Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Ila hii story ni uongo mtupu, kuna mtoto wa kike atajiamini kutembea usiku ivo?, na anatokaje nyumbani kwao bila wazazi kuskia?

Watoto wa mjini mtajulia wapi mambo ya bush...
 
Hapo pa kupigwa viboko assembly na wewe si mwanafunzi utunzi wako haujaenda sawa. HAIWEZEKANI. unapotunga jaribu kuwa makini sana ili usitoke sana mbali ya Uhalisia. Haijawahi tokea kosa la nyumbani mtu akaadhibiwe Shuleni tena si mwanafunzi. Hapo uwe makini.
Mimi imenitokea
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 22.




Baada ya kufika senta niliendelea na biashara yangu ya uuzaji wa miwa kama kawaida!,sasa ilipofika jioni muda ambao wanafunzi walikuwa wametoka shule,nilimuona Mwise siku hiyo tena akiwa na marafiki zake wakiwa wanakuja hapo senta,safari hii sikutaka kabisa mazoea na mtoto wa mtu,niliamua kuuchuna na sikuwa na shobo nae kabisa!.Sasa yeye alidhani uenda ningemuita ila mwanaune niliamua kula buyu la hatari!,alikuwa anajiangalisha kwangu lakini kila nikimcheki kwa jicho la kuibia najifanya kupiga stori na jamaa yangu aliyekuwa akiuza kata mbuga.

Walipo maliza kufanya kilichokuwa kimewapeleka hapo senta waliondoka huku mimi nikijifanya niko bize kipiga stori na jamaa lakini kiukweli moyo wangu ulikuwa unauma sana!.Siku hiyo mama mdogo hakuka kabisa hapo senta na sikufahamu sababu ni nini!.

Ilipofika jioni mida ya saa 12 nilirudisha ile miwa iliyokuwa imebaki kwa yule mama na mimi kuianza safari ya kurejea nyumbani.Nilifika nyumbani mida ya saa 1 usiku kuelekea saa 2,niliingia jikoni nikachukua dumu la maji nikaondoka zangu kuelekea lamboni kuchota maji ili nije kuoga nijiweke safi kwasababu Monica alikuwa ameniambia angekuja kunichukua!.

Sasa wakati napandisha nyumbani nikakutana na Ema akiwa bado amevaa nguo za shule akiwa na Deborah,mimi napandisha na wao wakiteremsha!.

Deborah "Mambo umughaka"

Mimi "Poa,vp?"

Deborah "poa!,aya baadae!"

Nilipata mashaka kidogo kwasababu haikuwaga tabia ya Deborah nikionana nae kuacha kupiga stori na mimi,sikuumiza kichwa sana maana niliamini mpumbavu Ema atakuwa amenikandia sana kwa demu wake!,kwasababu hata wakati Deborah ananisalimia jamaa alikuwa anajitembeza taratibu huku akinikaushia!.Basi nilibeba zangu dumu nikanyoosha zangu nyumbani!.
Nilipomaliza kuoga niliingia jikoni fasta kupika ili atakapokuja Monica akute nikiwa nimemaliza kila kitu!.Kama nilivyosema hapo awali ya kwamba,kule kwenye kile kijiji kutembea usiku haikuwa shida,shida ilikuwa ni wachawi tu,lakini mambo ya wezi na majambazi hayakuwepo kabisa,kuna matukio machache sana yaliwahi kufanyika kule senta yaliyohusu wezi lakini yalikuwa yakuhesabika na hayakujirudia tena!.

Nilipomaliza kupika nilichukua sinia nikafunika ugali nikauweka mezani,kisha nikachukua mabakuli ya mboga nikapakua mboga kisha nazo nikapeleka sebuleni,sasa niliendelea kuona ndani kwa Headmaster kuko kimya hata mwanga wa taa au tochi haukuonekana!.Nilisogea karibu nikaanza kugonga ule mlango kuwakaribisha kwa ajili ya chakula lakini nikaona kimya!,nilipoangalia vizuri mlangoni nikakuta kuna kofuli,basi niliamini watakuwa wametoka.

Basi nilichukua sahani nikakata ugali wa kunitosha size yangu nikaanza kula!.Nimekula mpaka namaliza si Ba'mdogo wala Maza mdogo aliyerudi,nikakumbuka uenda kwa kuwa ilikuwa ijumaa labda watakuwa wameondoka kwenda mjini,lakini isingekuwa rahisi kwasababu niliondoka kwenda senta nikawaacha hapo nyumbani,halafu pia ile Hiace ya kuelekea mjini ilikuwaga inaondoka saa 12 asubuhi,niliamini uenda watakuwa wametoka tu na walikuwepo hayo mazingira ya kijijini.Kilicho fanya pia kujiuliza uenda wakawa wameenda mbali ni kitendo cha Ema na mpenzi wake Deborah kujiachia usiku ule bila presha!.Nilirudishia ule mlango wa sebuleni nikarudi zangu chumbani kwetu!.

Mpaka inafika mida ya saa 3 sikumuona Ema na nikajua kabisa headmaster na mkewe watakuwa wameenda mbali.Mpaka muda huo sikumuona Monica hivyo nikaamua kujilaza huku nikiwa namsikilizia.

Haukupita muda nikasikia mlango wa nje unagongwa!,nilienda kuufungua ndipo nilikuta alikuwa Monica!.

Mimi "Karibu"

Monica "Ulikuwa umelala mpenzi wangu?"

Mimi "Nimekusubiri sana"

Monica "Nilikuwa napika,nisamehe"

Mimi "Sikunyingine usiwe unagonga bhana utaniletea shida!"

Monica "Unadhani mimi mjinga?"

Aliendelea "Nimejua hawapo ndiyo maana nimegonga"

Mimi "Umejuaje?"

Monica "Twende nyumbani tunachelewa"

Basi niliingia ndani nikavaa viatu nikatoka zangu,nilifunga ule mlango wa chumbani kwetu na komeo lakini sikuweka kufuli!.Ule wa nje nilirudishia tu tukaondoka zetu na Monica.Mara ya kwanza kutembea na Monica ilikuwa ni kutuliza tu uwendawazimu wa abdala kichwa wazi lakini sikumpenda kabisa,sasa kadri siku zilivyokuwa zikienda ndivyo ulikuwa uniambii kitu kwa yule binti wa kisukuma na kiukweli kuna wakati nilikuwa naona ni kwanini nilichelewa kumfahamu maana alikuwa akinijali sana,licha ya kwamba papuchi ilikuwa ni moja ya sababu ya kumpenda lakini sura yake nzuri pia ilinivutia zaidi,alichokuwa amekosa yule binti wa kisukuma ni matako makubwa tu ambayo ndiyo ulikuwa ugonjwa wangu wakati huo,lakini kwingine kote alikuwa amekamilika binti wa watu wala nisimseme vibaya!.

Mimi "Umeambia ulijua hawapo,umejuaje"

Monica "Nishakwambia mpenzi wangu usiwe unauliza uliza maswali,utaelewa tu siku moja"

Aliendelea "Nimemuona ndugu yako wakati nakuja akiwa na mpenzi wake"

Mimi "Umekutana nao?"

Monica "Kuna mahali nimewaona wanaongozana"

Mimi "Nadhani tupite pale kwao Deborah ili nikamuulize kama headmaster ametoka anarudi au harudi maana muda umeenda"

Monica "Ningekwambia lakini unaweza usiniamini,twende ukamuulize!".

Basi tulichepuka na kuacha ile njia kubwa na tukashika njia ya kuelekea kwao Deborah,basi tulipofika Monica alisimama kwa mbali kidogo hakutaka kuongozana na mimi!.

Monica "Nenda utanikuta nakusuniri hapa"

Nilipofika kwenye boma la ile nyumba kwa mbali nikaona taa ikiwa inawaka kwenye kile kinyumba alichokuwa akilala Deborah na nikaelewa watakuwa bado macho!.Basi nilipofika nikasikia watu wakiongea kwa sauti za chini lakini cha ajabu niligonga sana ule mlango bila mtu kutoka wala kuitikia!.Sikutaka kupoteza muda niliondoka zangu kimya kimya kama mtu aliyetengwa na wazazi wake,nilikuwa najiuliza maswali mengi sana nikawa nakosa majibu!.Nilifahamu kabisa Ema atakuwa amemlisha sumu mbaya Deborah kwasababu haikuwa kawaida ya Deborah kunidharau kiasi kile.

Monica "Umemkuta"

Mimi "Nimewasikia kabisa wanaongea lakini wamekataa kuniitikia"

Monica "Huyo ndugu yako anakiburi sana,wewe subiri ajifanye mjanja"

Aliendelea "Baba yako na mama yako mdogo kuna mahali wameenda na wangekuwa wanajua wanajisumbua wangebaki wakatulia"

Mimi "Kwani unajua walipoenda?"

Monica "Tuondoke tunachelewa"

Basi tulitembea kwa haraka kuelekea kwao Monica,jambo lilikuwa ni lilelile la kufika mapema ingawa palikuwa mbali.Sasa nilipofika niliwakuta watu kadhaa wakiwa pale nje wakiwa wamekaa wakipiga stori huku wakiwa wameshaa taa ikiwa juu ya jamvi.

Mama Monica "Karibu mwanangu"

Mimi "Shikamoo mama"

Mama Monica "Marhaba mwanangu,karibu"

Mama yake Monica alinyanyuka kwenye kiti alichokuwa amekaa akawa amenikabidhi nikalie.Basi haukupita muda nikaona Monica anebeba kimeza kidogo anakileta mahali nilipokuwa nimekaa!.Baada ya kuileta ile meza na kuiweka vizuri akawa ameingia ndani ndipo akaja na vyungu akawa ameviweka chini ya meza,alirudi tena akaja na mabakuli akaanza kupakua mboga,kisha akaendea ugali wa udaga na kuukarisha juu ya meza,alinikaribisha kwa kupiga magoti hadi chini!.

Mwanaume nikaanza kula,kumbe nilikuwa nimeachiwa bata ambaye alipikwa kwa ajili ya bibi yake aliyekuwa amekuja kuwatembelea,kwakweli nilikula sana japo nilikuwa nimeshiba maana nilimisi sana nyama ya bata!.Baada ya kumaliza kula mama yake Monica alianza kuongea kisukuma na yule mwanamke mzee ambaye nilifahamu kabisa ni bibi yake Monica kwasababu alikuwa amekwisha kunitonya!.

Mama Monica "Mwanangu,huyu ni mama yangu"

Mimi "Ooh sawa"

Baada ya kuongea na mimi kisha akawa anaongea na bibi yake Monica!.

Monica "Bibi hajui kiswahili ndiyo maana unaona mama anaongea nae kilugha"

Basi tuliendelea kupiga stori za hapa na pale na Monica, sasa muda ulivyozidi kwenda bibi yake Monica akasimana akawa ameingia ndani,nadhani aliingia kulala!.Baada ya kuingia ndani,mama yake Monica alisogeza kiti mahali nilipokuwa nimekaa na Monica.

Mama Monica "Mwanangu kwanza nikupe Pole kwa uliyayaona jana"

Mimi "Aaah mama wala usijali"

Mama Monica "Sasa mwanangu nisikilize kwa makini"

Aliendelea "Niliwahi kukwambia haya yote nayafanya kwa ajili ya binti yangu,nakuomba usije kumuacha mwenzako"

Mimi "Siwezi kumuacha mama"

Mama Monica "Sawa"

Aliendelea "Sasa ila mwalimu anachokifanya si jambo jema,angetulia ningemsaidia"

Mimi "Amefanya nini mama?"

Mama Monica "Maalimu anaenda kwa waganga akitaka kufahamu wanaomuaharibu"

Aliendelea "Mmmmh ngoja tumuone"

Mimi "Mama kwanini usimsaidie tu ba mdogo?"

Mama Monica "Yule mwalimu aliwahi kunitukana mwanangu,wewe hujui tu!,na hata niliposikia unaishi kwa mwalimu nilikujaribu ukanibebea kuni zangu,nilipoona wewe ni kijana mzuri na mwanangu kukupenda nikaona nikusaidie wewe!"

Aliponiambia ya kwamba nimewahi kumbebea kuni nilishituka sana lakini sikutaka kuonyesha!,niliendelea kujipa moyo nikiamini kwasasa hawezi kunifanyia jambo baya kwasababu nilikuwa kwenye mahusiano na binti yake,nilifahamu kabisa ile familia niya kishirikina lakini kwakuwa walikuwa wakinilinda sikuwa na namna!.

Mama Monica "Hata huko walipoenda wameenda kupoteza muda tu mwanangu"

Mimi "Kwani wameenda kwa mganga"

Monica "Wewe nilikwambia nikikuambia hutoniamini,ngoja mama akueleze sasa"

Mama Monica "kwani hujui mwanangu?"

Mimi "Nimetoka senta sijakuta mtu nyumbani mama"

Mama Monica "Hawawezi kukwambia mwanangu"

Aliendelea "Sasa kesho kuna vitu nitakupatia uende navyo nyumbani na nitakuja mwenyewe baadae kukuelekeza namna ya kufanya!"

Mama Monica "Kwakuwa hata hivyo yule mbwa anataka kuniulia nyinyi wanangu nitamshikisha adabu halafu baada ya hapo nitapandishwa cheo"
Inabidi uongozi wa jf ukulipe...hii story ni dope.

#MaendeleoHayanaChama
 
Monica aliokoka, kaolewa na mchungaji(haijulikani anachunga nini).
 
Kuna matukio fulani ya kichawi yalimtokea mdogo wangu wa damu 5 years back mpaka waleo hao walozi wanamsumbua sumbua sana na kumfatilia dogo! Wakati nasoma hii Story nilikua nilifuatilia hakua kwa step moja baada ya nyingine... na kuna vitu vingine UMUGHAKA umesimulia nikihusianisha na matukio yanayompata dogo umepita muleemuleeeee! Kiukweli Nawish sana kujua hizo dawa ili nimsaidie dogooo japo yeye mpaka waleo hatujui tuwafanyeje kuwaaibisha kisawasawa hao Wachawi wanaomsumbua!
Je upo tayari kwa visomo?
 
Kuna matukio fulani ya kichawi yalimtokea mdogo wangu wa damu 5 years back mpaka waleo hao walozi wanamsumbua sumbua sana na kumfatilia dogo! Wakati nasoma hii Story nilikua nilifuatilia hakua kwa step moja baada ya nyingine... na kuna vitu vingine UMUGHAKA umesimulia nikihusianisha na matukio yanayompata dogo umepita muleemuleeeee! Kiukweli Nawish sana kujua hizo dawa ili nimsaidie dogooo japo yeye mpaka waleo hatujui tuwafanyeje kuwaaibisha kisawasawa hao Wachawi wanaomsumbua!
Tuhakikishie wewe si Umughaka kwa ID nyingine unatengeneza target hapa....
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 19.



Kiukweli nilikuwa nimechukia sana namna nilivyodharirishwa pale shuleni mbele ya wanafunzi!,sikutaka kuonekana mkorofi na mkaidi,nilifanya kila nilichoambiwa ili mambo mengine yapite!,niliona angalau Ba'mdogo aniadhibu kuliko taarifa za kulala nje ningemfikia baba yangu hakika angeniua kwa kipigo na shule angeweza kuacha kunisomesha nikawa mchunga ng'ombe!.Japo nilifanya kosa la kulala nje bila taarifa lakini nilidhani ile adhabu ya kudharirishwa haikufaa hata kidogo na ilijaa uonevu mkubwa!.

Basi nilianza kutembea kutoka hapo Senta kuelekea nyumbani huku kile kichwa cha cherehani nikiwa nimejitwisha kichwani,kiukweli nilichukia sana lakini niliamua kujikaza mtoto wa kiumwe,niliamini hayo ni mambo ya kawaida tu na yangepita!.Kile kichwa cha cherehani hakikuwa chepesi kama nilivyodhani na ilipelekea nikawa nafika sehemu najitua kichwani nashikiria kwa mikono miwili lakini bado haikusaidia,kwahiyo nilichokifanya ilikuwa nakiweka begani angalau nikawa naona kuna unafuu!

Nilifika nyumbani nikiwa nimechoka sana na kwakweli kuanzia siku hiyo,mimi na Ema tulikuwa kama Paka na Panya,sikutaka kabisa jamaa aniambie chochote wala kunisogelea kwasababu nilimuona ni mnafiki!,mara kibao tu yeye nilikuwa nikimtunzia siri zake lakini jamaa yeye za kwangu hakutaka kabisa kuziweka moyoni.Kitendo cha kumwambia Ba'mdogo nilikuwa natembea na binti Monica tena mbele ya wanafunzi kilifanya nikamchukia sana jamaa!,na nilichoamua ni kwamba kama mbwai na iwe mbwai!.

Haikupita muda Maza mdogo naye akawa ametoka senta,kama kawaida yeye alikuwa akitoka senta alikuwa anaingia kuoga na kusubiri kula,wa kupika sana sana nilikuwaga mimi maana Ema nae alikuwa anajifanya kusoma kila alipokuwa akitoka shule,sasa nilikuwaga najiongeza tu kuingia jikoni kupika ili kuepuka matusi ya Ba'mdogo.
Siku hiyo nilikuwa nimechoka sana na nilikuwa nanuka jasho kwasababu ya zile kazi kuanzia asubuhi hadi ile usiku lakini sikuweza kuyasogelea maji kwasababu niliambiwa na Monica na akanionya nisiguse maji!.

Siku hiyo nililala kwa uchovu sana,namshukuru Mungu palipo pambazuka niliamka nikajiandaa kuondoka zangu senta,sasa nilichofanya nikupiga mswaki tu na kubadili nguo,sikutaka kabisa hata kunawa uso,nilipomaliza niliingia ndani kuwasalimia Headmaster na mkewe!.

Maza mdogo "Wewe unaenda halafu hicho kichwa cha cherehani nani atakipeleka?"

Nikawa kimya kwa muda huku nikiwa natafakari nini cha kujibu!.

Headmaster "Kwani kichwa cha cherehani sikuhizi unakileta nyumbani?"

Maza mdogo "Juzi sinilikwambia wanasema yule mama Mayala aliwahi kuibiwa kichwa cha cherehani pale kibandani kwake,unadhani chanzo cha Mama Mayala kuacha kushona ni nini?"

Headmaster "Sasa kwanini usiwe unamuomba mama Rebecca unakiacha pale nyumbani kwake kuliko kupata kazi ya kukileta huku!".

Maza mdogo "Ngoja nitajaribu kuongea nae!".

Headmaster "Wewe nenda uwahi kwenye shughuli zako bhana!"

Maza mdogo "Sasa nani atanisaidia kukipeleka senta"

Headmaster "Utakamata hapo mwananfunzi akusaidie"

Sasa mimi sikutaka kabisa kuonekana uenda nilichukia kukibeba kile kichwa,niliamua kujikaza na kumwambia ningekifata baada ya kupeleka miwa senta.

Mimi "Haina shida mama ngoja nikachukue miwa nipeleke senta halafu narudi kukichukua".

Maza mdogo "Sawa,uwahi sasa"

Sasa nilidhani uenda Headmaster alivyokuwa amemshauri ya kwamba angekamata pale shuleni mwanafunzi amsaidie kubeba kile kichwa na kukipeleka Senta angekubaliana nae lakini haikuwa hivyo,kitendo cha kuniambia niwahi kurudi kukibeba ilionyesha kabisa alifurahishwa na mimi kwenda senta na kurudi kukibeba!.Basi sikuwa na hiyana mtoto wa kiume nikaondoka zangu kuelekea kwenye mashamba ya mzee Masumbuko kwa ajili kufata miwa kama kawaida,ingawaje miwa iliyokuwepo haikuisha ila niliona ni heri nikakusanya ikawa mingi ili inipunguzie safari ya kila siku kuamka asubuhi na mapema kisa kuwahi miwa!.

Nilipofikisha ile miwa pale senta niliibwaga chini nikaondoka zangu kurejea nyumbani kwa kukimbia ili kuwahi kurudi!,sasa kuna sehemu nilifika nikamuona dogo mmoja akiwa kwa mbele kabeba kile kichwa cha cherehani huku Maza mdogo akiwa nyuma yake,nilipowafikia nilimwambia dogo anipe kile kichwa nimsaidie na yeye arudi shule!.

Nilijifanya kuchangamka na kutabasamu kiunafiki lakini kiuweli nilikuwa nimechukia sana,nikawa najiuliza kama alikuwa anajua angempatia mwanafunzi amsaidie kubeba kwanini alitaka nirudi tena?,kama kawaida yangu sikutaka maneno na mtu nikaamua kufunga bakuli langu ili mwanaharamu apite.Wakati huo kiukweli nilikuwa nimeanza kupoteza nuru ya muonekano wangu kwasababu ya kushinda kule senta wakati mwingine sili kabisa mchana na chakula nilikuwa nakutana nacho usiku tu!,mara nyingi nikiwa pale senta nilikuwa nashindia sana miwa!.

Tulifanikiwa kufika senta na nikakipeleka kile kichwa kwenye kibanda alichokuwa akishonea na mimi kwenda mpaka kwa yule mama ambaye nilikuwa nikilaza ile miwa,niliichukua nikaenda kuinganisha na ile niliyokuwa nimekuja nayo na kuanza kuuza!.Namshukuru Mungu siku hiyo niliuza sana ile miwa,japo haikuisha lakini mpaka kufika mida ya saa 10 alasiri ikawa imepungua kwa kiasi kikubwa!
Sasa nikiwa naendelea kuuza miwa yangu pale,kwa mbali nikamuona yule binti Mwise akiwa na binti mmoja wakiwa wamevaa sketi za shule na tisheti za kawaida wakiwa wanakuja hapo senta, sikufahamu kilichokuwa kimewaleta uenda walifata mahitaji kama watu wengine!.

Yule binti kiukweli ndiye alikuwa binti wa kwanza kwa hapo kijijini kuumiza na kuutesa moyo wangu,nilikuwa nampenda na kumtamani sana kutokana na shepu yake nzuri!,ila baada ya kuanza kutembea na Monica kiukweli upendo na matamanio yangu kwake yakaanza kupungua kwa kasi ya ajabu!.Walipofika karibu waliingia kwenye duka moja wakanunua kilichowaleta kisha wakatoka wakawa wanaelekea kwenye vibanda na maduka ya mbele ambako huko pia ndiko mama mdogo anakofanyia shughuli zake,sasa baada ya kugeuka na kutazama uelekeo niliokuwepo mimi,nikampiga mkono kwa ishara ya kwamba aje!.

Mwise "Narudi!"

Kwakuwa aliniambia anarudi nikasema ngoja nisubiri.Safari hii sikutaka kabisa kuwa na kimuhe muhe kwasababu sikuweza kujificha na ile biashara yangu na yeye alifahamu kabisa nilikuwa muuza miwa!,niliamini kama ni kumpata basi ningempata tu na kama ni kumkosa basi ningemkosa vilevile!.

Haukupita muda wakawa wanarudi na huyo mwenzie,sasa alipofika pale kwenye eneo langu la biashara akaanza kama kuonyesha nyodo na dharau.

Mwise "Nionjeshe muwa rafiki yangu!"

Mimi "Kwahiyo mimi leo nimekuwa rafiki yako?"

Mwise "Jamani!,kwani kuna ubaya wewe kuwa rafiki yangu?"

Basi nikamkatia pingili mbili za muwa yeye pamoja na mwenzie!,basi wakawa wanazungumza na huyo rafiki yake maneno ya kisukuma huku wakicheka kwa kicheko cha kichini chini!,kiukweli walikuwa wanikiteta kwa kisukuma na ishu kubwa walikuwa wakizungumzia zile stiki nilizokuwa nimelambwa na Headmaster mbele ya wanafunzi!,wao walidhani siwaelewi lakini hata kama sikuelewa kisukuma vizuri mtu alikuwa akiteta inafahamika kabisa!.

Walipomaliza kukwangua kwangua miwa kwa kisu akawa ameniambia wanaondoka kuwahi kurudi nyumbani,nikawa nimemuomba anivumilie angalau kwa dakika mbili nizungumze nae!,sasa yule mwenzake akawa amemwambia atamkuta mbele!.

Mwise "Sasa na wewe unaniacha nyanoko"

Mwenzie "Utanikuta mbele bhana"

Mwise "Mmh!,niambie mi nina haraka"

Mwise "Kwahiyo Mwise Ombi langu vipi lakini?"

Mwise "Ombi gani tena jamani"

Mimi "Kwani mara ya mwisho mimi na wewe tuliongea nini?".

Mwise "Siulianimbia unanipenda,nashukuru kwa kunipenda"

Mimi "Usinifanyie hivyo Mwise"

Mwise "Wewe si unaye mwanamke wako"

Mimi "Mwanamke gani tena jamani!?"

Mwise "Wewe ema kaniambia habari zako nyingi tu!,kumbe ulikuwa tu unataka unilale uniache"

Mimi "Daaah!,hebu achana na mambo ya Ema Mwise,Ema anashida kubwa na wewe yule unamfahamu akili yake".

Mwise "Mimi nachelewa bhana,kesho!"

Basi yule binti alianza kukimbia kumfuata mwenzie aliyekuwa akimsubiria.Niliamini kabisa kwa kilichotekea pale shule ukichanganya na uongo wa Ema,haikuwa rahisi mimi kumpata tena yule binti.Niliamua kujipa moyo ya kwamba mademu mabaya siku zote ndiyo yanayoringa lakini kuna muda bado nilikuwa nikifikiria kiuno cha yule binti na kuwaza kinavyo chakatwa na wanaume wengine,kiukweli nilikuwa naumia sana!.

Sikuwa na namna ilibidi niwe tu mpole ili maisha yasonge!.

Baada ya kukamilisha siku ya uuzaji wa miwa niliamua kurudi nyumbani na namshukuru Mungu safari hii sikurudi na kichwa cha cherehani kwasababu maza mdogo alipata pa kukiweka hapo senta.

Sasa nilifika nyumbani mida ya saa 1 usiku,nilielekea lamboni ile usiku kuchota maji ili nije nioge kwasababu nilikuwa sijaoga tangu jana yake!,sasa nilipotoka bafuni kuoga,nikawa nimeingia ndani kwa ajili ya kupaka mafuta!,sasa wakati napaka mafuta nikasikia kuna mtu ananipiga piga mgongoni kwa mkono akiashiria nigeuke!,sasa ile nimegeuka nikawa nimekutana na Monica uso kwa uso!.

Kiukweli nilishituka sana ila akanifanyia ishara ya kidole mdomoni akinitaka nisipige kelele wala kuongea!.

Mimi "Monica kuna nini mbona huko humu"

Monica "Vaa nguo tuondoke"

Mimi "Tuondoke twende wapi tena!?"

Monica "wewe vaa twende"

Mimi "Tunarudi lakini?,maana mwenzio jana jana nimepigwa kwasababu yako"

Monica "Hatuendi mbali tutakuwa nje hapo"

Basi baada ya kuvaa nguo,Monica akawa amenishika mkono na ghafla tukawa nje ya nyumba kwa pembeni kidogo.

Monica "Tusogee pale kwenye lile jiwe!"

Baada ya kufika pale kwenye lile jiwe akanitaka tukae pale na kuna watu tuwasubiri walikuwa wanakuja!.
mademu mabaya yanaongoza kwa kuringa[emoji23][emoji23]
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 25.





Baada ya Headmaster kutoka kuwasindikiza wageni,tuliamua kukaa kikao cha kifamilia na kuzungumza mambo kadhaa yaliyotuweka sawa.Sasa kila mtu alielekea chumbani kulala,baba mdogo na mkewe waliingia chumbani kwao,mimi na Ema pia tuliingia chumbani kwetu kulala.

Siku hiyo mle chumbani hakuna aliyepata usingizi kabisa,kabla ya kulala nakumbuka tulipakaa usoni dawa aliyokuwa ametupatia mama yake Monica,pia tukashikiria na zile hirizi mkononi kama alivyokuwa ameagiza tufanye!.Kadri muda ulivyokuwa ukisonga tuliona kimya,mimi nilianza kupitiwa na usingizi maana nilikuwa nimechoka sana!,kumbe wakati mimi napitiwa na usingizi,Ema yeye alikuwa macho kabisa na jamaa alikuwa na shauku ya kuona ni kitu gani kingetokea!.

Sasa ilipofika mida ya saa 8 usiku,nilishitushwa na Ema akiniamsha!.


Ema "Umesikia hicho kishindo?".

Mimi "Hapana,kishindo cha kitu gani?"

Ema "Kutakuwa na kitu nadhani!"

Ema alikuwa akiniambia kwa sauti ndogo kabisa na yenye uoga ndani yake!.

Mimi "Nyamaza"

Niliamka kitandani nikaenda kuwasha taa,nilifahamu kabisa kile kishindo Ema alichosikia hakikuwa cha kawaida na uenda wale jamaa wakawa wamekuja kama kawaida yao,kiukweli mimi kwa upande wangu sikuwa kabisa na hofu kwasababu kwa siku chache nilikuwa nimeshazoea yale mazingira ya kuwaona wachwawi laivu!.Nilimwambia na kumbusha Ema ya kwamba chochote atakachokiona asipige kelele wala kushituka!.

Haukupita muda,mara ghafla wakaonekana watu watatu wakiwa wamesimama mle chumbani huki wakiwa uchi kama walivyozaliwa,watu wale safari hii walikuja wawili wanaume na mmoja akiwa mwanamke!.Niliwaangalia kwa kuibia kama vile sielewi chochote!,Ema alikuwa akitetemeka sana na nilimpatia ishara ya kwamba atulie kabisa!.Basi nadhani yule mwanamke alihisi jambo maana niliona anamsogelea Ema akawa kama anamtisha aone kama amemuona,sasa alipoendelea kumtisha Ema nikaona anaweza kupiga kelele,nikaanza kumpigisha Ema stori ili kupotezea ile hali!.

Mimi "Mwanangu wewe piga kimya kabisa wala usimfanye chochote yule demu"

Ema "Yule demu mwanangu anazingua kinoma"

Mimi "Halafu Headmaster alisema ukamuamshe aandae yale masomo"

Ema "Halafu kweli umenikumbusha,ngoja nikamuamshe!"

Sasa wakati tunaongea yule mwanamke alirudi kwa wenzie na wakaendelea kushangaa shangaa,tulichokifanya na Ema pale kwa ule muda mfupi ni hakika walidhani hatuwaoni kumbe lengo lilikuwa ni kumuondolea Ema uoga na kuwapoteza maboya!.
Ema aliamka akatoka kwenda kumgongea Headmaster chumbani kwake ili aje ajionee!,sasa wakati Ema ameondoka,nilianza kujipigisha mruzi wa uongo na kweli ili kuikabili ile hali kwasababu ilikuwa inatisha si kitoto!..

Headmaster "Umughaka tacho omahe"

Baba alipotoka nje aliniita kwa kilugha nikawa nimetoka nje,sasa alianza kutueleza ya kwamba tusishituke na tuendelee kuwa watulivu,alitwambia Ema achukue madaftari tuelekee wote sebuleni ili iwe rahisi kuwakabili,mimi nilimwambia wao wakae sebuleni na mimi nirudi chumbani kukaa karibu na kibuyu kwa kazi maalumu!.
Basi wale watu wakawa wamepotea ghafla mle chumbani!,nilitoka nje kwenda kumwambia Headmaster.

Headmaster "Ngoja tusubiri,yawezekana wakawa wameshituka"

Mimi "Lazima warudi"

Headmaster "Halafu mbona yule mzee hayupo?"

Mimi "Uenda leo kawaagiza hawa"

Wakati tukiwa tunaendelea kuongea pale,Maza mdogo akamwambia Headmaster kwa kikurya kwamba,wale watu wako kule chumbani kwake na anawaona,Headmaster akamwambia atulie na asipige kelele!.Sasa tukiwa tunaendelea kuongea pale sebuleni huku Headmaster akijifanya kumpigisha Ema pindi,tukasikia kishindo kikubwa tena pale uani!.

Haukupita muda akawa ametokea yule mzee makono akiwa na usinga mkononi huku akiwa uchi kama wenzie!,akaja mpaka pale sebuleni huku tukiendelea kumpimia tu!,aliendelea kuangaza huku na huko na hatimaye akawa ameingia mle chumbani kwa Headmaster.Basi baada ya kuingia chumba cha Headmaster,Headmaster aliinuka kwa ghadhabu huku akisema "Lero n'uramanye uwe tombanyoko" (Leo utanitambua).

Sasa Headmaster alipoingia chumbani alijifanya kuongea na mkewe huku wakiwatazama,sasa nadhani mzee makono aliwaambia wale watu waende wakawalete watu wa kwenda kulima ili wakifika watuunganishe na sisi tuondoke!,wale watu watatu walitoweka wakamuacha mzee makono mle chumbani akitaka kufanya mambo yake ili amchukue Headmaster kama kawaida aje atuunganishe na sisi tuelekee kwenye kilimo cha usiku kisichokuwa na tija!.

Wale watu walipotoweka tu na mzee makono kubaki mwenyewe,Headmaster alichukua kile kibuyu alichopewa na mama yake Monica akakifungua,alipokifungua tu!,yule mzee akaanza kucheza kwa kuzunguka mle chumbani kama mwendawazimu!.Headmaster alituita tukaingia kumtazama,yaani kuna muda nilianza kumuonea huruma maana alikuwa kama amepagawa kwa kushikwa ugoni.

Kadiri muda ulivyokuwa ukienda,wale watu waliotumwa na mzee makono hawakurudi kabisa na nadhani watakuwa walishituka mapema!.Ile hali ilifanya maza mdogo kutoka kule chumbani akabaki mzee makono akizunguka chumba kizima kama mwendawazimu.Usiku huko hakuna mtu aliyepata usingizi kabisa,tumekuja kushangaa imefika saa 11 alfajiri bila kujua!.
Sasa ilipofika saa 12 asubuhi,Mama yake Monica alikuja akiwa na wale kina mama,alihuzunika sana kwanini tuliamua kuwaachia wale watu watatu wakaondoka!.


Mama Monica "Mwalimu nilikwambia,nadhani sasa unaniamini"

Headmaster "Sikuzote Msukuma nakuamini,si leo tu!".

Mama Monica "Kwanini mmewaachia wale washenzi?"

Headmaster "Wameondoka wenyewe"

Mama Monica "Nilikwambia wakifika tu,ungefungua kibuyu"

Headmaster "Nilipoingia chumbani kufungua kibuyu wakawa wameondoka akabaki mzee lameki"


Mama Monica "watasimuliana,hakuna kilichoharibika"

Aliendelea "Haya sema,unataka tumfanye nini huyu mzee"

Headmaster "Nadhani kama kuna uwezo muondolee uwezo wake asije akaponyoka halafu mengine utaniachia mimi"

Mama Monica "Huyu ameshakwisha,hapa hawezi kukuponyoka kamwe"

Aliendelea "Mimi namshughurikia halafu nakuachia wewe utajua cha kumfanya".


Basi mama yake Monica alimsogelea yule mzee akachukua ule usinga kisha akamvua shanga alizokuwa amejivika kuanzia begani kuteremkia kiunoni!,baada ya hapo kuna dawa alimpatia Headmaster akamwambia kukishapambazuka vizuri atampaka ile dawa na kisha atamuondoa mle ndani!.Mama yake Monica na wale kina mama waliondoka wakawa wamemuacha mzee makono humo ndani akizinguka kama mwehu!.

Kulipopambazuka,Headmaster alielekea kwa mwenyekiti wa kijiji na kutaka yowe ipigwe karibia kijiji kizima ili wananzengo wahalifiwe ya kwamba kulikuwa kuna tukio kubwa la kushangaza!,Basi yowe ilipigwa na watu wakawa wanakuja pale nyumbani huku wengine mikoni wakiwa wameshika mapanga na mafimbo!.Haukupita muda mrefu watu wakawa wamejazana pale nyumbani huku wengine wakichungulia dirishani wakishangaa lile tukio!.

Ilipofika mida ya saa 3 Asubuhi baada ya watu kujazana pale nyumbani,Headmaster alifanya kama alivyoambiwa afanye na mama yake Monica,baada ya kupakwa dawa yule mzee alikurupuka akawa anashangaa sana!,alikuwa akizunguka kitafuta usinga wake lakini hakuuona,ndipo Headmaster aliamrishwa na wananzengo ya kwamba amtoe yule mzee nje ya nyumba ili akapambane na viboko vilivyokosa huruma!.

Yule mwenyekiti aliamuru yule mzee avishwe nguo hadi kwenye ofisi ya serikali ya kijiji lakini wananzengo wakagoma,walisema inapaswa atembezwe kijiji kizima huku akila mboko na inapaswa siku hiyo hiyo ahame kijiji!.

Basi nakumbuka Headmaster alimuagiza Ema akalete viboko ili aanze nae mle ndani kwasababu alikuwa akimtafuta sana,viboko vilipoletwa kiukweli yule mzee alichezea kiasi kwamba sikutaka hata kuangalia,viboko vilipozidi aliamua kutoka ndani spidi akikimbilia nje,kufika nje wananzengo wakamdaka nako wakaanza kumsulubisha!.
Alitembezwa kijiji kizima huku akiwa uchi kama alivyozaliwa,kiukweli lilikuwa ni tukio la aibu mno!,sasa walipomfikisha kwake wananzengo hawakutaka mjadala,walimwambia avae nguo kisha atoke,alipotoka waliwasha moto nyumba yake na kila kitu kiliteketea kwa moto!.

Baada ya pale alirudishwa serikali ya kijiji na kutakiwa apotee kwenye kile kijiji ndani ya masaa 2!,hakutakiwa kubaki pale na wananzengo walimwambia watamuua endapo angebaki kwa siku hiyo!.

Lile tukio lilivuta hisia kubwa sana pale kijijini na kiukweli lilimpatia Headmaster ujiko na heshima sana ingawaje mimi ndiye niliyepambana sana mpaka kufikia ile hali.Headmaster aliogopeka sana tangu siku ile lile tukio litokee na hakukuwahi tena kuwa na mambo ya ajabu pale nyumbani.

Headmaster kwa baadae alihama ile shule na kuhamia huko Biharamulo ambako amejenga na anaishi hadi leo,mimi niliondoka na kurudi nyumbani kisha kuelekea shuleni Advance!.

Ema yupo hapo Shinyanga anauza duka la vipuri vya magari,amejenga na anaishi hapo hapo shinyanga.

Monica kuna wakati niliambiwa yupo Mwanza ila sijajua ni Mwanza sehemu gani!,kuna mtu nilikutana nae wa pale kijijini akawa ameniambia hivyo,kwasababu baada ya mimi kuondoka pale kijijini sikurudi tena hivyo tukawa tumepotezana na mpenzi wangu huyo!.

Mimi kwasasa nipo Dar es salaam napambana na maisha ya kukimbizana!,nina kiboda boda changu japo kimekwisha lakini tunapambana na maisha!.Kijiwe changu huwa ni hapo Bunju ndugu zangu!.



MWISHO.
Pongez kubwa Sana zikuendee UMUGHAKA stori hii imetufunza meeng Sana bro yamkini tumeinjoi,tumeelimika ....hongera zaidi kwa kuwa mvumilivu maana kuna wadau humu jf ni masononeko tu kama wanakulipa lakini yote tisa la muhimu *ASANTE KWA STORI NZURI *
 
Kuna matukio fulani ya kichawi yalimtokea mdogo wangu wa damu 5 years back mpaka waleo hao walozi wanamsumbua sumbua sana na kumfatilia dogo! Wakati nasoma hii Story nilikua nilifuatilia hakua kwa step moja baada ya nyingine... na kuna vitu vingine UMUGHAKA umesimulia nikihusianisha na matukio yanayompata dogo umepita muleemuleeeee! Kiukweli Nawish sana kujua hizo dawa ili nimsaidie dogooo japo yeye mpaka waleo hatujui tuwafanyeje kuwaaibisha kisawasawa hao Wachawi wanaomsumbua!
Pole Sana nicheki PM ....
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 25.





Baada ya Headmaster kutoka kuwasindikiza wageni,tuliamua kukaa kikao cha kifamilia na kuzungumza mambo kadhaa yaliyotuweka sawa.Sasa kila mtu alielekea chumbani kulala,baba mdogo na mkewe waliingia chumbani kwao,mimi na Ema pia tuliingia chumbani kwetu kulala.

Siku hiyo mle chumbani hakuna aliyepata usingizi kabisa,kabla ya kulala nakumbuka tulipakaa usoni dawa aliyokuwa ametupatia mama yake Monica,pia tukashikiria na zile hirizi mkononi kama alivyokuwa ameagiza tufanye!.Kadri muda ulivyokuwa ukisonga tuliona kimya,mimi nilianza kupitiwa na usingizi maana nilikuwa nimechoka sana!,kumbe wakati mimi napitiwa na usingizi,Ema yeye alikuwa macho kabisa na jamaa alikuwa na shauku ya kuona ni kitu gani kingetokea!.

Sasa ilipofika mida ya saa 8 usiku,nilishitushwa na Ema akiniamsha!.


Ema "Umesikia hicho kishindo?".

Mimi "Hapana,kishindo cha kitu gani?"

Ema "Kutakuwa na kitu nadhani!"

Ema alikuwa akiniambia kwa sauti ndogo kabisa na yenye uoga ndani yake!.

Mimi "Nyamaza"

Niliamka kitandani nikaenda kuwasha taa,nilifahamu kabisa kile kishindo Ema alichosikia hakikuwa cha kawaida na uenda wale jamaa wakawa wamekuja kama kawaida yao,kiukweli mimi kwa upande wangu sikuwa kabisa na hofu kwasababu kwa siku chache nilikuwa nimeshazoea yale mazingira ya kuwaona wachwawi laivu!.Nilimwambia na kumbusha Ema ya kwamba chochote atakachokiona asipige kelele wala kushituka!.

Haukupita muda,mara ghafla wakaonekana watu watatu wakiwa wamesimama mle chumbani huki wakiwa uchi kama walivyozaliwa,watu wale safari hii walikuja wawili wanaume na mmoja akiwa mwanamke!.Niliwaangalia kwa kuibia kama vile sielewi chochote!,Ema alikuwa akitetemeka sana na nilimpatia ishara ya kwamba atulie kabisa!.Basi nadhani yule mwanamke alihisi jambo maana niliona anamsogelea Ema akawa kama anamtisha aone kama amemuona,sasa alipoendelea kumtisha Ema nikaona anaweza kupiga kelele,nikaanza kumpigisha Ema stori ili kupotezea ile hali!.

Mimi "Mwanangu wewe piga kimya kabisa wala usimfanye chochote yule demu"

Ema "Yule demu mwanangu anazingua kinoma"

Mimi "Halafu Headmaster alisema ukamuamshe aandae yale masomo"

Ema "Halafu kweli umenikumbusha,ngoja nikamuamshe!"

Sasa wakati tunaongea yule mwanamke alirudi kwa wenzie na wakaendelea kushangaa shangaa,tulichokifanya na Ema pale kwa ule muda mfupi ni hakika walidhani hatuwaoni kumbe lengo lilikuwa ni kumuondolea Ema uoga na kuwapoteza maboya!.
Ema aliamka akatoka kwenda kumgongea Headmaster chumbani kwake ili aje ajionee!,sasa wakati Ema ameondoka,nilianza kujipigisha mruzi wa uongo na kweli ili kuikabili ile hali kwasababu ilikuwa inatisha si kitoto!..

Headmaster "Umughaka tacho omahe"

Baba alipotoka nje aliniita kwa kilugha nikawa nimetoka nje,sasa alianza kutueleza ya kwamba tusishituke na tuendelee kuwa watulivu,alitwambia Ema achukue madaftari tuelekee wote sebuleni ili iwe rahisi kuwakabili,mimi nilimwambia wao wakae sebuleni na mimi nirudi chumbani kukaa karibu na kibuyu kwa kazi maalumu!.
Basi wale watu wakawa wamepotea ghafla mle chumbani!,nilitoka nje kwenda kumwambia Headmaster.

Headmaster "Ngoja tusubiri,yawezekana wakawa wameshituka"

Mimi "Lazima warudi"

Headmaster "Halafu mbona yule mzee hayupo?"

Mimi "Uenda leo kawaagiza hawa"

Wakati tukiwa tunaendelea kuongea pale,Maza mdogo akamwambia Headmaster kwa kikurya kwamba,wale watu wako kule chumbani kwake na anawaona,Headmaster akamwambia atulie na asipige kelele!.Sasa tukiwa tunaendelea kuongea pale sebuleni huku Headmaster akijifanya kumpigisha Ema pindi,tukasikia kishindo kikubwa tena pale uani!.

Haukupita muda akawa ametokea yule mzee makono akiwa na usinga mkononi huku akiwa uchi kama wenzie!,akaja mpaka pale sebuleni huku tukiendelea kumpimia tu!,aliendelea kuangaza huku na huko na hatimaye akawa ameingia mle chumbani kwa Headmaster.Basi baada ya kuingia chumba cha Headmaster,Headmaster aliinuka kwa ghadhabu huku akisema "Lero n'uramanye uwe tombanyoko" (Leo utanitambua).

Sasa Headmaster alipoingia chumbani alijifanya kuongea na mkewe huku wakiwatazama,sasa nadhani mzee makono aliwaambia wale watu waende wakawalete watu wa kwenda kulima ili wakifika watuunganishe na sisi tuondoke!,wale watu watatu walitoweka wakamuacha mzee makono mle chumbani akitaka kufanya mambo yake ili amchukue Headmaster kama kawaida aje atuunganishe na sisi tuelekee kwenye kilimo cha usiku kisichokuwa na tija!.

Wale watu walipotoweka tu na mzee makono kubaki mwenyewe,Headmaster alichukua kile kibuyu alichopewa na mama yake Monica akakifungua,alipokifungua tu!,yule mzee akaanza kucheza kwa kuzunguka mle chumbani kama mwendawazimu!.Headmaster alituita tukaingia kumtazama,yaani kuna muda nilianza kumuonea huruma maana alikuwa kama amepagawa kwa kushikwa ugoni.

Kadiri muda ulivyokuwa ukienda,wale watu waliotumwa na mzee makono hawakurudi kabisa na nadhani watakuwa walishituka mapema!.Ile hali ilifanya maza mdogo kutoka kule chumbani akabaki mzee makono akizunguka chumba kizima kama mwendawazimu.Usiku huko hakuna mtu aliyepata usingizi kabisa,tumekuja kushangaa imefika saa 11 alfajiri bila kujua!.
Sasa ilipofika saa 12 asubuhi,Mama yake Monica alikuja akiwa na wale kina mama,alihuzunika sana kwanini tuliamua kuwaachia wale watu watatu wakaondoka!.


Mama Monica "Mwalimu nilikwambia,nadhani sasa unaniamini"

Headmaster "Sikuzote Msukuma nakuamini,si leo tu!".

Mama Monica "Kwanini mmewaachia wale washenzi?"

Headmaster "Wameondoka wenyewe"

Mama Monica "Nilikwambia wakifika tu,ungefungua kibuyu"

Headmaster "Nilipoingia chumbani kufungua kibuyu wakawa wameondoka akabaki mzee lameki"


Mama Monica "watasimuliana,hakuna kilichoharibika"

Aliendelea "Haya sema,unataka tumfanye nini huyu mzee"

Headmaster "Nadhani kama kuna uwezo muondolee uwezo wake asije akaponyoka halafu mengine utaniachia mimi"

Mama Monica "Huyu ameshakwisha,hapa hawezi kukuponyoka kamwe"

Aliendelea "Mimi namshughurikia halafu nakuachia wewe utajua cha kumfanya".


Basi mama yake Monica alimsogelea yule mzee akachukua ule usinga kisha akamvua shanga alizokuwa amejivika kuanzia begani kuteremkia kiunoni!,baada ya hapo kuna dawa alimpatia Headmaster akamwambia kukishapambazuka vizuri atampaka ile dawa na kisha atamuondoa mle ndani!.Mama yake Monica na wale kina mama waliondoka wakawa wamemuacha mzee makono humo ndani akizinguka kama mwehu!.

Kulipopambazuka,Headmaster alielekea kwa mwenyekiti wa kijiji na kutaka yowe ipigwe karibia kijiji kizima ili wananzengo wahalifiwe ya kwamba kulikuwa kuna tukio kubwa la kushangaza!,Basi yowe ilipigwa na watu wakawa wanakuja pale nyumbani huku wengine mikoni wakiwa wameshika mapanga na mafimbo!.Haukupita muda mrefu watu wakawa wamejazana pale nyumbani huku wengine wakichungulia dirishani wakishangaa lile tukio!.

Ilipofika mida ya saa 3 Asubuhi baada ya watu kujazana pale nyumbani,Headmaster alifanya kama alivyoambiwa afanye na mama yake Monica,baada ya kupakwa dawa yule mzee alikurupuka akawa anashangaa sana!,alikuwa akizunguka kitafuta usinga wake lakini hakuuona,ndipo Headmaster aliamrishwa na wananzengo ya kwamba amtoe yule mzee nje ya nyumba ili akapambane na viboko vilivyokosa huruma!.

Yule mwenyekiti aliamuru yule mzee avishwe nguo hadi kwenye ofisi ya serikali ya kijiji lakini wananzengo wakagoma,walisema inapaswa atembezwe kijiji kizima huku akila mboko na inapaswa siku hiyo hiyo ahame kijiji!.

Basi nakumbuka Headmaster alimuagiza Ema akalete viboko ili aanze nae mle ndani kwasababu alikuwa akimtafuta sana,viboko vilipoletwa kiukweli yule mzee alichezea kiasi kwamba sikutaka hata kuangalia,viboko vilipozidi aliamua kutoka ndani spidi akikimbilia nje,kufika nje wananzengo wakamdaka nako wakaanza kumsulubisha!.
Alitembezwa kijiji kizima huku akiwa uchi kama alivyozaliwa,kiukweli lilikuwa ni tukio la aibu mno!,sasa walipomfikisha kwake wananzengo hawakutaka mjadala,walimwambia avae nguo kisha atoke,alipotoka waliwasha moto nyumba yake na kila kitu kiliteketea kwa moto!.

Baada ya pale alirudishwa serikali ya kijiji na kutakiwa apotee kwenye kile kijiji ndani ya masaa 2!,hakutakiwa kubaki pale na wananzengo walimwambia watamuua endapo angebaki kwa siku hiyo!.

Lile tukio lilivuta hisia kubwa sana pale kijijini na kiukweli lilimpatia Headmaster ujiko na heshima sana ingawaje mimi ndiye niliyepambana sana mpaka kufikia ile hali.Headmaster aliogopeka sana tangu siku ile lile tukio litokee na hakukuwahi tena kuwa na mambo ya ajabu pale nyumbani.

Headmaster kwa baadae alihama ile shule na kuhamia huko Biharamulo ambako amejenga na anaishi hadi leo,mimi niliondoka na kurudi nyumbani kisha kuelekea shuleni Advance!.

Ema yupo hapo Shinyanga anauza duka la vipuri vya magari,amejenga na anaishi hapo hapo shinyanga.

Monica kuna wakati niliambiwa yupo Mwanza ila sijajua ni Mwanza sehemu gani!,kuna mtu nilikutana nae wa pale kijijini akawa ameniambia hivyo,kwasababu baada ya mimi kuondoka pale kijijini sikurudi tena hivyo tukawa tumepotezana na mpenzi wangu huyo!.

Mimi kwasasa nipo Dar es salaam napambana na maisha ya kukimbizana!,nina kiboda boda changu japo kimekwisha lakini tunapambana na maisha!.Kijiwe changu huwa ni hapo Bunju ndugu zangu!.



MWISHO.
Safi sana mkuu. Asante kwa stori murua, nitakutembelea kijiweni hapo tupige stori mbili tatu
 
Wakuu nipo kijiweni,kuna muda naamua kuangalia tu comments za wadau,marafiki na ndugu zangu wa JF nabaki kufurahi tu[emoji23][emoji23].

Yaani kama unahasira za kijinga JF haikufai maana unaweza mrushia mtu ngumi ingawaje niya upepo[emoji23][emoji23][emoji23].

Humu kuna watu wanakera

Humu kuna watu wanaudhi

Humu kuna watu wanachukiza

Humu kuna watu wanafurahisha

Humu kuna watu wanajua kila kitu.


Yaani ukitaka kupata raha na karaha wewe tembelea JF [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].

All in All nawependa sana ndugu zangu na tuonane muda si mrefu!

Kwa ufupi kuns ma-idiot wa kutosha, samia kazi anayo
 
Ntakuwa mchoyo wa fadhila nisiposema shukrani na hongera kwa hadithi nzuri iliyobeba uhalisia, kuwafurahisha watu bure free of charge na kuweka tamaa pembeni thawabu zako zinaongezeka. Ukiendeleza moyo huo utafika mbali kiongozi
 
Back
Top Bottom