Tukumbushane riwaya za kusisimua

Sitoweza kukisimuli coz sikijuwi vizuri.
Nilitokea kuazimwa na demu tukiwa safarini.
Nilikisoma ktk kurasa zake za mwanzo tu na
kutokea kukikipenda sana.
Kiliandikwa kwa lugha ya kifaransa na kimetafsiria ktk lugha 18 (pengine zimeshaongezeka. Na kimechapishwa kwa mara tofauti. Kinaitwa BARUA NDEFU KAMA HII.
 
Salamu kutoka kuzimu robert r msigwa, master of the game by sydney sheldon

mh! na ww huchelewi kubadilika. Badala ya 'orodha ya watakao uawa' umeweka chengine, kulikoni? Au ndiyo hiki hiki ulichokuwa umekikusudia?
 

sasa hii riwaya inaendela au?japo kwa nimeshaona movie nyingi za aina hii lakini si mbaya na kusoma pia
 
Beka amejitahidi san katika Mhanga wa ikulu...ukiisoma mtiririko wake kama kweli vile
 
jamani wandugu hivi vitabu vinapatikana kwelo siku hizi???natamani ningejua vilipo nakapate copy zangu maana ni mpenzi sana wa riwaya za zamani,anayejua plzzz anijulishe
 
jamani wandugu hivi vitabu vinapatikana kweli siku hizi???natamani ningejua vilipo nakapate copy zangu maana ni mpenzi sana wa riwaya za zamani,anayejua plzzz anijulishe
 
jamani wandugu hivi vitabu vinapatikana kweli siku hizi???natamani ningejua vilipo nakapate copy zangu maana ni mpenzi sana wa riwaya za zamani,anayejua plzzz anijulishe
 
Nakumbuka riwaya nzuri kama NJAMA,na wausika kama willy Gamba,velonica,zainabu e.t.c, dar es salaam usiku pia ilisisimua
 
hii thread imenikumbusha riwaya nzuri sana za zamani...
 
Katika Mhanga wa Ikulu namkumbuka dereva tax ambaye mapema aliweza kumgundua Dickson kuwa ni njagu lakini Frank hakuamini lol, Beka amefanya vizuri sana katika riwaya hii pamoja zile zilizokuwa zikitoka magazetini hasa ya yule mdada wa chuo aliyeshuhudia na kurekodi mauaji ya kutisha (jina la kitabu limenitoka kwani ni siku zimepita tangu nikisome)
 
mh! na ww huchelewi kubadilika. Badala ya 'orodha ya watakao uawa' umeweka chengine, kulikoni? Au ndiyo hiki hiki ulichokuwa umekikusudia?

Dah! Hapo kwenye redi umenifanya nivikumbuke vitabu vya Inspekta Fog na Kachero Haji
Kama vile Operesheni sukuma namba nane n.k hicho orodha ya watakaouwawa namkumbuka sana yule jamaa alikuwa anaitwa Sureish Kanji (Sumu ya nyoka mpenda Kifo) Ngoja niwadokezeni kuhusu MWIBA hiki nacho ni cha Beka mfaume, subirini kidogo tu baada ya hapo tutamtazama Husein Tuwa.
 
Nilikuwa sina nia ya kukitafuta.
Lakini kama bahati tu kukumbana nacho njiani.
Nikiwa Ubungo namsafirisha mtu anaenda mkoa si nikakiona, nimekinunua na kweli ni kizuri.
Kweli Beka kafanya kazi nzuri.
Now nimefika uk. wa 32 wakati mkurugenzi wa usalama wa taifa akiwa ameshauona mkanda wa video unaomuhusu Zumo. Hadithi ni nzuri sana.
 
Ikibidi Kufa Nife
Kikomo
Hadithi za Allan Quatermann
Alif Lela Ulela
Dunia Hadaa
Robinson Crusoe na Kisiwa Chake
Na ile riwaya tulikuwatunaisoma shule kwenye fasihi jina nimesahau ila kulikuwa na mtu anaitwa Bwana Mkubwa Lyanda wa jamhuri ya Unono!!
 
MWIBA
1
Wote wawili walikifuata kitabu kimoja cha riwaya katika duka moja la vitabu lililoko katikati ya jiji la Dar es salaam la Dar es salaam. Walipishana kwa dakika chache kuingia humo dukani. Wa kwanza alikuwa Tony aliyeingia kwenye duka hilo na kumuona muuza vitabu mwenye asili ya kiasia akijiandaa kulifunga duka. kitendo hicho kilimlazimisha Tony kuangalia saa yake mkononi, ilikuwa saa 11.02 jioni. Muuza vitabu aliacha shughuli aliyokuwa akiifanya na kuvuta mapazia kwa ajili ya kufunga madirisha, akarudi kaunta iliyotengenezwa kwa vioo na papi za aluminium ambako Tonny alisimama, akiwa nyuma ya kaunta Tonny akiwa mbelewakitazamana, Tonny akasema "Nataka kitabu cha MUHANGA WA IKULU kilichoandikwa na Beka Mfaume".

"Una bahati!" Alisema muuzaji huku akimpa kitabu alichoagiza Tonny. "Kwa nini?" Aliuliza Tonny. "Kwa nini? aliuliza Tonny "Kilibaki hiki pekee!" "Kweli nina bahati" alisema Tonny huku akitoa pesa kwenye mfuko wa suruali. "Kiasi gani?" Aliuliza. Muuza vitabu alitaja bei. Tonny akalipa. Wakati Tonny alipokuwa anasubiri chenji yake akaingia msichana kwenye duka hilo. Alikuwa ni msichana mzuri aliyeumbika mwenye sifa zote za kumfanya awe mshiriki wa kupanda jukwaani na kushindania taji la urembo. Msichana huyo alienda na kusimama kando na aliposimama Tonny, hakumsalimia yeyote! Tonny alimwangalia mara moja msichana huyo na kuugundua uzuri wake kwa haraka, akampuuza. Alimpuuza kwa sababu alijua hawezi kuwa chaguo muafaka kwa msichana huyo kimapenzi. Mwonekano wa msichana huyo ulizungukwa na mazingira ya hali bora ya kifedha yaliyomuwezesha kuwa na ujivuni, kunata, maringo ya kujiona mzuri na kutozoeleka kirahisi na watu hasa kwa mtu asiezoeana nae kama alivyo Tonny hapo alipo. Yote hayo yakawa yameweka tofauti kubwa iliyomtenganisha yeye na binti huyo. Yeye alikuwa ni mtoto wa kijiweni mwenye misamiati yote ya maneno ya kimjini na ambaye anaishi uswahilini maeneo ya Kijitonyama na atokae kwenye familia ya kimasikini!
Tonny alichukua chenji yake na kuondoka bila kumuangalia binti huyo ambaye alibadilisha hali ya hewa ya humo ndani na kuifanya inukie vizuri kutokana na manukato aliyojipaka.

"Nami nipe kitabu cha Muhanga wa Ikulu" Mrembo huyo alisema. Muuza vitabu alitabasamu na kusikitika. "Jamaa aliyetoka ndiye aliyemaliza kukinunua kilikuwa cha ni mwisho" alisema. "Mungu wangu!" Alilalamika mrembo huyo kwa lafidi ya Maringo.

***********
Mara baada ya Tonny kutoka kwenye duka hilo akakutana ana kwa ana na jirani yake anayeishi maeneo ya kijitonyama. Alisimama na kusabahiana nae. Wakati alipokuwa akisalimiana na jirani yake huyo yule msichana mrembo naye akatoka dukani, akamuona Tonny. Kumuona Tonny akiwa pale nje wazo la haraka likaingia kichwani mwa msichana huyo likamfanya asite kuingia kwenye gari alilokuja nalo ambalo alikuwa akiliendesha mwenyewe. Tonny na jirani yake wakaagana.

"Kaka samahani!". Hata hivyo kauli ya msichana huyo ilimfanya Tonny na jirani yake wote kwa pamoja wageuke na kumtazama msichana huyo. "Hapana ni huyu kaka!" Alisema yule msichana huku akimnyooshea kidole Tonny.

Jirani yake akaondoka lakini baada ya kuoiga hatua chache akageuka na kuangalia nyuma. Akamuona Tonny akiongea na yule msichana. Akajikuta akijiuliza ni kitu gani kilichomfanya msichana mzuri kama yule atake kuongea naye. Pengine anataka kuelekezwa sehemu! Alijiambia nafsini mwake kama kujipa sababu ya kujifariji. Lakini kwa nini amchague Tonny peke yake? alijiuliza na kujihisi akiingiwa na mchomo wa wivu! Hata hivyo akauridhisha moyo wake kwa kujua kuwa mazungumzo yao hayatakuwa ya mapenzi kwani wako daraja tofauti.

"Samahani naomba msaada wako!" Msichana alisema. Tonny alinyamaza akisubiri huo msaada anaoombwa.
"Naomba uniuzie hiki kitabu!" Msichana alisema na kuonyesha kitabu alichoshika Tonny mkononi. "Sidhani kama naweza kukuuzia!" "Kwanini?" msichana aliuliza kama vile ilikuwa ajabu kukataliwa ombi lake (TUTAENDELEA)
 

Mkuu hicho kitabu kimeandikwa na Mwandishi anaitwa Mariama Ba raia wa Senegali. Ni kizuri si haba nilikisoma miaka mingi sana ilopita. Duh leo raha mbona!!
 
Ehee! Ikawaje tena.... we r waitin 4 u.
 
Vinapatikana wapi hivi vitabu mnavyovitaja? Kuna duka lolote, kanda yoyote, mkoa wowote linalofahamika kama lina vitabu hivi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…