Tukubali au tukatae kwenye hii sayari ya Dunia katika nyanja ya Soka hakuna kama Pele wa Brazil

hakuna kama messi.

Sure kiongozi. Ukisikia "mti wenye matunda siku zote hupigwa mawe" ndio ujuwe Messi. Na ukitaka kujuwa mtu anatajwa sana ujuwe hana mpinzani kama ambavyo wanamnadi Messi.

  1. Messi
  2. Diego
  3. Pele
 
Kama alikuwa kilaza aliwezaje kutwaa kombe la dunia mara tatu? Hao kina messi walishatwaa mara ngapi ? Kwasababu wao wanacheza ulaya?

Nani katwaa makombe? Kwani yeye peke yake anacheza uwanjani? Kumbuka ile ni teamwork walikuwepo wakina garincha,didi n.k. kwahiyo na wakina Muller,Gortze na fabregas na wao tuwaite bora? De lima, lahm na gaucho na wao tuwaite bora??? Messi anawaumiza vichwa sana. Na bado ataendelea kuwaumiza kiongozi.mwenye mpira wake yule achananae, ni kipaji kutoka kwa muumba.

  1. MESSI
  2. DIEGO
  3. PELE
 
Hata kwa Maradona Messi hafiki. Messi achukue kombe la dunia na Argentina ndipo awasogelee hao nagwiji wa soka.
 
Kitu walichoangalia kwenye hili ni kwa sababu Argentina walifanya kampeni kubwa na kura zake karibia zote zilitoka kwao whilst kura za Pele zilikuwa world wide. Ukitoa kura zilizopigwa ndani ya mataifa yao(Brazil & Argentina) Pele alipata kura nyingi zaidi ya Maradona. Issue ya kucheza ligi za Ulaya nadhani haina mashiko kwa kuwa nyota wote wa Dunia walikuwa wakikutana kwenye World cup na utofauti wa viwango ulikuwa ukijidhihirisha wazi. Kila mtu anahaki ya kuwa na mitazamo yake lakini pale linapokuja suala la statistics nadhani uwanja wa mabishano haufai kuendeshwa kiushabiki. Kuna watu huwa wanakimbilia kusema mchezaji nyota fulani anavuma kwa sababu anacheza kwenye ligi isiyo na ushindani,sasa kwakuwa nyota karibu wote wa Dunia wanacheza ligi za Ulaya hivyo kipimo kizuri ni ligi ya mabingwa Ulaya.
 
They are brainwashed unaweza kuta mtu anamsifia gaucho alfu hana evidence zaidi ya kusema yule noma alikuwa ana entertain kumbe pumba tupu

Wapo wengi sana wa hivyo😀😀😀. Fuatilia comments zao humu humu jamiiforums utajionea, au nenda kwa shaffih dauda yani utacheka mkuu.
 
Naomba kujua kama tangu ujue soka hasa la majuu. Ulishawahi kusikia mchezaji yeyote nafananishwa na Pele?

Utasikia. New Maradona
New Christiano Ronaldo
New Gaucho nk

Huwezi kusikia new pele...
Neymar alifananishwa na Pele
 
Messi mbona anazidiwa hata na kijana ronaldinho gaucho. Pelle wa kwanza ila gaucho huwa akipita mtaani anaitwa ball dancer
 
Wechezaji zamani walikuwa wanajua na hakukuwa na technologia kama leo. Kuna mchezaji aligundua kuwa gori fupi halina vipimo baada ya kugonga mwamba Mara kadhaaa akaona akilalamika itapendeza zaidi na kweli magori yakaonekana vipimo vimepungua
 
Tatizo hakuna wa kumfananisha na pele
Mambo ya maajabu yakitokea mfano mtu kumwokoa mtoto mchanga anaezama ataambiwa amecheza kama pele
Sasa hivi hakuna wa kufananishwa na pele
Katika soka ni mtu wa pekee sana
 
Wingi wa makombe
Pele 36
Messi 25
Gaucho 18
Màradona 12
Pele alikuwa bora kwa kila kitu
Akiwa na miaka 17 tu anaibebesha brazil kombe la dunia 1958 tena akifunga bao 2 katika ushindi wa 4-0 dhidi ya sweeden
 
Mchezaji pekee aliyesababisha refa kupewa redi Kadi na kamati ya maamuzi baada ya kumtoa Pele Kwa Kadi, wakaamua waangalie wakasema haiwezekani, wakampa refa kadi
 
Pele ni mchumba tu kwa messi.tatizo Wabongo tunapenda sana kuongea. Ukweli unajulikana Messi ndiye baba wa soka ulimwenguni mtake msitake ukweli ndio huo.

Usiku mwema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…