Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

Nimesoma comments zote kiukweli zinafurahisha,kuhuzunisha na kukejelisha pia[emoji28].

Ebu mie niwape yangu japo Mungu alijua kurudisha Upinde kwangu baada ya kuuvunja wa mwanzo.

2000's (censored) nipo mwaka wa Mwisho chuo,napokea simu ya mzee "maliza uje kuna kazi nimekutafutia uje uanzie maisha".

Mwana tii!! Nadondoka job kwa cheo kikuubwa (ambacho wewe kama unge apply wangetaka 5 yrs experience,4.5+ GPA na makolokolo kibao)[emoji28],mie hiyo nimezama sijapata hata gamba chuoni litakuja mbele ya safari chezeea!!

Salary per month around 2M+ na mashehena kibaoo hapo toa madili na vishoka somewhere!!

Mchawi/wa kumlaumu ni "dereva wa bajaji" dogo junk flani hivi ..mwanzoni mwanzoni hapo natafuta pipi tu sijavuta hata kigoda cha mzungu aka Ndinga...huyo dogo ndio alikuwa ananitoa home mpaka job na kunirudisha kwa malipo ya mwezi kipande cha MIKOCHENI hapo...

Kipindi naanza job full kupiga kazi hasa mpaka mida ya saa mbili usiku hukoo ndio naachia ofisi...dogo wa bajaji hyo ratiba alikuwa anaijua...pia alijua mausha yangu yote kama nipo single...siku ya siku akanichoreshea kiramani flani "braza kwaninj uteseke kurudu home night wakat kuna pande flani unaweza kupozi na ukala matunda ya peponi"[emoji28].

Kwa kuanzia nikapelekwa "Massage Parlor" moja matata mnooo yani yani yani yani acheni tu.!!!

Kuingia watoto wa kila rangi afu wamesimama kama mwibaa hasaaa....(wazuri)..dogo akamuita matroni[emoji28][emoji28] "braza haya mambo ni mpya,mpe Menu atakayo shindwa kuisahau milele" ...matroni[emoji860]"yupo njema?!!"...dogo[emoji860]"weee mama wewee mie sitembeagi na wauza matunda[emoji28]"

Matroni[emoji860]"kama vipi na mie naingia mzigoni na vijana wangu kama 2 3 hv tusimamie show ya mgeni muheshimiwa mpya"

Dogo[emoji860]"fanya hivyo utakuja kunishukuru badae mchizi ana jiwe hasaa"

FUPISHA STORY:

Wanangu ee wa JF
Watoto wa hiyo parlor walichukua namba yangu wakaanza kuwa wananitafuta privately kila mmoja anataka kutumia opportunity kibinafsi.....

Dogo akanipeleka saloon hiyo wananyoa Mastaa tu full vidada vya instagram na bongo movie kibaoo hapo

Picha linaanza naingia tu kutupa jicho mwanangu Byser huyo hapoo mbele!! Sijacheki pembeni Nyandu tozy yule paleee naanza kuambaa ambaa Naona kiti cha kupumzikia ka chill Young dee paka rapper!!!

Nilivyotoka kunyoa pale naanza kupokea meseji kibao "braza mie msanii,najua kuimba nisimamie"
Mwingine "kaka mie ni model nahitaji support ya mavazi,location na cameraman wa maaana"!!

ITAENDELEA
But now Mungu kanipa second chance although najua laana zote za hapa bongo kupitia huyo "dogo wa bajaji"....
 
Nimesoma comments zote kiukweli zinafurahisha,kuhuzunisha na kukejelisha pia[emoji28].

Ebu mie niwape yangu japo Mungu alijua kurudisha Upinde kwangu baada ya kuuvunja wa mwanzo.

2000's (censored) nipo mwaka wa Mwisho chuo,napokea simu ya mzee "maliza uje kuna kazi nimekutafutia uje uanzie maisha".

Mwana tii!! Nadondoka job kwa cheo kikuubwa (ambacho wewe kama unge apply wangetaka 5 yrs experience,4.5+ GPA na makolokolo kibao)[emoji28],mie hiyo nimezama sijapata hata gamba chuoni litakuja mbele ya safari chezeea!!

Salary per month around 2M+ na mashehena kibaoo hapo toa madili na vishoka somewhere!!

Mchawi/wa kumlaumu ni "dereva wa bajaji" dogo junk flani hivi ..mwanzoni mwanzoni hapo natafuta pipi tu sijavuta hata kigoda cha mzungu aka Ndinga...huyo dogo ndio alikuwa ananitoa home mpaka job na kunirudisha kwa malipo ya mwezi kipande cha MIKOCHENI hapo...

Kipindi naanza job full kupiga kazi hasa mpaka mida ya saa mbili usiku hukoo ndio naachia ofisi...dogo wa bajaji hyo ratiba alikuwa anaijua...pia alijua mausha yangu yote kama nipo single...siku ya siku akanichoreshea kiramani flani "braza kwaninj uteseke kurudu home night wakat kuna pande flani unaweza kupozi na ukala matunda ya peponi"[emoji28].

Kwa kuanzia nikapelekwa "Massage Parlor" moja matata mnooo yani yani yani yani acheni tu.!!!

Kuingia watoto wa kila rangi afu wamesimama kama mwibaa hasaaa....(wazuri)..dogo akamuita matroni[emoji28][emoji28] "braza haya mambo ni mpya,mpe Menu atakayo shindwa kuisahau milele" ...matroni[emoji860]"yupo njema?!!"...dogo[emoji860]"weee mama wewee mie sitembeagi na wauza matunda[emoji28]"

Matroni[emoji860]"kama vipi na mie naingia mzigoni na vijana wangu kama 2 3 hv tusimamie show ya mgeni muheshimiwa mpya"

Dogo[emoji860]"fanya hivyo utakuja kunishukuru badae mchizi ana jiwe hasaa"

FUPISHA STORY:

Wanangu ee wa JF
Watoto wa hiyo parlor walichukua namba yangu wakaanza kuwa wananitafuta privately kila mmoja anataka kutumia opportunity kibinafsi.....

Dogo akanipeleka saloon hiyo wananyoa Mastaa tu full vidada vya instagram na bongo movie kibaoo hapo

Picha linaanza naingia tu kutupa jicho mwanangu Byser huyo hapoo mbele!! Sijacheki pembeni Nyandu tozy yule paleee naanza kuambaa ambaa Naona kiti cha kupumzikia ka chill Young dee paka rapper!!!

Nilivyotoka kunyoa pale naanza kupokea meseji kibao "braza mie msanii,najua kuimba nisimamie"
Mwingine "kaka mie ni model nahitaji support ya mavazi,location na cameraman wa maaana"!!

ITAENDELEA
But now Mungu kanipa second chance although najua laana zote za hapa bongo kupitia huyo "dogo wa bajaji"....
Mmh mkuu young dee miaka ya 2000, sio kahawa hii faza.[emoji3]

Sent from my itel P32 using JamiiForums mobile app
 
Mimi nimekulia familia ya kimaskini, no exposure ya biashara wala ya shambani nikazoea maisha ya kuunga unga. Nakumbk nimeajiriwa miaka 5 iliyopita tukadanganyana na wife nikope bank, awamu ya kwanza nikakopa mil 7, nikafungulia biashara mil 3. 5, 3.5 nyingne matumizi mengine, baada ya miezi 6 nikaenda kutop up aisee milioni 8.1 nikamtumia mshua mil 1, mil 1.2 nikanunua kiwanja, mil 2.3 nikanunua pikipiki hela nyingne km mil 1.5 nikaongeza kwenye biashara.

Movie la kutisha
Baada ya miezi 2 biashara ikafa, kiwanja mwaka wa 3 hakijajengwa, mshahara kidunchu yaani ni kapuku anayepumulia mpira nipo bush kila kitu hakiendi. Nimetafakari jinsi ya kuchomoka nimeshindwa, wadau naomba msaada wenu kimawazo.
 
Mimi nimekulia familia ya kimaskini, no exposure ya biashara wala ya shambani nikazoea maisha ya kuunga unga. Nakumbk nimeajiriwa miaka 5 iliyopita tukadanganyana na wife nikope bank, awamu ya kwanza nikakopa mil 7, nikafungulia biashara mil 3. 5, 3.5 nyingne matumizi mengine, baada ya miezi 6 nikaenda kutop up aisee milioni 8.1 nikamtumia mshua mil 1, mil 1.2 nikanunua kiwanja, mil 2.3 nikanunua pikipiki hela nyingne km mil 1.5 nikaongeza kwenye biashara.

Movie la kutisha
Baada ya miezi 2 biashara ikafa, kiwanja mwaka wa 3 hakijajengwa, mshahara kidunchu yaani ni kapuku anayepumulia mpira nipo bush kila kitu hakiendi. Nimetafakari jinsi ya kuchomoka nimeshindwa, wadau naomba msaada wenu kimawazo.
Kwanini biashara ilikufa?
 
Du acheni kunikumbisha, nilikuwa nafanya kazi sehemu flani wafanyakazi wenzangu wakashawish kampuni iwe inatoa mkopo Mara pa ikakubaliwa na wenzangu walichukua mkopo mkubwa na Mimi nikachukua 8ml, do kwanza sijazigusa mwezi mzima najaza mipango kwenye makaratasi, usiku naamka napanga mipango, nikapata wazo nidroo pesa zote nikae nazo Ndani.

Nikadraw, siku moja kama demu wangu kaniambia mbona siku hizi unapiga mahesabu sana na makaratasi mengi mezani, nikamwambia hamna mipango tu, Mara akajua Nina pesa, akaja home sijui alinitime VIP akaiba zote, kuna machinga nilimuambia aniletee pas original asijal gharama, siku kaja nachek bahasha sioni pesa nampigia simu Selina hapatikani, nauliza nkaambiwa ameenda Morogoro, jamaa anasema pasi elfu 40, kaiacha hapo,
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] duh!! Ivi videm
 
Duuh!

Mwanzoni mwa mwaka huu 2019 nikiwa sina muda mrefu sana kazini nilichukua mkopo wa 4,000,000/= kama staff. Mkopo huu ungekatwa kidogo kidogo kutoka kwenye mshahara wangu.

Mwanzoni nilijiaminisha sana kuwa nitafanyia biashara wazo nililokua nishaliulizia sana na kupata information za kuridhisha. Biashara hii kwa data nilizokusanya kwa wengi wanaoifanya ingenipatia angalau 15,000 - 20,000/= kila siku.

Nakumbuka nilikua nimeshamuambia jamaa mmoja ambae ameifanya biashara hiyo muda mrefu kuwa anitafutie wapi nitanunua vitetendea kazi kuna hela nitaipata hivi karibuni na akawa yupo standby. Kwakwel nilikua sitaki kupoteza muda sana kukaa na ile hela nilihofia itapotea. Plan zote nilishachora na nilikua najua kuwa vitu vikinyooka, baada ya kuulipa ule mkopo wote nitakua nishatengeneza faida kiasi gan. Kila kitu kilikuwa kimesetiwa kasoro account ya benk tu ndo ilikua haijasoma bado.

Mkopo ulipomaliza process ukawekwa kwenye account yangu. Asikuambie mtu, kuona zile sifuri sifuri tano, yani millioni na ushee kwenye balance yako ya benki kwa mara ya kwanza ni raha isiyoweza kuandikwa. Yani unajihisi tofauti. Ukiangalia balance unaona hii haiwezi kuisha nikitoa hapo 50k kununua kitu flani. Mdogo mdogo number zinaanza kushuka. Unasahau kabisa mipango yako. Nilikua naona iliyobaki mbona bado inatosha. Sina hofi natoa tu hela bila kuangalia balance

Kabla hata sijajinunulia kitu cha maana, wala kuwatumia wazazi wangu hela, nilimnunulia mpenzi wangu kitu flan cha gharama zaidi ya laki 4. Nilikua najiaminisha kuwa nampenda, na kusema kweli tabasamu lake pale ninapo mnunulia kitu huwa lilikua linanifanya nijione mimi ndo mwanaume haswa, siku hizi mwanaume pesa!

Zikaisha wiki kadhaa, hela ile ikawa imefika karbia nusu. Hapo nahitaj tena kulipa kodi, nikatoa na kodi humo humo, ikawa inazidi kupungua tu. Yule jamaa sikuwahi tena kumcheki kuhusu ile biashara na plan zote zikaota nyasi. Biashara sikuifanya wala kuiulizia tena tangia hicho kipindi. Wanaosema wakipata hela hawato filisika. Unaweza ukahisi unajijua vizuri wakati huna hela. Lakini ukiwa nazo unaweza ukawa mtu tofauti kabisa. Omba sana uwe na uwezi wa kujicontrol.

Ilifika muda sipendi hata kuangalia balance langu la ATM. Kila nikitoa pesa atm ni kama bahati nasibu, nikisiki pesa zinafanya priiiiiiiiiiiii nafurahi maana nilikua sina uhakika kama zitatoka. Kufilisika ni kubaya jamanj asikuambie mtu. Nimiezi kadhaa sasa imepita, hivi leo ile biashara ingenyooka ningekua nimeingia zaidi ya 1,500,000 lakini sasa hivi kila mwezi nakatwa zaidi ya laki 7 kama makato ya marehesho ya mikopo ambayo mengine imeongezeka kwa kua zilivyoanza kukatwa na hela tayr imeisha maisha yanakua magumu sana.

Ninavyoandika hapa, nataka nikope nipate hela ya kumalizia hii wiki nikisubiri mshahara mwengine. Maisha yamekuwa magumu mno. Najutia mengi sana, pesa yote imeyeyuka.

Nilichojifunza ni kuwa, tengeneza plan yako kabla hujapat pesa. Utakapo ipata tu! Anza muda muda huo huo kutekeleza kwanza plan zako, halaf kinachobakia tenga kidogo uienjoy. Yani usifikirie mara mbili. Ukianza tu kujifikiria ukiwa na hela, hapo hafikirii mtu yule yule ambae alikua hana, anafikiria mtu mwengine kabisa ambae ana pesa na wewe humjui huyu mtu kwahyo usimsikilize hata nusu. Fanya kwanza yenye faida.

Napia jambo jengine na la muhimu, hata kama ni mbaya vipi, angalia balance yako ya hela mara kwa mara. Unaweza jishtua mapema unatumia pesa vibaya.

M/Mungu nipe nguvu haya makosa nisiweze kurudia. Sijakata tamaa, Sasa hivi najua ukipata hela usipoiwekeza mapema kwa akili itaisha bila mpangilio. Na utaishi maisha magumu kuliko mwanzo.
Na ukipata tena hutajicontrol, if you dont know, now you know
 
Nilipewa kama zawadi na Mother, nianzishe firm yangu ya mambo ya Upimaji ardhi, nilinunua baadhi ya vifaa tu (kama 3 M) nikabaki na 26M, kilichomaliza hela ni 'kuhonga ' madem wa tegeta, mbezi beach, kawe,ubungo,nakumbuka Kuna demu nilimnunulia passo 5 M, na mambo mengine ya kuhonga honga na statrue nyingine hadi 26M ikaisha, nikauza vifaa vya survey vyote
ikaisha yote (3m).
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Japo kuwa humu zingine zina chumvi ila nimejifunza

2019 nikiwa sina lile wala hili kuna jamaa yangu akaniambia twende tukazamie migodi wapi hiyo Msumbiji basi tumefika kule tukapata kisehem tukapiga kama Zari hivi tukapata mzigo kwenda kupiga bei
Umetema kama m630 ukija kupiga pasu mtu mbili kama m300

Tokea hapo tukakataana urafiki kila mtu aliingia njia zake mana jamaa yangu akadai tukawekeze mim nikaona kuzeeshana mapema huku mi nikaenda zangu dar bila kupitia hom

Fika dar mkwanja si upo kwa bank nikakodi gest nzima nikatafuta mabamnsa kwaajili ya ulinzi tafuta pisi kali kama 10 hivi wakiwemo na mastaa wakike watatu nilikaanao pale gest kwa siku 10 na kubakiwa na laki mbili ya nauli ya kurudi hom mbeya fika hom nikala msoto wa ajabu haijawahi tokea toka nije duniani toka anga za mbali mwaka ukapita nakutana na jamaa yangu ana kampuni yake songea ya usafirishaji mizigo scania kama 23 kumbe mwenzangu aliwekeza kule kele kwenye migodi

Sio siri maumivu yalizidi kusikia hivyo nikamwomba anipe nafasi ya udereva kwenye kampuni yake mana nilikuwa nimepitia huko kabla
Kwakuwa tulikuwa kama ndugu

Akaniambia hapana siwezi kukupa nafasi tena asee kusikia hvy maumivu yalizidi nikajiona sifai nimetengwa na dunia baada ya hisia kunishinda nikatafuta sumu ya panya nikaenda mbali kdg na hom nikanywa
Imepita dakika mbili mwili ukaanza kunyong'onyea macho yanaanza poteza nuru machozi yakinilenga nikikumbuka yote niliyoyafanya ,
Nikasema Mungu naomba unisamehe kwa yote niliyokufanyia ambayo hayakukupendeza

Punde si punde nikiwa kwenye hali hiyo akatokea jamaa yupo na kipkpk akawa anasikia kama kilio hivi cha kugurumia sikujua kilichoendelea ila nilijikuta hospitali nimewekewa ma dripu tazama pembeni jamaa yangu yule wa migodi nimekaa hospitali siku sita

Nilivyokuwa fresh jamaa akaniambia sasa nazani umepata funzo kwenye maisha yako akaacha hom m2 kwaajili ya matumizi akanichukua tukaenda migodi akanipa eneo na kuniambia pambana

Nikatafuta nyoka yaani wafanyakazi lugha za migodi hizo, tukapiga kazi Mungu si asumani nikapata jiwe la pesa ndefu nakumbuka waliungana kama wanunuzi wa madini watatu kuuchukua ule mzigo nikawapa wale nyoka m200 kila mmoja, walikuwa nne nikaenda kwa jamaa akanipa somo jinsi ya kukaa na hela isipukutike hovyo bila kukusudia nakumbuka pesa yote aliniachia ninapo sema pesa ni pesa kweli

Akaniagizia kama Volvo za mizigo 14 hivi za kichina akawa anazisimamia yeye si unajua watu wa nchi hiyi wakijua unapesa ukikoswa na majambazi basi yatakukuta yale ya jamaa wa mtwara na polisi alijinyonga kwa taulo nchi hiyi ni mwiko kuwa na pesa za ghafla basi nikajenga ka nyumba kakisasa kwajili ya wazazi, fungua pub ya nguvu mbinga na dar anzisha kiwanda kidogo cha unga songea hayo yote nimefanya kwa mgongo wa jamaa sikutaka nijulikane kama nina pesa alafu nikamwambia nipe kazi kwenye hiyo kampuni yako nikawa kama dereva mtiifu baada ya wiki tunakutana kwa siri kujadili hali ya uchumi wetu na mpaka sasa hakuna anayejua mm nina shera kwenye kampuni ya jamaa zaidi ya family yangu maisha yangu ya kawaida sana na hata kwenda kwa miguu kazini kawaida kukaa kijiweni kucheza bao draft kawaida yote haya nimejifunza niliyopitia jamaa wanajua mm ni mwajiriwa wa rafiki yake na kuongea ooh alipata hela kachezea mpaka akanywa sumu ila hawajui kinachoendelea sina cha kupoteza ila nimejifunza sio hayo tu kuna mengi ndani yake ambayo ukifuatilia nyuz zangu utawapata japo nilididimia hapa katikati ila nimekaa sawa

Nb kufilisika sio mwisho changa upya karata zako yote yanawezekana mwanaume pambana kisawasawa acha kulia lia sijui ndio basi kazaaaa kubali kufa ukipambana acha kuwaza waza pambana mpaka uache alama kwenye dunia ameen

Na huu ndio ukumbusho wa picha kati ya pesa ambazo tulikuwa tukigawana hukoo machimbo enzi hizoo nikiwa kwa digar na jamaa zangu[emoji116][emoji116]2020View attachment 2098320
Kuna vitu haviko sawa
Alipata mil300 2019, adi unakutana nae tena alikuwa na scania 23, apo ni kama mwaka nyuma ina maana 2020 hivi au 21 mwanzon, yani baada ya mwaka moja akawa na scania 23, kuna uongo apa, maana kichwa kimoja cha scania ni mil70 mpaka 300 kutegemea na aina na upya na scania na treller ni kama milion100, sasa huo uongo sijui unautetea vipi

Umu kuna uongo mwing unanukia
 
Tatizo akili inarudi pale receipt inaposoma salio lako ni laki mbili [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] ndio unajiuliza hii niiiinunuliee halafu jibu linakujia pale pale haitoshi baada ya siku mbili unaenda toa laki na nusu halafu hukanyagi tena bank na ukipita karibu ni upande wa pili wa Barabara [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom