Tulia Ackson alipokuwa anazunguka na majeneza ili kuizika CHADEMA Mbeya, hawa viongozi wa dini ya Kikristo walikuwa wapi?

Tulia Ackson alipokuwa anazunguka na majeneza ili kuizika CHADEMA Mbeya, hawa viongozi wa dini ya Kikristo walikuwa wapi?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426

1660206274574.jpeg

Tukio la mashabiki wa Simba la kuingia na jeneza uwanjani limewakera wanaoitwa Maaskofu na viongozi wa dini na tumeshuhudia matamko kadhaa kutoka kwa Askofu wa Kikatoliki Kilaini na mzee wa mkono wa baunsa Gwajima. Sijaelewa kilichowatoa mafichoni, kama ni ushabiki wao kwa Yanga au ni kwa sababu ya jeneza au labda nifahamishwe kama watu hawa wameingia nchini Tanzania Wiki iliyopita, vinginevyo nitawashangaa.

Tulia Ackson katika harakati zake za kuusaka ubunge wa Mbeya Mjini, baada ya kutumwa na Magufuli alibeba majeneza na misalaba ya kila rangi kama Ishara ya kuizika CHADEMA. Alitembea Mbeya yote bila kificho chochote, mbona Kilaini na Gwajima walinyamaza?

Wakati huyu Tulia akifanya yote haya alikuwa Naibu wa Spika wa Bunge la Tanzania (sasa hivi ni spika kamili). Ni mtu aliyekuwa anajitambua, mbona hawa wacha Mungu hawakuwahi kukemea? Iweje leo mtu msela kama Tundaman akifanya aliyoyafanya Tulia wao wanapambana naye, kulikoni?​
 
Tukio la Tulia lilikuwa uhuni wa kisiasa na hili la Simba ni uhuni ndani ya soka. Yote yanaashiria upumbavu na ukosefu wa Maadili.

Kwa hiyo sikubaliani na ukimya wa viongozi hao kwa Tulia na nawaunga mkono walichofanya kwa Simba. Kipindi Tulia anafanya maigizo yake ndo kipindi unafiki ilikuwa sifa kubwa ya viongozi wa dini wakimpamba Rais wa wakati huo.

Tuseme kwa sasa baadhi akili zimewarudi na wanaongea vitu sahihi timely.
 
Tukio la Mashabiki wa Simba la kuingia na Jeneza Uwanjani limewakera wanaoitwa Maaskofu na viongozi wa Dini , na tumeshuhudia matamko kadhaa kutoka kwa Askofu wa Kikatoliki Kilaini na Mzee wa Mkono wa Baunsa , Gwajima...
Acha ujinga, we unaona alochokifamya ni sahihi, kwann achezee Iman za Watu. Tena wakristo wastaarabu angekumbana na waislam angechezea kichapa palepale, angejua hajui
 
Mtu/watu wana uhuru wa kutoa maoni yao wakati wowote, na huwezi kujua hilo wazo la kutoa hayo maoni kuhusu jambo husika litawajia lini.

Kwangu hao viongozi wa dini kutoa maoni yao sasa kuhusu uwepo wa lile jeneza uwanjani naona ni jambo la kawaida, muhimu hiyo precedence ndio itaanza kufuatwa kuanzia sasa.

Mbona wakati mwingine hao viongozi wa dini wakitoa maoni tunayoyataka mathalani kuhusu Katiba Mpya huwa tunayafurahia? basi tusiwapangie wakati gani waseme kitu gani, muhimu wasikilizwe.
 
Kwa tabia hizi za kipuuzi ambazo zinazidi kutamalaki katika jamii yetu ya Kitanzania ni lazima zikemewe bila ya kuangalia sura na hadhi ya mtu. Wote wanaoleta dhihaka kupitia vitu vya kiibada ni lazima wote wakemewe hadharani.

Kwa kuwa suala hili linazidi kujirudia mara kwa mara, hivyo basi maudhui ya washereheshaji hasa wasanii inapasa sasa yapitiwe kwanza kabla hawajafanya maonyesho au maigizo yao hadharani.

Vipo vyombo husika kama vile BASATA, vina wajibu sasa ya kuweka njia sahihi za kutambua kwanza maudhui ya wasanii ili kuepusha uwasilishaji wake ambao unaweza kuleta sintofahamu ama mihemuko kabla ya kuwekwa hadharani katika mkusanyiko wa watu wengi wenye imani na itikadi tofauti.
 
Tukio la Mashabiki wa Simba la kuingia na Jeneza Uwanjani limewakera wanaoitwa Maaskofu na viongozi wa Dini , na tumeshuhudia matamko kadhaa kutoka kwa Askofu wa Kikatoliki Kilaini na Mzee wa Mkono wa Baunsa , Gwajima...
Unazungungumzia viongozi wa dini wapi hao, hawa hawa wa bongo
 
Tukio la Mashabiki wa Simba la kuingia na Jeneza Uwanjani limewakera wanaoitwa Maaskofu na viongozi wa Dini , na tumeshuhudia matamko kadhaa kutoka kwa Askofu wa Kikatoliki Kilaini na Mzee wa Mkono wa Baunsa , Gwajima...
Mnapotosha,kilaini hajazungumzia uwepo wa jeneza.Kilaini amekemea matumizi ya msalaba katika tukio lile la simba,kumbuka msalaba ni alama katika Ukristu.

Jeneza hata mpangani analitumia.
 
Tukio la Mashabiki wa Simba la kuingia na Jeneza Uwanjani limewakera wanaoitwa Maaskofu na viongozi wa Dini , na tumeshuhudia matamko kadhaa kutoka kwa Askofu wa Kikatoliki Kilaini na Mzee wa Mkono wa Baunsa , Gwajima...
Nadhani tatizo ni msalaba na si jeneza. Hebu weka picha ya Tulia na majeneza yake tujikumbushe
 
Hakuna viongozi wa dini siku hizi bali tuna viongozi wa DILI. Ni unafiki tu umebakia.
 
Mnapotosha,kilaini hajazungumzia uwepo wa jeneza.Kilaini amekemea matumizi ya msalaba katika tukio lile la simba,kumbuka msalaba ni alama katika Ukristu.

Jeneza hata mpangani analitumia.
Je ni kweli msalaba ni alama ya Ukristo Kuna andiko lolote au ni porojo tu?
 
Acha ujinga, we unaona alochokifamya ni sahihi, kwann achezee Iman za Watu. Tena wakristo wastaarabu angekumbana na waislam angechezea kichapa palepale, angejua hajui
Jeneza ni imani😁 imani ya kifo? Hutaki sanduku lako lichezewe?
 
Back
Top Bottom