Tulio na bibi/babu wenye vituko na vibwanga tukutane hapa

Tulio na bibi/babu wenye vituko na vibwanga tukutane hapa

[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] yaani wazee wangu basi tuu,halafu babu yangu anapenda kuuliza SAA(muda)hata uwe umeenda Pluto hamjaonana miaka 20,ukiingiza tuu mguu ndani cha kwanza kukuuliza ni "hivi sasa ni SAA ngapi hapo"[emoji23] yani hana kummisi MTU wala nn hajui umerudi ukechooooka au vipi yy ni SAA tuu usipomjibu utamsikia " najua nawakera ila hamnipendi tuu"[emoji23] [emoji23] ..na ukimjibu labda SAA 6:30 mchana baada ya dk 2 anauliza tena....eeeh unatamani umkate vibao akalazwe muhimbili[emoji1] [emoji1]
Nimecheka sana [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji119]
 
Dah bibi angu alikua ana duka lake ambapo akikutuma chochote uende pale pale Na si kwngine yaan upite maduka karib matatu Ndo uende duka alitakalo...bas siku moja kanituma soda nikanunua kwny duka la kwanza looh nlijuta kumbe alikua ananichungulia kwa dirishan Bas ile nampa tu chupa ikatupwa chin pwaaaa "nimekwambia kanunue kule we umeenda apo doda zao wanapunja Sukar we mshenz sana "ha ha ha bibi alikua mtata sana ata mchele akigundua tu umenunua sehem asiyotaka utamwagwa ata uwe kilo kumi ha haja

Rest in peace bibi
 
Mim bibi yangu upande wa baba ana vituko huyo,anaongea kuanzia asubuhi mpaka tunaenda kulala
Bibi yangu hua anaamka saa 12 asubuhi ole wako uchelewe kuamka ataanza kusema sijui mtaolewa na kina nani mpo wavivu vivu tu
Akija mtu anauza mboga au chochote bibi atataka apunguziwe na kuanza kusema mbona hata sio kizuri chukua hela wewe unakataa pesa(cha kwake sasa bibi yangu weee umwambie apunguze bei mkali kama nini)
Alilazwa hospital hua ana kisukari hiyo hospital ilikua mpya so kukawa na wagonjwa baadhi ,jumla wakawa wanne akiwemo na bibi yangu,ikifika asubuhi anaanza kuwaamsha kua wafanye usafi wafue nguo zao,mara wakaoge yaan utafikiri ye nurse wa zamu
Akiwa hayupo kwake anaona kila kitu hakiendi anaona kama anaibiwa vitu so muda mwingi yupo nyumbani na anataka kila kitu kikae sehemu yake
Hata itokee safari hataki kuondoka kwake anaona wafanyakazi wataiba

Anapenda watoto wa kiume hakuna mfano wa kike kwake hawana maana kabisa

Akiwa hataki mtu aende kwake na akaenda ukimsalimia tu au kumuuliza chochote anakua mkali na kuanza kulalamika kua huyu kijana hana adabu anaweza niuliza maswali ya hivi mim mzee,,yule mtu akiondoka ,watakuja baba zangu wadogo anaanza kuwapa mashitaka sasa akiona hawamjali,akija mtoto wake mwingine anamuhadithia na kuongeza chumvi ili yule kijana apigwe basi wakiona vile wanajifanya kukasirika na kusema wanaenda kumtafuta yule kijana wamfundishe adabu,basi bibi akisikia hivyo roho kwatuu,

Bibi yangu anaweza sema hivi baadae kikiharibika kitu anawakana wote kua mmesingizia,,

Hapatani na mmewe kila mtu analala chumba chake,,wakianza kurushiana maneno na babu kila mtu ni mbaya,,ataanza kumwambia na ufe tu sijui unasubiri nin mzee mbaya wewe huna maana,,bibi anapenda watoto wake na wajukuu zake kuliko mmewe

Kuna kipindi nilienda kuwasalimia nikawa namtengea babu chakula ,,kabibi kanamuambia babu subiri dinazarde aondoke uone nani atakupa chakula utakula jeuri yako

Bibi yangu watoto wa kiume hata wafanye nin haoni ubaya,nyie wa kike sasa ataongea siku nzima

Akianza kusimulia kua ye alikua mzuri utasema sijui alikuwaje haha

Kila mda anataka mle ye hali ila nyie mle tu chakula ndio furaha yake

Akianza kuchamba siku hiyo tutacheka tu maana siku hizi kabakiza mdomo tu ,maana anakua kakaa kwenye kiti hawezi kutembea haraka kama zamani wala kupiga

Hali kwa watu akiamini sio wasafi kama yeye,akitembelea sehemu atakunywa soda tu chakula hagusi

Bibi yangu ana mdomo huyu ,babu yangu humuambia kwisha habari yako naenda kuoa msichana mdogo,,nae anamuambia nenda umechelewa tukutolee mabegi

Siku moja nilikuta wanagombania kahawa,bibi kamnyima babi kahawa,alitaka kuweka kwenye maziwa
Anamuambia kanunue pesa zako unapeleka wapi

Basi inabidi kesho babu akanunue ile kahawa kubwa

Babu yangu sasa,ana ng'ombe wengi anawapenda kuliko sisi wajukuu ,,ukimuomba hata mmoja anakuambia ng'ombe wangu wagonjwa wamevunjika miguu
Ameanza kusahau pesa hua tunamchenjia buku buku,,akitembea na laki anaweza nunua sweta la 10000 akauziwa 80000,siku hiyi ikabidi wamuambie wee aksema pesa zangu zinawahusu nin nyie,mbona nyie mkinunua kitu siwaulizi,nikinunua mim tu mnatoa macho,,
Bibi yangu sasa utafikiri 80000 zake aliongea na kusema yule kijana afungwe sijui nin,babu anamkatisha nyamaza we mwanamke mzee

Babu yangu siku moja ananipa pesa ile anatoa akadondosha kondom moja nilicheka mpaka nikaanguka chini

Akiona mkewe kalazwa hayupo siku nyingi nyumbani anasema mleteni mke wangu,akifika siku hiyo tu wanakosana hahaha

Hua nacheka mno mie ,bibi yangu anaweza badili maneno mpaka ukashangaa na kusema juu eti dina mim nilisema hivyo inabidi umfurahishe kua hakusema wakati alisema na sisi tulikuwepo

Babu yangu akiugua mkipeleka ile ile hospital siku nyingine anakataa,,kua hiyo hospital imemchosha nipelekeni Dar nipande ndege,,,inabidi wampeleke tu

Anaweza ondoka bila kuaga akapanda gari akaenda Arusha anaenda kumtafuta mtoto wa ndugu yake ni daktari na kumuambia naumwa sana,akipimwa hakuna kitu
Huku watamtafuta balaa,mpaka simu ipigwe ndio wanamfata

Babu anatupenda wajukuu wa kike kuliko wa kiume,,sie wakike ndii hutupa pesa wa kiume anaawaambia nendeni kwa bibi yenu huko

Hebu elezeeni visanga vua huko kwenu
Muda si mrefu naachana na JF imekuwa ya watoto
 
Dah bibi angu alikua ana duka lake ambapo akikutuma chochote uende pale pale Na si kwngine yaan upite maduka karib matatu Ndo uende duka alitakalo...bas siku moja kanituma soda nikanunua kwny duka la kwanza looh nlijuta kumbe alikua ananichungulia kwa dirishan Bas ile nampa tu chupa ikatupwa chin pwaaaa "nimekwambia kanunue kule we umeenda apo doda zao wanapunja Sukar we mshenz sana "ha ha ha bibi alikua mtata sana ata mchele akigundua tu umenunua sehem asiyotaka utamwagwa ata uwe kilo kumi ha haja

Rest in peace bibi
Hahahahah uwiii alikua jeuri,,eti wanapunja sukari
 
anaweka tu chumbani kwake ata kule kijijn ana makopo rum kwake ukiyatupa baada ya cku mbili unakuta tena@dinazarde
Umenikumbusha kuna mama mmoja anapenda makopo huyo sijui akizeeka itakuwaje
 
Hahahahah uwiii alikua jeuri,,eti wanapunja sukari
Ha ha ha alikua ni shida na Ni jeur kwel kina baba walimdekeza sana alikua hawez kutembea bas anajikongoja anakaa nje kibarazan kwake bas kila anaepita ata muuliza kile Mara iki mpaka jion ana Habari zoteeeee Za mji ha aha ha ha
 
Ha ha ha alikua ni shida na Ni jeur kwel kina baba walimdekeza sana alikua hawez kutembea bas anajikongoja anakaa nje kibarazan kwake bas kila anaepita ata muuliza kile Mara iki mpaka jion ana Habari zoteeeee Za mji ha aha ha ha
Hahahaha
Tuna kazi sijui na sie tutakuwa hivyo
 
Umenikumbusha my bibi Dina, ngoja nifanye nikamuone aise after Xmas
 
Mi babu yangu alikua mlevi sana....... Sasa akitoka kupiga pombe bahati mbaya hajakuta mtu........ Anachukua manati yake na mawe yakutosha aliokua anahifadhi ndani kwa ajili ya kuwindia ndege.... ...then anakaa mlangon.
Sasa hapo kila anaekuja kutoka misele anakula Stone zakutosha...kama kukwepa ndo utaisoma namba

Kuna Siku tulilala Kwenye shamba la chai mpka asubuhi mana mawe yalikua hayaishi...... Na anashabaa kinoma
 
Nimeishi na bibi kuanzia la kwanza hadi form 1.
Pamoja na utundu wangu, bibi ananipenda mpk kesho.

Bibi anawajukuu 15, lkn katika wote ole wake asikie kuna mtu ananisema vibaya, hata baba au mama.

Yani Gusa watu wote ila sio, mimi.

Bado yupo, na huwa nampigia sim mara kwa mara. Akisikia sauti yangu anafarijika sana.

Uzuri namjali vipesa vya pombe na nyamaa.

I love you Grandma
 
Mi babu yangu alikua mlevi sana....... Sasa akitoka kupiga pombe bahati mbaya hajakuta mtu........ Anachukua manati yake na mawe yakutosha aliokua anahifadhi ndani kwa ajili ya kuwindia ndege.... ...then anakaa mlangon.
Sasa hapo kila anaekuja kutoka misele anakula Stone zakutosha...kama kukwepa ndo utaisoma namba

Kuna Siku tulilala Kwenye shamba la chai mpka asubuhi mana mawe yalikua hayaishi...... Na anashabaa kinoma
Hahahahahaha
 
Nimeishi na bibi kuanzia la kwanza hadi form 1.
Pamoja na utundu wangu, bibi ananipenda mpk kesho.

Bibi anawajukuu 15, lkn katika wote ole wake asikie kuna mtu ananisema vibaya, hata baba au mama.

Yani Gusa watu wote ila sio, mimi.

Bado yupo, na huwa nampigia sim mara kwa mara. Akisikia sauti yangu anafarijika sana.

Uzuri namjali vipesa vya pombe na nyamaa.

I love you Grandma
Vizuri
 
Bibi yangu mkubwa yeye alikuwa anapeenda Sana shikamoo ,ukitaka ugomvi nae usimuamkie ,ila sasa yeye alikuwa anapokea hata shikamoo za wiki au mwezi unaweza ukamuamkia shikamoo 21 zote na akikuuliza una mwambie tu nilishakuamkia za wiki tutaonana jumapili
 
Nilkuwa na umri kama wa miaka 12...nilienda kumsalimu bibi mzaa baba Tukuyu siku ya kwanza nilipikiwa wali maharage...siku ya pili alipika samaki Ile jua linaanza kuzama akaniambia nitwange mihogo (majhabhu) kwa aajili ya ugali wangu usiku maana ye atakula ndizi choma (matoki)....bwana weee si nikaenda kucheza nikarudi usiku kama saa 2 hv...ile nafika tu nakuta ameshachoma ndizi ,,akapakua samaki bakuli mbili , yake akaweka ndizi zake alafu yangu akanipa bila chochote , Si nikamuuliza ugali uko wapi akajibu kwa kilugha "kyo ikhi gwhakanagha pakutika itasi""(ndo ule ambao ulikataa kutwanga mda ule)...nilikula samaki peke ake nikaenda Kulala ....nilijifunza kitu....R.I.P mke wangu (bibi)
 
Back
Top Bottom