Tukisema kuwa Yanga SC kuna Matatizo, Mgogoro na Kuhasimiana chini kwa chini baina ya Viongozi na akina GSM muwe mnatuelewa!

Mzukulu

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2020
Posts
1,401
Reaction score
2,641
Tulidanganywa hapa na Mhamasishaji wao na Msemaji wao Nugaz pamoja nae Bumbuli kuwa Kiungo Mshambuliaji wao wanayemtukuza kuliko hata Mtume Mohammed na Yesu Kristo ( Kiimani ) aitwae Bernard Morisson Raia wa nchini Ghana kuwa amesinya ( ameshasaini ) Mkataba mwingine wa kuendelea Kuitumikia na Kuichezea Klabu ya Yanga kwa miaka mingine Miwili.

Taarifa ambazo nimezipata kutoka huko huko kwa hawa Wanaohasimiana ndani ya Yanga SC zinasema kwamba kumbe Morisson bado hajasaini na Yanga SC kwa miaka hiyo Miwili tunayodanganywa na kwamba alisaini tu kwa miezi Sita ambayo imeisha Jumatatu ya Wiki hii. Sababu ya Morisson Kuwagomea Yanga SC anataka alipwe Kwanza Tsh 120 Milioni asaini Yanga SC wana Tsh 70 Milioni tu.

Kazi ipo mwaka huu!

Karibu sana Simba SC Bernard Morisson.
 
Mchezaji kushine Yanga sio lazima iwe hivyo tako1 ..Manara alilielezea vizuri hili usafini
 
Yanga viongozi wanatuangusha. Jamani solition ni kuibinafsisha tu Yanga kwa wenye mahela yao. Team haina hela ila ina wasemaji wawili. Yaani unabaki kushangaa tu.
 
Nafikiri sio yanga tu inadhoofika na soka la tanzania kwa ujumla.
Kama kweli anataka hoyo 120M utakuta mzawa yupo anadai 2M au 3M labda wala hawamuangalii mchezaj wa hivi atahitaji metal pyschology kuwa sehemu hii.

Nafikiri ifike mahali tuwe modern zaidi. Taasis ina idara nyingi hizo idara waajiriwe watu wenye taaluma hizo na weledi huo, sio kubebana kisa ni mzee wa muda mrefu klabuni ni mchezaji wa zamani. Soka letu halitafika huko (kushindana na wanaojua).
 
Yanga viongozi wanatuangusha. Jamani solition ni kuibinafsisha tu Yanga kwa wenye mahela yao. Team haina hela ila ina wasemaji wawili. Yaani unabaki kushangaa tu.

Tajiri gani atakubali kukaa na utopolo..!?
Hiyo hata ukimpa Dk shika bure hachukui!
Ni suala la muda tu, hao GSM wanawachora tu, wataikacha timu soon, wanataka waishushe daraja kwanza!
 
naona maumivu ya tarehe 8 march bado yanasumbua vichwa vya mazuzu fc. swali la kujiuliza ni kwamba zile bl 20 za mo zilishatolewa? vinginevyo ni upuuzi kuhoji ya jirani wakati kwako kupo hovyo tuuuuu
 
Si mnajitapa kuwa GSM wana Fedha za Kumwaga na ndiyo kila Kitu Kwenu, sasa inakuwaje hiyo Tsh Milioni 120 tu ya Kumpa Morisson hawana?
Una uhakika na unachokisema au kukalia tako 1 kumefanya fuse zikate kichwani kwako?
 
Yanga viongozi wanatuangusha. Jamani solition ni kuibinafsisha tu Yanga kwa wenye mahela yao. Team haina hela ila ina wasemaji wawili. Yaani unabaki kushangaa tu.
Wewe unamuamini huyo Shafiih Dauda, Timu Ina Afisa Habari ambaye ndio Hassan Bumbuli na Mhasishaji ambae ndio huyo Antonio Nugaz the same as hao Mikia wana Afisa Habari ambae n Yule Gift Macha na Mhamasishaji wao huyo Haji manara !!!
 
Tajiri gani atakubali kukaa na utopolo..!?
Hiyo hata ukimpa Dk shika bure hachukui!
Ni suala la muda tu, hao GSM wanawachora tu, wataikacha timu soon, wanataka waishushe daraja kwanza!
Tajiri gani atakubali kukaa na utopolo..!?
Hiyo hata ukimpa Dk shika bure hachukui!
Ni suala la muda tu, hao GSM wanawachora tu, wataikacha timu soon, wanataka waishushe daraja kwanza!
umekaa dume zima unasifia simba wana hela za yule muhindi MO,
 
Huyo morison aache bangi tz hakuna mcheza anaefikia thamani ya milioni 5
 
Ukitaka kujua ujuha wa Utopoliga FC waulize Ukowapi Mkataba wao ns Laliga na ulikuwa na Vipengele gani vya kuinufaisha Utopolo?
[emoji23][emoji28][emoji23][emoji28][emoji23][emoji28]utopolo ni watu wa ajab sana yaan wao ukiwauliza hata hawajui watanufaikaje na mkataba ila wanachojua n kwamba wao wana mkataba na la ligga
 
Mambo ya Yanga waachie wenyewe. Stori ya hivi hata mimi naweza kuitunga nikabadili tu characters
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…