Tulifufua ATCL kichwa kichwa

Tulifufua ATCL kichwa kichwa

The Genius

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2018
Posts
822
Reaction score
2,095
Moja kati ya uwekezaji kichaa tuliowahi kufanya ni huu wa ndege. Narudia ili MATAGA wasije kuninukuu vibaya. Sisemi kwamba hatukupaswa kufufua ATCL, ila tulitakiwa kabla ya kufufua tuwe na mkakati wa kujua shirika litajiendeshaje.

Lakini hatukufanya hivyo. Tumefufua ATCL kichwakichwa bila kuwa na mkakati wa kibiashara. Matokeo yake ndio haya tunayoyasikia kwa CAG leo.

Kwa kifupi hakuna ndege ya ATCL inayoruhusiwa kuruka kwenye anga la kimataifa zaidi ya India ambapo tuna kibali. Tukienda hata hapo Sudani kwa maskini wenzetu tunakamatwa. ATCL inadaiwa na mamlaka ya usafiri wa anga kimataifa (ICAO) jumla ya TZS 47.4Bilioni ambapo 45Bil ni deni halisi na 12.4Bil ni riba.

Wakati huohuo ATCL inadaiwa Sh71.48 bilioni na wakala wa ndege za serikali (TGFA) ambayo ni tozo ya kukodisha ndege na fedha ya akiba ya matengenezo. Jumla walikua wanadaiwa 79.62 bilioni, lakini wamelipa 8.14 bilioni, na hivyo kubaki na deni la 71.48 bilioni.

Wakati huohuo mwaka jana ATCL imepata hasara ya 60 Bilioni kwa mujibu wa ripoti ya CAG. Kama haitoshi ndege za ATCL zikiharibika leo haziwezi kutengenezwa kwa sababu ATCL haijalipa 71.48 Bilioni ambazo ni gharama za matengenezo.

Kwahiyo tumenunua ndege ambazo haziruhusiwi kuruka nje (zaidi ya India, Chato na Nyakanazi [emoji1]). Zikiharibika hazitengenezeki, na zinajiendesha kwa hasara ya mabilioni ya pesa kila mwaka. Tukiulizwa tunajitetea eti mashirika yote ya ndege hupata hasara. Uzwazwa.!

Mwendazake alikua na nia njema ya kufufua ATCL lakini hakutaka kushauriwa. Yeyote aliyejaribu kumshauri aliitwa kibaraka wa mabeberu. Nia njema ya mwendazake ilikosa mpango mkakati.

Ni sawa na mtu ana nia ya kuwa daktari lakini hajui asome nini. Kutokana na kukosa exposure anakomaa kusoma Agriculture na Geography. Ukimshauri masomo sahihi ya kusoma anagombana na wewe. Anaamini unataka kumkwamisha asifikie ndoto zake.

Mwishowe unamuacha aende anavyotaka. Akija kushtuka safari ya MUHAS imekufa anajikuta chuo cha ufugaji nyuki Tabora. Hiki ndicho kilichotokea kwa mwendazake. Kila aliyemshauri kwa nia njema aligombana nae. Akajikuta anaenda tu bila dira. Na matokeo yake ni haya yalioelezwa na CAG jana.
 
1949282.jpeg
 
Mimi sioni shida shirika lilivyofufuliwa na wala halikuwa wazo baya tatizo ninaloliona hapa na likirekebishwa mara moja mambo yatakuwa mazuri sana, tatizo lenyewe ni mwendazake alipowageuza ATCL kuwa wasemaji wa viwanja vya ndege na wapangaji wa viwanja vya ndege wakati hiyo siyo kazi yao mpaka kuondoa ndege za mashirika mengine binafsi kwenye viwanja vya ndege ambao wangeshindana kibiashara hata wao wasingepata hasara maana wangekuwa wanakesha kutengeneza mikakati ya biashara yenye ushindani na sehemu zote zenye biashara wangekwenda vizuri tu maana bei ingeshuka na viwanja vingejengwa vingi nchi nzima maana hakuna asiyependa kuwahi anapokwenda, pia sehemu ambapo wasingetaka kwenda wangeacha tu mbona bukoba kutoka Mwanza kulikuwa na zile ndege ndogo zilikuwa zinakwenda huko na mambo yapo sawa tu hata huko Chato ingekuwa hivyo zingetumika ndege ndogo Kama za bukoba tu, tena Mimi nikifika kwa Raisi ntamshauri Kama wataendelea kutuletea hasara hakuna haja ya kuwalipa mishahara na wafanyakazi wapunguzwe wanaobaki waunganishe idara, ndege ni muhimu sana lakini siyo kwa mtindo wa kupewa shirika moja tu mpaka nauli inakuwa kubwa watu wanaona Bora wasafiri kwa magari yao binafsi angalau wanaweza kusave hela kidogo kuliko kupanda mandege yenye gharama Kama vile ni big deal wakati hiyo ni biashara inatakiwa ifanyike kulingana na uchumi wa wananchi.
 
Alafu kingine kinachokwamisha biashara ya ndege ni huko bungeni na wanasiasa maana wengi ndo wanamakampuni ya mabasi hivyo naona wanakwamisha makusudi Ili watu waendelee kusafiri kwa mabasi huku wakipoteza muda njiani kwa vipato vyao vidogo na wao wanapanda ndege wanawahi wanapokwenda. Kila mkoa unatakiwa uwe na kiwanja cha ndege Kama stand zilivyo kila mkoa na mashirika ya ndege ya binafsi yaruhusiwe kuwekeza watu wapande ndege wawahi wanapokwenda haya mambo ya kuona kutumia vitu vya kisasa kurahisisha maisha ni dhambi hayafai kabisa au napo tutasingizia mabeberu wanatukwamisha kupanda ndege? Wanataka tupande mabasi na treni za kufika baada ya wiki Ili tuendeleze uvivu wetu wa kuwa magoigoi.
 
Kama hayati alinunua ndege bac wengine walio bakia madarakan walipe deni la ICAO pole pole lzm maisha yaendelww msikeahe kulalamika tu hasara ni kitu cha kawaida kwa makapuni haya ya ndege
 
Back
Top Bottom