James Comey
JF-Expert Member
- May 14, 2017
- 8,759
- 14,831
Na gazeti tulikuwa tunanunuaYaani mtu akianzisha simulizi wanataka bandika bandua wakati hadithi za Shigongo zilikuwa zinatoka wiki kwa wiki na hawakulalamika
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Na gazeti tulikuwa tunanunuaYaani mtu akianzisha simulizi wanataka bandika bandua wakati hadithi za Shigongo zilikuwa zinatoka wiki kwa wiki na hawakulalamika
Kwa wiki hadi wiki sio na hatulalamiki 😂😂😂😂Na gazeti tulikuwa tunanunua
UMUGHAKA mbona sijaona neno DINYANA wakati mlikesha na Monie halafu mama kakukabizi mke na mtoto in advance.Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 23.
Baada ya mazungumzo ya muda mrefu pale nje,mama yake Monica alituaga akawa ameingia ndani kwa ajili ya kulala,basi na sisi hatukutaka kupoteza muda kabisa tukawa tumeingia ndani ya kwa ajili ya kulala.Ilipofika asubuhi niliamaka mapema nikawa nimemwambia Monica inapaswa nielekee nyumbani!,siku hiyo nakumbuka ilikuwa jumamosi.
Monica "Subiri basi mama aamke kwanza"
Basi Monica alinipatia maji nikanawa uso kisha nikarudi ndani kusubiri hadi mama yake aamke maana alikuwa ameniambia usiku ya kwamba angenipatia kitu ambacho ningeenda nacho nyumbani ili kitusaidie!.
Ilipofika mida ya saa 1 asubuhi mama yake Monica alikuwa ameshaamka na alikuja kugonga mle ndani nilimo lala ili atusalimie,wakati huo nilikuwepo mimi peke yangu na Monica alikuwa yupo jikoni akiandaa uji kwa ajili ya mlo wa asubuhi!.
Mama Monica "Hujambo baba"
Mimi "Sijambo mama,shikamoo!"
Mama Monica "Marhaba,baba yangu"
Aliendelea "Mbona mapema yote hii,unawahi wapi?"
Mimi "Nilitaka kuwahi nyumbani mama nikaendelee na shughuli zangu,siunajua tena ninapaswa kuelekea senta"
Mama Monica "Ni kweli baba"
Aliendelea "Basi njoo umsalimie bibi yako"
Basi nilitoka mle chumbani nikaelekea mpaka nje ya mlango wa ile nyumba aliyokuwa amelala bibi yake Monica!.Kwakuwa kisukuma changu kilikuwa cha salamu tu na kuombea maji ilibidi mama yake Monica niwe naongea halafu na yeye anamtafusiria bibi maana alikuwa hakijui kiswahili hata tone!.
Baada ya salamu na mazungumzo mafupi,mama yake Monica akawa amenitolea kiti nje akanitaka nikae nisubiri uje uive ninywe wakati ambao yeye ananiandalia mitishamba na dawa aliyokuwa ameniambia angenipatia.Kiukweli niseme tu ukweli,mama yake Monica alitokea kunipenda sana na kuna muda nilikuwa nikifika pale kwa Monica najihisi niko kwenye dunia nyingine,mara kwanza nilikuwa naogopaga sana,lakini baada ya kuhakikishiwa usalama wangu,kwakweli sikuwa naogopa tena!.Yule mama alikuwa yuko radhi afanye jambo lolote ili mimi na mwanaye tusalimike!.
Basi haukupita muda Monica akawa ameivisha uji na maboga akatenga kwenye jamvi!,nilishuka kutoka kwenye kiti na kukaa kwenye jamvi kwa ajili ya kupata brekifasti!,kama ambavyo nilisema hapo awali,ile familia haikuwa na hela ila ilikuwa na uchawi wa kutosha!,kunywa uji usiyokuwa na sukari halikuwa jambo la mjadala na kiukweli japo sikuwahi kunywa uji wa sukari hapo kwa Monica lakini uji ulikuwaga mtamu sana kwasababu walikuwa wakiweka maziwa!,hivyo kuufanya kuwa mtamu sana!.Nilipomaliza kupata ile brekifasti,mama yake Monica aliniita ndani ya nyumba kubwa kule alikokuwa amelala bibi yake Monica.
Mama Monica "Mwanangu nisikilize kwa makini!"
Aliendelea "Najua wewe na mwanangu mtakwenda kuniletea mjukuu hivi karibuni,hivyo wewe ni mtu muhimu sana kwasasa katika familia hii"
Mama Monica "Najua Mwalimu Wambura ni Mkurya wa Musoma huko na ndiyo maana ni mjeuri,ila wewe nimekupenda kwakuwa unanisikiliza sana mwanangu,nakuomba usije ukachukua roho ya mwalimu Wambura!"
Aliendelea "Naamini hautanitesea mwanangu pekee Monica"
Mama Monica "Baba yake alikufa angali bado mdogo,hivyo nimemlea kwa matatizo makubwa mno!"
Aliendelea "Tulihamia huku baada ya kufukuzwa huko Ilungu-Magu,na hii yote ni kwasababu ya baba yake Monica"
Mama Monica "Haya yote unayoyaona tumerithishwa na huyu bibi yako unayemuona ningali binti mdogo"
Aliendelea "Kwakuwa baba yake Monica alitaka kuniulia mwanangu wa pekee kwenye michezo yao,ndipo huyu bibi yako tukasaidiana kummaliza kabla hajafanya jambo baya".
Aliendelea kusema "Baada ya mambo kuharibika ndipo tukahamia hapa,kutoka huko Ilungu".
Aliendelea kusema "Hivyo nikuombe mwanangu,hata nikifa leo,nakuomba umtunze mwenzio kwa gharama kubwa maana aliniambia anakupenda sana".
Aliendelea kusema "Mwanangu hajasoma,lakini ni mwerevu na anajua mambo mengi,hivyo na wewe nakuomba umpende!.
Kiukweli siku hiyo mama yake Monica aliamua kunipasulia ukweli kuhusu mwananye na familia yake kwa ujumla, ndipo nikaona kabisa nilikuwa nimethaminiwa kwa kiasi kikubwa na ile familia.
Mimi "Mimi nampenda sana Monica mama na sitaki kumpoteza na yote uliyoongea nimekusikia!".
Mama Monica "Sawa nisubiri nakuja".
Mama yake Monica aliingia chumbani akawa anazungumza na bibi yake Monica kisukuma.Sasa wakati nikiwa nasubiri mama atoke chumbani,ndipo Monica naye akawa ameingia ndani!.Haukupita muda mama yake Monica alitoka ndani akiwa amebeba furushi la mfuko wa rambo la blue!.
Alianza kuufungua ule mfuko kisha kutoa vitu ambavyo sikuvielewa.
Mama Monica "Kamata hii"
Aliendelea "Hiyo niliyokupa ukifika pale nyumbani kwenu,nenda kule nyuma lilipo dirisha la chumba cha Mwalimu na uhakikishe unachimbia chini usawa wa dirisha!".
Mimi "Sawa mama"
Aliendelea "Kamata na hii"
Alisema " Hii naomba umwambie mwalimu aogee yeye na mkewe,halafu wakimaliza kuoga wajipake hii hapa".
Aliendelea kusema "Wewe na mwenzio pia mfanye hivyo hivyo,baadae nitakuja mimi mwenyewe na nitakupatia maelekezo namna ya kufanya"
Mama Monica "Nataka kumsaidia mwalimu ili aepukane na hii fedheha ya yule mpumbavu na wenzie"
Aliendelea "Mwalimu amewahi kunitusi na tulikuwa hatusalimiani,ila inapaswa akushukuru sana wewe".
Mimi "Mwalimu hatakataa nikimwambia?"
Mama Monica "Wewe mwambie,akikataa shauri yake"
Aliendelea "Kama anataka kuondoa fedheha na kumuahibisha mbaya wake mwambie atumie,akikataa usimlazimishe muache".
Mimi "Nashukuru sana mama"
Mama Monica "Andaeni sherehe kesho mtafurahi na itakuwa fedheha hapa kijijini"
Basi baada ya mama yake Monica kunikabidhi zile dawa nikawa nimeaga na kuondoka kurudi nyumbani.Muda huo ilikuwa yapata saa 3 asubuhi.
Baada ya kutembea kwa muda namshukuru Mungu nikawa nimefika nyumbani salama,nilipofika mida hiyo bado sikumkuta mtu yeyote pale nyumbani!.Basi niliingia stoo nikachukua jembe nikazunguka kule nyuma ya nyumba ambako kulikuwa na dirisha la chumba alichokuwa analala Ba'mdogo.Nilichimba haraka haraka na kufukia ile dawa kama ambavyo mama yake Monica alikuwa amenielekeza.
Nilipomaliza nilirudisha jembe stoo kama kawaida,nilichukua dumu la maji nikaelekea lamboni kuchota maji ili nije nikaoge ile dawa ambayo alinipatia maelekezo na kututaka wote tuoge kama tunataka kuwa salama ikiwemo Headmaster na mkewe!.Basi baada ya kumaliza kuoga nilianza zoezi la kuosha vyombo na kumwaga ule ugali nikiyokuwa nimeupika jana na ukakosa walaji!.
Baada ya ile kazi iliyochukua muda wangu mwingi,niliingia ndani kulala!.Nilishituka nikiwa naamshwa na Ema mida ya Saa 7 mchana,wakati huu jamaa alikuwa akijechekelesha chekelesha na nikajua kutakuwa na kitu lazima kwasababu haikuwa kawaida yake,mara nyingi alikuwaga akiharibu mahali basi alikuwa akinichangamkia sana kwakuwa mimi nilikuwa mtetezi wake!.
Mimi "Vipi".
Ema "Mwanangu si Headmaster amenifuma nampiga Deborah mate"
Mimi "Amekufuma wapi"
Ema "Situlikuwa tumesimama pale karibu na ule muale".
Mimi "Sasa amewaona vipi"
Ema "Yaani mwanangu na mimi sifahamu,nimeshituka namuona huyu hapa"
Mimi "Amekwambia nini"
Ema "Ametuchora tu,hajaniambia chochote"
Nilijua tu atakuwa ameharibu mahali na ndiyo maana akajifanya kuja kwangu na kuanza kujichekesha!,kimoyo moyo nilimuhurumia maana nilijua fika stiki atakazokutana nazo si za kitoto!.
Sasa ilipofika mida ya saa 9 alasiri nilitoka zangu ndani na kwenda kumsalimia Headmaster ambaye alikuwa amesharudi,lakini haikuwa kawaida yake nilivyomuona,kiukweli alio alionekana kama mtu aliyekata tamaa na kuchoka kwingi,sasa sikufahamu huko alipokuwa ameenda kilikuwa kimemkuta nini!.
Headmaster "Hivi mwalimu Dani huwa unafahamu anapokaa"
Mimi "Hapana,sijawahi kufika kwake"
Headmaster "Hebu mwambie huyo mjinga aje nimuagize"
Basi nilitoka kwenda kumuita Ema.
Headmaster "Wewe mwalimu Dani siunapafahamu anapokaa?"
Ema "Eeenh,napajua"
Headmaster "Nenda ukimkuta umwambie akupatie mzigo wangu,na uwahi kurudi".
Basi baada ya Ema kuondoka,nilimwambia baba nilikuwa nina mazungumzo nae yeye pamoja na mama.
Headmaster "Kwani huwezi kuniambia mimi mpaka awepo mama yako mdogo?"
Mimi "Ni vizuri akiwepo na mama baba"
Headmaster "Sawa,nilimuacha kwa mama Salome,ngoja tumsubiri arudi".
Nilitaka awepo Maza mdogo maana nilifahamu ningemwambia Headmaster angeweza kukataa,ila Maza mdogo akiwepo isingekuwa rahisi yeye kukataa!.
Hatari"""Basi nilipofika aliniambia nisogee mahali alipokuwa amesimama ambapo ilikuwa mbele ya wanafunzi!.
Sasa kwa sauti akaanza kuwaambia wanafunzi "Huyu mjinga muda huu ndiyo anarudi nyumbani tangu jana,mara zote tumekuwa tukisema ng'ombe mwenye mapembe marefu!?"
Wanafunzi "Ni kumkata mapembeeeeee"""
Hiki ni kipande kilichonifanya nikacheka kwa sauti kubwaaa
Sent from my TECNO CG7 using JamiiForums mobile app
Mtu wa kumpangia kwani aliamua yeye mwenyewe kuileta hapa, lakini hata huduma ya bure inabidi uitoe bila kunyanyasa watu na kama hutaki basi usitoe hiyo huduma wala hakuna wa kukulazimisha ila siyo unatoa huku inavisababu kibaoUzuri ni kuwa humlipi,humchangii bando,hujui maisha yake hivo si vema kuanza kumsema vibaya ni vema ukashukuru kwa kidogo unachokipata.....sisi wanadamu ni wazuri wa kuona makosa tu lakini mafanikio hatuyazungumziii hivo msimpangie mleta uzi huu
Uko kama mimi tu, nikiikuta nasoma haipo napotezea....nikiingia mara mbili tatu haijapostiwa nasepa mazimaHuwa nawashangaa vijana wanalalamikia story utazani hawana kazi za kufanya,mi nikikuta story nasoma mtunzi asipoweka nakausha siku nikiikuta nasoma tena ,asipoiweka muda mrefu naisahau kama kulikuwa na story nafatilia maendelea kuperuzi vingine
Leo umughaka umepatwa na nini? Mteja kakimbia na nauli umemkimbiza mpaka dodoma? Tusubiri ukirudi uje kusimulia tena? Maana na wewe kuna siku uliahirisha ulisema bodaboda yako tairi iliisha upepo. Siku nyingine iligonga mtu, siku nyingine ikawa inasumbua kuwaka. Siku nyingine ukasema mteja alikukwaza....we jamaa umeanza hadi kuringa.Wakuu nipo kijiweni,kuna muda naamua kuangalia tu comments za wadau,marafiki na ndugu zangu wa JF nabaki kufurahi tu[emoji23][emoji23].
Yaani kama unahasira za kijinga JF haikufai maana unaweza mrushia mtu ngumi ingawaje niya upepo[emoji23][emoji23][emoji23].
Humu kuna watu wanakera
Humu kuna watu wanaudhi
Humu kuna watu wanachukiza
Humu kuna watu wanafurahisha
Humu kuna watu wanajua kila kitu.
Yaani ukitaka kupata raha na karaha wewe tembelea JF [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
All in All nawependa sana ndugu zangu na tuonane muda si mrefu!
[emoji23][emoji23][emoji23]Leo umughaka umepatwa na nini? Mteja kakimbia na nauli umemkimbiza mpaka dodoma? Tusubiri ukirudi uje kusimulia tena? Maana na wewe kuna siku uliahirisha ulisema bodaboda yako tairi iliisha upepo. Siku nyingine iligonga mtu, siku nyingine ikawa inasumbua kuwaka. Siku nyingine ukasema mteja alikukwaza....we jamaa umeanza hadi kuringa. Nimekuona juzi unaendesha boda boda yako kwa mbwembwe barabarani.uje ugongwe au upate ajali tu upate excuse.
Kwa hyo hi ujafatiliaa au mnk umeweka kambi kbsa hapaUko kama mimi tu, nikiikuta nasoma haipo napotezea....nikiingia mara mbili tatu haijapostiwa nasepa mazima
UMUGHAKAVile umughaka alivyomfanya mzee makono
View attachment 2386450