Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

mazowea yana taabu thwabia zikiliinganaaa
[media]http://www.youtube.com/watch?v=H-1c_xz_Ke0&feature=related[/media]
 
1.

Huyu Tabia Mwanjelwa naye sijui yupo wapi wazee wa Mbeya tupeni habari, halafu wazee wa Kariakoo Mkulu Ford wa sokoni Karikaoo aliyeimbwa na Safari Sounds ya kina Gurumo na Bitchuka, yupo wapi siku hizi?
Tabia Mwanjelwa yupo ujerumani akiendeleza libeneke, ingawa sio kwa kasi kama ile aliyokuwa nayo huko bongo
 
na haya ndio mambo ya kulee tulikoenda vamia na kubadilisha rais..
[media]http://www.youtube.com/watch?v=rxWwxvURZxI&feature=related[/media]

sie twapaita ngajiza
 
Baada ya kutoka Bima Lee, Mulenga alijiunga na Bendi ya MK Group. Kule alikuwa na kina Mbombo wa Mbomboka, Kasongo Mpinda Clayton na Marehemu Kalala Mbwembwe na kina Sid Morris (Barkeys?) Mafumu Bilal Bobenga. Wimbo maarufu pale kama unakumbuka ni 'Kibela Acha Chuki' Sina hakika ila nadhani huko ndiko umauti ulipomkuta.

Tuko pamoja.
Kibao cha Kibela acha chuki kiliongezewa utamu na keyboard iliyokuwa ikipapaswa na Asia Daruwesh(RIP)...
 
Ilikuwa ukivivaa halafu jua likakuwakia mchana inakuwa ni kasheshe.

Ingawa haya sio makatambuga a.k.a matairi yenyewe yaliyotulea kule vijijini. Bado yapo kwa wingi tu kule vijijini, ndio "kiatu" wanachomudu Watanzania wengi na kinadumu sana. Jamii za wafugaji nchini wanakipenda sana.
 
Mkuu GT,

Mkulu Ford yupo wapi tena mkuu, maana kuna wakati alivuma sana pale sokoni Kariakoo?
 
Mkuu GT,

Mkulu Ford yupo wapi tena mkuu, maana kuna wakati alivuma sana pale sokoni Kariakoo?

Hayo yoote tuyaache kwa sasa ES

hivi ushakata tiket ya harusi december? mimi tayari nimepata offer nzuri tuu na with EMIRATES.

On a flipside naona nyie huko mtaenjoy zaidi maana shughuli ikiisha bongo inahamia NY
 
Source: Fadhili William's legacy

Fadhili William’s legacy spans the whole of East Africa
By Duncan Mwanyumba


The Late Fadhili William (second from left) in a 1966 picture with some members of the Equator Sounds Band: Charles Sonko (Ugandan) - left; Nashil Pichen (Zambian) - second from right; and Peter Tsotsi (Zambian) - right. (Picture courtesy of East African Standard Ltd).

As the Nairobi Fadhili William Anniversary Organising Committee was preparing to hold the 1st anniversary since the death of the internationally-acclaimed Kenyan author/composer of the song 'Malaika'- who passed away at a Nairobi Hospital on 11th February 2001- a thought suddenly crossed my mind that I should call up Peter Colmore, the renowned 83-year old retired producer and entertainment icon (whom I had not yet met personally at the time), not only to extend an invitation but, also, to seek his help. Peter Colmore not only promptly accepted to attend the occasion, but, also, proceeded to give an interesting list of local and East African celebrities whom he felt should not be left out of such a memorial event. He gave out the names, for instance, of Mzee Pembe, Gedion Mwanyigha -formely of he Police Band and the Father of Sheila Mwanyigha of Kiss FM- and, also, Ally Sykes-the President of the All Africa Travel & Tourism Association, etc.

Although I had not, similarly, met Mzee Ally Sykes before, I was equally surprised to obtain the latter's prompt acceptance, over the telephone, of the invitation to the Grand Regency Hotel, Nairobi, on mentioning the late Fadhili William's name. He had known both the late Fundi Konde and Fadhili William in the 1940s and 1950s, in Army and entertainment circles, respectively. Such has been the spontaneous and overwhelming outpouring of support that has characterized the crusade to promote Fadhili William's rich musical and cultural legacy as well as those of his East African peers.

A talent scout

On the legendary Peter Colmore himself-I gathered from him that he had virtually stamped the whole of East and Central Africa from the late 1940s as a music talent scout; he is easily credited with developing the music careers of artistes like John Bosco Mwenda and,Edward Massengo both of whom he had fished out of the Belgian and French Congo. He observed that in those days, unlike nowadays, music promoters were multi-cultural 'think-tanks' who would endeavour to bring artistes and musicians together from across the African Continent. It is not surprising therefore that he succeeded in bringing together under one roof a motley company of artistes such as Athman 'Kipanga', Edward Massengo, Franck Humplick, Fadhili William-then of the famous Jambo Boys Band -in the 'East African Railways & Harbours Showboat Programme' of which he was the producer in 1959/60.The Programme's records and pictures are still well-kept in the Kenya Railways Archives from which we stand to benefit.

Professional lobby


The Late Fadhili William (left), in pensive mood during a negotiation session. He is accompanied by his Legal Counsel, Duncan Mwanyumba. (Photo by John Prospero)

The ensuing invitations for Fadhili's 1st anniversary not only netted in a representative of the Kenyan Attorney-General on copyright, Martha Maina, but, also, the Chairperson of the Law Society of Kenya, Miss Raychelle Omamo! Although some emphasis was placed on inviting Fadhili's peers as demonstrated indirectly by the presence of the children of Daudi Kabaka-David and Mary, the desire was, more importantly, however, to sensitise the copyright authorities on the general plight of local musicians and their dependant families.

In my view, the copyright issue is rendered more critical, from the economic standpoint, by the fact that whereas many foreign (western) artistes supplement their incomes from other incidental activities such as film-acting and can therefore afford not to actively pursue their own copyright protection, their East African counterparts, however, barely survive even from their own original compositions, let alone the filming industry, as the latter industry is barely existing in the region.

The aim of Fadhili William memorial trophy

It was not, however, until the Fadhili William Trophy that I have personally donated in perpetual memory of the late icon reached the hands of the Kenyan Minister for Education, Henry Kosgey in the latter's Jogoo House Boardroom on 30th July 2002, that the public message began to sink in: Inculcating a culture that recognises artistes and musicians during their lifetime-away from a culture that merely waits to euologise them after their death! The Fadhili William Trophy was donated for the purpose of identifying and promoting young East African artistes and musicians of outstanding talent and promise to compose original songs in the multi-ethnic Kiswahili language; in addition, it is intended thereby to increase local awareness of original composers' legal rights.

The East African Community

As I came to Tanzania over a year ago, I was determined not to leave behind in Kenya my ideals for a respected music profession and clientele. I will be forgiven for believing, that, the spirit of Fadhili William could draw out and lift up the voices of young talents beyond the annual Kenya Schools and Colleges Music Festival at which the William Trophy was floated.

This is how the decision therefore to host the three deceased musicians 'photo Exhibitions here in Arusha-Fadhili William (Kenya), Mbaraka Mwinshehe (Tanzania) and, Philley Lutaaya (Uganda)-reached after much consultation and building of consensus, was born However, I must confess to my initial loud personal curiosity for the late renowned Tanzanian crooner Marijani Rajab who is still revered both in Tanzania and Kenya; The problem with him, however, was more to do with protocol than anything else, as Mbaraka Mwinshehe, whose music is still very popular, according to his official music distributors-Tamasha Corporation Limited of Nairobi-was the elder of the two artistes.

The Malaika Concept


The Late Fadhili William in a joint performance of ‘Malaika’ with Usha Uthup, an Indian international singer, at the International Casino, Nairobi in the late 70's. (Courtesy of E.A. Standard Ltd)

It is only logical that in celebrating the life and music times of Fadhili William in Arusha, through photographs, music, and dances, the 'Malaika Concept'-i.e, bringing people together, be invoked and expounded, thus: The song 'Malaika' itself is a tale of a man who so loves the 'angel' but is too poor to afford her dowry! In African tradition, such a suitor' would appeal for communal help to marry off the 'angel' The 'Malaika Concept' extends, however, beyond the personal beauty of the 'angel' to symbolise all that is good and beautiful in the African traditional context of shared values and social responsibilities .The 'Malaika Concept' can extend even to community peace and tranquility, which guarantees, that, individual dreams and aspirations are fulfilled through mutual help and co-operation as it does in the renowned Kenyan 'Harambee' spirit. The 'Malaika Concept' in this way, then, universally transcends all racial, ethnic, religious and/or cultural barriers. Finally, the 'Malaika Concept' envisages even reconciliation'-a peaceful encounter and co-existence between African traditional foes!

The Malaika festival

As Fadhili's legacy spans the whole of East Africa and beyond, the Arusha photo Exhibitions should serve also as the 'drum beat' to herald and publicise the impending 'Malaika Festival' in Nairobi, Kenya, with probable, simultaneous ripple effects in the three East African Capitals, respectively.

The Festival is now tentatively scheduled to be held from Tuesday 11th February 2003 i.e, Fadhili's 2nd anniversary, through to Sunday 16th February 2003. The Festival- a natural but, conscious progression from the foregoing series of programmed events- while paying ultimate tribute to Fadhili William and other fallen East African Music Heroes, is intended, also:

a) to show-case budding East African talents and b) to fuel the nascent public crusade to pursue and protect East African musicians' intellectual property rights with Fadhili William as the torchbearer.

Charity beneficiaries

In keeping with the above-mentioned universal ideal for the 'common good', and, in the promotion of their respective legacies, it is fitting that the proceeds of sale of these memorial events do benefit the following charitable causes, in order of priority:

a) Three Aids orphanages in Kenya, Uganda and Tanzania, respectively, since, aids is the single most devastating scourge now common to the three East African member-states;

b) the Special Olympic Movements for the mentally challenged in Kenya, Uganda and Tanzania, respectively, since, Fadhili William sang for and supported the Movement's Kenyan Chapter in 1998;

c) Music promotion and Education in East Africa.

Appeal to sponsors

Although Organisations whose objectives and ideals that promote 'the East African Community Spirit' are especially targeted in this appeal, others, too, in the East African spirit of 'Harambee' are, equally, welcome to donate to the designated charities through the appropriate Co-ordinating National Committees of the three East African member-states.

Duncan Mwanyumba is the Convenor of the Malaika Festival/Legal Counsel to the family of the late Fadhili William/Secretary to the Malaika-cum - E.A. Cultural Night, Arusha
 
duh! inaonekana kuna watu mmenda sana umri humu duh!
hizi post za huku na mahojiano yote kweli yamefinya mtoto kabisa na nakubaliana na wewe mkuu. lakini wamenisaidia kujifunza historia ya nchi yetu katika nyanja zote. this is my favorite post kwa kuondolea stresses
 
Hivi nani anayejua mtu aliyeimba kwa mara ya kwanza kabisa na ambaye ni mtunzi wa wimbo wa MALAIKA? Maana watu wanakopi tu miaka nenda, miaka rudi sijui kama familia yake inapata chochote!

Masahihisho kidogo, kumbe hata serikali haijui mtunzi wa wimbo huu. Majibu ya Bendera haya hapa:

Na. 160
Asili ya Wimbo Maarufu wa Malaika
MHE. PARMUKH SINGH HOOGAN aliuliza:-

Kwa kuwa, Wimbo maarufu wa ‘Malaika' asili yake ni Mkoa wa Kilimanjaro – Tanzania; na kwa kuwa, waimbaji wengi wa kigeni kama vile Bonny M, Mariam Makeba n.k, wamekuwa wakiimba wimbo huo:-

Je, nchi yetu inanufaika vipi na wimbo huo kutoka kwa waimbaji wageni?

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Parmukh Singh Hoogan, Mbunge wa Kikwajuni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu inanufaika kwa njia mbalimbali pale ambapo waimbaji wengi wakiwemo wa ndani na nje ya nchi wanapoimba wimbo wa Malaika na nyimbo nyingine nyingi zinazohusu nchi yetu ya Tanzania. Kwa kutumia mfano alioutoa Mheshimiwa Parmukh Singh Hoogan, ambapo waimbaji wa kigeni kama vile Bonny M, Mariam Makeba n.k ambao wamekuwa wakiimba wimbo maarufu wa Malaika, Serikali inanufaika sana kutokana na wimbo huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, wimbo huo unaitangaza nchi yetu duniani. Lakini pia kwa vile wimbo huo umeimbwa kwa lugha ya Kiswahili, hivyo basi wanaitangaza lugha yetu ya Kiswahili. Kwa namna nyingine, pindi wimbo huo unaposikika, wasikilizaji wanatambua kama kuna lugha ya Kiswahili na asili yake.

Aidha, wasikilizaji wa wimbo huo hushawishika kujifunza lugha ya Kiswahili. (Makofi)

MHE. PARMUKH SINGH HOOGAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na faida hizo alizozisema Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina taarifa kuna nchi moja jirani inanufaika kifedha. Mheshimiwa Naibu Waziri anasema nini kuhusu hilo?

MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri majibu. Sasa nchi hiyo sijui ni nchi gani. Nafikiri tuendelee na swali lingine la nyongeza. Mheshimiwa Mbunge, kama unaijua nchi hiyo nitaomba umnong'oneze Mheshimiwa Naibu Waziri ili basi aende akafuatilie yatusaidie hayo mapato yaweze kuja katika nchi yetu ya Tanzania pia.

MHE. HAROUB SAID MASOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya majibu mazuri sana na ya kuridhisha ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa, sisi wengine humu ndani Bungeni tulikuwa waimbaji ni vyema tukamjua huyo mtunzi wa wimbo huo na yeye mwenyewe anafaidika na nini huyo mtunzi? (Makofi)

MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, nafikiri Mheshimiwa Naibu Waziri amesikia swali hilo au kama anamfahamu hebu atwambie huyo mtunzi. Mheshimiwa Naibu Waziri majibu.

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI NA MICHEZO:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba wimbo huo unaojulikana kwa jina la Malaika ulitungwa na Mtanzania ambaye alikuwa anamsifia mpenzi wake anayeitwa Malaika, na kwa bahati mbaya kwa utafiti wote na wataalam wote wamefanya mpaka sasa hivi jina la huyo aliyeutunga halijajulikana, lakini ni Mtanzania anayetoka Kilimanjaro. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini anafaidikaje? Kwa bahati mbaya kama walivyosema Mheshimiwa Parmukh Hoogani na Mheshimiwa Haroub Masoud, aliyefaidika na kupata hakimiliki na mirahaba ya wimbo huo ni mzee mmoja ambaye amefariki ni Mkenya anaitwa Fadhili Williams, yeye ndiye aliyekuwa anafaidika na wimbo huo kwa sababu yeye ndiye aliyeurekodi. Sasa Sheria za hakimiliki ni kwamba anayerekodi kwa Sheria za Kenya ndiye anayepata mirahaba. (Makofi)

MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, labda tumsikie Mheshimiwa Teddy Kasella-Bantu kwa sababu ni Mbunge wa siku nyingi anaweza akawa anamjua huyo mtunzi.

MHE. TEDDY L. KASELLA -BANTU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kukiri kwamba pamoja na kwamba ni Mbunge wa siku nyingi simfahamu.
(Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na majibu mazuri ya nyongeza naomba niulize swali moja la nyongeza dogo. Kwa kuwa, wimbo wa Malaika na nyimbo 10 nyingine huwa zinatakiwa ziendelee hivyo hivyo bila kubadilisha lafidhi au maneno na sasa vijana wa siku hizi wanauimba wimbo huo wanaubadilisha. Je, Serikali inasemaje kuhusu ubadilishwaji huo?

MWENYEKITI: Mheshimwia Teddy Kasella-Bantu swali lako kwa kweli kulijibu kwa haraka ni swali ngumu sana. Nitaomba uwasiliane na Mheshimiwa Naibu Waziri ili muweze kusaidiana.

Waheshimiwa Wabunge, tuendelee na swali linalofuata. Lakini leo kwa kweli ni challenge kwa wimbo huo na nadhani Wizara yetu ya Habari, Utamaduni na Michezo inatakiwa kufanya kazi ya ziada kwenye eneo hilo.
 
Mzee hapo nimekukubali khaaaswa
kunamtu mmoja kama ninakumbuka vizuri jina lakeanaitwa ROY Bashekanako huyu alikuwa wapi?pia kuna bendi moja ambayo sijaiyona hapa baoni inaitwa MULE MUVA au ni mtindo huo
Naile bendi iliyo piga ile wimbo wa milima ya kwetu nibendi gani ile wkuu
ninfikiria ni kida waziri lakini sikumbuki bendi gani



Wimbo wa 'Milima ya Kwetu' ambao ulitamba sana miaka ya katikati ya 80' ulipigwa na bendi ndogo ya 'Super Rainbow Orchestre' waimbaji wakiwa ni Eddy Sheggy (RIP) na msichana Emma Mkello (RIP) na wengine. waliimba kibao hicho wakitokea nairobi walikokuwa wakipiga mziki na hiki ndio kilikuwa kibao chao cha kwanza nchini ambacho kilivuma sana. Baada ya hapo Eddy ndio akaendelea na Vijana, Bima, Washirika Tanzania Stars na kadhalika
 
kUNA ZILE SEMI ZA ZAMANI AMBAZO NI ZA KISANII ZILICHANGAMSHA SANA LUGHA YETU:

1. DU KINAA - POA TU
2.KATA NGWALA- PIGA MTAMA
3.PEKOSI- SURUALI PANA CHINI
4.RAIZONI -VIATU VIREFU
5. NYAPU - Msichana
6.SHADA - Bangi


7. Mgogoro - WoWowo
8. Salama au macho? Tutakula au Fitina? - Maamboo?
9. Basi Haya/Basi Ok - Hamna noma!
1o. Tutayafiksi - Nitayashughulikia!

Tuendelee...!!
 
Nikweli kabisa mkuu, huyu Zahiri alikuwa na vibao vingi sana vikali, hicho ulichokitaja ni Kristina namba moja, kuna Kristina namba mbili, halafu nafikiri unakumbuka "Kabwe", ziko namba moja na mbili, halafu kibao chake kingine "Twende Kijijini",

Zahiri aliweza pia kuandika jina kubwa sana la muziki hapa nchini, lakini baadye hali mbaya ya uchumi ikamfanya ahamie Nairobi, ambako kwa kweli sijawahi kusikia vibao vayke akiwa huko, lakini najua kuwa baadye alirejea bongo, na siku hizi anapiga solo, yaani peke yake kwenye hoteli moja kubwa hapa chini.




Hata akiwa hapa hapa nchini Zahir Ally baada ya kutoka Kimulimuli aliweza kujiunga na bendi kadhaa nchini na kuendelea kutoa vibao kadhaa vilivotokea kupendwa sana kama pale miaka kama minane ama kumi iliyopita aliposhiriki kuunda bendi mpya ya 'Mass Media le Dance' na kuimba kuimba kiba kikali cha 'Beatrice' akishirikiana na 'Mtoto wa Malaika' (RIP).
'nipe nafasi niwe mpangaji wa kudumu
ndani ya moyo wako x2
moyo thabiti ulojaa mapenzi sawasawa na yangu x2,
tuishi sote milele ee, beaatrice x2,
kama watoto wazuri wapendezao,

Lakini mwaka 1987 Zahir Ally pia alishiriki na Sambulumaa iliyokuwa na akina Nguza Viking na Rahma Shalli kuimba kibao cha 'Mariam Cleopatra' kilichotokea kuwa miongoni mwa vibao vilivyopendwa sana miaka hiyo
'bahati mbaya nilioa zamani,
ningefunga ndoa na wewe,
mapenzi yananivunja mgongo,
.
 
huyu nae anaingia kwenye historia yetu katika picha
 

Attachments

  • 62539.jpg
    62539.jpg
    19.3 KB · Views: 140
7. Mgogoro - WoWowo
8. Salama au macho? Tutakula au Fitina? - Maamboo?
9. Basi Haya/Basi Ok - Hamna noma!
1o. Tutayafiksi - Nitayashughulikia!

Tuendelee...!!
  • 11. Gangwe
  • 12. Du kinaa
  • 13. Mezea
  • 14. Bitozi
  • 15. Tinabuu
 
Last edited:
jamani naamini wengi wetu tumekaa vijiweni/maskani,ambavyo in one way or another vilishape destiny zetu.mimi ni mwana HARLEM,kijiwe shule ya msingi muhimbili,tulikuwa na football team vilevile,me i was only a cheerleader.ujana unasumbua kwa hiyo vitu kama wee ilikuwa kama kazi,nakumbuka tukielekea madebeni mbowe tulipitia MISSISSIPI(nyuma ya library)kwa mzee musa.Those were the days,unfortunately washikaji wengi,with time,they just fell off the rails
 
duh! inaonekana kuna watu mmenda sana umri humu duh!

Hivyo ndivyo Jamiiforums ilivyojengeka. Ndiyo maana tunashauriwa kuwa wastaarabu kwa wanaJF wote hata kama tusipokubaliana nao katika misimamo. Wengine wao wana umri zaidi ya babu zetu, na haitii heshima kwetu kutumia lugha chafu kwa watu wenye umri wa kiwango hicho.
 
Back
Top Bottom