika wali na maharage tukishakula tunafua nguo tunalala kabisa hapo hapo mpaka asubuhi...ikifika saa 10 tunavaa uniform tunaenda nje ya shule kutembea tembea ili tusishtukiwe

Sasa ijumaa kuamkia jumamos kabla mtihani wa mock wengi hatukwenda kulala shule walienda watu watatu tu...walivyofika wakasoma mpaka saa 7 usiku wakavizia mlinzi kaenda kwake ...wenyewe wakaenda kwenye madirisha ya chemistry laboratory wakaanza kukomba zile test tube zilizokaa meza ya kwanza kabisa pale dirishani...wakakusanya meza kama tatu hivi wanajaza kwenye mabegi yale makubwa nia yao wakauze kariakoo

Mlinzi akawaona na anawafaham vizuri...basi bhna akawaambia mbona mnataka kunifukuzisha kazi...kesho yake asubuhi tukaitwa wavulana wotee tuliokuwa tunalalaga pale shule mlinzi akatusema sanaa...mwisho akasema andikeni barua ya kukubali kama mmekutwa na vifaa vya shule ama laasivyo nitapeleka hii kesi kwa mwalimu mkuu jumatatu asubuhi...akaendelea kusema hii barua itakuwa kama makubaliano kati yangu na nyie..siku ijitokea mmeiba tena napeleka kwa mwalimu pamoja na hizi barua ila hii kesi ya leo nimewasamehe nyie andikeni barua

Hapa mlinzi alituchezea akili ukizingatia tulishapanick...tukaandika barua tukizani yatakuwa yameisha...jumatatu asubuh tupo kwenye mtihani wa Civics wa mock tunaona mlinzi amebeba yale mabegi na barua zipo mkononi anaelekea kwa headmistress...nilichanganyikiwa hata kuandika essay nilishindwa...(tulifeli hiyo mock kama kuku..wavulana wote chaliii)

Nikawaangalia wenzangu nikaona wapo kwenye sura za unyonge sana, mtihani ulivyoisha tukaitwa pale tukafungiwa darasa moja...anatoka mmoja mmoja kwenda kuhojiwa kwenye jopo la walimu..tokea saa 4 mpaka saa 8 tulivyomaliza kuhojiwa tukapelekwa kufanya mtihani wa pili wa geography

Shule nzima ilitujua aisee kesi ilikuwa nzito kila sehem tunaitwa wezi..yaani tulivyomaliza mtihani headmistress akiingia darasani anatuchoropoa wavulana anatutoa nje ni mwendo wa viboko tutaje wapi vifaa vilikuwa vinapelekwa..haipiti wiki bila kupigwa viboko...ila walikuja kukutwa na hatia ni wale waliokamatwa ile siku na wengine wawili...wakaambiwa warudi nyumbani kama wakitaka kurudi shule kuendelea kusoma waje na hela ya vifaa vilivyovunjika tokea mwaka uanze...walipigiwa mahesabu kila mtu aende na laki 4...

Wanangu nimewakumbuka sanaaa...[emoji119]
 
Nikiwa form 3 nakumbuka nilishawahi kuitwa "MWAKASEGE" Kisa niligongansha magari bwana alafu 1 kati yao c akapandisha anataja jina langu tu na kuomba aitiwe niende alipo....
 
nakumbuka tu tuliiba ndoo ya nyama kwenye siku ya graduation
 
Maisha ya shule yana mengi sana kuanzia chekechea hadi chuo mambo ni mengi.

Kudandia gari la Mh. Paul Kimiti akamwambia dereva asisimame hadi atufikishe pale shule, sisi tunashangaa gari linaongeza spidi tu kupanda kilima cha pale Chuo cha Ushirika kama unaenda uwanjani, huu ulikuwa msala wangu wa kwanza kwenye safari ya elimu.
 
Mm niliwahi kupigana na mwalimu wa kiume mnoko mstalini/assembly
kisa sijachomekea aliniwasha fimbo ya mgongoni ilinitia uchizi nilijikuta nimemrushia ngumi tatu za uso.....
mwalimu tii chini watu wwww.....!!!
Hapa haukupata kweli kile kibarua fulani kinakuwaga kizito kubeba kupeleka nyumbani.
 
Nilitoloka shule advance,nikarudi nyumbani kwenye harusi ya bro,alafu mshua hakunkuliza kitu,nikakaa wiki nikarudi Tena shule Tena mchana,nikakutana na second master nipo kwenye pikipiki km sio Mimi vile
 
Daah maisha yangu ya shule yalikuwa ni safari ngumu sana kuanzia shule ya msingi mpaka chuo kikuu, katika hatua zote niliwahi kufukuzwa kwa muda kama ifuatavyo:
Nikiwa shule ya msingi darasa la sita kuna jamaa alikuja kurudia mitihani,yaani alimaliza std 7 shule fulani akafeli ndo akaja shule niliyokuwa nasoma kuanza darasa la sita kwa majina ya mwanafunzi aliyeacha shule, basi bwana jamaa akawa rafiki yangu sana kwa kuwa nilikuwa najiweza darasani halafu nilikuwa kaka mkuu,siku moja kipindi cha mapumziko ya saa nne tukanunua miwa kwenda nayo darasani,tukaanza kuitafuna na huyo mshikaji wangu kwa kuwa mwalimu aliyetakiwa kuja kufundisha hakuingia darasani,darasa letu halikuwa na madirisha (yaani yalikuwa yana frem tu za madirisha).Tulipokuwa tunakula miwa kumbe mwalimu mkuu msaidizi anapita nyuma ya madarasa kukagua,hatuna hili wala lile mara paah huyo hapo,tukakimbia,akauliza darasani ni akina nani wanakula miwa na kutupa maganda nje,tukatajwa akatuita nje,aisee yule mwalimu alikuwa hodari wa kuchapa fimbo na kila mwanafunzi alijua hilo,kufika nje alipotuita akaanza na mshikaji wangu akamwambia ainame kwa ajili ya mboko,jamaa kapokea fimbo kama sita za kiume,mm baada ya kuona sijajaradia na fimbo zile za matakoni zingeiingia kama zote nikagoma kuinama chini badala yake nikamwambia anichape mkononi, mwalimu aligoma katu katu baada ya kunilazimisha sana tukataka kushikana mashati,jamaa hapohapo akanitimua shule kwa muda wa wiki moja, wanafunzi wenzangu wakajitokeza kupigwa kwa niaba yangu ili nisamehewe, mwalimu akakaza,nikabeba begi langu hadi nyumbani.Kimbembe ikawa naanzaje kuwaeleza wazee wangu kisanga hicho,baada ya kuniona siende shule Jumatatu iliyokuwa inafuata nikaulizwa vipi kulikoni,nikawachana ukweli baadaye siku hiyohiyo nikaambiwa jiandae twende shuleni mpaka kwa huyo mwalim,akawaambia mm nina tabia mbaya blabla nyingi,nikapigwa fimbo mbili nikaruhusiwa kuendelea na shule.
Visanga vya level zingine vitaendelea........
 
Back to Box 2,Songea Boys hiyo 2012 nakumbuka ilikuwa siku ya Alhamis siku pendwa ya kula nyama.Ratiba ilikuwa nyama tule mchana ila wakaipeleka usiku,kama kawaida ilivyofika jioni mi Kama table leader nikapanga foleni ya kuingia jikonu kubeba ugali na mboga.Foleni ilikuwa ndefu kidgo mpaka kuja kunifikia kigiza kilikuwa kishaingia,nikazama jikoni nikabeba ugali then nikarudia mboga (nyama).Wakati nipo jikoni kwa bahati mbaya umeme ukakatika ghafla halafu ndo kwanza nilikuwa nachagua dishi lenye nyama nzuri,yaani kitendo Cha kukatika umeme ghafla halafu nipo jikoni ikawa fulsa kwangu nikachukua dishi la pili lenye nyama nikamimina kwenye dishi langu maana ilikuwa unaruhusiwa kubeba dishi moja tu lenye vipande kumi ambalo Ni sawa na idadi ya watu kumi.
Sasa wakati natok ile harakaharaka usije umeme kuwska ghafla nikaaibika nikajikuta nakanyaga ndani ya madishi yaliyo na nyama kwa kuwa kulikuwa na Giza Ile nafika tu kwenye mlango wa kutoka nnje umeme huooo,kuangalia miguuni kwenye suruali nimeloana Hadi viatu yaani michuzi ya nyama Ila namshukuru Mungu sikukamatwa na kiongozi wa msosi,hili tukio nikikumbuka huwa nacheka Sana.
 
Mm niliwahi kupigana na mwalimu wa kiume mnoko mstalini/assembly
kisa sijachomekea aliniwasha fimbo ya mgongoni ilinitia uchizi nilijikuta nimemrushia ngumi tatu za uso.....
mwalimu tii chini watu wwww.....!!!
Noma sana aisee
 
Back to Box 2,Songea Boys hiyo 2012 nakumbuka ilikuwa siku ya Alhamis siku pendwa ya kula nyama.Ratiba ilikuwa nyama tule mchana ila wakaipeleka usiku,kama kawaida ilivyofika jioni mi Kama table leader nikapanga foleni ya kuingia jikonu kubeba ugali na mboga.Foleni ilikuwa ndefu kidgo mpaka kuja kunifikia kigiza kilikuwa kishaingia,nikazama jikoni nikabeba ugali then nikarudia mboga (nyama).Wakati nipo jikoni kwa bahati mbaya umeme ukakatika ghafla halafu ndo kwanza nilikuwa nachagua dishi lenye nyama nzuri,yaani kitendo Cha kukatika umeme ghafla halafu nipo jikoni ikawa fulsa kwangu nikachukua dishi la pili lenye nyama nikamimina kwenye dishi langu maana ilikuwa unaruhusiwa kubeba dishi moja tu lenye vipande kumi ambalo Ni sawa na idadi ya watu kumi.
Sasa wakati natok ile harakaharaka usije umeme kuwska ghafla nikaaibika nikajikuta nakanyaga ndani ya madishi yaliyo na nyama kwa kuwa kulikuwa na Giza Ile nafika tu kwenye mlango wa kutoka nnje umeme huooo,kuangalia miguuni kwenye suruali nimeloana Hadi viatu yaani michuzi ya nyama Ila namshukuru Mungu sikukamatwa na kiongozi wa msosi,hili tukio nikikumbuka huwa nacheka Sana.
Dah kweli ilikuwa noma, yaani hap lazima ujicheke sana.
 
Me nilikuwa sijaleta visa lakini acha nianze na hiki kimojawapo, wakati niko secondary kuna mwalimu mmoja alikuwa mtata sana shule nzima anaogopeka mwembamba sana hana hata nyama, yaani hautamani hata kupishana naye hakawii kukupa msala, sasa kwa kuwa nilihamia kutoka shule nyingine nikasema acha siku moja nimtingishe kaingia kwenye dormitory asubuhi asubuhi kaanza kuchapa washikaji ambao hawajadamka vitandani alivyofika kwangu nikajifanya kama niko usingizini, alivyonikurupua na fimbo aisee nilipiga ngumi za mvululizo na kichwa juu nikijifanya nina wenge la usingizi, masela wakaanza kupiga kelele oya zeebaba ni mwalimu huyo ndio nikajifanya kama wenge limekata nikaanza kuomba msamaha hapo hapo akaniambia niende baadaye ofisin akaenda kunisemea kwa walimu wengine japo walimu siku zote wako upande wao mmoja tu ndio alikuwa ananitetea kwamba yawezekana alikuwa na usingizi sasa kama ww umemchapa akiwa usingizini ndio hasara zake hizo.

Nilipewa adhabu lakini ndio ilikuwa mwisho wa yule teacher kuja Dom asubuhi asubuhi, tulikuwa hatusemeshani mpaka nimemaliza shule.

Visa vingine vitaendelea viko vingi tu, ipo ya kuchukua counter book za form one baada ya msela wa form 6 kujifanya mwalimu wa hesabu me nikatumwa nikusanye madaftari tukapita nayo yote yakiwa mapya yameandikwa ukurasa mmoja tu [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
,,😄😄😄😄😄😄
 
Mm niliwahi kupigana na mwalimu wa kiume mnoko mstalini/assembly
kisa sijachomekea aliniwasha fimbo ya mgongoni ilinitia uchizi nilijikuta nimemrushia ngumi tatu za uso.....
mwalimu tii chini watu wwww.....!!!
""et " watu wewewww"" 😄😄😄😄😄
 
""et " watu wewewww"" 😄😄😄😄😄
Hata mimivsitosahau 1986nilijikuta nampa mwalimu za Tyson alipokuwa ananitandika na viatu usoni nikiwa darasa la saba!😎😎nilisimamishwa shule mkuu wa shule akaona itakuwa shida wakinifukuza,maana mwalimu alikuwa ananipiga usoni na viatu.
 
Nilimkonyeza Mwalimu wa Kike nikiwa Darasa la Sita...shughuli hiyo niliifanya nikiwa kwenye foleni ya kusahihishiwa Lugha ya Malkia.

Nilipigwa sikuwahi pigwa vile...na baadae Mwalimu akawa rafiki yangu saaaana.Alipojua kuwa ni balehe ile😀😀
Mwalimu Mkuu kilimuuma sana kumbe alikuwa anafukuzia..sasa ndiye kila akikaa natafutiwa kosa nakula kichapo.

Madam alipoona hivyo akanisafisha mana Shule nzima nilijulikana na nilikuwa kadogo dogo..kuwa Muhuni mwenzenu muoneni.
 
Back
Top Bottom