Dah, mmenikumbusha mbali saaaaaaaana sana. Enzi za Tosa. Na marehemy mzee DUDU!
Characters zinazonikosha na nazikumbuka mpaka leo ni pamoja na:
1. Paschal Joseph Mugasa- Classs Monitor CBG 1990-1992. Jamaa alikuwa mnoko usipime. Naambiwa siku hizi amekuwa, ameacha
2. Muhidin Amour; duh usiseme!
3. Angolwisye Malaiso, bonge la football striker, sijui iko wapi hii kijana
4. Lugano aka MC na panki lake ilikuwa raha sana.
5. Makinya: jamaa nilikuwa namhusudu sana intellectually. Sijui kama si padre huyu?
6.Mwalwambile: aisee kweli Mungu anaumba viumbe wake, sina la kuongeza!
7. Mwalimu anaitwa Maulaga; huyu akanifanya niogope kuwa mwalimu. Ngoma full time iko drunk- ulanzi, komoni, ugimbi ++++
8. Maradona: kwa kweli mpira wa miguu bongo ni kwa wasiosoma. jamaa angeendeleza fani angekuwa ni sawa na Asamor Gyan
Natamani kurudi pale, angalau kutembelea tu. Sijui pako vipi now? Jamaa aliniambia pikipiki na daladala zinapanga foleni kusubiri watorokaji wakati sisi tulikuwa tunakula 5 km na ikibidi 19 km to town fresh kabisa.
Oh! Tosa weee! Nilikuwepo hapo 1981-1983 (EGM). Umenikumbusha mbali sana. Nakumbuka nilivyotumia akili nyingi sana kukwepa fimbo ya DUDU alipoamua kuwashughulikia Kidato cha sita wote kwa kuwachapa viboko vinne @ yeye peke yake. Nilifaulu kupitia dirisha la jikoni nikarukia upande wa magharibi. Kwa kufanya hivyo nilifaulu kutopigwa kiboko hata kimoja na DUDU mpaka nilipomaliza kidato cha sita.
I was there A' level 1984 - 86, duuuuuuuuuu inanikumbusha mbali HeadMaster Dudu Second Master bwana mmoja mchaga aliyekuja kuwa HeadMaster Azania
Enzi za Marehemu Mpogole "DUDU"
M
Madella Annex
Mabweni Ya Azimio na Mwenge
Madarasa ya Form V PCB na PCM
Madarasa ya Form 6 EGM na CBG
Uwanja wa Basketi picha hii imepigwa kwa juu kule Mandella Annex
KWELI KABISA, Nilitaka kuandika hivi hivi, mpigaji alikuwa kasimama karibu na shule ya Msukanzi kama sikosei. na Idete shambani ndio lilikuwa eneo salama. mnakumbuka kipindi cha mapera idete na siafu?kutoka picha ilipopigwa nyuma njia ya kwenda uwanja wa mpira, kushoto ni nyumba ya masista, kulia njia ya kwenda ipamba.
mbele- kupanda ndio tosa. Asante kwa aliye tukumbusha enzi hizo za Dudu.
wakati wa mgomo baada ya FFU kutinga sie wakazi wa mandela enoe salama lilikuwa shamba la mahindi pembeni na nyumba ya dudu
Vitu vya Wagalitia huwa ni Makini sana.
Yaani serikali isingetaifisha Shule hizi wangekuwa mbali zaidi.
Mnaweza kuweka na Madrasa zilizotaifishwa tuzijue?
Tosa boys sio wapiga gitaa kama wa Pugu na Minaki.
Tosa huwezi kuifaidi kama
~hujaenda shambani na bustanini Idete
~hujatembea kwa mguu toka Tosa hill hadi Junction kwa miguu
~hujaenda kwa masista kununua "bans"
~hujaenda Msiwasi ground
~hujaenda half mile, the most luxurious place ever in the hill
~hujaenda power station hadi Ipamba
Kakuruvi, hebu ongezea ktk list.
Acha kudanganya watu hapo penye nyekundu.
Kwanza Mkwawa hakumuua Zelewisky aka Nyundo kwa mikono yake, bali aliuliwa na majeshi ya Mkwawa.
Pili, Nyundo aliuliwa eneo la Lundamatwe karibu Ilula (mpaka leo mnara wa kaburi lake upo just about 20 mts away from Moro-Irg road). Lundamatwe kuna umbali mkubwa sana hadi Tosa.
Tatu, mapigano yaliyohusisha mlima huo (kabla haujaitwa Tosamaganga) kati ya Mkwawa na wajerumani siyo zamu hiyo aliyokuwepo Nyundo.
Naweka sawa tu, tuendelee na mada.
Mkuu enzi hizo ukichaguliwa kujiunga pale mtaani unaagwa kwa sherehe. Chezea special School wewe. Mkuu hiyo sifongo umenikumbusha mbali sana, chumvi yenyewe ukitaka kuweka ni ya mawe mpaka usage. Dona na maharage daily mboga mboga zinauzwa na mabeki tatu wa walimu pale jikoni kwa chini, nyuma ya bwalo kwa wenye uwezo.NILIKUWA PALE 1987-89 PCB1, TOSAMAGANGA NI MOJA YA SHULE YENYE NA SIFA YA AINA YAKE KIELIMU NA KINIDHAMU ENZI HIZO, NAMKUMBUKA MWALIMU KASANDA ALIKUWA BALAA KWA FIZIKIA, MIDADI IKIMPANDA ANATUMIA LAB KOTI YAKE KUFUTA UBAO (Alikuwa ni mtaalamu kwelikweli yeye na warusi akina Verichko na Terminov) Kulikuwa na mtaalamu wa Biolojia Mwalimu Kisenime alikuwa -Classification, biochemistry....) Kulikuwa na warussia mume na mkewe Verichko walikuwa wakali sana kwa chemistry, pia na mrusia mwingine alikuwa anaitwa Shabunin. Namkumbuka mwalimu mmoja alitupokea pale anaitwa Mwakabanje...alitutisha sana tulipoingia....Alikuwa ametayarisha reagents lab ameandika instruction ubaoni... Tulipoingia Lab tutasubiri maelekezo.... Akatuuliza kwanini tumeduwaa, ni kweli sisi tumefaulu kusoma pale Tosamaganga ama ni watalii...Alikuwa serious sana yule mwalimu... Bush politician - MKINGA na Mwalimu Chitinde, Mwl Mahenge, Ila kulikuwa na Mwl anaitwa Mgunya alikuwa Noma sana yule Bounsa.... Namkumbuka headmaster Mpogole AKA DUDU alikuwa anasimamia sana suala la elimu, Yeye alikuwa anataka kukuona wakati wote una kijitabu ama karatasi unasoma hata akikukuta Ipamba ukatoa kakijitabu na kujifanya unasoma anakuacha.... Ila kuna time alikuwa anakumezea na ukiona mmeitwa assembly basi ujue kuna wanafunzi anawatafuta either aliwakuta town, ama ipamba, ama njia panda kule mseke, ama kwenye ulanzi huko Msukanzi maana alikuwa na kumbukumbu nzuri sana. Pamoja na mengine yote namshukuru sana MUNGU kusoma pale mbali na matatizo ya kunya uji usio na sukari - Sifongo, Lakini ELIMU YA PALE ILIKUWA KIBOKO....