Prakatatumba abaabaabaa
JF-Expert Member
- Aug 2, 2022
- 1,842
- 6,087
Wazee wa baka bencha mpo (ilininichukua miaka mingi kujua kwamba Ilikua inamaanisha back bench yaani seat ya nyuma 😁😁).
Nimeingia secondary Mwanza pale nyakabungo nikazingua vibaya mno nikafukuzwa Shule nikahamia Thaqafa secondary kwa ogweyo na opiyo nikatandika zero takatifu.
Kiukweli nilizingua sana sikuwahi kupenda kusoma kabisa, ukorofi Mimi, mipira Mimi, utoro ndio Ilikua jadi yangu, Mibangi sana naenda Shule saa 2 saa 5 nimepotea (nyakabungo Hapo).....
Thaqafa pale nimeruka ukuta kwenda kuzurura town (nilipelekwa boarding na mzee) niliona Shule kama mateso tu, Mwisho wa siku nikapata division zero nzuri tu.
Nimekuwa baba Sasa kiukweli siwezi kumdanganya mtoto wangu kwamba nilikua na akili saaana (kama wazazi mnavyowadanganya watoto wenu) Ila vice versa mtoto wangu Yuko la kwanza naona kama anajitahidi sio kama Mimi baba ake labda karithi akili kutoka kwa mama ake.
Navyoyaona maisha kwa Sasa, Kuna watu wamezaliwa ni given wako na uwezo tu msuli kidogo matokeo makubwa, wapo ambao walikua na msuli temboo matokeo sisimizi kama ya kwangu tu.
Nimezaliwa kwenye familia ambayo wengine walipata division one Lakini Mimi nilipata zero je Mimi ni kilaza? 😁😁 Au sikua serious?
MTAZAMO WANGU
Elimu ni nzuri sana, ukitaka kua na pesa kwenye elimu basi inabidi usome saaana kwa viwango vya juu basi Hapo utamiliki pesa, pasipo elimu Kuna viwango ambavyo uwezi kuzifikia.
Baada ya kupata zero mzee wangu alinambia neno moja, POPOTE PALE ULIPO KATIKA ENEO ULIPO UFANYE KAZI KWA JUHUDI NA BIDII SAAANA, Uwe umesoma au hujasoma juhudi na bidii nadhani ndio ufunguo wa kutengeneza milo mitatu kwa siku, hii ndio principle ninayotembea nayo huku mashambani.
Wenzangu tuliopata zero je tunajuta? Je, unatamani kurudi shule kusawazisha makosa? Mtoto wako akipata zero utaumia?
Nimeingia secondary Mwanza pale nyakabungo nikazingua vibaya mno nikafukuzwa Shule nikahamia Thaqafa secondary kwa ogweyo na opiyo nikatandika zero takatifu.
Kiukweli nilizingua sana sikuwahi kupenda kusoma kabisa, ukorofi Mimi, mipira Mimi, utoro ndio Ilikua jadi yangu, Mibangi sana naenda Shule saa 2 saa 5 nimepotea (nyakabungo Hapo).....
Thaqafa pale nimeruka ukuta kwenda kuzurura town (nilipelekwa boarding na mzee) niliona Shule kama mateso tu, Mwisho wa siku nikapata division zero nzuri tu.
Nimekuwa baba Sasa kiukweli siwezi kumdanganya mtoto wangu kwamba nilikua na akili saaana (kama wazazi mnavyowadanganya watoto wenu) Ila vice versa mtoto wangu Yuko la kwanza naona kama anajitahidi sio kama Mimi baba ake labda karithi akili kutoka kwa mama ake.
Navyoyaona maisha kwa Sasa, Kuna watu wamezaliwa ni given wako na uwezo tu msuli kidogo matokeo makubwa, wapo ambao walikua na msuli temboo matokeo sisimizi kama ya kwangu tu.
Nimezaliwa kwenye familia ambayo wengine walipata division one Lakini Mimi nilipata zero je Mimi ni kilaza? 😁😁 Au sikua serious?
MTAZAMO WANGU
Elimu ni nzuri sana, ukitaka kua na pesa kwenye elimu basi inabidi usome saaana kwa viwango vya juu basi Hapo utamiliki pesa, pasipo elimu Kuna viwango ambavyo uwezi kuzifikia.
Baada ya kupata zero mzee wangu alinambia neno moja, POPOTE PALE ULIPO KATIKA ENEO ULIPO UFANYE KAZI KWA JUHUDI NA BIDII SAAANA, Uwe umesoma au hujasoma juhudi na bidii nadhani ndio ufunguo wa kutengeneza milo mitatu kwa siku, hii ndio principle ninayotembea nayo huku mashambani.
Wenzangu tuliopata zero je tunajuta? Je, unatamani kurudi shule kusawazisha makosa? Mtoto wako akipata zero utaumia?