Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 11.





Zile kelele za wanafunzi hazikunishitua sana kwakuwa nilidhani uenda ingekuwa mambo ya kiuanafunzi tu huko shuleni.

Niliingia ndani kumsalimia Ba'mdogo na mkewe halafu mimi niondoke zangu nikachukue miwa ili nielekee kuuza.Sasa nilimsalimia Ba'mdogo lakini hakuwa akijibu,nilidhani uenda angekuwa amewahi shuleni,nilimsalimia pia Maza mdogo lakini nae hakujibu chochote,sasa nikasema Maza mdogo yeye nikimsalimiaga huwa kama kawaida yake anauchuna!.Niliamua kuondoka zangu niwahi kwa mzee Masumbuko.
Sasa nilipotoka nje kukiwa kumeshamiri mapambazuko,niliendelea kusikia wanafunzi wakipiga kelele kwa mshangao huku wengine wakicheka na kuzungumza kisukuma!,kwakuwa njia ile iliyokuwa ikipita lamboni kuelekea kwa mzee Masumbuko ilikuwa ikipita nyuma ya madarasa ya shule!,ikabidi nisimame kuwaangalia na kuwatazama wale wanafunzi kilichokuwa kinawafanya wapige kelele na kuendelea kucheka huku wengine wakiteta kwa lugha ya kisukuma.

Basi kwakuwa walikuwa wanachungulia darasani ikabidi na mimi nisogee kuchungulia kuona walichokuwa wanashangaa,sasa ile nimefika kuchungulia nikamuona Ema na mama mdogo wakiwa wamelala kwenye sakafu wakiwa wamejifunika shuka jeupe,yaani walivyokuwa wamelala ni kama mtu na mkewe.
Nilihamaki na kushangaa sana,ikabidi nizunguke haraka kuingia darasani nione nini kilikuwa kinaendelea!.Sasa mpaka wakati huo hakukua na mwalimu hata mmoja pale shuleni,wanafunzi nao walikuwa wachache huku wengi wakiwa wanaongezeka kuja shuleni.Nilipoingia ndani ya darasa ambapo niliwakuta wanafunzi wengine wakishangaa,sikutaka kuuliza maana ile ilikuwa ni aibu ya karne.

Nilianza kumwamsha Ema kwa kumshitua na kumpiga piga mabega hatimaye akashituka,aliposhituka akaanza kupiga miayo na kujinyoosha kana kwamba ni mtu aliyekuwa na hangover ya pombe,baada ya kushituka na kujitambua alikuta wanafunzi wengi wakicheka na wengine wakiwa wanashangaa;mara ghafla Maza mdogo naye akawa ameshituka ghafla mpaka kupelekea sehemu ya kifua chake kubaki wazi na maziwa kuonekana mbele ya wanafunzi,alibaki anahamaki kama mwendawazimu!.
Kwakuwa walikuwa wamejifunika shuka moja na wote wakiwa uchi,nilimaambia dogo mmoja avue sweta limsitiri Ema ili akimbie nyumbani,ndivyo ilivyokuwa.

Nilimpa lile sweta Ema nikamwambia asimame alivae liwe kama sketi ili atoke aende nyumbani,ingawaje aliposimama alikuwa uchi na wanafunzi walishuhudia kila kitu!,mama mdogo yeye alikuwa akivuta lile shuka ili kujisitiri na ndipo nilimnyanyua na kuondoka naye huku akiendelea kushangaa amefikaje hapo na nini kilikuwa kinaendelea.Wanafunzi waliokuwepo mpaka wakati huo wengi walikuwa wakicheka na wengine kushangaa ni kitu gani kile!.

Sasa tulipofika nyumbani Maza mdogo alikuwa akiniuliza ni nini kimetokea na kwanini wamejikuta wakiwa uchi pale darasani.Mimi sikuwa na majibu zaidi ya kushangaa.Kumbe wakati huo tunajadili pale headmaster alikuwa amelala chumbani,sikufahamu wakati namsalimia alikuwa akinisikia ama la!.

Ba'mdogo "Hebu niwekee maji ya kuoga"

Alikuwa akimwambia mkewe lakini mkewe akawa anamshangaa headmaster.

Maza "Ina maana ba'Mary kinachoendelea wewe hukijui?"

Ba'mdogo "Kuna nini?"

Maza "Nimefikaje shuleni tena nikiwa uchi mbele ya wanafunzi?"

Ba'mdogo "Shuleni uchi,uchi kivipi?"

Ba'mdogo "wewe siumetoka muda si mrefu kuniamsha ukaniambia nachelewa shuleni,sasa umetoka saa ngapi kwenda shule ukiwa uchi?"

Baada ya kauli ile ya Ba'mdogo nikajisemea ndo yale yale ya Ema ya siku ile kuning'inizwa juu ya kenji.Baba mdogo ni kama alikuwa aelewi chochote kabisa na muda huo yeye alikuwa anadai Maza mdogo alikuwa ndani amelala.

Maza "Mungu wangu hiki ni nini?"

Basi hakutaka kupoteza muda akawa ameingia ndani!,basi Headmaster nilijaribu kumuelezea lile tukio lilivyokuwa lakini ni mtu ambaye ilionekana kama hakubaliani nalo,yeye akakomaa kwamba mkewe alikuwa chumbani na ndiye aliyemuamsha awahi shuleni.
Siku hiyo ikawa gumzo hapo kijijini na shuleni pia,talk of the town ikawa hiyo stori ya mke wa mwalimu!,Mazungumzo ya wengi walisema uenda mke wa mwalimu walikuwa na mahusiano na Ema na siku hiyo baada ya mizagamuano ya muda mrefu walichoka wakapitiwa na usingizi,wengi waliamini hivyo japo mimi niliamini lile tukio halikuwa la kawaida!.

Siku hiyo sikuondoka kuelekea kufata miwa ikabidi nitulie nyumbani,sasa nilijaribu kumuuliza Ema uenda alikuwa amifahamu jambo lolote!.

Ema "Yaani sielewi hata nilifikaje pale"

Mimi "Ina maana hukujua kama umelala na Maza mdogo?"

Ema "Mimi nimeshituka tu naona wanafunzi kaka,sielewi kiukweli nilifikaje pale"

Kiukweli hali ile haikuwa nzuri lakini nilibaki kucheka kama mazuri vile lakini hali ilikuwa inatisha sana,japo halikuwa jambo jema,lakini kimoyo moyo nilikuwa nasema angalau sasa Maza mdogo atapunguza mdomo wake!.

Headmaster baada ya kwenda shule muda haukupita alirudi nyumbani,sasa akawa anajaribu kumuuliza mke wake kama lile jambo ni kweli!,basi kumbe kuna wanafunzi shuleni pia walikuwa wamemueleza vilevile kama ambavyo nilimueleza,sasa akaamua kuwarudisha wanafunzi wote nyumbani na kikaitishwa kikao cha kijiji siku hiyo hiyo.Sikutaka kukosa kwenye kile kikao kwasababu nilikuwa mmoja wa mashuhuda na wanafunzi kadhaa!.

Kikao kile kilizungumza mambo mengi mno,kila mwanakijiji alikuwa akizingumza jambo lake.Wapo ambao walikuwa wanasema hizo tabia za kijinga zikome mara moja na wapo wengine waliokuwa hawakubalini na lile jambo.
Sasa yule mzee ambaye nilikutana naye ile jioni wakati natoka kuuza miwa akaniambia nimsalimie mwalimu,yeye pia alikuwa ni mmoja wa watu waliofika kwenye kile kikao na hakukubaliana na lile jambo.

Mzee "Kwanini kila siku ni nyie tu na siyo kwa watu wengine?"

Mzee "Hapo naanza kupata mashaka kidogo"

Mzee aliendelea "Juzi ilikuwa kwa kijana wako na tukaja mpaka kwako mwalimu,leo tena mambo ni yaleyale,ili jambo lingekuwa kwa watu wengine hapo kungekuwa na walakini,kila siku mambo haya yawapate nyie tu?,sisi tutaamini vipi mwalimu?,kama hutaki kuendelea na shule basi bwana na uache lakini hatuwezi kila siku hatuwezi kuwa tunazungumzia mambo yale yale yanayotokea kwa mtu yuleyule"

Mzee "Ingekuwa uchawi hata sisi ungetupata pia,sasa yawezekana mkeo na huyo kijana anayekaa kwako ni wapenzi!"

Sasa hili suala la Ema na Maza mdogo kuwa wapenzi naona wanakijiji wengi walilishupalia kama kweli vile!.

Akasimama mwana kijiji mwengine akasema "Hiki kituko hakijawahi kutokea kwenye hiki kijiji,na mimi sikubaliani na kwamba eti ni uchawi,haiwezekani kabisa!,huyo dogo na mkeo watakuwa wapenzi na uenda mkeo alitoka ndani akakuacha umelala wao wakaja kufanya yao na wakapitiwa na usingizi,hivyo mwalimu nikuombe umchunguze mkeo!"

Watu wengi waliunga mkono ile kauli ya mzee na huyo jamaa.

Headmaster alishindwa aseme nini mbele ya ile kadamnasi,sasa mwenyekiti wa kile kijiji ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa kile kikao alisema kile kijiji hapo mwanzo ni kweli kulikuwaga na habari za washirikina,lakini baada ya kuitisha vikao kadhaa yale mambo yakapotea.


Mwenyekiti " Mimi niseme tu kwamba,yawezekana haya mambo yakawa yamerudi,mimi pia nikiongozi wa kimila na kama haya mambo yamejirudia ningefahamu mapema sana,sasa nadhani Mwalimu unakumbuka tukio la kijana wako,na nilikwambia pia tusiendelee kudhani ni ushirikina kumbe kijana wako ndiye mkorofi amewachokoza wenzie wakaamua kumuadhibu kwa style ile,hivyo nikuombe umchunguze na kijana wako pia".

Basi kile kikao baada ya kuchukua masaa kadhaa kikawa kimemalizika lakini jibu lilikuwa ni kwamba Ema yawezekana alikuwa na mahusiano na mke wa mwalimu.Tulitawanyika pale na kila mtu kwenda kuendelea na shughuli zake.

Headmaster hakutaka kabisa kuamini ya kwamba siku hiyo Ema alilala na Mkewe kwenye darasa,alichoamini yeye ni kwamba siku hiyo mkewe alikuwa chumbani wamelala wote,yaani ni kama mtu ambaye alikuwa amepofushwa!

Kiukweli lile tukio lilikuwa ni gumzo sana hasa ukienda hadi senta huko na nadhani pia kwa upande wa Maza mdogo ni tukio ambalo hatokuja kulisahau kwenye maisha yake.Baada ya siku kusonga lile tukio likawa kama linafifia.

Sasa Maza mdogo akawa naye ameanza kushona cherehani pale senta,alikuwa akitoka asubuhi anarejea jioni,muda ambao mimi nilikuwa nikimaliza shughuli ya kuuza miwa inabidi nimshubiri na yeye amalize tuongozane kurejea nyumbani.

Sasa nakumbuka siku moja nimeamka asubuhi mida ya saa 12 ili niwahi kusudi kuepuka jam ile ya asubuhi bafuni,nimeoga nimemaliza nikavaa kama kawaida ili niende sasa kusalimia kule ndani halafu niondoke zangu mdogo mdogo kuchukua miwa.
Nilifungua mlango wa pale sebuleni ili kuingia ndani niwasalimie Headmaster na mkewe,sasa ile nimengia ndani hapo sebuleni,aiseee nilishuhudia mzigo mkubwa wa mavi ambayo kikawaida kama ungeyapima kwenye sufuria,basi yangeweza kufikia kilo 3,mavi yale yalikuwa yamenyewa juu ya meza na ilionekana aliyekuwa ameyanya alikuwa amekula ugali wa mtama,kwasababu kile tunachokula ndiyo tunachokinya!,Sasa harufu ilikuwa kali sana na kiukweli nilishindwa kuelewa waliwezaje kulala ndani kukiwa na harufu kali kiasi kile,baada kushuhudia ule mzigo nikarudishia mlango kwenda kumshitua Ema ili aje ajionee!.
Wahuni wameweka makimba mezani[emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom