Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Sijui jamaa katusahau!!?
Ushauri: -
Akijitokeza msimuliaji mwingine ambaye anataka kusimulia stori yake, basi aiandike pembeni yote, ndipo ailete hapa. Akifanya hivyo, atakuwa amewasaidia wasomaji kuokoa muda, kwa namna fulani. Binafsi, kila baada ya muda fulani, nashika simu na kuutafuta uzi huu, na kuchungulia kama kuna kipya kilichoongezwa! Yaani, hata shughuri zangu zinaathirika!
Unataka mtu afanye kulingana na will yako mkuu. Huwezi jizuia kwani ukisoma story ukaimaliza unadhani itakuongezea Nini. Umeshasoma story ngapi na Nini ulichoongezeka ama kuongezeka kwa maisha yako.
Sasa umeona kichwa chako kinakuendesha kinataka Raha ivyo ivyo kwa mafanikio kifanye kila wakati usome hata kitabu ujue Tiba za miti inayotuzunguka. Umeona hapa kichwa hakitaki kabisa. Sasa Raha unadhani inakuongezea.
Delay instant gratification
 
Nahisi sasa inaelekea ukingoni hii story maana star yaani UMUGHAKA na Monica sasa wameiva na kuwa mchuzi mix.

Mchawi mzee makono nae kalianzisha na Umughaka huku Monica kwa usaidizi wa mama yake ambae pia anampenda kijana Umughaka mpenzi wa mwanae ameahidi kumsaidia na kumlinda.

Kinachoenda kumkuta mzee Makono hatokaa akisahau, mark my words. Huyu mzee Makono kawasumbua sana kwa mwalimu mkuu kwani kuna mtoto wake anakitaka au anatoka na ki Monica halafu Ema akaingilia akaning'inizwa. Kisha UMUGHAKA nae kaingilia kashikishwa kalio la mama mdogo. Sasa Monica kaingia mzimamzima kupambana na mzee Makono[emoji1787]. Tusubiri na tushudie hadi mwisho.

Huu ni uchambuzi wa yaliyopita na yajayo
Nami nahisi Debora ambaye aligombana na Monica kisa Emma ndiye mtoto wa mzee makono[emoji23][emoji23]
 
Wapo wanaosema chai japo kwangu Mimi iwe au isiwe nilipenda tangu nisome tu jina la simulizi!
Huko duniani tunakofahamiana yupo jamaa anaitwa George Iron Mosenya yule bwana kwangu mimi ndio bingwa wa simulizi kwa kizazi hiki na nikiwa naisoma hii nakumbuka simulizi yake moja inakwenda kwa jina la MAMAAKE MAMA
IPO wapi mkuu Mimi sikuimaliza huwa naitafuta Sana
 
Ndugu zangu nisameheni sana leo nilikuwa kwenye matatizo ya kifamilia.

Nilienda huku bunju ambako nafanyia shughuli zangu kama kawaida,sasa nikiwa huko nikapigiwa simu na mke wa brother kwamba kuna mgogoro wa kifamilia,sasa nimefika pale nikakuta kuna kashikashi la kufa mtu lilipolekea mimi na brother kutwangana makonde hasa!.

Sasa kwa hasira nilizokuwa nazo nimejikuta hata kuendesha pikipiki kwa umakini nashindwa ikapelekea kupata ajali,ingawa sijaumia sana ila nimepata vimichubuko vya hapa na pale ila pikipiki imeumia!.

Hivyo mniwie radhi ndugu zangu leo imekuwa siku mbaya sana kwangu!.
Ntarudi
 
[emoji1483][emoji1483]
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 14.




Kila mcheza ngoma alisimama ghafla na kumtizama yule mzee ambaye ilionekana kabisa alikuwa kiongozi wao.Baada ya hapo alinyoosha mkono juu akiwa ameshika usinga(mkia wa mnyama)ambao sikuweza kufahamu ulikuwa wa mnyama pori au mnyama wa kufugwa!.

Alipoteremsha mkono chini niliona watu wote wameweka mikono mbele kuonyesha unyenyekevu huku vichwa vikitazama chini.Sasa yule mzee alianza kuongea kwa sauti kubwa mno!.

Mzee alisema "Ng'wana Charles"

Aliendelea "Ng'wana ndekeja"

Baada ya kusema hivyo nikaona ananyoosha usinga kuwapa ishara hao aliowaita wasogee mbele,sasa nikaona wazee wawili wamesogea mbele huku wakiwa wameinamisha nyuso chini na mikono imewekwa mbele kuashiria unyenyekevu wa hali ya juu!.

Mzee akasema "Ng'wenagi umnho ng'wenuyo aha"

Basi wale wazee waliondoka na kuingia kwenye ile nyumba ya mama yake Monica,hawakuchukua muda wakawa wametoka ndani huku wakiwa wamembeba mtu ambaye sikumuona kwa haraka,sasa baada ya kumfikisha yule mtu na kumbwaga pale kando ya ule moto ndipo nikamuona vizuri nikawa nimemtambua!,alikuwa ni mzee ambaye alijinasibu ni mganga aliyekuja pale nyumbani kuweka zindiko na kutupiga chale za kutosha!.

Basi yule mzee ambaye ilionekana ndiye mkubwa pale akawa toa amri tena ya kuanza kupiga ngoma na kucheza!,sasa wakati wanacheza kwa kuzunguka ule moto,akajitokeza mama mmoja ambaye alikuwa amejifunga shanga kiunoni na kiremba cheusi kichwani huku mkononi akiwa ameshika kisu!,sasa akamsogelea yule mzee ambaye alikuwa akishanga shangaa kama tahira pale chini,yule mama akafika akamkamata kichwa akaanza kumyoa nywele!.

Wakati mambo yote hayo yanaendelea,mimi na Monica tupo tunachungulia kwenye ule upenyo wa mlango na Monica alinizuia kabisa kutopiga kelele!.

Sasa baada ya lile tukio la kumnyoa yule mzee nywele kukamilika,yule mama alichukua zile nywele akaziweka kwenye kitu kama sahani halafu akamkabidhi yule ambaye alionekana ni kiongozi,sasa wakati anamkabidhi kama kawaida uso uliinama chini kuashiria unyenyekevu!.Baada ya hapo yule mama akaanza kumvua yule mzee nguo zake zote!,alipomaliza aliinama chini kwenye akachukua vitu ambavyo sikuvifahamu akaanza kumpaka yule mzee!.Baada ya kumaliza lile tukio la kumpaka yule mzee vitu visisvyo julikana,akaondoka kinyume nyume kurudi kwenye mstari kuuungana na wenzie kuendelea kucheza ngoma.

Sasa haukupita muda yule mzee tena akatoa ishara ile ngoma ikasitishwa!,baada ya hapo ilikuwa kitendo cha kufumba na kufumbua wakawa wametoweka pale kwenye lile eneo na ghafla kukawa na giza kuu!,nilitaka kufahamu kiliendelea nini na hivyo ikabidi nimuulize Monica.

Mimi "Mbona hawaonekani?"

Monica "Unataka nikupeleke walipoelekea?"

Mimi "Hapana"

Monica "Nakupenda wewe sana ndiyo maana nimekuleta ujionee mwenyewe"

Monica "Mimi nitakulinda wala usiogope"

Aliendelea kusema "Wameelekea kwenye sherehe za kula nyama"

Monica "Ile miembe miwili mikubwa ya kwenye ile njia ambayo tumekutana si unaikumbuka?"

Mimi "Ndiyo"

Monica "Ndo wako hapo"

Mimi "Sasa hapa wameondokaje?"

Monica "wewe bado mdogo ukikuwa utaacha kuuliza uliza maswali"

Sasa nilikuwa nashangaa binti anayeniambia mimi mdogo nabaki kumshangaa kwasababu ulikuwa ukiniangalia mimi na yeye utajua kabisa yeye ndiye mdogo!.

Monica "Halafu wewe una mizimu mikali sana ndiyo maana nataka uwe mume wangu"

Mimi "Mizimu mikali?,mizimu mikali kivipi?"

Monica "Umekuwa ukiwasumbua sana wanapokuwa wakila nyama zao"

Nikashituka sana nikabaki nashangaa mle ndani ambako mpaka muda huo kulikuwa na giza totoro!.

Monica "Unakumbuka siku unapita pale kwenye miembe usiku uliona nini?"

Mimi "Nakumbuka kuna siku nilikuwa natoka senta kuangalia mpira nikaona moto unawaka kwenye ile miembe"

Monica "Achana na mambo ya moto,wewe hukuwahi kuona mtu pale?"

Aisee,sasa nikawa najiuliza huyu binti matukio yote hayo yeye alionaje?,kiukweli nilianza kuingia uoga ila akawa ananisihi ya kwamba nisiogope na yeye yupo kwa ajili ya kunisaidia!.

Monica "Yule mtu uliyemuona siku ile aliliwa nyama,sasa wewe umekuwa ukiwasumbua kupita ile njia kwasababu hakuna mtu anayepita ile njia usiku kama ule".

Aliendelea kusema "Kwa ujasiri ulionao waliona wakujaribu kuona kama unawaona na ndiyo maana walikutega na kukutisha na ulivyotishika na kukimbia wakaona kumbe huna lolote"

Mimi "Sasa nawatesaje?"

Monica "Pale kwenu ni wewe ndiye ambaye huwezekaniki na sijui kwanini,wewe unanyota nzuri mno"

Mimi "Yule mganga amefanya kosa gani"

Monica "Yule ni mjeuri,anaenda kuliwa nyama".


Akaendelea kusema "Kuna siku mama yangu alienda kusenya kuni na mlikutana njiani ukamsaidia zile kuni,hivyo mama yangu akakupenda sana"

Mimi "Mbona sikumbuki siku ambayo nimebeba kuni za mama yako?"

Monica "Wewe bado mtoto mdogo nimekwambia acha maswali utaelewa tu".


Kiukweli nilikuwa ninawaza na kujiuliza sana lakini nakosa majibu!,ndipo sasa nikajua uenda matukio mengi pale nyumbani yalikuwa yanasababishwa na hilo kosi hatari lilikuwa likicheza ngoma,sikutaka kumwambia mama yake ni mchawi ingawa nilimshuhudia kwa macho yangu,nilidhani uenda ningemwambia kuhusu mama yake angenibadirikia mle ndani na nikaipata freshi,sikutaka kabisa kutengeneza matatizo!.

Baada ya maongezi ya muda mrefu mizagamuano ikachukua nafasi!,sasa nikawa nimemwambia Monica inapaswa baada ya mizagamuano ikifika saa 10 usiku anisindikize kurudi nyumbani ili asije akajua mtu yeyote kwamba nilitoka usiku.

Monica "Nalekotogwa natokoreka"

Mimi "Ndiyo nini?"

Monica "Wewe naye,utajifunza lini kisukuma!"

Monica "Nakwambia nakupenda na sitokuacha"

Basi sikutaka kumjibu na mimi akili yangu haikuwa kwake kabisa,kilichokuwa kinanipeleka kwake ni kumpatia maji ya uzima wa milele abdala kichwa wazi ili asihangaike na kiu.
Basi baada ya kasi ya mizagamuano ni kama Monica alipitiwa na usingizi,mimi sikuweza kabisa kupata usingizi kwasababu ya kile nilichokuwa nimetoka kukishuhudia pale!.

Sasa baada ya muda kupita nikiwa natafakari huku usingizi ukianza kunipitia,ghafla nikasikia kishindo kikubwa nyuma ya ile nyumba tulimolala!,sasa nikajaribu kupeleka mkono ili nimpapase Monica ashituke ili na yeye asikie lakini hakukuwa na mtu kwenye godoro!.

Nilikurupuka nikaanza kupiga kelele za uoga kama mwehu!
[emoji1483]
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 16.




Wakati tunaondoka Monica alikuwa amechukia sana na haikuwa kawaida yake,niliwaza sana itakuwaje maana niliona Ema ameondoka kwa hasira kuelekea nyumbani baada ya mimi kufika pale!.Basi nilikuwa mpole huku binti wa watu akiniongoza kuelekea nisikokufahamu.

Mimi "Tunaelekea wapi?"

Monica "Wewe twende acha hayo maswali yako".

Mimi "Lakini si tunawahi kurudi?"

Baada ya kuona maswali yamekuwa mengi,Monica alisimama akawa ananisukuma sukuma kwa mkono akiniambia "Hivi lini utafunguka hayo macho yako?,hivi wewe unajiona upo kawaida?"

Monica "Huku nimekuja kwa ajili yako,kama unataka hurudi kwenu wewe rudi lakini kitakachokukuta utajua mwenyewe!"

Mimi "kwani kuna nini Moni?"

Monica "Yaani unataka kuwa tahira kama huyo ndugu yako"

Aliendelea "Nishakwambia kila kitu tangu jana kwamba nitakulinda usiku na mchana lakini unajitoa ufahamu!"

Monica "Kama unanipenda na unaniamini twende,lakini kama huniamini rudi kwenu,njia hiyooo nyeupe".

Monica alikuwa mkali sana baada ya kuona kama namchosha kwa maswali ambayo yeye aliamini kabisa majibu yake uenda nikawa nayafahamu,sikuwa na namna ikabidi nijifanye kondoo niongozane nae kusikofahamika.

Mimi "Mbona jamaa alikuwa amekasirika?"

Monica "Achana nae mjinga yule,itakula kwake"

Monica "Mimi leo nimemueleza ukweli kwamba wewe ni mpenzi wangu"

Mimi " Siulisema lakini iwe siri Moni?"

Monica "Nimefika pale kwa mambo mengine kabisa,sasa yeye akaanza kuleta mambo yake ya niache kumsumbua,mimi nikamwambia sijaja hapa kwa sababu hiyo,kilichonileta sicho unachofikiria,na kama ni mapenzi kwasasa mpenzi wangu ni umughaka siyo wewe"

Aliendelea "Basi ndiyo kama ulivyotukuta,alipokuona akasema niongee na wewe na kwa hasira akaondoka,sasa mimi ulitaka nifanyeje?".

Mimi "Ninavyo mjua yule,hatutaongea mwaka mzima".

Monica "Nimekwambia achana nae,utakipata".

Basi tulitembea kwa muda mrefu kidogo huku tukiendelea kupiga stori za hapa na pale,yule binti Monica kiukweli mpaka wakati huo nilikuwa nampenda sana toka ndani ya moyo wangu!,na alikuwaga jasiri sana asiyeogopa chochote!.Sasa kwakuwa alikuwa amenihakikishia ulinzi kama mpenzi wake,sikuwa na hofu kama angeweza kunifanyia jambo lolote!.

Baada ya safari ya dakika kadhaa,tuliiacha njia na kuingia kwenye shamba moja kubwa la mihogo,tulitembea mle kwenye lile shamba kwa takribani dakika 2 tukawa tumefika kwenye mji mmoja ambao ulikuwa umezungukwa na mashamba ya mihogo,sasa baada ya kufika pale ghafla nikawaona wanawake watatu ambao kwa haraka haraka sikuweza kuwatambua kwakuwa walikuwa kwa mbali kidogo!.Monica aliniambia nisubiri hapo pembeni na yeye akawa amewafuata wale kinamama na kuanza kuzungumza nao kisukuma.

Sasa ghafla nikaona wale kina mama wananikimbilia na walipofika wakawa wamenishika kwa kunitaka nifanye haraka nisogee walipokuwepo wao.Basi wakamwambia Monica kwa kisukuma kwamba aingie ndani na alete jamvi ili nikalie.Sasa wale kina mama nikawa nimewatambua baada ya kuwa nimewaona kwa karibu,mmoja alikuwa mama yake Monica,na wale wawili walikuwa wale kina mama ambao nilionana nao njiani wakati natoka kuchukua miwa kwa mzee masumbuko ile Asubuhi,kumbuka hao wote akiwamo na mama yake Monica walikuwa ni miongoni mwa watu waliokuwa wakicheza ngoma ule usiku pale kwao Monica.

Sikuelewa kwa nini Monica alinipeleka pale na sikufahamu ni kitu gani kilikuwa kikiendelea!.Baada ya lile jamvi kuletwa na kuwekwa chini,mama yake Monica akaniambia nisimame na nivue nguo zangu zote nibaki kama nilivyozaliwa!.Basi ikabidi nifanye kama alivyoniambia.

Sasa baada ya kumaliza kuvua nguo,akaniambia nikae pale katikati ya jamvi;Mama mmoja kati ya wale niliokutana nao ile asubuhi nikaona anachukua maji kwenye chungu akawa anakunywa kwa kupiga fundo kisha ananitemea,alinitemea yale maji mwili mzima mpaka yalipomalizika kwenye kile chungu!.Baada ya hilo zoezi la kutemewa maji walinizunguka wote wale kina mama akiwemo mama Monica wakaanza kunipaka vitu ambavyo sikuelewa ilikuwa ni kitu gani,harufu yake haikuwa nzuri kiukweli na nilibaki kushangaa tu!.

Waliendelea kunipaka kwa haraka na walipomaliza,mama mmoja akaniambia nisimame.Sasa baada ya kusimama yule,yule yule mama ambaye ndiye alikuwa akinitemea yale maji,niliona mkononi ameshika kitu kama usinga wa mnyama na akaanza kuchovya ule usinga kwenye chungu kiingine kilichokuwa pembeni akawa kama ananichapa na ule usinga uliojaa yale maji aliyokuwa akichovya kwenye kile chungu.
Wakati anaendelea kunitandika na ule usinga alikuwa akinuia kwa kisukuma.

Sasa baada ya lile zoezi la kuchapwa na usinga,mama yake Monica alimwambia binti yake aingie ndani awashe kibatari alete,baada ya kuletwa kile kibatari kukawa angalau na mwanga pale nje,sasa mama yake Monica akanisogeza kwa pembeni kulipokuwa na jiwe lilikuwa lichongwa kama kigoda akaniambia nikae.(Lile jiwe nadhani ni yale mawe ambayo huwa wanasagia nafaka kama mtama,udaga, na ulezi,lilikuwa ni jiwe fulani ambalo lilikuwa limekaa kama bakuri).

Basi baada ya kukaa hapo akaanza kunichanja kwa kisu kilichokuwa kikali mithili ya wembe,amenipiga chale za kutosha karibia mwili mzima.Baada ya kumaliza lile zoezi nikatakiwa nikae kwanza uchi ili niendelee kukauka kisha ndipo nikatakiwa kuvaa nguo.Sasa baada ya kuwa nimemaliza kuvaa nguo ndipo mama yake na Monica na wale kina mama wakaanza kuzungumza na mimi,kile kitendo kilikuwa ni kitendo cha haraka sana ambacho hakikuchukua hata saa nzima!.

Mama Monica "Mkwe wangu hujambo mwanangu"

Mimi "Sijambo mama,shikamoo"

Mama Monica "Maraba mwanangu"

Mama Monica "Baba huu ulimwengu una watu wabaya sana,lazima tukulinde mwanangu".

Basi mimi nikawa nimetulia tu sikusema jambo lolote,mama yake Monica akaanza kuongea na mwanaye kisukuma na nadhani alimwambia aniambie kilichokuwa kinaendelea!.

Monica "Umughaka dhumuni la mimi kukuleta huku kama nilivyokwambia ni kukulinda mpenzi wangu,sitaki baya lolote likukute kwasababu nakupenda na wewe ndiye mama yangu anataka unioe!"

Aliendelea "Unakumbuka kile kishindo cha jana kilichofanya mpaka ukakimbia?"

Mimi "Ndiyo,nakumbuka!"

Monica "Basi yule mtu alikuwa ametumwa na baba yake ili waje kukuchukua,ndipo nikamuwahi kupambana nae kabla hajaleta madhara,sasa aliponizidi nguvu nilimuita mama yangu akaja kunisaidia na akawa ameondoka naye"

Aliendelea "Sasa lile jambo limeleta shida kwa huyo mshirika mwenzao na mama na kuna vita inaendelea"

Kiukweli nilikuwa nimekodoa macho huku nikiendelea kusikiliza kinaga ubaga ile stori ya Monica ambayo nilikuwa hata siifahamu.

Monica "Kuna mzee mmoja ambaye naye jana alikuwa akicheza ngoma na hutoweza kumfahamu,sasa yule mzee kumbe wakati wakiwa kule miembeni alimuagiza mwanaye aje akuchukue akupeleke kwake wakakufanyie michezo yao".

Aliendelea kusema "Sasa baada ya yule mzee kuona mwanaye amedhibitiwa alikasirika sana na mama anasema walikaa kikao wakamtaka atoe sadaka kwa kufanya lile jambo kwa mshirika mwenzie".

Monica "Sasa yule mzee alisema kwa wenzie kwamba anataka aisambaratishe nyumba ya mwalimu na lazima awapeleke mbele ya kamati iliyomuagiza sadaka nyinyi nyoote ingawaje alitumwa mtu mmoja tu kama fidia"

Sasa baada ya kusema yale maneno nilishituka sana na ndipo akili yangu ikafunguka kwa haraka sana!,kwa haraka nikamuwaza uenda atakuwa ni mzee makono kwasababu ndiye niliyekutana naye akawa amenipa vitisho vingi kuhusu tulichomfanyia mwanaye!,pia nikajua uenda atakuwa ndiye maana usiku nae alikuwa miongoni mwa wacheza ngoma pale kwao Monica!.

Mimi "Kuna mzee mmoja anaitwa Makono,je mama mnamfahamu?"

Baada ya kuuliza vile lile swali wakashituka sana na mama yake Monica akaniambia "Unamjua mzee Makono?"

Mimi "Ndiyo mama"

Mama yake Monica "Ndiyo huyo huyo anataka kukutoa sadaka mwanangu,sitakubali!"

Basi wakaanza kuzungumza kwa kisukuma huku wakionekana kusikitika!.

Mimi "wakati natoka senta nimekutana naye jioni akanitisha sana kuhusu mwanae"

Mama Monica "Ndiyo maana tumekuleta hapa maanangu tukutengeneze vizuri,huyo makono ni mtoto mdogo sana kwetu,nitamshughulikia".

Basi kwakuwa hali haikuwa nzuri siku hiyo kutokana na Makono na genge lake kupanga kwenda kufanya uhalifu wa kichawi pale nyumbani,mama yake Monica na wale kina mama wakaniambia leo sipaswi kabisa kukanyaga pale nyumbani na nitalala hapo kwa hao kina mama mpaka asubuhi!.

Mimi "Je sitaonekana"

Mama Monica "Baba hapa ni kiboko,hakuna wa kukanyaga hapa"

Aliendelea "Tumekupika na hakuna wa kukusogelea na hata wakija hakuna wa kukuona,ondoa shaka mwanangu"

Mama Monica "Huyu huyu makono tuliyemfundisha kazi anataka kuniulia mwanangu na mkwe wangu?,atanijua mimi ni nani,nitamuaibisha mpaka atajuta"
Umughaka mwisho upewe mikoba
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 16.




Wakati tunaondoka Monica alikuwa amechukia sana na haikuwa kawaida yake,niliwaza sana itakuwaje maana niliona Ema ameondoka kwa hasira kuelekea nyumbani baada ya mimi kufika pale!.Basi nilikuwa mpole huku binti wa watu akiniongoza kuelekea nisikokufahamu.

Mimi "Tunaelekea wapi?"

Monica "Wewe twende acha hayo maswali yako".

Mimi "Lakini si tunawahi kurudi?"

Baada ya kuona maswali yamekuwa mengi,Monica alisimama akawa ananisukuma sukuma kwa mkono akiniambia "Hivi lini utafunguka hayo macho yako?,hivi wewe unajiona upo kawaida?"

Monica "Huku nimekuja kwa ajili yako,kama unataka hurudi kwenu wewe rudi lakini kitakachokukuta utajua mwenyewe!"

Mimi "kwani kuna nini Moni?"

Monica "Yaani unataka kuwa tahira kama huyo ndugu yako"

Aliendelea "Nishakwambia kila kitu tangu jana kwamba nitakulinda usiku na mchana lakini unajitoa ufahamu!"

Monica "Kama unanipenda na unaniamini twende,lakini kama huniamini rudi kwenu,njia hiyooo nyeupe".

Monica alikuwa mkali sana baada ya kuona kama namchosha kwa maswali ambayo yeye aliamini kabisa majibu yake uenda nikawa nayafahamu,sikuwa na namna ikabidi nijifanye kondoo niongozane nae kusikofahamika.

Mimi "Mbona jamaa alikuwa amekasirika?"

Monica "Achana nae mjinga yule,itakula kwake"

Monica "Mimi leo nimemueleza ukweli kwamba wewe ni mpenzi wangu"

Mimi " Siulisema lakini iwe siri Moni?"

Monica "Nimefika pale kwa mambo mengine kabisa,sasa yeye akaanza kuleta mambo yake ya niache kumsumbua,mimi nikamwambia sijaja hapa kwa sababu hiyo,kilichonileta sicho unachofikiria,na kama ni mapenzi kwasasa mpenzi wangu ni umughaka siyo wewe"

Aliendelea "Basi ndiyo kama ulivyotukuta,alipokuona akasema niongee na wewe na kwa hasira akaondoka,sasa mimi ulitaka nifanyeje?".

Mimi "Ninavyo mjua yule,hatutaongea mwaka mzima".

Monica "Nimekwambia achana nae,utakipata".

Basi tulitembea kwa muda mrefu kidogo huku tukiendelea kupiga stori za hapa na pale,yule binti Monica kiukweli mpaka wakati huo nilikuwa nampenda sana toka ndani ya moyo wangu!,na alikuwaga jasiri sana asiyeogopa chochote!.Sasa kwakuwa alikuwa amenihakikishia ulinzi kama mpenzi wake,sikuwa na hofu kama angeweza kunifanyia jambo lolote!.

Baada ya safari ya dakika kadhaa,tuliiacha njia na kuingia kwenye shamba moja kubwa la mihogo,tulitembea mle kwenye lile shamba kwa takribani dakika 2 tukawa tumefika kwenye mji mmoja ambao ulikuwa umezungukwa na mashamba ya mihogo,sasa baada ya kufika pale ghafla nikawaona wanawake watatu ambao kwa haraka haraka sikuweza kuwatambua kwakuwa walikuwa kwa mbali kidogo!.Monica aliniambia nisubiri hapo pembeni na yeye akawa amewafuata wale kinamama na kuanza kuzungumza nao kisukuma.

Sasa ghafla nikaona wale kina mama wananikimbilia na walipofika wakawa wamenishika kwa kunitaka nifanye haraka nisogee walipokuwepo wao.Basi wakamwambia Monica kwa kisukuma kwamba aingie ndani na alete jamvi ili nikalie.Sasa wale kina mama nikawa nimewatambua baada ya kuwa nimewaona kwa karibu,mmoja alikuwa mama yake Monica,na wale wawili walikuwa wale kina mama ambao nilionana nao njiani wakati natoka kuchukua miwa kwa mzee masumbuko ile Asubuhi,kumbuka hao wote akiwamo na mama yake Monica walikuwa ni miongoni mwa watu waliokuwa wakicheza ngoma ule usiku pale kwao Monica.

Sikuelewa kwa nini Monica alinipeleka pale na sikufahamu ni kitu gani kilikuwa kikiendelea!.Baada ya lile jamvi kuletwa na kuwekwa chini,mama yake Monica akaniambia nisimame na nivue nguo zangu zote nibaki kama nilivyozaliwa!.Basi ikabidi nifanye kama alivyoniambia.

Sasa baada ya kumaliza kuvua nguo,akaniambia nikae pale katikati ya jamvi;Mama mmoja kati ya wale niliokutana nao ile asubuhi nikaona anachukua maji kwenye chungu akawa anakunywa kwa kupiga fundo kisha ananitemea,alinitemea yale maji mwili mzima mpaka yalipomalizika kwenye kile chungu!.Baada ya hilo zoezi la kutemewa maji walinizunguka wote wale kina mama akiwemo mama Monica wakaanza kunipaka vitu ambavyo sikuelewa ilikuwa ni kitu gani,harufu yake haikuwa nzuri kiukweli na nilibaki kushangaa tu!.

Waliendelea kunipaka kwa haraka na walipomaliza,mama mmoja akaniambia nisimame.Sasa baada ya kusimama yule,yule yule mama ambaye ndiye alikuwa akinitemea yale maji,niliona mkononi ameshika kitu kama usinga wa mnyama na akaanza kuchovya ule usinga kwenye chungu kiingine kilichokuwa pembeni akawa kama ananichapa na ule usinga uliojaa yale maji aliyokuwa akichovya kwenye kile chungu.
Wakati anaendelea kunitandika na ule usinga alikuwa akinuia kwa kisukuma.

Sasa baada ya lile zoezi la kuchapwa na usinga,mama yake Monica alimwambia binti yake aingie ndani awashe kibatari alete,baada ya kuletwa kile kibatari kukawa angalau na mwanga pale nje,sasa mama yake Monica akanisogeza kwa pembeni kulipokuwa na jiwe lilikuwa lichongwa kama kigoda akaniambia nikae.(Lile jiwe nadhani ni yale mawe ambayo huwa wanasagia nafaka kama mtama,udaga, na ulezi,lilikuwa ni jiwe fulani ambalo lilikuwa limekaa kama bakuri).

Basi baada ya kukaa hapo akaanza kunichanja kwa kisu kilichokuwa kikali mithili ya wembe,amenipiga chale za kutosha karibia mwili mzima.Baada ya kumaliza lile zoezi nikatakiwa nikae kwanza uchi ili niendelee kukauka kisha ndipo nikatakiwa kuvaa nguo.Sasa baada ya kuwa nimemaliza kuvaa nguo ndipo mama yake na Monica na wale kina mama wakaanza kuzungumza na mimi,kile kitendo kilikuwa ni kitendo cha haraka sana ambacho hakikuchukua hata saa nzima!.

Mama Monica "Mkwe wangu hujambo mwanangu"

Mimi "Sijambo mama,shikamoo"

Mama Monica "Maraba mwanangu"

Mama Monica "Baba huu ulimwengu una watu wabaya sana,lazima tukulinde mwanangu".

Basi mimi nikawa nimetulia tu sikusema jambo lolote,mama yake Monica akaanza kuongea na mwanaye kisukuma na nadhani alimwambia aniambie kilichokuwa kinaendelea!.

Monica "Umughaka dhumuni la mimi kukuleta huku kama nilivyokwambia ni kukulinda mpenzi wangu,sitaki baya lolote likukute kwasababu nakupenda na wewe ndiye mama yangu anataka unioe!"

Aliendelea "Unakumbuka kile kishindo cha jana kilichofanya mpaka ukakimbia?"

Mimi "Ndiyo,nakumbuka!"

Monica "Basi yule mtu alikuwa ametumwa na baba yake ili waje kukuchukua,ndipo nikamuwahi kupambana nae kabla hajaleta madhara,sasa aliponizidi nguvu nilimuita mama yangu akaja kunisaidia na akawa ameondoka naye"

Aliendelea "Sasa lile jambo limeleta shida kwa huyo mshirika mwenzao na mama na kuna vita inaendelea"

Kiukweli nilikuwa nimekodoa macho huku nikiendelea kusikiliza kinaga ubaga ile stori ya Monica ambayo nilikuwa hata siifahamu.

Monica "Kuna mzee mmoja ambaye naye jana alikuwa akicheza ngoma na hutoweza kumfahamu,sasa yule mzee kumbe wakati wakiwa kule miembeni alimuagiza mwanaye aje akuchukue akupeleke kwake wakakufanyie michezo yao".

Aliendelea kusema "Sasa baada ya yule mzee kuona mwanaye amedhibitiwa alikasirika sana na mama anasema walikaa kikao wakamtaka atoe sadaka kwa kufanya lile jambo kwa mshirika mwenzie".

Monica "Sasa yule mzee alisema kwa wenzie kwamba anataka aisambaratishe nyumba ya mwalimu na lazima awapeleke mbele ya kamati iliyomuagiza sadaka nyinyi nyoote ingawaje alitumwa mtu mmoja tu kama fidia"

Sasa baada ya kusema yale maneno nilishituka sana na ndipo akili yangu ikafunguka kwa haraka sana!,kwa haraka nikamuwaza uenda atakuwa ni mzee makono kwasababu ndiye niliyekutana naye akawa amenipa vitisho vingi kuhusu tulichomfanyia mwanaye!,pia nikajua uenda atakuwa ndiye maana usiku nae alikuwa miongoni mwa wacheza ngoma pale kwao Monica!.

Mimi "Kuna mzee mmoja anaitwa Makono,je mama mnamfahamu?"

Baada ya kuuliza vile lile swali wakashituka sana na mama yake Monica akaniambia "Unamjua mzee Makono?"

Mimi "Ndiyo mama"

Mama yake Monica "Ndiyo huyo huyo anataka kukutoa sadaka mwanangu,sitakubali!"

Basi wakaanza kuzungumza kwa kisukuma huku wakionekana kusikitika!.

Mimi "wakati natoka senta nimekutana naye jioni akanitisha sana kuhusu mwanae"

Mama Monica "Ndiyo maana tumekuleta hapa maanangu tukutengeneze vizuri,huyo makono ni mtoto mdogo sana kwetu,nitamshughulikia".

Basi kwakuwa hali haikuwa nzuri siku hiyo kutokana na Makono na genge lake kupanga kwenda kufanya uhalifu wa kichawi pale nyumbani,mama yake Monica na wale kina mama wakaniambia leo sipaswi kabisa kukanyaga pale nyumbani na nitalala hapo kwa hao kina mama mpaka asubuhi!.

Mimi "Je sitaonekana"

Mama Monica "Baba hapa ni kiboko,hakuna wa kukanyaga hapa"

Aliendelea "Tumekupika na hakuna wa kukusogelea na hata wakija hakuna wa kukuona,ondoa shaka mwanangu"

Mama Monica "Huyu huyu makono tuliyemfundisha kazi anataka kuniulia mwanangu na mkwe wangu?,atanijua mimi ni nani,nitamuaibisha mpaka atajuta"
Asante kiongozi
 
Back
Top Bottom