asiyetabirika
Member
- Oct 14, 2019
- 46
- 56
Kumkopesha pesa jamaa/ndugu muda mwngine kumekuwa na changamoto sana kwenye urudishaji wa deni, nimegundua kwa sehemu kubwa mkopaji huwa akija kukopa kwa upole huku akitia huruma huku akiwa na ahadi za uhakika juu ya siku ya kulipa deni, sasa kimbembe ukisha mkopesha zinapoanza kusogezwa siku za kulipa deni na sababu lukuki zilizo nje ya makubaliano.
Hii tabia imeua sana mahusiano mazuri kati ya ndugu,jamaa na marafiki yaani unakuta watu wanagombana sababu ikiwa mmoja alimkopesha mwezake ila hakulipwa na mkopaji hana dalili za kulipa na muda mwingine nae utakuta analeta ukorofi kwa kujibu vibaya au analeta sababu dhaifu na visingizio visivyo eleweka na wakati mwingine kama upo mbali nae anaweza asiwe ahapokea simu yako kabisa.
Sasa kama wewe ulikutwa na visanga hivi vya kumkopesha mtu na akakusumbua kulipa hadi ukaona upotezee au kugombana nae kabisa na kuvunja urafiki/mahusiano mazuri yaliyokuwepo kabla ya kukopeshana, tupe kisa chako jinsi ilivyokuwa...
Hii tabia imeua sana mahusiano mazuri kati ya ndugu,jamaa na marafiki yaani unakuta watu wanagombana sababu ikiwa mmoja alimkopesha mwezake ila hakulipwa na mkopaji hana dalili za kulipa na muda mwingine nae utakuta analeta ukorofi kwa kujibu vibaya au analeta sababu dhaifu na visingizio visivyo eleweka na wakati mwingine kama upo mbali nae anaweza asiwe ahapokea simu yako kabisa.
Sasa kama wewe ulikutwa na visanga hivi vya kumkopesha mtu na akakusumbua kulipa hadi ukaona upotezee au kugombana nae kabisa na kuvunja urafiki/mahusiano mazuri yaliyokuwepo kabla ya kukopeshana, tupe kisa chako jinsi ilivyokuwa...