Tulia Ackson: Serikali itafute utaratibu wa mpito wa kuwatazama watu wanaojitolea kwenye kada Mbalimbali ili wapewe kipaumbele kwenye ajira

Kama huna cha kuwaambia watu heri ya kukaa kimya kuliko maudhi kama haya.
 
Ni jambo jema maana kama mtu hana sifa Kwa nini umpe.nafasi ya kujitolea?

Wekeni utaratibu ambao taasisi zinazowahitaji Ili ziutumie kuwapata then nafasi ikipatikana wapewe kipaombele.

Kwanza ndio staili nzuri ya kupata Watumishi royal maana wanakuwa wanajitolea

Mwisho tabia ya kutoa Ajira za mkataba harafu mnakuja Kuajiri wapya sio sawa
 
Upuuzi mtupu, hapa tunahamisha tatizo tu Connection zitahamia kwenye kupata nafasi ya kujitolea, kama ilivyo sasa ajira bila connection haipatokani
 
Mawazo ya Mh. Spika ni mazuri. Ila je, ni utaratibu gani au upi rasmi wa Serikali wa kutoa nafasi hizo za kujitolea vijana? Na nani anaratibu? Isijekuwa ni wa kichamachama au kindugu. Zamani tuliona waliomaliza chuo au form six wanapangiwa straight na serikali[ Azimio la Musoma] vituo vya kujitolea then ndo baadaye wanapata ajira rasmi. Vitu kama hivi vimeachwa,haijulikani utaratibu gani rasmi unatumika kwenye jambo kubwa kama aliloshauri Mh. Spika.
 
Mkuu,uko sahihi.
 
Ripoti ya CAG ya upigaji wa kutisha ndio imeshapotezewa?
 
Kujitolea kitakuwa ni kichaka cha watoto wa wakubwa kupendelewa!! Labda kama hizo nafasi za kujitolea zitolewe kwa wazi kwa kushindanishwa na PSRS ihusike kwenye mchakato huo moja kwa moja! Kujitolea hakuwezi kuwa ni sifa ya kupata ajira hata kama anayejitolea ni kilaza wa kutupwa!!
 
Mwanzoni nikasoma Vibaya nikajua Utaratibu wa serikali ya Mpito...
BTW hii ishu huwa ni ngumu Sana kwa sababu unakuta Wazoefu wengi (Waliojitilea) hawana Connection nyingi kuliko fresher wanaotoka chuo watoto wa vibompa

,Watoto wa wanene unakuta wako 200 na wana rafiki zao zile za "Daddy na Rafiki yangu na yeye Hana ajira"...
Halafu unategemea wewe uliyeko kazini kujitokea utapata kweli

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…