Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Ninaamini kuwa vyama vya upinzani vilikuwepo, hata wakati tunapata uhuru si TANU ilivishinda vyama vingine vya upinzani, au?

Wakuu wa Upinzani vipi historia huko mbona mnatuagusha jamani?

Miaka ya vyama vya upinzani ilikuwa kabla na baada ya uhuru kwa Tanganyika na Zanzibar... Hii ni kati ya miaka ya 1950-1960

Tanzania Bara
  • UTP -United Tanganyika Party
  • ANC-African National Congress
  • AMNUT- All Muslim National Unity of Tanganyika
  • TANU-Tanganyika African National Union

Huko Zenj Vyama vikumbwa vilikuwa
  • ZNP-Zanzibar Nationalist Party
  • ZPPP-Zanzibar and Pemba Peoples Party
  • ASP- Afro - Shirazi Party
 
Last edited:
Hivi nani anayejua mtu aliyeimba kwa mara ya kwanza kabisa na ambaye ni mtunzi wa wimbo wa MALAIKA? Maana watu wanakopi tu miaka nenda, miaka rudi sijui kama familia yake inapata chochote!
 
kumekuwa na claims na counterclaims kuhusu who really gave the world this song,but all in all,the buck stops with FADHILI WILLIAMS,who legally put the song under is name. could this song be the mother of all songs to ever come out of EAST AFRICA?
 
kumekuwa na claims na counterclaims kuhusu who really gave the world this song,but all in all,the buck stops with FADHILI WILLIAMS,who legally put the song under is name. could this song be the mother of all songs to ever come out of EAST AFRICA?

Huyo Fadhili Williams ni Mtanzania?
 
as far as i understand fadhili williams ni mkenya.inasemekana huu mwimbo ulipigwa tanzania mwanzo,nakumbuka hadi picha ya huyo so called malaika,akiwa mtu mzima nimashaiona katika magazeti,huyo malaika ni mwenyeji wa kilimanjaro,lakini kama hujuavyo wakenya ni mijitu sharp,kabla sisi hatujajua copyright ni nini,fadhili akatumia vacuum iliyoibuka,ya wimbo kupigwa na kila mtu,yeye aka u copyright.the rest is history
 
kUNA ZILE SEMI ZA ZAMANI AMBAZO NI ZA KISANII ZILICHANGAMSHA SANA LUGHA YETU:

1. DU KINAA - POA TU
2.KATA NGWALA- PIGA MTAMA
3.PEKOSI- SURUALI PANA CHINI
4.RAIZONI -VIATU VIREFU
5. NYAPU - Msichana
6.SHADA - Bangi
 
kumekuwa na claims na counterclaims kuhusu who really gave the world this song,but all in all,the buck stops with FADHILI WILLIAMS,who legally put the song under is name. could this song be the mother of all songs to ever come out of EAST AFRICA?

nakumbuka wakati wa bunge la bajeti. naibu waziri Bendera alilijibu swali la mtunzi wa wimbo huu, ngoja nikipata muda wa kupekenyua makabrasha nitawaletea lakini kama unaweza kupekuwa kwenye tovuti ya Bunge, nadhani ipo kwenye hansard, tatizo zikumbuki ilikuwa tarehe gani.
Lakini kimsingi wimbo ulitungwa na mtanzania mzaliwa wa mkoa wa kilimanjaro (kama sikosei). Huyu mkenya fadhili williams alifanikiwa kuurekodi na kujiwekea hati miliki ndio maana unajulikana kama wake
 
Katambuga

Kuna wakati hivi vilikuwa viatu vya kawaida kabisa kwa Watanzania. siku hiz watu huvaa kwa madoido tu

attachment.php
 

Attachments

  • Katambuga.JPG
    Katambuga.JPG
    30.6 KB · Views: 470
1. Unajua Tanzania, pamoja na siasa zetu enzi zile, lakini bado tulikuwa na nafasi ya ku-socialize hasa kwenye ma-Disco na muziki wa Dance, kwenye hili ni lazima tuwe fair kuwa Mwalimu hakuwa na tatizo kabisaa.

2. Ni kweli kwamba ex- DJ Gerard, au kama alivyokuwa akifahamika kwa jina la "Jerry Kotto", alitokea kuwa mmoja wa the best DJs mjini Dar, na ni kweli kwamba alikuwa na matatizo ya kusoma, lakini Jerry alikuwa na tabia moja nayo ni akipata Album au Tape hukaa chini na kuisikiliza mwanzo mpaka mwisho, akisikia ngoma anayoamini kuwa ni safi basi husimamisha na kuweka alama kwanza kwenye Tape/Album na pia kwenye namba ya ile song, sasa akingia kupiga Disco huzikumbuka nyimbo zote zilipo na ni zipi, tena bila ya tatizo.

3. Kwa kadri ninavyokumbuka tumewahi kuwa na Ma-DJ waliokuwa waburudishaji na wakali, kwa sababu pamoja na kwamba wao yaani ma-DJ walikuwa sio wapigaji hasa wa zile nyimbo, lakini siku zote mchele ni ule ule, ila mapishi ndio hubadili matokeo, hata ma-DJ nao ilikuwa ni hivyo hivyo, kwa kweli ningeomba kuwakumbuka tena kwa nafasi zao, wale wote yaani ma-DJ waliowahi kutuburudisha mjini Dar kama ninavyowakumbuka na pia msaada unakubalika iwapo kuna niliowasahau au kuwaweka kwenye nafasi wasizofaa:-

1. DJ Justin Kusaga - Clouds (Morogoro).
2. DJ Kali Kali (Kalikawe) - YMCA/Mbowe.
3. DJ Ebbo Night Woo Jack! (Bob Rich Mazula) - Msasani Beach.
4. DJ Chris Phaby "The Lover" - Mbowe/Margott.
5. DJ Choggy Sly (Choggo Salum) & DJ JPP (John Peter Pantalakis) - Msasani Beach/Rungwe Beach
6. DJ Roma Pop Juice (RIP) - Mwanayamala.
7. DJ Jerry Kotto (Gerard) - Mbowe RSVP Club.
8. DJ Nigger Jay - YMCA.
9. DJ DC Washington (RIP) - Rungwe Beach.
10. DJ Lucas
11. DJ Tito Jackosn (Tito Kalumanga) - Rungwe Beach.
12. DJ John Bure
13. DJ Joe Kusaga (Joseph Kusaga) & DJ Stewart (Sterwart Chiduo) - Clouds.
14. DJ Kim (Kim) - Rungwe Beach.
15. DJ Kessy (Kessi) - Blue Sky Disco.
16. DJ Eddy - Magomeni.
17. DJ Super Deo (Deo) - YMCA/Margott.

4. Kwa upande wa muziki wa Dance, pia tilkuwa na bendi za wazawa na wageni, hasa kutoka Zaire na wao pia kulingana na nafasi zao kimuziki as I remmember, na time pia lakini pia msaaada unakubalika:-

1. End of The 60s:-

1. Orch. Morogoro Jazz - Mbaraka Mwinshehe (RIP).
2. Orch. Cuban Marimba - Salum Abdallah (RIP).
3. Orch. Nova Success - Baba Gaston (Nairobi).
4. Orch. Nuta Jazz - Muhidini Gurumo (Ilala - Msondo Ngoma).
5. Orch. Tabora Jazz - Wema Abdalalh/Shem Karenga (Tabora).
6. Orch. Western Jazz - Wema Abdallah (Sikukuu street Kariakoo, Dar).
7. Orch. Dar Jazz - Dar.
8. Orch. Unyanyembe Jazz - (Nyanyembe Tabora.)
9. Orch. Kilwa Jazz - Ahmed Kipande/Juma Mrisho (Kilwa).
10. Orch. Police Jazz - Dar.
11. Orch. Atomic Jazz - John Kijiko (Tanga).
12. Orch. Kilombero Jazz - (Kiwanda cha Sukari Kilombero).
13. Orch. Butiama Jazz - Ifakara.
14. Orch. Boma Liwanza - (Zaire/DSM).
15. Orch. Banangenge - Fataki Masumbuko Ya Dunia (Zaire/DSM).

2. In the 70s. to 80s:-

1. Orch. Super Volcano - Mbaraka Mwinshehe (Morogoro).
2. Orch. TK Lumpopo - Juma kilaza (Morogoro).
3. Orch. Afro 70 - Patric Balisidya (DSM).
4. Orch. Urafiki Jazz - Juma Mrisho (DSM).
5. Orch. Nuta Jazz - Muhidini Gurumo (DSM).
6. Orch. Marquiz du Zaire - Chinyama chiyanzi (Zaire/DSM).
7. Orch. Vijana Jazz - Andoro/Maneti (DSM).
8. Orch. Safari Trippers - Marijani Rajabu (DSM).
9. Orch. Mwenge Jazz - George Mpupua (JWTZ- DSM).
10. Orch. JKT Kimbunga - Mzee Zakaria (DSM).
11. Orch. Kimuli muli - Zahiri Zoro (JKT Mafinga/DSM)
12. Orch. Simba Wa Nyika - Wilson & George Peter (Arusha/Nairobi).
14. Orch. Dar International - Abel Baltazari/Marijani Rajabu (DSM).
15. Orch. Police Jazz - Moshi William (DSM).
16. Orch. BarKeys - George Mhando (DSM).
17. Orch. Sola TV - (Temeke - DSM).
18. Orch. Makassy - Mzee Makassy (Zaire/DSM)
19. Orch. Nkashama Nkoi - Ndala Kasheba (RIP) (Zaire/DSM).
20. Orch. Matimila - Remmy Ongalla (Songea/DSM).
21. Orch. Sunburst - Kassim Magati (DSM).
22. Orch. Tanzanite - Nembo (DSM).
23. Orch. Toma Toma - Thomas (DSM).
24. Orch. Mpakani Kyauri Voice - Mzee Khatibu Itei Tei (DSM).
25. Orch. Mlimani Park - Abel Baltazari/Gurumo (DSM).
26. Orch. Doble O - King Kiki (Zaire/DSM).
27. Orch Safari Sound - Mbombo wa Mbombo-Ka/King Kiki/Ndala Kasheba (Zaire/DSM).
28. Orch. Mk Group - Kossongo Mpinda/shem Karenga (DSM).

Huenda kuna niliowaacha, lakini ninaamini kuwa ma-DJ tulionao sasa na bendi za muziki, ni kuanzia in 90s hadi leo ni almost wale wale na bendi ni zile zile ingawa cha kusikitisha sana ni kwamba kama ni bendi zilizopo leo labda hazizidi nne, zingine zote zilikufa kifo cha mende, lakini ni vyema kukumbuka kuwa katika enzi zile za 70s, 80, na mwanzoni mwa 90s pamoja na msiha kuwa magumu kidogo siku zote tulikuwa na burudani kabambe ambazo some of us zilitusaidia sana kuendelea kuyakabili maisha, knowing kwamba kuna weeek end kwenda kula mangoma na kuku za kibongo bongo.

Heshima Mbele Wakuu.


Namuona hapa Choggy Sly (RIP) akiwa kazini enzi hizo huko Silversands:

attachment.php


Nadhani alikuwa akivinjari zaidi mitaa ya Rungwe Oceanic, siyo Rungwe Beach, au vipi mkuu FMES. Hivi Rungwe Oceanic iliishia wapi?
 

Attachments

  • ChoggySly.jpg
    ChoggySly.jpg
    31.2 KB · Views: 412
Inasikitisha kuona idadi ya vijana mashuhuri wa Kitanzania waliofariki hata kabla ya kufikia umri wa 40 au 50. What happened? Is it only AIDS that took such a toll on our youths or what? The late Marijani was a year behind me at Aga Khan. Ray Abdul was my classmate. Patrick Balisidya was a friend. And all these DJ's who came years later.
 
tancat almasi ya kasoloo na kyanga songa...ilikuwa ikinisuuza sana ...kweli hiizi raha jamani....kuna ule wimbo..wao..

...".safari sio kifo"

safari sio kifoooo.,mama watoto...
subiri nitarudiii mama watoto..
nikirudi mama nitakuletea zawadi..
..zawadi mama ,mama watotoo..
nikirudi mama ..pokea mikono miwili...

YELELE ooh mama ..yelele...

alfu inaendelea rap..yao..

eee kebba kebba kebaa..kebaaaa.

fimbo..fimbo..fimbo...logoda..logoda ...

mangalaaaa!!!!

mangala dance!!!![MSISAHAU KUNA SOLO KALI SANA LINAPIGWA KWENYE WIMBO HUU...

baada ya pacha kutoka walikuja kuungana na kina chunusi na kuunda bendi ya NGORONGORO HEROES BAND..ikaja kufa...

wazee MNAONAJE SERA YA VIWANDA YA MWALIMU.....KWELI TUTARUDI KULE KWELI...???MAANA ILIKUWA SERA YA KUHAKIKISHA KILA MKOA UNAKUWA NA VIWANDA ...ILI WATU WASIKIMBILIE MJINI..AU DAR ES SALAAM WOTE....DISTRIBUTION OF NATIONAL RESOURCES....

IDADI YA VIWANDA ALIVYOJENGA NYERERE NDANI YA MIAKA 20...KWANINI SIKU HIZI VIONGOZI WETU WANAOTAWALA MIAKA 10 WANASHINDWA KUJENGA HATA NUSU YAKE????
 
Mkuu kichuguu,

2440d1221580699-tukumbuke-zamani-historia-ya-taifa-letu-katika-picha-katambuga.jpg


Hii kiatu imenikumbusha mbali sana. Hahaha, kuna ambazo zinaonekana kwa mbali nakumbuka mamangu alikuwa anapenda kutinga kwa sana!
 
field marshall,dj kalikali ni marehemu,baadaye akaibuka mdogo wake katika fani ya reggae kwa jina kalikawe naye vilevile ni marehemu.
jamani humu ukumbini inabidi tuseparate the man from the boys.NAULIZA je kuna member yoyote humu kacheza disco sansui lililokuwa seaview.

Kula tano mkuu....... Ukiondoka mokasini na kishati cha kubana.....dah!! Longi mkulu...
 
Huyu Ike akatukatia umeme juzi ikabidi kuchemsha maji ya moto na kuweka kwenye ndoo kwenda kuoga. Nilipochukua lile bakuli na kuanzia kujimwagia nikajikuta nacheka na kusema "there nothing more Tanzanian than this".... Hata umeme uliporudi I just had to do it one more time, najiuliza hivi pamoja wale tunaokaa ughaibuni hasa katika nchi hizi za kimagharibi bado tunaweza kuswitch ule uswahili wetu on demand?

a. Kutengeneza kata na kuweka ndoo kichwani
b. Kubeba kuni
c. Kupulizia moto ili upike
d. Kuchinja kuku bila kusahau Bismillah na kuelekeza Kibla au kutafuta mtoto wa Kiislamu aje akuhalalishie?
e. Kutengeneza kamba ndefu halafu watoto wote wa kiume (sometimes na wakike) mnaingia na mmoja wenu kujifanya yeye dereva wa Uda!
f. Kuhakikisha unatoa kitanda cha "telemka nikukaze" jua likitoka ili kipigwe pigwe najua na kuua kunguni?
g. Kutegea tegea wachuuzi wa samaki wapite, kule Tanga kulikuwa na jamaa anapitaga na dagaa kwenye tenga la basikweli; leo utamuona Kwaminchi ukikatakata kona utakutana naya Chumbageni! anapiga kelele "aeeeeh daggaaaaaa"! No 1 800 number!
h. Kwa wale wa kijijini jinsi gani tunaswitch kutoka kwenye gari na kusubiri usafiri wa baskeli au wa mguu kwenda kuwaona wazazi. Na hakuna kitu cha kukumbushia kama wale tuliosafiri na mabasi yale ya "Kauru"! na hata malori ya Tumbaku!
i. Lakini kabla ya kuletewa haya makompyuta na makideo bwelele mambo yote yalikuwa "kijiweni" literally. Hakuna mahali watu walikuwa wanapigana fix kama kijiweni! Na always kuna yule jamaa mmoja ambaye asipotokea jioni hiyo kijiwe hakinogi!
j. Halafu yupo yule jamaa ambaye mtaa mzima mnamjua kuwa ni "bishoo"! Na huwezi kumsahau yule binti ambaye kila msela mtaani anamfukuzia halafu ndo mgumu kichizi!
k. Kule Mwanza kama kuna vitu vilikuwa vinasisimua ni kwenda ziwani kuoga; upande mmoja kina dada wanaoga kivyao na kwingine vijana tena mchana kweupe msiniulize kwanini? Nenda ushuhudie hasa mitaa ya watani zetu kule UK a.k.a Ukerewe na UZ a.ka Uzinza!
 
Mwakjj,
Somethings will never change. Ninaporudi nyumbani siku za kwanza huwa naona shida sana kuoga maji ya baridi. Lakini after a few days naenjoy sana tu. Pia umetambua kuwa nyama iliyopikwa kwenye jiko la mkaa ni tamu kuliko iliyopikiwa kwenye jiko la umeme?
 
Huyu Ike akatukatia umeme juzi ikabidi kuchemsha maji ya moto na kuweka kwenye ndoo kwenda kuoga. Nilipochukua lile bakuli na kuanzia kujimwagia nikajikuta nacheka na kusema "there nothing more Tanzanian than this".... Hata umeme uliporudi I just had to do it one more time, najiuliza hivi pamoja wale tunaokaa ughaibuni hasa katika nchi hizi za kimagharibi bado tunaweza kuswitch ule uswahili wetu on demand?

a. Kutengeneza kata na kuweka ndoo kichwani
b. Kubeba kuni
c. Kupulizia moto ili upike
d. Kuchinja kuku bila kusahau Bismillah na kuelekeza Kibla au kutafuta mtoto wa Kiislamu aje akuhalalishie?
e. Kutengeneza kamba ndefu halafu watoto wote wa kiume (sometimes na wakike) mnaingia na mmoja wenu kujifanya yeye dereva wa Uda!
f. Kuhakikisha unatoa kitanda cha "telemka nikukaze" jua likitoka ili kipigwe pigwe najua na kuua kunguni?
g. Kutegea tegea wachuuzi wa samaki wapite, kule Tanga kulikuwa na jamaa anapitaga na dagaa kwenye tenga la basikweli; leo utamuona Kwaminchi ukikatakata kona utakutana naya Chumbageni! anapiga kelele "aeeeeh daggaaaaaa"! No 1 800 number!
h. Kwa wale wa kijijini jinsi gani tunaswitch kutoka kwenye gari na kusubiri usafiri wa baskeli au wa mguu kwenda kuwaona wazazi. Na hakuna kitu cha kukumbushia kama wale tuliosafiri na mabasi yale ya "Kauru"! na hata malori ya Tumbaku!
i. Lakini kabla ya kuletewa haya makompyuta na makideo bwelele mambo yote yalikuwa "kijiweni" literally. Hakuna mahali watu walikuwa wanapigana fix kama kijiweni! Na always kuna yule jamaa mmoja ambaye asipotokea jioni hiyo kijiwe hakinogi!
j. Halafu yupo yule jamaa ambaye mtaa mzima mnamjua kuwa ni "bishoo"! Na huwezi kumsahau yule binti ambaye kila msela mtaani anamfukuzia halafu ndo mgumu kichizi!
k. Kule Mwanza kama kuna vitu vilikuwa vinasisimua ni kwenda ziwani kuoga; upande mmoja kina dada wanaoga kivyao na kwingine vijana tena mchana kweupe msiniulize kwanini? Nenda ushuhudie hasa mitaa ya watani zetu kule UK a.k.a Ukerewe na UZ a.ka Uzinza!

l. Ongezea ya kule Unguja na Pemba, kwenda baharini kuogelea na kujisaidia haja kubwa. Kazi inakuwa ni kuogelea kuyakimbia yasikufuate.




---------------
 
Yaani huu uzi "thread" unanikumbusha kwa kunikumbusha. Kuna siku hadi machozi yanatoka mamsapu anauliza kulikoni; mbona ukiingiaga kwenye tovuti hiyo unakuwa so emotional? namwambiaga ni kukumbuka kuleee nilikotoka.
Mkuu MKJJ ahsante sana na dondoo zako hapo ni kweli.
Kutengeneza kamba ndefu halafu watoto wote wa kiume (sometimes na wakike) mnaingia na mmoja wenu kujifanya yeye dereva wa Uda!
mi ndo nilikuwa mwekaji wa hizi kamba hadi kuna wakati fulani maza akaja kuzitupa, nilimmaindi...
Kutegea tegea wachuuzi wa samaki wapite, kule Tanga kulikuwa na jamaa anapitaga na dagaa kwenye tenga la basikweli; leo utamuona Kwaminchi ukikatakata kona utakutana naya Chumbageni! anapiga kelele "aeeeeh daggaaaaaa"! No 1 800 number!
Hii nayo kwa saanaa tu na hata mchuuzi mwenyewe alijua target area zake; wapi wananunua na saa ngapi. Hakukuwa na telemaketaz wala nini; na biashara ilikuwa inakwenda....Lakini tu kukuweka sawa ukitokea kwa minchi sio straight Chumbageni lazima upitie kisosora kidogo maana ukila juu kwa juu ni lazima upitie barabara ya kapiko ambako hakuna wanunuzi...
Huyu Ike akatukatia umeme juzi ikabidi kuchemsha maji ya moto na kuweka kwenye ndoo kwenda kuoga. Nilipochukua lile bakuli na kuanzia kujimwagia nikajikuta nacheka na kusema "there nothing more Tanzanian than this".... Hata umeme uliporudi I just had to do it one more time, najiuliza hivi pamoja wale tunaokaa ughaibuni hasa katika nchi hizi za kimagharibi bado tunaweza kuswitch ule uswahili wetu on demand?
Mie nafanyaga once in a blu moon. Kuoga kwa ndoo tena na kata hasaa. Kukuna nazi kwa mbuzi sio za makopo ya Walmart.
Yaani we acha tu nyumbani ni nyumbani tu.......
 
l. Ongezea ya kule Unguja na Pemba, kwenda baharini kuogelea na kujisaidia haja kubwa. Kazi inakuwa ni kuogelea kuyakimbia yasikufuate.




---------------

😀
Bara mpaka majuzi mito inatumika kwa mtindo huo... sasa kazi kwa yule aliyekuwa upande wa mto unapoelekea...
 
Last edited:
jasusi,umenikumbusha hii mutu ray abdul,hivi huyu alikuwa undercover cop au janja yake. i remember alikuwa friends na mtoto mmoja wa nyerere,hivyo ikulu alikuwa anaingia kama kwake,alaafu jamaa could talk,he had more then hundred names
 
kwenye picha ya choggy sly kulia kwake nadhani ni abdul shalamar,bingwa wa kucheza ROBOT,jamani ni ajabu na kweli but how come no one has mentioned ADDY SALLY,i believe he was allready in the game before all them Dejays
 
Back
Top Bottom