Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Na wewe uje basiZiba kama ziba.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Mzee MAKONO hatuwezi kumsamehe:
1.Kumshika makalio mamdogo bafuni
2.Kumlaza Emma na Mamdogo darasani
3.Kula kuku yote jikoni
4.Kunya sebuleni juu ya meza, mavi mazito ya ugali wa ulezi.
Asee Kuna mama mmoja anaitwa mama shilogile Maarufu Sana hapo ziba bado yupo?Na wewe uje basi
Mura leo umeingia Cha kike muraomwitoTulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 13.
Niliamka taratibu nikajifanya kumshitua jamaa ili nione kama alikuwa akisikia,nilitaka kama angenisikia basi nimwambie naelekea chooni!,sasa kwakuwa alikuwa amelala usingizi wa pono,niliamka nikafungua mlango taratibu kisha nikairudishia!.Nilifungua mlango wa nje taratibu nikatoka nikakuta yule binti Monica akiwa nje ananisubiri!.
Monica "Yaani muda huu mlikuwa mmelala?"
Mimi "Kwani saa ngapi sasa?"
Monica "Bado mapema sana"
Sasa muda huo ninazungumza naye ilikuwa yapata mida ya saa 5 usiku,sikuwa na saa lakini kwa makadirio sisi tuliingia kulala mida ya saa 3 usiku na baada ya yeye kuja ilikuwa imepita muda kidogo!.
Sasa kwakuwa nilikuwa tayari nishakuwa na hamu na papuchi,sikutaka kabisa kuwaza umbali tutakao tembea kwenda kwao,cha msingi ni mimi kufika na kumcharaza stiki za kutosha na kurudi mapema nyumbani.Kwakuwa mpaka muda huo hapo kijijini sikuwa kabisa na demu mwingine wa kuzugia ilibidi niwe mpole tu kwa yule binti ili angalau niwe napooza njaa ya mashine!.
Basi tulianza kutembea kwa haraka huku nikiwa nimemshika kiuno kana kwamba atanitoroka!.
Monica "Mimi nakupenda sana wewe umughaka,yaani sasa hivi najikuta tu nakupenda"
Mimi "Lakini Moni mimi na wewe tunaiba tu,Ema akijua najua tutakosana"
Monica "Wewe achana nae huyo,mbona yeye anatembea na Deborah"
Monica "Huyo mjinga nitamkomesha aliniambia atanioa kumbe alitaka kupata anachokitaka kwangu halafu aniletee dharau,hanijui vizuri binti Makoye".
Aliendelea kusema "Nilikwambia leo nyumbani kuna ngoma za mwana lemi,ndo maana nimekuja kukuchukua"
Mimi "Ngoma za mwana lemi ndiyo ngoma gani?"
Monica "Wewe twende tu utaona"
Monica "Tukifika nyumbani utafanya kila nitakachokuambia lakini,sawa?"
Mimi "Sawa"
Sasa mwanaume nikadhani ile kuniambia nitafanya kila atakachosema ilikuwa ni kumbadili kila style wakati wa mizaguamuano,moyoni nilifurahi sana na nikawa nina shauku ya kufika nyumbani kwao haraka ili nikaikung'ute papuchi mpaka ichakae!.
Mimi "Mama yako yupo?"
Monica "Yupo ila atakuwa bize kwenye ngoma".
Basi tulitembea kwa dakika kadhaa tu tukawa tumekaribia nyumbani kwao,nilipata mshangao sana kwakuwa haikuwa kawaida kwasababu nyumbani kwao ilikuwa mbali sana!,sasa nikawa najiuliza au kwasababu ni usiku na hakuna kashikashi njiani ndo maana tumefika mapema?,niliwaza pia siku ile nilivyokutana na Monica pale kwenye viwanja vya mnada na namna tulivyokwenda kwao haikuchukua muda mrefu,nilidhani uenda kwasababu ilikuwa usiku hivyo kujikuta unatembea kwa haraka kwasababu hakuna jua wala nini!.
Sikuwa kabisa na mawazo uenda yule binti anaweza kufanya namna yeyote kwasababu hakuwahi kunionyesha jambo lolote baya nala kutisha mpaka nimtilie shaka,isipokuwa ni ile siku moja tu ambayo nilimuona pale lamboni akichuma yale majani ya kutengeneza majamvi ndipo kama nilishangaa namna alivyotokea mbele yangu ghafla!.Basi nikajipa moyo kwasababu alikuwa ananipenda hata kama angekuwa ni mbaya asingenifanyia ubaya mimi.
Kabla ya kwenda kuingia ndani,aliniambia nimsubiri kwanza anarudi.Aliondoka akaenda akazunguka nyuma ya nyumba yao ambako kulikuwa na shamba la mihogo akaingia ndani!.Nilimsubiri pale kwa takribani dakika 5 hivi akawa amekuja na kimfuko cha rambo kilichokuwa kimefungwa ambacho sikufahamu ndani kulikuwa na nini!.
Monica "Chuchumaa chini"
Basi nikachuchuma chini,akakifungua kila kimfuko kisha akatoa vijifuko vingi vingi vilivyokuwa vimefungwa kwa kukazwa sana!.Sikumuuliza chochote nikawa nabaki kumuangalia anataka kufanya jambo gani.
Sasa kwakuwa lilikuwa giza totoro,sikuweza kuona mle ndani ya tule tujifuko tudogo tudogo kulikuwa na kitu gani.
Monica "Kama nilivyokwambia leo hapa nyumbani kuna ngoma,nataka nikupake hii dawa ili wakati wa ngoma usije kuonekana na wacheza ngoma wanaweza kukufanya kitu kibaya na mimi nitaadhibiwa"
Basi akilini mwangu nikasema uenda alitaka kabla ya mizagamuano tukacheze ngoma ya kisukuma iliyoitwa "Mwana lemi" kama alivyokuwa ameniambia hapo awali.
Basi alianza kunipaka ile dawa usoni,miguuni na mikononi na kuna nyingine akawa amenipa ili niirambe.Baada ya lile zoezi akaniambia tuondoke twende ndani!.Safari hii wakati tunaelekea kwenye kile kinyumba cha nyasi alichokuwa akilala Monica tulizunguka kwa nyuma ambako ilibidi kukanyaga matuta ya mihogo na kuingia ndani,ile siku ya kwanza kulala hapo nakumbuka tulipitia moja kwa moja mbele ya nyumba,ila safari hii imekuwa tofauti!.
Nilipofika ndani Monica aliniambia nikae kwa kutulia na kila atakachukuwa akiniambia basi nifanye.Alinisogelea karibu akanivua nguo zote nikabaki mtupu,alipomaliza alianza na yeye kuvua nguo zote,kwakuwa mle ndani kulikuwa na giza totoro hakuna aliyemuona mwenzie kiufasaha,sasa sikujua kama yeye alikuwa akiniona ama la!,alianza kunipaka dawa ambayo sikuitambua mwili mzima na alipomaliza alinipatia mkononi na mimi akasema nimpake,sasa wakati nampaka kufika kiunoni nikakuta amevaa shanga!,nilishangaa sana siku hiyo kumuona ana shanga kiunoni kwasababu siku ile ya kwanza hakuwa na shanga kabisa!.
Basi nikaendelea kumpaka ile dawa kuzunguka mwili mzima,wakati huo abdala kichwa wazi alikuwa amesimama akionyesha kuwa na kiu ya maji ya mdimu!.
Baada ya kumaliza lile zoezi,Monica akawa amenitaka nikae kwenye godoro.
Monica "Umughaka mimi nakupenda sana na nia yangu ni kukusaidia"
Mimi "Kunisaidia na nini Moni?"
Monica "Wewe unadhani uko salama?,hivi huwa hujiulizi kwanini wewe hayakukuti?"
Mimi "Ma nini ambayo hayanikuti"
Monica "Yaani wewe nae umezidi utahira,pamoja na kukueleza tu hujiongezi!"
Aliendelea "Subiri utajionea ila naomba usije kupiga kelele,sawa?"
Mimi "Sawa"
Basi wakati tukiwa mle ndani tukiongea,ghafla nikaona miale ya moto ikitokea nje,ilionekana kuna moto ulikuwa umewashwa,Sasa Monica akanifanyia ishara ya kwamba nifunge domo langu na nisishituke!.Baada ya muda nikaanza kusikia ngoma zinapigwa kwa nguvu huku sauti za kina mama na wanaume wakiwa wanaimba kwa kisukuma.
Zile ngoma zikaanza kukolea huku nikisikia vishindo vya watu kama wakiruka na kucheza!.Sasa baada muda kupita kidogo,Monica akanifanyia ishara ya kwamba nisimame nimsogelee alipokuwa,niliposogea ndipo akaniambia nichungulie kwenye upenyo wa ule mlango wa bati!.Sasa kile kinyumba kilivyokuwa kimejengwa kilikuwa cha mviringo kama simtank(nadhani waliokulia vijijini watakuwa wanazifahamu nyumba hizo),sasa kutokana na kile kinyumba kilivyokuwa kimejengwa,mlango wa kile kinyumba hata kama ungefungwaje,kwa juu kulikuwa na uwazi mkubwa uliowezesha kuchungulia nje na kuona kwa uzuri!.
Basi nikachungulia nje nikaona moto mkubwa mno ukiwa umewashwa pale mbele ya nyumba yao Monica,pia nikawaona watu wake kwa waume wakiwa uchi kama walivyozaliwa(uchi wa mnyama)wakicheza kwa kuzunguka mduara,mpiga ngoma alikuwa mwanaume ambaye yeye alikuwa pembeni kabisa,sasa wakati wakiwa wanazunguka ule mduara huku wakiimba ngoma,nikamuona mama yake Monica naye akiwa mmoja wao,nilipoendelea kutazama vizuri nikamuona na yule mzee ambaye nimewahi kukutana naye jioni wakati natoka Senta akanisalimia kisha akaniambia nimsalimie headmaster,nilipomuuliza jina akaniambia anaitwa Makono.
Pia ni huyu huyu mzee wakati wa kikao pale shuleni baada ya lile sakata la Ema na Maza kukutwa wamelala darasani ndiye aliyekuwa akichangia na akisema mambo ya ushirikina hayakuwepo hapo Kjijini.
Nikabaki nimekodoa macho na nikawa kimya kabisa,sasa baada ya zile ngoma kupigwa kwa sana na wao kuuzunguka ule moto,ghafla kuna mzee akapiga kelele kwa kisukuma akisema "Bhebheeeeeeee",kisha mpiga ngoma akaacha kupiga ile ngoma na watu wote wakasimama.
Watu wanadharau sana[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]! Ile meza sidhani kama walipata ujasiri wa kutenga chakula na kula kwa amani [emoji1787]
Acha uvivu, kama story hii inakushinda kusoma utaweza kusoma mikataba ya kazi/biashara na kuielewa!?Wekeni samari
Ngoja wataalam wa mambo watatupa experience yaoSina uzoefu huo[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Hili neno "KUDINYWA" sijalisikia likitamkwa zaidi ya kule kwetu Mbeya!Evelyn Salt Pole weeeee..... unaenda kudinywa kwenye kakibanda ka Monica
Kuna vitu ukinahakikishia nitakuja chap.Na wewe uje basi
Mnadinyana kwenye mashamba ya nguniani, mkitoka mnaenda kula migagiHili neno "KUDINYWA" sijalisikia likitamkwa zaidi ya kule kwetu Mbeya!
Mswahili mpe tu heading vingine atajazia yeyeFungua Uzi Basi nasi tuburudike na maisha.