Think Hard
JF-Expert Member
- Feb 12, 2015
- 318
- 303
- Thread starter
- #21
Mkuu nilikua nawaza sana kuhusu maisha niliyoyapitia..Ukienda mchafu wanakagua usafi, ukienda msafi hawakagui.
Dah! mleta mada leo umenikumbusha mbali sana.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu nilikua nawaza sana kuhusu maisha niliyoyapitia..Ukienda mchafu wanakagua usafi, ukienda msafi hawakagui.
Dah! mleta mada leo umenikumbusha mbali sana.
Mkuu huyo madam alikua shiidaHa ha ha.. Mtoa mada umenikumbusha mbali sana.. Shule niliosoma ilikua ukifanya kosa ,madam anataka ununue ufuta(ladu) kwake la sivyo utakula mvua ya fimbo...
Mie sijasoma Kijijini but enzi hizo shule za mjini nazo ilikuwa kama Kijijini tu, matangazo ya mwl wa zamu, kesho mtakuja na maji, mfagio, mbolea, jembe, maua, jiwe hapo bado mfuko wako wa daftari na bado unatakiwa uwahi namba, kweli tumetoka mbali.Tuliosoma kijijini hata wakimbizi wana nafuu, kwa siku moja unatumwa kuni, mbolea, kopo la maji, fagio, jembe, mfuko wako wa rambo wa daftari yani ukimwona mwanafunzi kwa mbali mkimbizi chamtoto.
Sio tumetoka mbali, haya mambo bado yapo ktk shule nyingi vijijini. Ila nimejiapiza, watoto wangu hawatosoma shule hizo ni bora nibebe bunduki nikaibe.Mie sijasoma Kijijini but enzi hizo shule za mjini nazo ilikuwa kama Kijijini tu, matangazo ya mwl wa zamu, kesho mtakuja na maji, mfagio, mbolea, jembe, maua, jiwe hapo bado mfuko wako wa daftari na bado unatakiwa uwahi namba, kweli tumetoka mbali.
Siku ya kupika sayansi kimu, mnabeba kuni, sahani utayotumia kulia chakula
Tehtehteh, watoto wa siku hizi wana raha, basi la shule linamfuata hadi getiniSio tumetoka mbali, haya mambo bado yapo ktk shule nyingi vijijini. Ila nimejiapiza, watoto wangu hawatosoma shule hizo ni bora nibebe bunduki nikaibe.
Kama umesoma st Kayumba utakuwa una aidia na haya...
1. Unaenda shule umechelewa unakuta mwalim anakamata wachelewaj unaamua urudi nyumbani
2. Unachukua kimbegu cha ubuyu unasugua sakafuni af unamuunguza mwenzio
3. Mkiruhusiwa tu unakimbia unataka uwe wa kwanza kwenye njia yenu y kurudia nyumban
4. MTU akikukera unamfungia shule (mnapigana baada ya kufunga shule)
5. MTU akikunyima kitu chake unamwambia "Ahaa eeh utaona sa nne"
6. Wadada wembamba ndo wanaongoza kwa kusuta wenzao
7. Ukiibiwa daftar jipya unalia kuliko hata uliloandika
8. Unajaza mapeni kwenye mkebe(compass) na mengine hayaandiki
9. Vifaa vingine kwenye mkebe hujawahi hata kuvitumia mfano bikari labda utolee mwiba
10. Hakuna habari nzur kama kuambiwa Leo hamna shule au mwalim hayupo
11. Habari mbaya zaidi n kurud nyumban kutoka shule una njaa af unaambiwa chakula mgeni kaja tumempa
12. Mtoto wa mwalim utamgundua tu kwanzia sweta begi na viatu vyake
13. Usiombee umpige mtoto wa mwalim utataman uache shule
14. Unatengeneza kifutio cha ndala af unatishia eti kinafuta hadi peni
15. Ukaguzi na huna ufagio.. unaomba chelewa kwa watu af unaongeza kijiti katikati
16. Siku ukienda na ufagio wanakagua maji, ukienda na maji wanakagua kuni au mbolea
Dah shule zetu hizi!!
Ipi umeipitia wewe
Ha ha haaa tTuliosoma kijijini hata wakimbizi wana nafuu, kwa siku moja unatumwa kuni, mbolea, kopo la maji, fagio, jembe, mfuko wako wa rambo wa daftari yani ukimwona mwanafunzi kwa mbali mkimbizi chamtoto.
Hahahahahah, huo mchezo wa kumulikwa na vioo tulifanyiwa kipindi flani skuli, tukawasemea kwa mwalimu wakala kichapo cha mbwa mwizi...Nimetoboa watu na bikari sana ,na kioo changu spesho wakati wa paredi ,nimeona sana vyupi vilivyotoboka dah
Hahahahaha aiseee nilikua na degree ya chabo sikuwahi shitakiwa kwa hilo swalaHahahahahah, huo mchezo wa kumulikwa na vioo tulifanyiwa kipindi flani skuli, tukawasemea kwa mwalimu wakala kichapo cha mbwa mwizi...
Isije tu ikawa wewe ni mmojawapo UncleBen
Ha ha ha ha ha haaa,ulikuwa na vituko aisee, UncleBen utoto una mengi sana,ya kuchekesha na ya kusikitisha.Hahahahaha aiseee nilikua na degree ya chabo sikuwahi shitakiwa kwa hilo swala
Halafu kuna nyigine nilikua natembea na lensi sasa jua likiwaka naweka juu ya utosi wa mtu aloo inachoma ile
Hahaha dah kuna wakati natamani ningerudi kwenye miaka 12 hivi ,vioja vyangu vingi vilianza na miaka 12 ,nishapiga paka alikula njiwa wangu ,niliua halafu nikamchuna ,kuona haitoshi bado nikaning'iniza kichwa chake chumbani kwa siku tatu ,hee bi mkubwa anashangaa harufu kuja kushuhudia aisee aliogopa kuanzia hapo akajua huyu jamaa ana hasira mbaya ,tuachane na habari hizi tunajaza uzi wa watu bureHa ha ha ha ha haaa,ulikuwa na vituko aisee, UncleBen utoto una mengi sana,ya kuchekesha na ya kusikitisha.
Mbabe mnyonge? wababe walikuwa wanapitisha mkong'oto sasa kujihami ilikuwa ni kung'ata,mawe au hizo bikariDah!! Ulikua mbabe sana wewe..