puza46b
Member
- Nov 3, 2010
- 91
- 261
TULINGANISHE SERA ZA MAGUFULI, LISU NA MEMBE:
Tukielekea kwenye uchaguzi tumeanza kuona washabiki wakibezana na kuhoji sera za washindani wao. Wapo waliomwambia Lisu kuwa yeye ni kutukana tuu hana hoja. Kuna waliosema Magufuli anatumia vitisho na kulazimisha watanzania wampende. Na mwisho kuna wanaodai Membe katumwa na kitengo kufanya kazi yakuchafua upinzani na Zitto kabwe alikuwa project yake ya kuiharibu chadema.
Wahenga wanasema wahukumu watu kwa matendo yao kuliko maneno yao. Lakini pia kuna wale wanaosema muongeaji sana ni vigumu kuficha anachowaza.
Sasa basi, ningependa kutumia hii mada kuorodhesha hoja mbalimbali za hawa wagombea wetu wakuu watatu. Disclaimer: sijasoma ilani za vyama vyao nasinampango wa kuzisoma kwa sababu naamini kinachotoka midomoni mwao kinaonyesha nini wanawaza:
KATIBA
Lisu:
WAKULIMA:
Lisu:
WAFANYAKAZI
Lisu:
VIWANDA
Lisu:
WAFANYABIASHARA
Lisu:
MAHUSIANO YA KIMATAIFA
Lisu:
MIUNDO MBINU
Lisu:
ZANZIBAR
Lisu:
MALIASILI
Lisu:
Mwisho ningependa kusisitiza kuwa haya ni yale niliyoyasikia kama kuna mengine nikiyasikia mbeleni nitaendelea kuyaandika hapa.
Pia Moderators kama mnataka kuratibu hii mada kwa kuendelea kuweka orodha ya mambo wanasiasa wanatu ahidi mnakaribishwa. Kelele zitakuwanyingi kwenye siasa mwaka huu tunahitaji mahali ambapo tunaweza kuelewa nini wanajaribu kusema.
Heshima za dhati kwa wagombea wengine ambao sijawaorodhesha hapa. Hoja zenu sijazisikia na sina uhakika kama mna nia ya kweli ya kuliongoza taifa au mmefuata rudhuku.
Tukielekea kwenye uchaguzi tumeanza kuona washabiki wakibezana na kuhoji sera za washindani wao. Wapo waliomwambia Lisu kuwa yeye ni kutukana tuu hana hoja. Kuna waliosema Magufuli anatumia vitisho na kulazimisha watanzania wampende. Na mwisho kuna wanaodai Membe katumwa na kitengo kufanya kazi yakuchafua upinzani na Zitto kabwe alikuwa project yake ya kuiharibu chadema.
Wahenga wanasema wahukumu watu kwa matendo yao kuliko maneno yao. Lakini pia kuna wale wanaosema muongeaji sana ni vigumu kuficha anachowaza.
Sasa basi, ningependa kutumia hii mada kuorodhesha hoja mbalimbali za hawa wagombea wetu wakuu watatu. Disclaimer: sijasoma ilani za vyama vyao nasinampango wa kuzisoma kwa sababu naamini kinachotoka midomoni mwao kinaonyesha nini wanawaza:
KATIBA
Lisu:
Atabidili katiba na ni swala atakalolishughulikia siku 100 za kwanza.
Atapunguza madaraka ya Raisi kuondoa dhana ya Raisi mfalme
Atawezesha miji, wilaya na kata ziwawajibishe watendaje wake kwa kufuta kuteuliwa.
Atafanya bunge liweze kumuwajibisha raisi - raisi anatumikie watu na siyo vinginevyo
Magufuli:Hakurudisha muswada wa katiba bungeni
Watendaji wote wanamtumikiwa raisi.
Membe:Atabadili katiba kama Lisu alivyosema. Sijaona uchambuzi wake zaidi
WAKULIMA:
Lisu:
Atawapunguzia makato na vizuizi vya kuuza mazao
Atawaruhusu wauze mazao popote wanakopata bei nzuri (bila kuangalia national food security)
Atawapa uhuru wa kufanya biashara yao bila kuingiliwa
Magufuli:Analinda chakula kuwafae watanzania kwanza (national security)
Yuko tayari kuingilia soko la mazao kama anaamini ni faida kwa taifa
Membe:Atawapunguzia makato kama lisu
Atawapa uhuru wa kuuza mazao wapate faida
Atatoa nyezoza kuwasaidia kwenye kilimo (hii zitto huiongelea sana)
Ataanzisha bima ya kuwalinda wakulima (sera ya zitto pia)
WAFANYAKAZI
Lisu:
Atawapandisha Madaraja
Atawalipa hela zote ambazo hawakuongezewa miaka mitano iliyopita
Magufuli:Mishahara itapanda baada ya kumaliza kujenga miundo mbinu
Membe:Atawapandisha Madaraja
VIWANDA
Lisu:
Ataweka mazingira mazuri ya uwekezaji kwa kupunguza manyanyaso ya kodi
Magufuli:Inchi inahitaji viwanda kukua kiuchumi na kuondoa umaskini
Tanzania ya viwanda inawezekana na atahakikisha mpaka 2025 uchumi wa viwanda umeimarika
Membe:Ataweka mazingira mazuri ya uwekezaji
WAFANYABIASHARA
Lisu:
Ataondoa ubugudhaji wa wafanyabiashara
Atabadili TRA ili isiwe chombo cha kunyanyasa wafanyabiashara
Atapunguza kodi kwa wafanyabiashara
Magufuli:Kila mtu anawajibu wa kulipa kodi
Membe:Sera zake zinafanana na Lisu
MAHUSIANO YA KIMATAIFA
Lisu:
Tanzania siyo kisiwa inahitaji mahusiano mazuri
Atafufua mahusiano na nchi nyingine
Magufuli:Tanzania ni tajiri haiko tayari kudhalilishwa na nchi nyingine
Yuko tayari kuvunja mahusiano kama hayana tija kwa taifa.
Membe:Atatumia ujuzi wake wa kidiplomasia kurudisha mahusiano ya kimataifa
MIUNDO MBINU
Lisu:
Hata wakoloni walijenga miundo mbinu hivyo isitumike kuwanyanyasa watanzania
Kila serikali inawajibu wakujenga miundo mbinu na yeye ataiendeleza
Magufuli:Anajenga miundo mbinu ili iwe chachu ya kukua viwanda.
Miundo mbinu itawapunguzia gharama wafanyabiashara (reli na umeme)
Membe:Atahakikisha mradi wa bandari ya bagamoyo unakamilika
ZANZIBAR
Lisu:
Zanzibar watakuwa na haki sawa katika muungano
Zanzibar watapata fare share katika pato la taifa (hapa sikumwelewa kama alimaanisha nusunusu)
Hataingilia kazi kubwa iliyofanya na Maalimu katika kutetea haki ya wazanzibari.
Magufuli:Haliongelei hili
Membe:Zanzibar watakuwa na haki sawa katika muungano
MALIASILI
Lisu:
Atawaruhusu wawekezaji wa nje kushiriki kwenye kuvuna maliasili
Hatuna technolojia au hela ya kuvuna hizo maliasili sisi wenyewe na hata sasa wavunaji wakuu ni wageni.
Magufuli:Tanzania lazima ipate pato kubwa kwenye madini
Sisi ni donor country hatuhitaji mabeberu.
Membe:Atawarudisha wawekezanji
Atahakikisha miradi mkubwa ya LNG unakamilishwa
Mwisho ningependa kusisitiza kuwa haya ni yale niliyoyasikia kama kuna mengine nikiyasikia mbeleni nitaendelea kuyaandika hapa.
Pia Moderators kama mnataka kuratibu hii mada kwa kuendelea kuweka orodha ya mambo wanasiasa wanatu ahidi mnakaribishwa. Kelele zitakuwanyingi kwenye siasa mwaka huu tunahitaji mahali ambapo tunaweza kuelewa nini wanajaribu kusema.
Heshima za dhati kwa wagombea wengine ambao sijawaorodhesha hapa. Hoja zenu sijazisikia na sina uhakika kama mna nia ya kweli ya kuliongoza taifa au mmefuata rudhuku.