Tuliosoma Shule ya Sekondari Tosamaganga tukutane hapa

Inanikumbusha mbali sana, wadau mliopitia hapo mpooooo!

View attachment 31724
Ni vigumu kusoma Tosamaganga usifanikiwe maishani. Labda kwa wanafunzi wa siku hizi. kwa miaka ya tisini, mazingira na commitment za mwanafunzi binafsi zilimprogram awe fighter katika maisha.Tulijiita wagumu kwa maana tunaweza pitia shida zozote kuelekea mafanikio. Umenikumbusha shule yangu maana niliwahi kuwa kiongozi wa bweni la Azimio. Wakati ule hapakuwa na polluters (wasichana) nasikia siku hizi wapo! hata hivyo asante kwa picha zenye kumbukumbu nzuri maana zimenipa faraja mie pengine na wengine tuliopo nje ya nchi yetu. Hawa walimu wako wapi? CONTRAR, MALARE, MRISHO, na wengine katika miaka ya 90s
 
Enzi za Marehemu Mpogole "DUDU"

M


Madella Annex



Mabweni Ya Azimio na Mwenge



Madarasa ya Form V PCB na PCM



Madarasa ya Form 6 EGM na CBG




Uwanja wa Basketi picha hii imepigwa kwa juu kule Mandella Annex

mapinduzi na ujamaa vipi?
 
Mkuu umesahau zile ofisi kuu ambazo kabla ya kuingia inabidi upunguze baadhi ya nguo uzitundike nje ilikupunguza harufu ukirudi kwa wenzako. Si nyingine ni HALF MILEEEEEEEEE...... Teheteheteheeeeeee
 
Ile Mandela Annex wakati tunaitumia kulikwa na fununu kuwa lingefungwa kutokana na ubovu. Kuna kipindi lilikuwa linatikisika floor, vipi limekarabatiwa?
 
Kanisa lipo mkuu, angalia picha ya kwanza kabisa upande wa kushoto wa Mpogole (Dudu) utaona kanisa la RC. Unless unaulizia kanisa la dhehebu lingine.
 
Kanisa lipo mkuu, angalia picha ya kwanza kabisa upande wa kushoto wa Mpogole (Dudu) utaona kanisa la RC. Unless unaulizia kanisa la dhehebu lingine.

Asante nimepitia picha nimeona na nime-edit text yangu. Asante sana.
 
Matuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuure - kachote umeme! I miss it! Wapi akina double man, given mariki, power, ... msela..., nk

Where is Given Marik? Matola naye yuko wapi? Ndio footballer wenu miaka ile
 
Ahsante sana. Hicho ndicho kisima cha elimu ya Sayansi

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Mugasa! haahhahaaa, I know this man, siku hizi busara kibao!! kumbe alipita huko??
Joseph Pascal Mugasa ni Daktari wa Falsafa (Ph.D holder), he is a good man, mpenda mabadiliko kisiasa, na ni Mbunge mtarajiwa.
 
Nakumbuka sana hivi vitu

Nyali
Sumu
Pola

Watu maarufu
Malata
Mama mongoi
Vai

Maeneo ya kwenda kuuza sura
Iringa girls ( japo baadae tuliwapiga chini nafasi yao ikaenda kwa ifunda girls)

Kwa mama myovela
Walimu ninaowakumbuka
Charwe
Ka 50
Etc

Dah manesi wa ipamba ndio wengine tulikua twajipoozea hukooo
 

Attachments

  • 1434367409886.jpg
    69.4 KB · Views: 191
  • 1434367444148.jpg
    9.9 KB · Views: 438

daah kambi langu hilo tosamaganga aisee pana raha zake bwana
 
Nimemaliza hapo miaka ya 2000+.......
Nimeishi bweni la Azimio namba 8, Mapinduzi 58 na Chemba yangu ilikuwa Mandela anex...

I'll not stop remember This GWANTANAMO LOOKS PLACE.

 

Mussa Mohamed, alikuwa PCM , nilikuwa miongoni mwa watu waliokuwa kwenye safu ya kumchukulia rollcall na pass ya kwenda mjini, bahati mbaya ticha wa zamu alikuwa ananifahamu nikashindwa kwenda akajitosa jamaa anaitwa Juma Bundala, inshort jamaa hakwenda kutafuta feki coz NECTA ilikuwa bado karibia miezi 2, jamaa alienda dar kuwanunukia washkaji wawili simu ambao ni Siriri na Mashaka, mussa alitaka kupata cha juu ndo ikawa bahati mbaya akakutwa na mauti, it was 2003 April tunajiandaa na NECTA
 
Ngoja nisubiri wale wakongwe wenzangu wa enzi ya Headmaster Dudu na Discipline Master mwenye sura kama Mugabe Mr. Mavika tukumbushie enzi.
 

Alikua anaitwa musa mohamed alikua ni best yangu sana akitokea st antony na mm nikitokea pugu na nilijuana nae kwenye tuition za pre form V buguruni na mm ndio nilikua namuitikia rollcol na alikwenda dar si kuchukua feki bali kuchukua simu za kuuza kuna mtu mmoja anaitwa mashaka alikua ni mshamba lakini ana hela sana alitokea kahama ndio alikua anataka simu so cha juu kilikua kikubwa nakumbuka aliondoka shule j5 kwenda dar na ilipofika j2 mchana tukawasiliana kwamba anarudi j3 yaani kesho yake wakati jioni ya hiyo j2 ndio anakufa sisi hatujui mbaya zaidi home kwao kurasini hawakujua kama yupo dar coz alifikia geto kariakoo kwa rafiki zetu waliokua wanasoma benjamini..ile kufika j3 asubuhi mashaka akamtuma rafiki yake anaitwa ayubu mgube akachukue ruhusa(pass) kwa jina la mussa ili mussa akirudi awe kama alienda town tu kwa kuomba ruhusa.Na kama wewe ndio ulikua mwl wa zamu basi ndio ulitoa hiyo ruhusa kwa vile mussa ulikua humjui.Ilipofika saa 3 siku hiyo ya j3 ndio taarifa zinafika shule kwamba mussa kafariki jana yake saa 12 jioni tena Dar,walimu wakirudi kwenye data mussa anaonekana yupo shule na amechukua ruhusa asubuhi ya kwenda iringa mjini howcome alikua dar tena??ilikua bonge ya msala ikabidi ifanyike parade ya dharura ticha wa zamu akaanza kukagua sura iliyoomba ruhusa asubuhi kwa bahati nzuri alimtambua ayubu ndie aliyeomba ruhusa kwa jina la mussa na kumsachi ile ruhusa alikua nayo mfukoni!!!alichezea bakora nyingi sana na sunspesion yeye na mashaka mpk siku ya mtihani...dah umenikumbusha majonzi!!kwa tosa msiba ni km ulikua room namba 29 mwenge maana watu ndo walikua wanakuja kunipa pole..!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…