Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

hela
Kuna bro wangu kakata 250,000,000 ndani YA miezi 14 hivi sasa Hana HatA mia mbovu....sio mda ataanza kuongea peke yake road
hela bhana zina mambo mengi...ndo maana huwa sishangai mtu kufirisika..ila huwa naomba Mungu siku nikikamata tena hela anipe hekima na busara juu ya kuzitumia.

Kuna kijana juzi alienda kwa baba yake kuomba mtaji aendeleze kiduka chake cha spare..mzee akampa 28M jioni yupo na masela anawanunulia bia..Akasema ngoja aende kampala kufata spare..huwezi kuamini alirudi na Toolbox tu..ila 28M zimekatikia kampala mji wa starehe sana ule
 
Nimecheka utafikiri mazuri
Kuna jamaa yetu alipewa hela baada ya mzee wake kufariki million 29.Kipindi hiko kuna nyumba inauzwa million 7 tukamshauri anunue wapi.Yeye alidai mipango yote bandari salama.Bwana kwanza hiyo safari kutoka Kahama to Dar ,Nzega alilala huku anakula bata,Singida hivyo hivyo Dodoma bata kwa kwenda mbele,Moro mwendo uleule.Baada ya mwaka kupita namuona tena Kahama nilimwambia "ntakutandika makofi ".Baada ya kuanza kuniambia kaka unajua hutu tubiashara twa kuuza mafuta ya vibaba na nyanya chungu tunalipa watu hawajui tu.Kwa sasa hana hata 100 tunambeba ndugu yetu kinachopatikana tunagawana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji1] [emoji1] [emoji1] . Nilikuwa nakaanga mayai 10 kila siku.
Nikienda bar. Mbuzi choma ya 10,000.
Kuhonga sasa.kuvaa usiseme.
Mara ya mwisho Naenda ATM. Kuna 4,500..
Nilikuwa mdogo.ila HeLa za kukinga tu hazina Baraka
Hiyo nickname yako inahusiana na hiii story
 
Back
Top Bottom