Tukiwaendekeza Kibajaji na Msukuma hakika maendeleo tutayasikia kwa wenzetu

Tukiwaendekeza Kibajaji na Msukuma hakika maendeleo tutayasikia kwa wenzetu

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
9,524
Reaction score
13,682
Nimesikia vizuri mchango wa Prof. Muhongo bungeni na kutafakari kwa makini. Nilichosikia ni takwimu na maelezo yaliyoshiba ukweli na uhalisia wa hali ya sasa ya dunia. Amechambua namna gani rasilimali tulizonazo zinaweza kuinua uchumi wetu kama tutazitumia vizuri na kwa wakati. Muhongo ametoa takwimu na si maneno matupu ya kupamba mtu.

Aidha nimesikia michango ya Kibajaji na Msukuma. Michango yao imejaa kejeli na vitisho kwa Muhongo na wote wenye mawazo mapya na tofauti na Magufuli. Muda wote wamakuwa wakisifia na kumuenzi Magufuli. Hawana takwimu zo zote za ku-support hoja zao. Wamesahau kuwa sasa ni muda wa kijadili mpango wa maendeleo na bajeti.

Nimeona baadhi ya watu wakiwapongeza Kibajaji na Msukuma huku wakimrushia matusi Prof. Muhongo. Nadhani huu ni muelekeo potofu na kama hautarekebishwa tutajikuta Taifa halina dira na linaangamia. Tanzania kama Taifa lazima tutafute mwelekeo sahihi kwa pamoja kwa kutumia rasilimali watu na vitu tulivyonavyo.
 
Nadhani ipo haja ya kurekebisha kipengele cha education qualification za kugombea ubunge. Hawa wakina Kibajaji na Msukuma hawana mchango wowote wa maana katika kuishauri serikali badala yake wanapotosha na kubeza michango ya wataalamu juu ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. La kuhuzunisha zaidi hata spika anaonekana akiunga mkono upotoshaji kuwa Kibajaji ni bora na smart kuliko wataalamu!! Very sad
 
Bunge limekuwa kikao cha ccm spika Ndugai anawauliza mtampa Kibajaji Unec wabunge wanashangilia aibu Msukuma ndio katoa hoja hii bungeni
 
Nimesikia vizuri mchango wa Prof. Muhongo bungeni na kutafakari kwa makini. Nilichosikia ni takwimu na maelezo yaliyoshiba ukweli na uhalisia wa hali ya sasa ya dunia. Amechambua namna gani rasilimali tulizonazo zinaweza kuinua uchumi wetu kama tutazitumia vizuri na kwa wakati. Muhongo ametoa takwimu na si maneno matupu ya kupamba mtu.

Aidha nimesikia michango ya Kibajaji na Msukuma. Michango yao imejaa kejeli na vitisho kwa Muhongo na wote wenye mawazo mapya na tofauti na Magufuli. Muda wote wamakuwa wakisifia na kumuenzi Magufuli. Hawana takwimu zo zote za ku-support hoja zao. Wamesahau kuwa sasa ni muda wa kijadili mpango wa maendeleo na bajeti.

Nimeona baadhi ya watu wakiwapongeza Kibajaji na Msukuma huku wakimrushia matusi Prof. Muhongo. Nadhani huu ni muelekeo potofu na kama hautarekebishwa tutajikuta Taifa halina dira na linaangamia. Tanzania kama Taifa lazima tutafute mwelekeo sahihi kwa pamoja kwa kutumia rasilimali watu na vitu tulivyonavyo.
Ndio ma supper star wa Ndugai..
 
Sawa Prof Muhongo katoa takwimu.Ni takwimu za kupamba.Takwimu zisizo na ufumbuzi.Musukuma katoa ufumbuzi ,wa namna gani ,madini yalindwe.Katoa experience nzuri sana.Nafikiri huu usomi was kupamba tu ,ambao upon too theoretical hawezi tusaidia.Ni usomi was mabeberu.
 
Sawa Prof Muhongo katoa takwimu.Ni takwimu za kupamba.Takwimu zisizo na ufumbuzi.Musukuma katoa ufumbuzi ,wa namna gani ,madini yalindwe.Katoa experience nzuri sana.Nafikiri huu usomi was kupamba tu ,ambao upon too theoretical hawezi tusaidia.Ni usomi was mabeberu.
Takwimu za kupamba ni zipi hizo? Msukuma katoa ufumbuzi gani ambao haupo hivi sasa?

Kumbuka kinachojadiliwa ni mpango wa maendeleo na bajeti, pia namna ya kuongeza mapato ya serikali. Hivi ndivyo Muhongo kajadili.

Kwa maoni yako Msukuma katoa usomi wa kizalendo?
 
Nadhani ipo haja ya kurekebisha kipengele cha education qualification za kugombea ubunge. Hawa wakina Kibajaji na Msukuma hawana mchango wowote wa maana katika kuishauri serikali badala yake wanapotosha na kubeza michango ya wataalamu juu ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. La kuhuzunisha zaidi hata spika anaonekana akiunga mkono upotoshaji kuwa Kibajaji ni bora na smart kuliko wataalamu!! Very sad
Tunapima uhalisia wa maisha kati ya msomi na asiye soma,maisha haayahitaji mbwembwe na KiswaEngish hata kidogo,wala maisha ya Afrika hayana cha teknolojia wala sijui vitu gani vinavyo lazimishwa,uhalisia wa maisha tunaona wasomi ndiyo waliyo shindwa na wasio wasomi ndiyo walioweza

Huwezi kujaza ujinga watu wa sasa maana wasio soma wenyewe mtaani wanawaonea huruma waliosoma kwa kua kila walicho kianzisha kimeferi vibaya

Hatukatai kua na wasomi ktk maeneo husika,kazi za Doctors,Engineers na wengineo lakini siyo kama kwenye ubunge. Ubunge unapigiwa kura na wananchi hao hao wasio soma na ndiyo wanao ishi maisha halisi ya mTanzania,acha wakatetewe na hao hao darasa la7 maana wao ndiyo wanajua nje ndani jinsi maisha yalivyo

Mengine haya sijui ya wasomi kuchambua vitu viwe ni baadhi yake tu mana mtu unaweza mkuta ana shahada ya uzamivu wa kilimo lakini anazidiwa ujuzi na mkulima mwenyewe aliyeko shambani na hajasoma kwa sababu maisha hayo anayaishi...acheni mbwembwe mfundishwe maisha yenyewe
 
Sawa wasomi wenyewe unawataka hawa wa kufaulu kwa kutumia magaka na kutumia ma past paper, nenda huko vyuo vikuu ukajioneee
 
Nimesikia vizuri mchango wa Prof. Muhongo bungeni na kutafakari kwa makini. Nilichosikia ni takwimu na maelezo yaliyoshiba ukweli na uhalisia wa hali ya sasa ya dunia. Amechambua namna gani rasilimali tulizonazo zinaweza kuinua uchumi wetu kama tutazitumia vizuri na kwa wakati. Muhongo ametoa takwimu na si maneno matupu ya kupamba mtu.

Aidha nimesikia michango ya Kibajaji na Msukuma. Michango yao imejaa kejeli na vitisho kwa Muhongo na wote wenye mawazo mapya na tofauti na Magufuli. Muda wote wamakuwa wakisifia na kumuenzi Magufuli. Hawana takwimu zo zote za ku-support hoja zao. Wamesahau kuwa sasa ni muda wa kijadili mpango wa maendeleo na bajeti.

Nimeona baadhi ya watu wakiwapongeza Kibajaji na Msukuma huku wakimrushia matusi Prof. Muhongo. Nadhani huu ni muelekeo potofu na kama hautarekebishwa tutajikuta Taifa halina dira na linaangamia. Tanzania kama Taifa lazima tutafute mwelekeo sahihi kwa pamoja kwa kutumia rasilimali watu na vitu tulivyonavyo.
Sijawahi kuamini watu jamii ya Lusinde wanaweza kuleta lolote jema nchini.
 
msukuma ni aina ya watu ambao waliacha akili zifanye kazi baada ya elimu za darasani kuwashinda.

wasomi wetu wengi wakiwamo vijana wahitimu,ni aina ya watu ambao wameamua kuitegemea elimu kwenye kila jambo.

leo hii msukuma anaonekana hamnazo sababu kwa mchango wake kuna mapanya buku wanakwenda kukosa upigaji.
 
Back
Top Bottom