Asante kwa jf humu tunaongea bila kujuana hata katika vitu ambavyo huwa hatupendi kuviweka wazi kama kuchapiwa maana ni aibu, humu hatujuani inakuwa rahisi kuweka mambo wazi...
kisa changu
Nilimuaga ex girlfriend wangu kwamba nimepata safari ya kikazi nitakua nje ya mji kwa muda flani kuna tajiri anataka nimwekee makabati nyumba anayofanyia finishing anyokaribia kuhamia, nilifika huko lakini nilikuta kuna wenzangu wengine kwa hio kazi iliisha mapema , niliwahi kurudi nikiwa nimeshalipwa na tajiri kama laki 3 hivi, nilifika kwangu kuweka begi na kisha nikaanza safari ya kwenda kwa ex wangu, nilifika kwake nilimkuta hayupo, nikaanza safari ya kurudi nikaona wacha nipate chakula lodge flani ya karibu,
wakati nakula wali kuku kwa jeuri ya pesa nilizopata huko kibaruani nikaona kuna gari rav 4 imekuja pale lodge, nilipatwa na mshangao kuona ex wangunae kashuka nje ya hio gari, kiukweli alikuwa amependeza hio siku nadhani alienda saloon, nikawa siamini amini nachokiona na yeye muda huo hajaniona,
jamaa aliingia ndani sikuona alichoenda kufanya ila itakuwa alienda kufanya malipo ya chumba, nilimpigia simu ex muda huo huku namcheki akawa ananiambia yupo kwenye daladala anarudi kwake alienda sokoni, machozi yalikuwa yananilenga, yule jamaa aliporudi akamchukua ex wangu wakaingia ndani, aaaaahhh!! maumivu makali mno!!
hata msosi ukageuka mchungu, nililipa na kuondoka hapo hapo,,, siwezi kuanzisha varanga kwa demu ambae kwa maamuzi yake kakubali kuliwa..
nilifika gheto nampigia lakini simu inaita tu, hapa nikawa navuta picha game imeiva, huo moto anaopelekewa huko si wa kitoto, niliumia sana kwakweli..
nilienda pharmacy ya karibu kununua sleeping pills (vigonge vya usingizi) maana mawazo yalinisonga sana, nilirudi geto nikagonga vidonge viwili nikajilaza kitandani huku naendelea kuwaza lakini usingizi ukanichukua.
kesho yake naamka kama kawaida ila daah!! nikakumbuka kilichotokea jana nikacheki simu nikaona ex alinipigia kama mara tatu hivi na kuacha mesej kwamba alikuwa kanipigia sipokei, ila muda alionipigia hapo nilicheki ilikuwa ni baada ya masaa mawili na nusu hivi.
kesho yake nilimwambia aje geto, ile kafika akaanza kujifanya kamaindi sikupokea simu ila akaanza kujifanya anajichekesha kufurahi nimewahi kurudi na kanimisi sana, alikuwa anaona siku zinakuwa ndefu bila mimi na blah blah kibao, mimi namchora tu, nikaanza kumpiga maswali pale moja kwa moja kwamba jana alieshuka nae ni nani,, akaanza kama kujistukia hivi akawa anakazia kwamba alikuwa kwake,,, nilimnasa kibao cha nguvu huku nikiwa na hasira ili ajue nipo seriois,, akaanza kulia, namwambia unalia kwanini lakini akawa analia machozi mengi namuonea na kwamba sio yeye, nilimnasa vibao vingine viwili vya nguvuu... akaanza kukiri na kuniomba msamaha sijui hatarudia, haikuwa nia yake, bla bla bla,,,,, nilifungua mlango nikamwambia its over!, hatuwezi kuendelea ....
Aliondoka huku akijifuta futa machozi ambayo huenda yalikuwa ya kinafki tu, nikajikaza kiume kwamba siwezi kuumia kisa malaya,,, baada ya masaa kama matatu hivi maumivu yalianza kurudi kwa spidi kali sana, sikuweza kuyamudu kwakweli, ilibidi tu niende kazini kujishughulisha hivyo hivyo, na niliporudi nilienda kukimbia uwanjani,,,hii ikawa ratiba yangu kwa wiki hivi lakini maumivu hasa wakati wa kulala niliyapata aisee,, kidume kuna siku nikaanza kuwaza jinsi ex alivyokuwa anapelekewa moto, nilidondosha machozi kama mtoto mdogo.
Nilikuja kupata mwengine ndio nikawa napooza pooza maumivu na mwishowe nikasahau kabisa,,,,
KISASI::
Kwa sasaHuyo jamaa ndie aliemuoa ex wangu, lakini ch ajabu mpaka leo ex wangu ni kama analazimisha mawasiliano, ikitokea sherehe yoyote tu ananitumia mesej pasaka njema, idi njema, n.k ila namjua anachotaka ni ukaribu, hilo nilihakikisha kuna siku nilikutana nae nikamwambia twende kwangu alikubali kabisa na nilipanga nimgonge nilipize kisasi ikiwezekana nimtumie kabisa picha huyo jamaa lakini nikapiga chini huo mpango,,,, ni kwamba huyu ex mda wowote nikimtaka hata kesho asubuhi anaweza kunipa mzigo lakini nafsi inanisuta, sioni hata ambacho ntafaidika nacho ni kama nilikubali yaishe tu maisha yaendelee.Sijajua kwa huko mbele lakini naomba nienelee na msimamo huu huu.