Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Ilikuwa ukivivaa halafu jua likakuwakia mchana inakuwa ni kasheshe.

Umewahi kusikia Masai Barefoot Technolgy? Angalia MBT :: HISTORY! Mhandisi wa kiswiss anasema alichunguza wamasai wanavyotembea akagundua kuwa design ya kutembea kwao inaondoa maumivu ya mgongo! Ingawa yeye anadai aliona wanavyotembea peku peku lakini nina wasiwasi alikwiba design ya kata mbuga. Sasa hivi, hivi viatu vya MBT vinauzwa kwa bei mbaya sana! Anasema aliangalia wamasai wanavyotembea akagungua kuwa viatu tunavyovaa vyote feki. Jamaa anapeta!

Hya ngoja sisi wa Pango Disco la wakina Sunburst ( maarufu kwa wimbo wao wa ukuti ukuti)tukae pembeni!
 
Nadhani wengi mtakumbuka .....mambo ya raizoni, bugaluu na afro.....bila kusahau mambo ya breakdance ....

Afro


Raizoni


Bugaluu


Breakdance - from YouTube

[media]http://www.youtube.com/watch?v=UYFDYX4i2EY[/media]
 
hayo makatambuga uchunguzi umebaini,yanatoa mionzi,ambayo in the long run,inaweza kusababisha upofu kwa mtumiaji
 
harsui ya nani hiyo mkuu?

ahhhhh mbona unataka tumwage mchele kwenye kuku wengi?

Inaelekea wewe si mwendaji kwenye harusi...hivi ushasahau kuwa december kuna shughuli ya yule jamaa anayeoa kule magharibi?

Au ndo utu uzima ushakuingia?
 
BRAZAMENI alipokuwa anakamua about a year ago......

Mtanisamehe lakini najua wengi wenu humu JF mlikuwa Joni visomi na najua pia kuwa ambao hawakusoma mlikuwa mabaharia,na of course wengi wenu mnatokea mikoani na Dar mekuja miaka 1- iliyopita... lakini vile vile nilitaka kuwafahamisha kuwa early 80's kulikuwepo hili kundi la KU na sie wengine tulikuwepo siku ile ya jumamosi walipokuja CINE CLUB kurekodi video yao ya MSELA






Masela hawa wako wapi sasa...!!

Kwa wale tuliokuwa tukifwatilia kwa karibu muziki huu wa kizazi kipya wakati unaanza kuchipua,tutaungana mkono kuwa vijana walitokea mbali kiana na bila shaka katika harakati zao za kuukuza muziki huu walikutana vizingiti vingi na vya kila aina,mfano naweza kumtolea rafiki yangu Robert ambaye ilifikia wakati wazazi wake wakawa wanaingia na Radio zao chumbani ilimradi tu kumnyima bwana mdogo haki zake za msingi tena za kikatiba za kusikiliza muziki aliokuwa akiuf*gilia eti kwa maelezo kuwa muziki huo ni wa kihuni na usiokuwa na maadili hata kidogo.

Hapa kushoto ni KU Crew,katikati ni Terry kutoka HBC na kulia ni Mr II.Enzi hizooooo

Lakini kadri miaka ilivyokuwa ikizidi kusonga na wasanii kuendelea kuwa wabishi na kuachia mipini mipya tena kwa hela ya ngama waliyokuwa wakiidunduliza kwa taaabu kubwa, huku wakiwa hawapati maslahi yoyote ya maana zaidi ya ujiko tu...hatimaye wasanii walianza kuongezeka taratibuu jambo lililokuwa likiwachanganya zaidi wazazi wengi waliohisi vijana wamechanganyikwa.

Left ni Saigon na katikati ni Dola Soul kutoka the Diplomatz,kulia kwao ni Mr Paul...enzi hizoooooo

Yote hayo yalichangiwa na wengi tu kuanzia waandishi,vituo vya radio, mapromoter na kadhalika.....Jambo kubwa la kujiuliza wengi wa waanzilishi wa vita hiyo kubwa ya kuupigania muziki huu hawajulikani walipo.

Na leo hii itakuwa si vibaya hata kidogo tukiweza kuwakumbuka kwa pamoja wachache tu ambao mchango wao hata kama ni mdogo lakini umeweza kuifikisha Bongo Flava hapa tulipo na kuweza kuufanya muziki huu uwe kioo cha muziki wa vijana kwa Afrika Mashariki na Kati.

Hapa kushoto ni Caz T kutoka (BANTU POUND GANGSTER),katikati ni Bonny Harmony kutoka(AFRO REIGN),na kulia ni Rashid Ziada (KR) kutoka GWM ambaye pia ni mwasisi wa kundi la Wanaumeela TMK.

Kati ya tutakao wakumbuka wengine wanaendelea na muziki na wengine hatuko nao duniani kwa sasa, wengine hatujui walipo na wanafanya nini! tunajua wengi wangependa kujua wako wapi maselaaaa?


JE UNAWAKUMBUKA MASELA HAWA ?

Saleh Jabir
Adili a.k.a. Nigga One (R.I.P)
Afro Reign
K. U Crew
Bantu Pound
4 Kreuz Flava
Hard Blasters
Weusi Wagumu Asilia3
Sos B (ameongezwa na tony-serena znz)
Rhymson (KU Crew)
E-Attack
Fresh X
Kool Mooccc
Columba Mwingira - mawingu Band
OJ - Mawingu Band
Sindila
De-Plow-Matz
II Proud
G.W.M.

WATANGAZAJI WA RADIO (RADIO 1)
Master t
Mike mhagama

MAPROMOTER
Kim Magomelo (Kim & the Boyz)

STUDIOS
Container la Master J
Don bosco Studios
Sound Crafters

Je unazikumbuka video hizi za kwanza kwanzaaaaaa ?
1.Oyaa Msela oyaaaaa (Mawingu Band)
2.Usiige mambo ya mjini (Hard Blasters)
3.Kukurukakara zako (Sos B)


KUMBI
Kilimanjaro pool side
FM Club (zamani Lang'ata Social Hall)
Silent Inn club (umeongezwa na Frank Suura)

 

Attachments

  • kwanza.jpg
    44.9 KB · Views: 260
wale wanawake waliokuwa wakifanya kazi hapa walikuwa wajinga sana walikuwa na mashine ya Credit Card mbovu watu wamewalia sana pesa hawa jamaa...ulikuwa unaweza kulipa holiday ya ZENJI na kadi yoyote ile bila wao kustukia kitu
 

Attachments

  • 332510550_f070efb9fe_b.jpg
    72.9 KB · Views: 247

Sawa sawa mkuu, lakini alivipiga hivyo vibao baada ya kurudi toka Nairobi, kwa sababu hata kwenda alitoroka kwa muajiri wake JKT, alirudi mwanzoni mwa kati kati ya 90s, baada ya JKT kufa, maana bila hivyo angeenda moja kwa moja munga'nda, hivi vibao ni kweli ameshirki kuvipiga tena ule wa Cleopatra na mimi ninao mkuu, lakini ilikuwa ni baada ya kurudi, otherwise uko sawa na mengine yote na shukrani!
 
GAME THEORY,hiyo video ya MSELA ilirecordiwa early 80's sasa sisi watoto wa mjini tulikuwa wapi?au ni early 90's wakati sisi wengine tumeshaanza
 

loh lahaula! naona waheshimiwa wamejichangaya hapa. nadhani ingebidi
waende copyright society of tanzania (cosota) wakapate majibu kuhusu hakimiliki.

kuhusu mtunzi, nakumbuka kuna kipindi mzee mmoja kutoka moshi alijitokeza gazetini (sikumbuki ni gazeti gani ila kati ya uhuru au mzalendo) na kudai yeye ndiye mtunzi wa wimbo huo na kwamba alikuwa anafahamiana na fadhili william. alidai kunasiku alimuimbia fadhili huo wimbo na fadhili akaunasa na mengine yaliyofuatia ni historia.
 
Last edited:
7. Mgogoro - WoWowo
8. Salama au macho? Tutakula au Fitina? - Maamboo?
9. Basi Haya/Basi Ok - Hamna noma!
1o. Tutayafiksi - Nitayashughulikia!

Tuendelee...!!

hapo kwenye "salama au macho? tutafika au fitina" kulikuwa na kiendelezo cha
"ndege itatua au kiwanja kimejaa topee" lol
 
nakumbuka kwenye miaka ya 75-76 kuna meli nadhani ya kijapani ilitia nanga bandarini halafu kwa nyuma ilikuwa imeandikwa "KISHTOBE". wasela wakatoka na msemo "kishtobe nibebee" na wadada wenye uani (wowowo) kubwa walikuwa wakikatiza sehemu sehemu utasikia watu wakisema "kishtobeee mwanangu!)
 

unanikumbusha kuna wakati baadhi ya jamaa walikuwa wakialikwa
kila mnuso kwa sababu walitegemewa wangekuja na santuri
kali. hata ma-gate crushers walikuwa wanashika santuri mkononi
hivyo wanakaribishwa bila tatizo.

mkuu kijiwe cha harlem ndio kile kilikuwa kwenye njia ya kupandisha
muhimbili hospital (kati ya muhimbili primary na makaburi ya
tambaza)ambapo kuna vijana "marastafari" walikuwa na
kitu kama kigenge hivi?
 

unanikumbusha jamaa wa sunburst walikuwa na wimbo unasema
"sikitiko mpenzi, mola ataumbua
mapenzi jama yamenitoka hivi,
kukosa mwana kimpenzi cha roho,
sikutambua hayo yotee, dua njema mwenzangu n
nakuombea

kosa langu mwenyewe, sikulima shamba
ningelima shamba, mazao bora ningepata
ningelima shamba chakula bora ningepata
ooh kosa langu kubwa...

pia walikuwa na wimbo wanasema
"kipapa kipapapa kipapa kipa
kinyunyu kinyunyunyu kinyunyu kinyu"

aah acha tu.
 

...ebwanaaaa eeehh! chini ya mkwaju mpaka alipokuja yule mwalimu 'mnoko' wa shule ya muhimbili, Mwl Ndossi ndipo ulipokatwa, kisa, Pius Makene alimpa kibano mpaka akaishia kuitafuta wrist watch yake ipo mavumbini!,.... duuuh, enzi hizo kuna yule mgiriki Brian, kijiwe cha kujifundishia magitaa ya kina kina Andy Swebe, kina Galinoma nk... safi sana!


...hapana mkuu, makaburi ya Tambaza ni huku nyuma, barabara ya Maliki, kijiwe cha Harlem ni karibia na uwanja wa barafu, kati ya Muhimbili Primary na Tambaza Secondary, unapandishia juu unatokea mitaa ya Silver Oak, nk...

Hicho kijiwe unachosema wewe labda ni kile mbele ya Scout, ...yeah, kina "Jah Toto" na Vw Combi lao, ha ha ha...😀

Historia
Enzi hizo kuna mambo ya balozi wa nyumba kumi kila mtaa, balozi shurti awajue wageni wote wanaoingia mtaani/ hata kama ni wageni was iku mbili lazima ajulishwe! na bendera ilikuwa inapepea nyumbani kwake!
 

Duh! mkuu leo umenikumbusha washikaji lontime hawa, vipi mkuu nipenyezeee kwa PM akam una wamasiliano nao mpaka leo, maana Pius Makene "Mario Kempes" nilikula naye shule kule Kwiro Secondary, na Anisile Swebe "Bichwa" nilikula naye pimary, duh long time! Galinoma nakumbuka enzi zake pale NBC Posta ya zamani! bitozi sana!

Mkuu Ahsante Sana!
 
Wakubwa mimininaulizia baadhiya timu zetu za mitaani ambazo zilikuwa niwaka sana miaka hiyo napia zimetoa baadhiya wachezaji wazuri na taifa kwa ujumlamoja kwa moja niaelekea upande wa wilaya ya kinondoni wakati huo pale manzese kulikwa na timu kama vile SIFA utd Ambayo imetoa wachezaji wengi kama vile madaraka suleman,idd suleman kibode,hawa walikuwa simba kama sikosei pia abdallah waswa,hamis mbuzi ,hiitimu ilikuwa makaaziyake nipale tiptop [kwa alibay]au kwa yusuf mkimbizi
Pia kulikuwa timu za wababe kama vile faru hawa faru kwa hakika ilikuwa timu moja ya wahuni kiasi refarii lazima kwanza onyeshe kisu kwenye kiuno ndio awacheshe hawa jamaa sijui hii timu kama bado ipo
ninakumbuka sana enzi za chakacha la wakina faruku,
pia kuna mzee mmoja alikuwa maarufu sana ukanda wa kinondoni akiitwa mzee mwinyihija.
mwenye kujua chochote niwakuu mwageni katrika huu uwanja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…