Boogman
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 2,439
- 5,612
Kuvuja c linavuja kila mwezi[emoji849]Kwamba linavuja ama? [emoji28][emoji28]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuvuja c linavuja kila mwezi[emoji849]Kwamba linavuja ama? [emoji28][emoji28]
Pakizibwa itakuajje?Kuvuja c linavuja kila mwezi[emoji849]
OhooooooTulichomfanya Yule mchawi hata kuja kusahau - 2
Sasa siku moja nakumbuka ilikuwa kati kati ya wiki nadhani kati ya J4 au J5, siku hiyo kulikuwa kuna mashindano ya Uefa champions ambapo timu yangu pendwa ilikuwa ikicheza na Chelsea.
Nilijiandaa mapema kabisa ilipofika mida ya saa 1 usiku nikamwambia Dingi mdogo anipe ruhusa na bila ajizi akaniruhusu kwenda kutazama kabumbu, japo alinisisitiza nisiende maana wakati wa kurudi ingekuwa shida lakini mwanaume sikutaka kuelewa hata kidogo. Baada ya kuona nimekuwa mbishi na mpira uko kwenye damu aliamua kuniruhusu huku akisema "Uwe makini maana huu mji siyo huko ulikotoka, huu mji una wenyewe".
Basi nikamuomba yule jamaa tuondoke nae jamaa akagoma akasema yeye anajisomea,sikutaka kuchelewa ikabidi niondoke zangu. Plani yangu ilikuwa ni kwamba niondoke hiyo saa 1 ili kufika kwenye ngoma 2 niwe nimefika nikapige soga na kubadilishana mawazo na mashabiki wengine pale kwenye banda huku tukisubiri mpira uanze.
Sasa kwenye ile njia ya kwenda hapo senta ulikuwa ukifika katikati ya senta na mahali ninapoishi kulikuwa na miti miwili mikubwa mno ya miembe ambayo sikuwahi kuona ikitoa miembe kwa miaka 2 niliyokaa hapo kijijini.Ile miembe ilikuwa pembeni ya ile njia,yaani ile barabara ilikuwa ikipita katikati ya ile miembe miwili mikubwa.
Kwa kuwa siku hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu kwanza kupita hapo usiku nilikuwa naona kawaida tu na wala sikuogopa chochote.
Baada ya kufika kwenye banda la mpira ilibidi nisubiri hadi luninga itakapowashwa,ulipofika muda jenereta liliwashwa na tukaingia ndani kwa ajili ya kutazama mpira,kama nilivyosema mechi ilikuwa kati ya Arsenal na chelsea na ilikuwa ligi ya mabingwa hiyo ilikuwa mwaka 2004. Arsenal tulipigwa Goli 2-1 tukiwa kwenye uwanja wetu wa nyumbani Highbury,nakumbuka Goli letu lilifungwa na Jose Antonio Reyes huku yale ya Chelsea yalifungwa na Frank lampard na mchezaji mwingine ambaye nishamsahau!
Basi bana baada ya mechi kumalizika hiyo mida ya saa tano usiku kila mmoja akatawanyika kwenda alikotoka na mimi nikashika njia yangu kurudi nilikotoka,Japo ile mechi tulipoteza lakini furaha yangu mimi ilikuwaga kuwaona Arsenal tu hata ifungwe vipi nilikuwa napata amani ya moyo.
Sasa ile njia niliyotokea mimi nilijikuta nipo pekee yangu kwasababu kule nilipokuwa nina kaa ilikuwa ni njia maalumu ya kwenda shule na nyumba za walimu,hivyo hakukuwa na mwana kijiji aliyekuwa akielekea kule,basi nikaanza kutembea kuelekea nyumbani!
Kila nilipopiga hatua ndivyo ukimya ulivyokuwa kuwa ukitawala,kulikuwa na giza la kitakatifu kwa usiku huo,zilikuwa ni sauti za wadudu wale waliao usiku tu ndizo zilisikika.Nilipotembea sana ndipo sasa kwa mbali baada ya kuikaribia ile miembe kama umbali wa mita 500 nikaona ikiwaka moto mkubwa sana. Ilibidi nisimame kwanza nitazame vizuri uenda nilikuwa sijaona vizuri.
Kweli bana!,ilikuwa ni ile miembe ikiwaka moto, sasa nikawa najiuliza ni nani alikuwa amewasha ule moto?,basi nikajipa moyo nikaendelea kupiga hatua nikiamini uenda kulikuwa kuna watu wikuwa wameichoma kwa bahati mbaya,sasa ajabu kadiri nilivyokuwa nikisogea ndipo moto nao unapungua!,kiukweli nilibaki kushangaa sana na wakati huo akili yangu haiwazi mawazo ya kijinga kuhusu wachawi!
Basi baada ya kufikia kabisa ile miembe sikuona moto wala moshi,sasa nilipofika katikati ya ile miembe,nilihisi kama watu wanacheka kwa nguvu mno huku mwili wangu ukisismka sana!,yaani hadi nilihisi vinyweleo vimesimama, nilichofanya niliinama nikakamata ndala nilizokuwa nimevaa nikatoka nduki kama mwendawazimu, sasa baada ya kufika mbele kabisa ilibidi nisimame nipumzike maana nilikuwa nahema kama mbwa mlafi!,Niligeuka tena kuitazama ile miembe kwa mbali nikashangaa kuona tena ikiwaka moto,kiukweli ilibidi niondoke hilo eneo kwa haraka sana.
Namshukuru Mungu nilifika nyumbani usiku huo ikiwa inakaribia saa 7 usiku,nilimgongea yule dogo ambaye kwa wakati huo alikuwa yuko macho bado akiendelea kupiga buku.Baada ya kunifungulia mlango alishangaa nikihema kwa nguvu kama nilikuwa nafukuzwa.
Jamaa "vipi mbona unahema sana"
Mimi " Nilikuwa nakimbia niwahi kufika"
Jamaa " Mpira umeisha?"
Mimi " Umeisha ila tumepigwa"
Sasa baada ya maswali na majibu kadhaa hapo ndani ikabidi nimuulize yule jamaa maswali kadhaa!.
Mimi " Hivi ulishawahi kutembea usiku huku"
Jamaa "Hapana,mwisho wangu ni saa 12 tu inapaswa niwe ndani,siunamjua tena ticha alivyo mkora!"
Mimi " wakati narudi nimepita pale kwenye miembe nimekuta inawakata moto"
Jamaa "Ile miembe ya kule chini?"
Mimi " Eenh ile ya pale chini"
Jamaa " Ina maana imechomwa moto?"
Mimi " Hapana,yaani wakati naikaribia ilikuwa inawaka moto,ila baada ya kuifikia nikakuta hakuna moto wowote na nikasikia pipo zinacheka kishenzi"
Baada ya kumsimulia jamaa akaanza kucheka sana huku akiniambia "Kijana naona unachezea kifo"
Jamaa" Ile njia haifai hata kidogo sema tu nilishindwa kukwambia,siku nyingine ukiwa unaenda mpirani uwe unapitia ile njia ya kule lamboni"
Sasa jamaa njia aliyoniambia ni njia ndefu mno ya kuzunguka,lakini ile ya kwenye miembe ni fupi.
Jamaa " Hapa mbona sisi tumepata taabu sana,usione sasa hivi kumetulia ukadhani tulikuwa salama"
Mimi " Kumetulia kivipi?"
Jamaa " Kuna siku nimerudi kutoka shule kuja kupika nikakuta mavi ya mtu kwenye dumu la unga"
Jamaa akaendelea " Tumefanyiwa vituko mno hadi ikabidi Ticha akaitisha kikao cha wazazi na wana kijiji na akatishia kuondoka huku ndipo angalau mambo yakapungua,huku ni hatari sana kijana kuwa muangalifu utapotea"
Baada ya jamaa kunipa maelezo hayo kidogo niliogopa sana na shida ikawa nitaangalia wapi mpira?
Sehemu ya tatu
Utam juu ya utam[emoji39]Pakizibwa itakuajje?
Ambapo ni mbele ya hapa au nyuma ya hapa kwamba huko ni fupi fupi zaidi????KULE TELEGRAM TUPO SEHEMU YA 20😂😂😂😅😅😅
Mazeee kitu tayari mkuje mkujee!!Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 15.
Nilifungua ule mlango ulokuwa umefungwa kwa komeo nikatoka nje na kuanza kukimbia kama mwendawazimu.Niliingia kwenye shamba la jirani na hapo kwao Monica lililokuwa na mahindi madogo saizi ya magoti kisha nikalala chini!.Nilishindwa kuelewa mpaka muda huo binti Monica atakuwa yupo wapi maana mlango haukufunguliwa na yeye ndani hakuwepo!.Sasa nilinyamaza kimya ili kuona ni kitu gani kilikuwa kinaendelea.
Baada ya kama dakika 20 hivi,nikawa nasikia sauti ya Monica ikiniita kuashiria kunitafuta,mimi niliendelea kukaa kimya huku nikichukua tahadhari na nilidhani uenda asiwe Monica nikaingia chaka!.Kwa mbali niliona ule mlango wa ile nyumba unagunguliwa mtu akaingia ndani kisha akatoka tena akawa anaita.Baada ya kujiridhisha kwamba alikuwa Monica ndiye aliyeniita,niliamua kusimama na kujipangusa mchanga uliokuwa umenijaa kwenye tumbo na magoti na hii ilikuwa ni baada ya mimi kulala chini!,mpaka wakati huo nilikuwa kama nilivyozaliwa maana nilipokurupuka sikukumbuka hata nguo nimeziweka sehemu gani!
Monica "Uko wapi?"
Monica alijifanya kuniuliza niko wapi kana kwamba alikuwa hanioni,ila nilichoamini mimi ni kwamba alikuwa akiniona tu vizuri!.Niliondoka kuelekea ule uelekeo alokuwa amesimama Monica.
Monica "ulikuwa wapi?"
Mimi "Nilikuwa pale"
Monica "Sasa huku nje umefata nini!?"
Mimi "Wewe ulienda wapi?"
Monica "Mimi mbona nilikuwepo?"
Mimi "Ulikuwepo wakati nimekutafuta sikuoni!?"
Monica "Kuna mjinga mmoja nilikuwa namshikisha adabu"
Mimi "Mjinga gani?"
Monica "Hukusikia napigana na mtu"
Mimi "Mimi sijasikia,nilichosikia ni kishindo kikubwa nyuma huko nageuka nakuangalia na wewe hauonekani,ndiyo nikatoka kukimbia"
Monica "Nilikwambia umughaka nitakulinda usiku na mchana,kuna mjinga alikuja kutaka kunijaribu,nimepambana nae alitaka kunishinda nikamuita mama"
Mimi "Kwahiyo mama yupo ndani!"
Monica "Mama amemchukua amempeleka wakamtengeneze vizuri!"
Basi baada ya kuniambia maneno yale ilibidi tuingie ndani,kiukweli nilikuwa nina hofu sana na nilijilaumu kwanini nimeingia kwenye mahusiano na yule binti,kibaya zaidi siku zilivyokuwa zikienda ndivyo na mimi nilikuwa siambiliki wa kuelezeka kwa yule binti!,ilifikia pointi ambayo nisipokuwa nikimuona nilikuwa ninapata mawazo sana.
Mida hiyo ilikuwa yapata saa 9 usiku na tangia hapo sikupata usingizi tena,ilipofika mida ya saa 10 kuelekea saa 11 ambapo niliona kabisa kama kuna miale ya mapambazuko,nilimwambia anisindikize kurudi nyumbani.
Monica "Mbona unawahi hivyo?"
Mimi "Nadhani unamjua Ema alivyo muongo,na najua kama aliamka kwenda chooni akakuta sipo sijui itakuwaje,lazima tu amwambie Ba'mdogo"
Monica "Yule hawezi kuamka mpaka wewe ufike"
Mimi "Wewe yule humjui vizuri!"
Monica "Basi tufanye kidogo halafu ndiyo uende"
Kiukweli sikuwa kabisa na hamu tena ya mizagamuano ila kwakuwa alitaka sikuwa na namna,ikabidi tulianzishe tena!.Fimbo ziliendelea mpaka sasa nikawa nasikia majogoo yanawika huko nje kuashiria kumepambazuka!.Nilivaa zangu nguo na yeye pia akavaa na safari ya kunisindikiza kwetu ikachukua nafasi.Monica hakutaka kabisa kuniacha njiani,alihakikisha mpaka naingia ndani ndipo na yeye anarudi kwao.
Ilikuwa ni kama kuonekana kwao ni mbali lakini nilipokuwa nikitembea na yeye sikuwahi kuona wala kuhisi umbali wowote,hebu fikiria umbali wa zaidi ya kilometa 6 lakini ndani ya dakika kama 10 mnajikuta shafika!,haya yalikuwa ni maajabu ya binti wa kisukuma Monica.Basi baada ya kuhakikisha nimefungua mlango na kuingia ndani na yeye aliondoka kurudi kwao.
Nilisukuma mlango nikaingia ndani nikakuta Ema bado amelala,sasa sikufahamu aliamka wakati mimi sipo ama la!.Kwakuwa kulikuwa kumepambazuka sikutaka kujiegesha maana niliona ningepitiwa na usingizi,nilijifanya namuamsha jamaa ili nione!.sasa baada ya kumpiga piga na mkono,jamaa alishituka sana!.
Mimi "nimekushitua?"
Ema "Maanangu nilikuwa naota"
Mimi "Ooh,jana ulichoka sana nini!"
Ema "Yaani sijawahi kulala usingizi mtamu kama wa leo"
Mimi "Kumekucha kijana jiandae uende skonga"
Ema "Leo sidhani kama nitaenda"
Mimi "Shida nini?"
Ema "Nahisi kuchoka tu"
Sasa jamaa alikuwa ananieleza huku akiendelea kupiga miayo ya kufa mtu!.Nilipoendelea endelea kumdodosa ndipo nikagundua tangu ule usiku nilipotola hakuwa ameamka hata kidogo!.
Basi kulipopambazuka zaidi nilielekea lamboni kuchota maji ya kuoga na kurejea nyumbani,basi baada ya kumaliza kila kitu niliingia ndani kumsalimia Headmaster na mkewe na kisha mimi kuelekea kwa mzee masumbuko kuchukua miwa ya kwenda kuuza.Sasa wakati unatoka hapo kwa mzee masumbuko ili uikamate njia ya kuelekea Senta,kulikuwa kama na makutano ya njia,njia moja ndiyo njia ambayo ilikuwa inatoka kwenye uwanja unapofanyikia mnada na ukipandisha nayo inakupeleka moja kwa moja kwa kina Monica kule Masairo,njia nyingine ni njia ambayo ilikuwa inakupeleka mpaka lamboni ambako unatokea mpaka shuleni,na njia nyingine ndiyo njia ambayo nilikuwa naipita mimi kuelekea senta kila ninapotoka kuchukua miwa!.
Sasa wakati naikamata njia ambayo ilinipaswa kupita kwa mbele kuna kina mama walikuwa wakija wakiwa wawili,mmoja wapo nikama nilimuona kwenye zile ngoma pale kwao Monica ule usiku!,sasa walizungumza kisukuma halafu wakawa wananitazama sana,nikama walikuwa wananiteta!,waliponipita nilihisi kabisa wanaendelea kunitazama,sasa nilipofika kwa mbele nikautua ule mzigo wa miwa nikajifanya kama naufunga kwa kukaza,nikawaangalia kwa kuibia ndipo nikaona wananitazama na nikama wakawa wanazungumza kwa kubishana!,walipoona nawaangalia wakaondoka huku wakionekana kama kunishangaa!.
Sasa nikabaki namuangalia yule mama ambaye nilimuona ule usiku nikabaki kushangaa tu,kiukweli ukikutana naye hivi kwa mara moja na ukiambiwa mambo anayoyafanya huwezi kabisa kuamini!.Nilijitwisha zangu zigo la miwa na kuondoka huku nikishindwa kuelewa kwanini wale kina mama walikuwa wakiniangalia kwa makini sana!.
Siku hiyo biashara ya miwa ilikuwa mbaya sana,kiukweli tangu asubuhi hadi jioni niliuza pingili tatu tu za muwa,basi kwakuwa nilijua biashara siku zote haifanani sikutaka kujipa presha kabisa,nilipanga Headmaster akiniuliza nitamaambia ukweli ya kwamba biashara imekuwa ndivyo sivyo,basi ilipofika jioni nilienda kupeleka miwa kwa yule mama aliyekuwa akinifadhia na mimi kuondoka kueleke nyumbani,wakati wote nilikuwaga naondoka hapo senta mida ya saa 12 jioni na kufika nyumbani mida ya saa 1 kuelekea saa 2.
Sasa nilipotembea kwa umbali mrefu,huku nikiwa naendelea kuitafakari siku,mara ghafla mbele yangu akatokea yule mzee Makono ambaye pia alikuwa mmoja aa wale watu waliokuwa wakicheza ngoma ule usiku,nilishangaa sana kwasababu eneo nililokutana nae,ndilo aneo ambalo siku ile nilikutana nae na akanitaka nikamsalimie Headmaster,safari hii nilishituka sana mpaka akashangaa!.
Mzee makono "Unishituka nini wewe!"
Mimi "Mzee shikamoo"
Mzee makono "Kwahiyo hujashituka jana leo ujifanye kushituka!"
Kiukweli nilishangaa sana na ghafla uoga mkuu ukaniingia,nilishindwa hata kukimbia nikabaki nimepigwa na bumbuwazi,sasa nilibaki kushangaa kwasababu iliwezekana vipi jana kuniona na wakati Monica aliniambia sababu ya yeye kunipaka ile dawa ni kusudi nisionekane na wacheza ngoma kama adui na wahisi mimi ni mmoja wao!,pili nikajiuliza yeye mzee makono alinionaje?,Sasa wakati naendelea kutafakari nisijue cha kufanya,akaendelea kuniambia kwamba
Mzee makono "wewe na kale kakondefu mmeshirikiana kunitesea mwanangu!,si ndiyo?"
Akaendelea "Nataka leo unitambue mimi ni nani!"
Sikutaka kabisa kumjibu yule mzee nikawa nimebaki kimya kwa bumbuwazi,basi baada ya kuniambia maneno hayo akasonya kwa kufyonza kisha akaondoka!,kiukweli ongea ya yule mzee alionekana kabisa amechukizwa sana na alikuwa na hasira mno!.
Sikufahamu kwa haraka haraka ni kitu gani kilikuwa kimemkasirisha na ni nani aliyekuwa amemtesa mwanaye!.
Basi kutokana na uoga niliyokuwa nao,nikaanza kukimbia ili kuwahi nyumbani,safari hii nilipofika pale kwenye miembe nilipita kwa spidi kali mno kama kipanga na sikutaka hata kugeuka nyuma!.
Sasa nilipofika karibu na nyumbani nilimkuta Monica akiwa amesimama anaongea na Ema.
Ema "Haya huyo hapo ongea nae"
Baada ya kusema hivyo Ema akawa anaelekea ndani!.
Mimi "Kwani kuna nin?"
Monica "Tuondoke hapa"
Mimi "Nakupenda umughaka,nakuomba tuondoke,utajua huko huko"
Basi Monica akanishika Mkono tukaongozana kuelekea nisipopafahamu.Mpaka muda huo hata ndani sikufika kabisa.
Mimi "Tunaenda wapi?"
Monica "Nilikwambia nitakulinda kwa gharama yeyote,huyo mjinga anajifanya mjanja muache".
Yani kule tuko mbele zaidi mpaka Headmaster nae keshakuwa mchawi hatari😜😜😜Ambapo ni mbele ya hapa au nyuma ya hapa kwamba huko ni fupi fupi zaidi????
UMUGHAKA for president 2025Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 12
Jamaa alipokuja akafungua mlango na kutazama aliondoka ghafla ameshika pua kutokana na ile harufu namna ilivyo kuwa ya kutisha.
Ema "Nani Kanya hayo mavi?"
Mimi "Sijui"
Mimi "Nimeamka kuja kusalimia ndiyo nakutana na hii hali"
Ema "Headmaster bado amelala?"
Mimi "Bado sijajua,hebu ngoja niwagongee"
Nilienda kujaribu kugonga ule mlango lakini ulifunguka wenyewe kuashiria ulikuwa wazi,basi nikaanza kuita lakini hakukuwa na mtu mle chumbani aliyeitikia!,niliamua kusukuma ule mlango na kuchungulia chumbani kwa Headmaster lakini hakukuwa na mtu!.
Basi nilitoka nikamwambia Ema Headmaster na Mkewe hawapo chumbani.
Ema "Mmmh huu mji aisee mimi utanishinda"
Mimi "kwanini?"
Ema "Hivi unadhani hii hali niya kawaida?,hivi siunakumbuka nilikwambia kuna siku nimekuta mavi kwenye lile debe la unga!"
Ema "Haya mambo si yakawaida,mimi shule ikifungwa sidhani kama nitarudi huku tena"
Mimi "Dingi atakuwa ameenda wapi?"
Ema "Inaonekana wameamka mapema kuna mahali watakuwa wameenda,na nadhani haya mavi niya muda huu tu,Headmaster angekuwa ameyaona najua angetuamsha!".
Basi nilimwambia Ema tuibebe ile meza na kuitoa nje ili kuifanyia usafi,niliingia stooni nikachua jembe nikawa nakokota yale mavi kutoka mezani na kuangukia chini,baada ya kuisha juu ya meza,nilienda kuzoa michanga na kuyafukia yale ya pale chini na kuanza kuyazoa na kwenda kuyatupa huko nje!.Baada ya kuiosha ile meza ikabidi niianike juani ili ipigwe na jua la kutosha!.
Nilipomaliza na kufanya ndani usafi niliondoka zangu kuelekea kwa mzee masumbuko kwa ajili kufata miwa.Sasa siku hiyo sikuona kile kibanda cha Maza mdogo kikifunguliwa,nilihisi uenda aliamua asije tu kwa kuchoka kwasababu kama kweli walitoka yawezekana akawa alichoka.Ile jioni baada ya kumaliza biashara yangu ya uuzaji miwa nikaamua kurudi zangu nyumbani kama kawaida.
Nimefika nyumbani mida ya saa 2 usiku nikakuta hapo uwani yupo mzee mmoja ambaye alikuwa amekaa kwenye stuli,nilimsalimia na kuingia zangu chumbani kwetu.Sasa muda kidogo nikasikia sauti ya Headmaster ikisema "umesharudi?"
Mimi "Ndiyo baba,shikamoo"
Ba'mdogo "Nani umughaka?"
Mimi "Ndiyo baba ni mimi"
Ba'mdogo "aah mi nilidhani ni huyo mpumbavu,nimemwagiza muda sasa sijui linafanya nini huko"
Ba'mdogo "Hebu nenda ukamuangalie huyo mjinga kwa mzee masalu,ukimkuta umwambie achume kabisa na fimbo aje nazo"
Mimi "Sawa baba"
Ba'mdogo "Kimbia bhana na muwahi hapa".
Basi nikatoka nduki kuelekea kwa mzee mmoja aliyekuwa na ng'ombe wa kutosha hapo kijijini akifahamika kama mzee masalu,sikuwahi kufika kwa huyo mzee ila kwasababu ya umaarufu wake pale kijijini nilikuwa nikimfahamu na kwake pia palikuwa pakifahamika.Nilifanikiwa kufika kwa huyo mzee hiyo mida ya saa 2 kuelekea saa 3 usiku.
Nilipofika nilikuta bado watu wako nje wakipiga soga,nilisogea kwa mtu mmoja ambaye ni mwanamke nikamsalimia na kujitambulisha ya kwamba nilikuwa nimeagizwa na mwalimu Wambura.Basi nikawa nimemuomba aniitie mzee masalu ili niweze kumuulizia kuhusu Ema.
Yule mama aliniambia "Hebu Nenda kwenye lile zizi kule utamkuta huko anakagua mbuzi"
Basi nikazunguka nyuma ya nyumba kuliko kuwa na zizi la mbuzi,nilimkuta mzee akiwa na vijana kama 3 wakiendelea kusavei kwenye lile zizi huku wakiongea kisukuma,nilimsalimia mzee na ndipo nikajitambulisha kwake.
Mzee Masalu " Ooh yule kijana wa mwalimu wambura mbona nimempa na ameondoka muda mrefu"
Mzee masalu "Uenda mtakuwa mmepishana,ametoka hapa muda si mrefu"
Mimi "Sawa mzee mimi naondoka"
Mzee Masalu "Sawa msalimie mwalimu".
Basi sikutaka kupoteza muda nikatoka nduki kurudi nyumbani kumpelekea taarifa Headmaster.Nilipofika nyumbani nilimkuta Ema naye akiwa amefika lakini inaonekana Headmaster alikuwa amemgombeza sana maana alikuwa amevimba kama chura!.
Sasa kumbe jamaa alikuwa ameagizwa damu ya ng'ombe,na yule mzee niliyemkuta pale nyumbani wakati mimi natoka senta kuuza miwa alikuwa mganga,hivyo alikuja kwa ajili ya kufanya zindiko pale nyumbani.Wakati wa asubuhi kumbe Headmaster na mkewe walidamka kwenda kijiji kingine kwa ajili ya kumleta huyo mtaalamu na kiboko ya wachawi kama alivyojinasibu!.
Tulitakiwa kila mtu kuvua shati na kupigwa chale kichwani,mgongoni na kwenye mbavu!,basi lile zoezi lilipokamilika kuna dawa huyo mganga akawa ameichimbia katikati ya nyumba na kututaka kila mmoja kukaa kwa matako huku tukiangalia mashariki na kisha kutamka maneno aliyokuwa akituelekeza!.
Baada ya kumaliza kufanya vimbwanga vyake akawa ameaga ya kwamba aondoke na sisi tukae kwa amani huku tukisubiri kuona matokeo!.
Sasa usiku wakati tukiwa tumelala Ema akawa ananiambia.
Ema "mwanangu unajua nilipita kwa Deborah"
Mimi "Muda gani?"
Ema "Si wakati Headmaster ameniagiza"
Mimi "Kumbe ndiyo maana tumepishana"
Ema "Headmaster naye mnoko tu!"
Mimi "Kwanini?"
Ema "Mwanangu amenitukana kishenzi?"
Mimi "Ni-kupiga kimya tu,sasa utafanyaje"
Ema "Mwanangu halafu debo aneniambia yule mtoto ameeleweka"
Mimi "Nani,Mwise au?"
Ema "Si alikwambia atakupa rafiki yake!."
Mimi "Daaah mi nikajua Mwise"
Ema "Mwanangu yule sura mbaya kakuroga nini!,mbona unampenda hivyo"
Mimi "we acha tu!"
Ema "Halafu lile mbona jepesi tu,wewe subiri kesho shule"
Basi tulilala siku hiyo na hakukuwa na mauzauza hata kidogo.Kutokana na yale mauzauza pale nyumbani ilifika sehemu tukayaona niya kawaida kabisa!.
Kulipopambazuka kama kawaida niliamka nikajiandaa na kwenda kuwasalimia Headmaster na mkewe kisha nikaondoka zangu kwenye kibarua cha uuzaji wa miwa.
Sasa siku hiyo ilipofika mida ya saa 10 jioni nilimuona Ema akiwa anakuja na yule binti mwenye shepu iliyokuwa ikiichanganya nafsi yangu akifahamika kwa jina la Mwise,baada ya kuwaona kwa mbali nilianza kuufuta mdomo wangu ambao ulikuwa umetapakaa uchafu wa miwa na ndipo nikakaa sawa sawa kumkabili Mwise!.
Ema "Ooya demu wako huyu hapa bhana nimemleta akusaidie kuuza miwa".
Ema alivyokuwa mpumbavu alikuwa ananiambia halafu anacheka!,daah nilisikia uchungu wa aibu lakini ningefanya nini?,basi baada ya jamaa kumfikisha yule demu pale aliondoka akaelekea kibandani kwa Maza mdogo ili sisi tuendelee na mazungumzo.
Kiukweli yule binti nilikuwa nampenda ingawaje alionekana sura haivutii.
Sasa nikawa najiuma uma pale hata cha kumwambia nikakosa,nashukuru yeye alikuwa mcheshi na akawa amenianza!.
Mwise "Hivi wewe ndiye unakaaga pale kwa Headmaster eeeh"
Mimi "Yeah ni mimi,yule ni baba yangu mdogo"
Mwise "oooh,kumbeee"
Mwise "Mmh niambie sasa maana nataka kuwahi nyumbani"
Mimi "kwani Ema hajakwambia?"
Mwise "Huyo mjinga amenitoa nyumbani hata hajaniambia chochote"
Mimi "Lini utapata muda nina maongezi na wewe"
Mwise "jamani muda wenyewe ndiyo huu,wewe niambie tu"
Mimi "Unaitwa nani?"
Mwise "Ina maana Ema hajakwambia jina langu?"
Mimi "Ema hajaniambia"
Mwise "Naitwa Mwise"
Mimi "ooh Mwise,unajua mimi nakupenda"
Mwise "ndo hicho tu ulitaka kuniambia?"
Mimi "Yes,ndi hicho tu"
Mwise "Sawa mimi naondoka"
Basi yule binti akaondoka huku nikiendelea kumtazama anavyotingisha dunia kwa msambwanda wake aliyotunukiwa.Nilijiona mjinga na domo zege kwa kumbwelambwela kwa mwanamke niliyekuwa nikimtamani kwa muda mrefu!.
Haukupita muda Ema naye akawa amekuja pale huku akitaka kujua nini kimeendelea,niliamua kumdanganya Ema kwamba binti kakubali na ameniahidi tungeonana siku si nyingi kumbe haikuwa hivyo!.Basi tuliendelea kupiga stori hapo kijiweni na ilipofika mida ya saa 12 nilifunga mzigo nikapeleka kwa yule mama aliyekuwa akinihifadhia na mimi kuondoka na Ema kuelekea nyumbani.
Basi wakati tukiwa tunatembea kuelekea nyumbani huku tukipiga stori za hapa na pale,ghafla kwa mbele nikamuona yule binti Monica demu wa Ema akija akiwa na mabinti wenzie wawili!.
Mimi "Demu wako huyo anakuja"
Ema "Mkaushie,mi sikataki wala nini!"
Basi tulipowafikia yule binti akatusalimu,Ema aliuchuna lakini mimi nilimuitikia.Sasa Ema yeye akawa anaendelea na safari bila kujali,mimi nikaona isiwe kesi ngoja niongee nae.
Monica "Huyo mwenzako mbona asalamii"
Mimi "Mi sijui bhana"
Mimi "Unatoka wapi?"
Monica "Natoka kwa mama mdogo naelekea nyumbani"
Monica "Huyo ndugu yako tangu awe na huyo debora wake kiburi kimemjaa,ngoja tutaona"
Basi sikutaka kusema kitu ikabidi ninyamaze.
Monica "Njoo basi nyumbani leo"
Mimi "Itakuwa ngumu Monica"
Monica "Kwanini?"
Mimi "Sitoweza kutoka,wewe siunajua itakuwa usiku na nalala na Ema,nitaaga naenda wapi?"
Monica "Mimi nakupenda sana na wewe ndiye mama yangu anakufahamu ,usijali nakuja kukufata"
Mimi "Sasa ukija itakuwaje?"
Monica "Hilo niachie mimi,kwanza leo nyumbani kuna ngoma za mwana lemi,nakufata"
Mimi "Unajua inabidi iwe siri isifahamike"
Monica "Hata wakijua wewe ni mtu wangu,hakuna wakunitisha"
Monica "Naenda lakini narudi,hivyo kajiandae".
Basi niliondoka nikawa namkimbilia Ema ambaye alikuwa amefika mbali.
Ema "Huyo mjinga anakwambia nini!"
Mimi "Nilikuwa tu namtuliza ili asijisikie vibaya"
Ema "Mimi sikataki ila kenyewe kutwa kunitafuta tu"
Basi kwakuwa hakujua nilikuwa namtafuna,sikutaka kabisa na mimi kumwambia chochote.
Ingawaje kale kabinti hakakuwa na ndundu(msambwanda)kama wa mwise,mimi nilikuwa ninapooza njaa tu!,sikutaka mambo mengi.
Sasa ilipofika mida ya saa 3 usiku,niliskia sauti ya Monica ikiniita nje,niliamka kujifanya najinyoosha na nilipomtazama Ema nilikuta amelala isivyo kawaida.
Kimehappen shoo MidekoTulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 15.
Nilifungua ule mlango ulokuwa umefungwa kwa komeo nikatoka nje na kuanza kukimbia kama mwendawazimu.Niliingia kwenye shamba la jirani na hapo kwao Monica lililokuwa na mahindi madogo saizi ya magoti kisha nikalala chini!.Nilishindwa kuelewa mpaka muda huo binti Monica atakuwa yupo wapi maana mlango haukufunguliwa na yeye ndani hakuwepo!.Sasa nilinyamaza kimya ili kuona ni kitu gani kilikuwa kinaendelea.
Baada ya kama dakika 20 hivi,nikawa nasikia sauti ya Monica ikiniita kuashiria kunitafuta,mimi niliendelea kukaa kimya huku nikichukua tahadhari na nilidhani uenda asiwe Monica nikaingia chaka!.Kwa mbali niliona ule mlango wa ile nyumba unagunguliwa mtu akaingia ndani kisha akatoka tena akawa anaita.Baada ya kujiridhisha kwamba alikuwa Monica ndiye aliyeniita,niliamua kusimama na kujipangusa mchanga uliokuwa umenijaa kwenye tumbo na magoti na hii ilikuwa ni baada ya mimi kulala chini!,mpaka wakati huo nilikuwa kama nilivyozaliwa maana nilipokurupuka sikukumbuka hata nguo nimeziweka sehemu gani!
Monica "Uko wapi?"
Monica alijifanya kuniuliza niko wapi kana kwamba alikuwa hanioni,ila nilichoamini mimi ni kwamba alikuwa akiniona tu vizuri!.Niliondoka kuelekea ule uelekeo alokuwa amesimama Monica.
Monica "ulikuwa wapi?"
Mimi "Nilikuwa pale"
Monica "Sasa huku nje umefata nini!?"
Mimi "Wewe ulienda wapi?"
Monica "Mimi mbona nilikuwepo?"
Mimi "Ulikuwepo wakati nimekutafuta sikuoni!?"
Monica "Kuna mjinga mmoja nilikuwa namshikisha adabu"
Mimi "Mjinga gani?"
Monica "Hukusikia napigana na mtu"
Mimi "Mimi sijasikia,nilichosikia ni kishindo kikubwa nyuma huko nageuka nakuangalia na wewe hauonekani,ndiyo nikatoka kukimbia"
Monica "Nilikwambia umughaka nitakulinda usiku na mchana,kuna mjinga alikuja kutaka kunijaribu,nimepambana nae alitaka kunishinda nikamuita mama"
Mimi "Kwahiyo mama yupo ndani!"
Monica "Mama amemchukua amempeleka wakamtengeneze vizuri!"
Basi baada ya kuniambia maneno yale ilibidi tuingie ndani,kiukweli nilikuwa nina hofu sana na nilijilaumu kwanini nimeingia kwenye mahusiano na yule binti,kibaya zaidi siku zilivyokuwa zikienda ndivyo na mimi nilikuwa siambiliki wa kuelezeka kwa yule binti!,ilifikia pointi ambayo nisipokuwa nikimuona nilikuwa ninapata mawazo sana.
Mida hiyo ilikuwa yapata saa 9 usiku na tangia hapo sikupata usingizi tena,ilipofika mida ya saa 10 kuelekea saa 11 ambapo niliona kabisa kama kuna miale ya mapambazuko,nilimwambia anisindikize kurudi nyumbani.
Monica "Mbona unawahi hivyo?"
Mimi "Nadhani unamjua Ema alivyo muongo,na najua kama aliamka kwenda chooni akakuta sipo sijui itakuwaje,lazima tu amwambie Ba'mdogo"
Monica "Yule hawezi kuamka mpaka wewe ufike"
Mimi "Wewe yule humjui vizuri!"
Monica "Basi tufanye kidogo halafu ndiyo uende"
Kiukweli sikuwa kabisa na hamu tena ya mizagamuano ila kwakuwa alitaka sikuwa na namna,ikabidi tulianzishe tena!.Fimbo ziliendelea mpaka sasa nikawa nasikia majogoo yanawika huko nje kuashiria kumepambazuka!.Nilivaa zangu nguo na yeye pia akavaa na safari ya kunisindikiza kwetu ikachukua nafasi.Monica hakutaka kabisa kuniacha njiani,alihakikisha mpaka naingia ndani ndipo na yeye anarudi kwao.
Ilikuwa ni kama kuonekana kwao ni mbali lakini nilipokuwa nikitembea na yeye sikuwahi kuona wala kuhisi umbali wowote,hebu fikiria umbali wa zaidi ya kilometa 6 lakini ndani ya dakika kama 10 mnajikuta shafika!,haya yalikuwa ni maajabu ya binti wa kisukuma Monica.Basi baada ya kuhakikisha nimefungua mlango na kuingia ndani na yeye aliondoka kurudi kwao.
Nilisukuma mlango nikaingia ndani nikakuta Ema bado amelala,sasa sikufahamu aliamka wakati mimi sipo ama la!.Kwakuwa kulikuwa kumepambazuka sikutaka kujiegesha maana niliona ningepitiwa na usingizi,nilijifanya namuamsha jamaa ili nione!.sasa baada ya kumpiga piga na mkono,jamaa alishituka sana!.
Mimi "nimekushitua?"
Ema "Maanangu nilikuwa naota"
Mimi "Ooh,jana ulichoka sana nini!"
Ema "Yaani sijawahi kulala usingizi mtamu kama wa leo"
Mimi "Kumekucha kijana jiandae uende skonga"
Ema "Leo sidhani kama nitaenda"
Mimi "Shida nini?"
Ema "Nahisi kuchoka tu"
Sasa jamaa alikuwa ananieleza huku akiendelea kupiga miayo ya kufa mtu!.Nilipoendelea endelea kumdodosa ndipo nikagundua tangu ule usiku nilipotola hakuwa ameamka hata kidogo!.
Basi kulipopambazuka zaidi nilielekea lamboni kuchota maji ya kuoga na kurejea nyumbani,basi baada ya kumaliza kila kitu niliingia ndani kumsalimia Headmaster na mkewe na kisha mimi kuelekea kwa mzee masumbuko kuchukua miwa ya kwenda kuuza.Sasa wakati unatoka hapo kwa mzee masumbuko ili uikamate njia ya kuelekea Senta,kulikuwa kama na makutano ya njia,njia moja ndiyo njia ambayo ilikuwa inatoka kwenye uwanja unapofanyikia mnada na ukipandisha nayo inakupeleka moja kwa moja kwa kina Monica kule Masairo,njia nyingine ni njia ambayo ilikuwa inakupeleka mpaka lamboni ambako unatokea mpaka shuleni,na njia nyingine ndiyo njia ambayo nilikuwa naipita mimi kuelekea senta kila ninapotoka kuchukua miwa!.
Sasa wakati naikamata njia ambayo ilinipaswa kupita kwa mbele kuna kina mama walikuwa wakija wakiwa wawili,mmoja wapo nikama nilimuona kwenye zile ngoma pale kwao Monica ule usiku!,sasa walizungumza kisukuma halafu wakawa wananitazama sana,nikama walikuwa wananiteta!,waliponipita nilihisi kabisa wanaendelea kunitazama,sasa nilipofika kwa mbele nikautua ule mzigo wa miwa nikajifanya kama naufunga kwa kukaza,nikawaangalia kwa kuibia ndipo nikaona wananitazama na nikama wakawa wanazungumza kwa kubishana!,walipoona nawaangalia wakaondoka huku wakionekana kama kunishangaa!.
Sasa nikabaki namuangalia yule mama ambaye nilimuona ule usiku nikabaki kushangaa tu,kiukweli ukikutana naye hivi kwa mara moja na ukiambiwa mambo anayoyafanya huwezi kabisa kuamini!.Nilijitwisha zangu zigo la miwa na kuondoka huku nikishindwa kuelewa kwanini wale kina mama walikuwa wakiniangalia kwa makini sana!.
Siku hiyo biashara ya miwa ilikuwa mbaya sana,kiukweli tangu asubuhi hadi jioni niliuza pingili tatu tu za muwa,basi kwakuwa nilijua biashara siku zote haifanani sikutaka kujipa presha kabisa,nilipanga Headmaster akiniuliza nitamaambia ukweli ya kwamba biashara imekuwa ndivyo sivyo,basi ilipofika jioni nilienda kupeleka miwa kwa yule mama aliyekuwa akinifadhia na mimi kuondoka kueleke nyumbani,wakati wote nilikuwaga naondoka hapo senta mida ya saa 12 jioni na kufika nyumbani mida ya saa 1 kuelekea saa 2.
Sasa nilipotembea kwa umbali mrefu,huku nikiwa naendelea kuitafakari siku,mara ghafla mbele yangu akatokea yule mzee Makono ambaye pia alikuwa mmoja aa wale watu waliokuwa wakicheza ngoma ule usiku,nilishangaa sana kwasababu eneo nililokutana nae,ndilo aneo ambalo siku ile nilikutana nae na akanitaka nikamsalimie Headmaster,safari hii nilishituka sana mpaka akashangaa!.
Mzee makono "Unishituka nini wewe!"
Mimi "Mzee shikamoo"
Mzee makono "Kwahiyo hujashituka jana leo ujifanye kushituka!"
Kiukweli nilishangaa sana na ghafla uoga mkuu ukaniingia,nilishindwa hata kukimbia nikabaki nimepigwa na bumbuwazi,sasa nilibaki kushangaa kwasababu iliwezekana vipi jana kuniona na wakati Monica aliniambia sababu ya yeye kunipaka ile dawa ni kusudi nisionekane na wacheza ngoma kama adui na wahisi mimi ni mmoja wao!,pili nikajiuliza yeye mzee makono alinionaje?,Sasa wakati naendelea kutafakari nisijue cha kufanya,akaendelea kuniambia kwamba
Mzee makono "wewe na kale kakondefu mmeshirikiana kunitesea mwanangu!,si ndiyo?"
Akaendelea "Nataka leo unitambue mimi ni nani!"
Sikutaka kabisa kumjibu yule mzee nikawa nimebaki kimya kwa bumbuwazi,basi baada ya kuniambia maneno hayo akasonya kwa kufyonza kisha akaondoka!,kiukweli ongea ya yule mzee alionekana kabisa amechukizwa sana na alikuwa na hasira mno!.
Sikufahamu kwa haraka haraka ni kitu gani kilikuwa kimemkasirisha na ni nani aliyekuwa amemtesa mwanaye!.
Basi kutokana na uoga niliyokuwa nao,nikaanza kukimbia ili kuwahi nyumbani,safari hii nilipofika pale kwenye miembe nilipita kwa spidi kali mno kama kipanga na sikutaka hata kugeuka nyuma!.
Sasa nilipofika karibu na nyumbani nilimkuta Monica akiwa amesimama anaongea na Ema.
Ema "Haya huyo hapo ongea nae"
Baada ya kusema hivyo Ema akawa anaelekea ndani!.
Mimi "Kwani kuna nin?"
Monica "Tuondoke hapa"
Mimi "Nakupenda umughaka,nakuomba tuondoke,utajua huko huko"
Basi Monica akanishika Mkono tukaongozana kuelekea nisipopafahamu.Mpaka muda huo hata ndani sikufika kabisa.
Mimi "Tunaenda wapi?"
Monica "Nilikwambia nitakulinda kwa gharama yeyote,huyo mjinga anajifanya mjanja muache".
Boss weekend leo tupia eps za kishantaTulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 15.
Nilifungua ule mlango ulokuwa umefungwa kwa komeo nikatoka nje na kuanza kukimbia kama mwendawazimu.Niliingia kwenye shamba la jirani na hapo kwao Monica lililokuwa na mahindi madogo saizi ya magoti kisha nikalala chini!.Nilishindwa kuelewa mpaka muda huo binti Monica atakuwa yupo wapi maana mlango haukufunguliwa na yeye ndani hakuwepo!.Sasa nilinyamaza kimya ili kuona ni kitu gani kilikuwa kinaendelea.
Baada ya kama dakika 20 hivi,nikawa nasikia sauti ya Monica ikiniita kuashiria kunitafuta,mimi niliendelea kukaa kimya huku nikichukua tahadhari na nilidhani uenda asiwe Monica nikaingia chaka!.Kwa mbali niliona ule mlango wa ile nyumba unagunguliwa mtu akaingia ndani kisha akatoka tena akawa anaita.Baada ya kujiridhisha kwamba alikuwa Monica ndiye aliyeniita,niliamua kusimama na kujipangusa mchanga uliokuwa umenijaa kwenye tumbo na magoti na hii ilikuwa ni baada ya mimi kulala chini!,mpaka wakati huo nilikuwa kama nilivyozaliwa maana nilipokurupuka sikukumbuka hata nguo nimeziweka sehemu gani!
Monica "Uko wapi?"
Monica alijifanya kuniuliza niko wapi kana kwamba alikuwa hanioni,ila nilichoamini mimi ni kwamba alikuwa akiniona tu vizuri!.Niliondoka kuelekea ule uelekeo alokuwa amesimama Monica.
Monica "ulikuwa wapi?"
Mimi "Nilikuwa pale"
Monica "Sasa huku nje umefata nini!?"
Mimi "Wewe ulienda wapi?"
Monica "Mimi mbona nilikuwepo?"
Mimi "Ulikuwepo wakati nimekutafuta sikuoni!?"
Monica "Kuna mjinga mmoja nilikuwa namshikisha adabu"
Mimi "Mjinga gani?"
Monica "Hukusikia napigana na mtu"
Mimi "Mimi sijasikia,nilichosikia ni kishindo kikubwa nyuma huko nageuka nakuangalia na wewe hauonekani,ndiyo nikatoka kukimbia"
Monica "Nilikwambia umughaka nitakulinda usiku na mchana,kuna mjinga alikuja kutaka kunijaribu,nimepambana nae alitaka kunishinda nikamuita mama"
Mimi "Kwahiyo mama yupo ndani!"
Monica "Mama amemchukua amempeleka wakamtengeneze vizuri!"
Basi baada ya kuniambia maneno yale ilibidi tuingie ndani,kiukweli nilikuwa nina hofu sana na nilijilaumu kwanini nimeingia kwenye mahusiano na yule binti,kibaya zaidi siku zilivyokuwa zikienda ndivyo na mimi nilikuwa siambiliki wa kuelezeka kwa yule binti!,ilifikia pointi ambayo nisipokuwa nikimuona nilikuwa ninapata mawazo sana.
Mida hiyo ilikuwa yapata saa 9 usiku na tangia hapo sikupata usingizi tena,ilipofika mida ya saa 10 kuelekea saa 11 ambapo niliona kabisa kama kuna miale ya mapambazuko,nilimwambia anisindikize kurudi nyumbani.
Monica "Mbona unawahi hivyo?"
Mimi "Nadhani unamjua Ema alivyo muongo,na najua kama aliamka kwenda chooni akakuta sipo sijui itakuwaje,lazima tu amwambie Ba'mdogo"
Monica "Yule hawezi kuamka mpaka wewe ufike"
Mimi "Wewe yule humjui vizuri!"
Monica "Basi tufanye kidogo halafu ndiyo uende"
Kiukweli sikuwa kabisa na hamu tena ya mizagamuano ila kwakuwa alitaka sikuwa na namna,ikabidi tulianzishe tena!.Fimbo ziliendelea mpaka sasa nikawa nasikia majogoo yanawika huko nje kuashiria kumepambazuka!.Nilivaa zangu nguo na yeye pia akavaa na safari ya kunisindikiza kwetu ikachukua nafasi.Monica hakutaka kabisa kuniacha njiani,alihakikisha mpaka naingia ndani ndipo na yeye anarudi kwao.
Ilikuwa ni kama kuonekana kwao ni mbali lakini nilipokuwa nikitembea na yeye sikuwahi kuona wala kuhisi umbali wowote,hebu fikiria umbali wa zaidi ya kilometa 6 lakini ndani ya dakika kama 10 mnajikuta shafika!,haya yalikuwa ni maajabu ya binti wa kisukuma Monica.Basi baada ya kuhakikisha nimefungua mlango na kuingia ndani na yeye aliondoka kurudi kwao.
Nilisukuma mlango nikaingia ndani nikakuta Ema bado amelala,sasa sikufahamu aliamka wakati mimi sipo ama la!.Kwakuwa kulikuwa kumepambazuka sikutaka kujiegesha maana niliona ningepitiwa na usingizi,nilijifanya namuamsha jamaa ili nione!.sasa baada ya kumpiga piga na mkono,jamaa alishituka sana!.
Mimi "nimekushitua?"
Ema "Maanangu nilikuwa naota"
Mimi "Ooh,jana ulichoka sana nini!"
Ema "Yaani sijawahi kulala usingizi mtamu kama wa leo"
Mimi "Kumekucha kijana jiandae uende skonga"
Ema "Leo sidhani kama nitaenda"
Mimi "Shida nini?"
Ema "Nahisi kuchoka tu"
Sasa jamaa alikuwa ananieleza huku akiendelea kupiga miayo ya kufa mtu!.Nilipoendelea endelea kumdodosa ndipo nikagundua tangu ule usiku nilipotola hakuwa ameamka hata kidogo!.
Basi kulipopambazuka zaidi nilielekea lamboni kuchota maji ya kuoga na kurejea nyumbani,basi baada ya kumaliza kila kitu niliingia ndani kumsalimia Headmaster na mkewe na kisha mimi kuelekea kwa mzee masumbuko kuchukua miwa ya kwenda kuuza.Sasa wakati unatoka hapo kwa mzee masumbuko ili uikamate njia ya kuelekea Senta,kulikuwa kama na makutano ya njia,njia moja ndiyo njia ambayo ilikuwa inatoka kwenye uwanja unapofanyikia mnada na ukipandisha nayo inakupeleka moja kwa moja kwa kina Monica kule Masairo,njia nyingine ni njia ambayo ilikuwa inakupeleka mpaka lamboni ambako unatokea mpaka shuleni,na njia nyingine ndiyo njia ambayo nilikuwa naipita mimi kuelekea senta kila ninapotoka kuchukua miwa!.
Sasa wakati naikamata njia ambayo ilinipaswa kupita kwa mbele kuna kina mama walikuwa wakija wakiwa wawili,mmoja wapo nikama nilimuona kwenye zile ngoma pale kwao Monica ule usiku!,sasa walizungumza kisukuma halafu wakawa wananitazama sana,nikama walikuwa wananiteta!,waliponipita nilihisi kabisa wanaendelea kunitazama,sasa nilipofika kwa mbele nikautua ule mzigo wa miwa nikajifanya kama naufunga kwa kukaza,nikawaangalia kwa kuibia ndipo nikaona wananitazama na nikama wakawa wanazungumza kwa kubishana!,walipoona nawaangalia wakaondoka huku wakionekana kama kunishangaa!.
Sasa nikabaki namuangalia yule mama ambaye nilimuona ule usiku nikabaki kushangaa tu,kiukweli ukikutana naye hivi kwa mara moja na ukiambiwa mambo anayoyafanya huwezi kabisa kuamini!.Nilijitwisha zangu zigo la miwa na kuondoka huku nikishindwa kuelewa kwanini wale kina mama walikuwa wakiniangalia kwa makini sana!.
Siku hiyo biashara ya miwa ilikuwa mbaya sana,kiukweli tangu asubuhi hadi jioni niliuza pingili tatu tu za muwa,basi kwakuwa nilijua biashara siku zote haifanani sikutaka kujipa presha kabisa,nilipanga Headmaster akiniuliza nitamaambia ukweli ya kwamba biashara imekuwa ndivyo sivyo,basi ilipofika jioni nilienda kupeleka miwa kwa yule mama aliyekuwa akinifadhia na mimi kuondoka kueleke nyumbani,wakati wote nilikuwaga naondoka hapo senta mida ya saa 12 jioni na kufika nyumbani mida ya saa 1 kuelekea saa 2.
Sasa nilipotembea kwa umbali mrefu,huku nikiwa naendelea kuitafakari siku,mara ghafla mbele yangu akatokea yule mzee Makono ambaye pia alikuwa mmoja aa wale watu waliokuwa wakicheza ngoma ule usiku,nilishangaa sana kwasababu eneo nililokutana nae,ndilo aneo ambalo siku ile nilikutana nae na akanitaka nikamsalimie Headmaster,safari hii nilishituka sana mpaka akashangaa!.
Mzee makono "Unishituka nini wewe!"
Mimi "Mzee shikamoo"
Mzee makono "Kwahiyo hujashituka jana leo ujifanye kushituka!"
Kiukweli nilishangaa sana na ghafla uoga mkuu ukaniingia,nilishindwa hata kukimbia nikabaki nimepigwa na bumbuwazi,sasa nilibaki kushangaa kwasababu iliwezekana vipi jana kuniona na wakati Monica aliniambia sababu ya yeye kunipaka ile dawa ni kusudi nisionekane na wacheza ngoma kama adui na wahisi mimi ni mmoja wao!,pili nikajiuliza yeye mzee makono alinionaje?,Sasa wakati naendelea kutafakari nisijue cha kufanya,akaendelea kuniambia kwamba
Mzee makono "wewe na kale kakondefu mmeshirikiana kunitesea mwanangu!,si ndiyo?"
Akaendelea "Nataka leo unitambue mimi ni nani!"
Sikutaka kabisa kumjibu yule mzee nikawa nimebaki kimya kwa bumbuwazi,basi baada ya kuniambia maneno hayo akasonya kwa kufyonza kisha akaondoka!,kiukweli ongea ya yule mzee alionekana kabisa amechukizwa sana na alikuwa na hasira mno!.
Sikufahamu kwa haraka haraka ni kitu gani kilikuwa kimemkasirisha na ni nani aliyekuwa amemtesa mwanaye!.
Basi kutokana na uoga niliyokuwa nao,nikaanza kukimbia ili kuwahi nyumbani,safari hii nilipofika pale kwenye miembe nilipita kwa spidi kali mno kama kipanga na sikutaka hata kugeuka nyuma!.
Sasa nilipofika karibu na nyumbani nilimkuta Monica akiwa amesimama anaongea na Ema.
Ema "Haya huyo hapo ongea nae"
Baada ya kusema hivyo Ema akawa anaelekea ndani!.
Mimi "Kwani kuna nin?"
Monica "Tuondoke hapa"
Mimi "Nakupenda umughaka,nakuomba tuondoke,utajua huko huko"
Basi Monica akanishika Mkono tukaongozana kuelekea nisipopafahamu.Mpaka muda huo hata ndani sikufika kabisa.
Mimi "Tunaenda wapi?"
Monica "Nilikwambia nitakulinda kwa gharama yeyote,huyo mjinga anajifanya mjanja muache".
Aisee!? Kumbe kuna raha kudate na vichawiMonica "Nilikwambia nitakulinda kwa gharama yeyote,huyo mjinga anajifanya mjanja muache".
Nipe link ya Telegram basi kijanaYani kule tuko mbele zaidi mpaka Headmaster nae keshakuwa mchawi hatari[emoji12][emoji12][emoji12]
umughaka na Monica ni walokole[emoji41][emoji41][emoji41]
Kuvuja c linavuja kila mwezi[emoji849]