Hapana boss, hakuna kitu kama kuzitapika tena!
Pia uhalisia uko hivyo mkubwa, hakuna hata moja lililotimia ambalo ni tangible kwasababu ya mama! Semina feki zimerudi, michakato imerudi (tunakaa na majaa ya tiaraei, wanasema mambo ni bulbul sasa hivi), zile gari zilizofichwa sasa ziko barabarani, mimi bunafsi nishanywea mbele ya NITAKUPOTEZA(unanijua mimi nani) dk suu tu mara 4 sasa! Kupewa doc za polisi kwa sasa ni bidhaa, huna hela hupewi, wazi kabisa unaulizwa UNA PESA gari yako ikaguliwe(vehicle inspector)?
Niambie, MKALIFANYIE KAZI ngapi umezisikia na MIREJESHO mingapi umeipata mpaka sasa?
Siko kukosea au kumponda mama ila ukweli ndio huo, tuliambiwa amebana matumizi kwenda USA kwa commercial airline, nini kimetokea safari ya Scotland?
Anasema safari zake zinaleta pesa ndani, kwa nani zinaenda hizo pesa? Kama tozo zinaenda kwenye madarasa, za uviko zinaenda kwenye madarasa, na si ajabu za mazingira nazi zitaenda kwenye madarasa.
Haya si mambo tuliyoyasikia awamu ya nne? Wengi wakisema, bora ale ila atuachie na sisi tule?
Sasa fikiria, wanaonufaika na upigaji ni 1.666% ya waTz wote, 98% wanaendelea kuwanufaisha hawa 2% kwa jasho, machozi na damu. 2% wanasomesha watoto wao nje, 20% Kayumba na Kata n.k
Wapi ujenzi umeanza wa madarasa ya tozo kabla hata ya Uviko?