Mkuu walikuwekea 8m cash kwenye account yako?Mimi nilikopa milioni 8 ada na meals. Nikanunua kiwanja 3m. Nyingine matumizi kidogo na ada. Kile kiwanja nilichonunua miaka 12 nyuma leo thamani yake ni 50m.
HESLB nawalipa kila mwezi hela yao 30,000.
Asante sirikali.
Swali zuri sana hili.Mkuu walikuwekea 8m cash kwenye account yako?
nakopa zngu kwa ndugu jamaa na marafiki..Ilikuwa mwaka 2011 mwezi wa 7 mara yangu ya kwanza kuchukua mkopo benki, Tsh 3m. Ule mkopo niliufanyia biashara vizuri na nikarejesha bila changamoto kubwa ndani ya miezi 6. Wale maafisa mikopo wakafurahia na kunishauri nichukue mwingine wa Tsh 5m. Nikafikiria na baada ya mwezi nikachukua mkopo mwingine. Ikawa kama bahati wakati nachukua mkopo nikawa nimepata tenda ya kushona uniform za shule flani.
Nikaona hili ni dili zuri na kwa bahati wateja wangu wakanilipa pesa za advance zaidi ya 90%. Kilichofuata nikaamua nitafute mafundi wazuri Nairobi wanishonee uniform zote. HAPA NDO BALAA LILIPOANZA. Niliingia choo cha kike. Mkenya niliyempa kazi kumbe ni mshenzi mno... kadhulumu watu wengi sana. Ni kweli ofisi anayo na mafundi anao ila kwa bahati mbaya huwa hatimizi makubaliano. Ujinga mwingine niliofanya ni kumlipa karibu hela zake zote.
Hadi shule zinafunguliwa Januari sikuwa nimepeleka nguo yoyote kwa mteja. Basi presha ikaanza kutoka kwa mteja wangu ambaye pia alikuwa anawashiwa moto na wanafunzi + wazazi. Baada ya kusumbuana na mzabuni wangu nikaona isiwe ishu nichukue hela za kwenye biashara yangu niliyoombea mkopo wa 5m ili kupambana na tatizo ambalo lilikuwa limefikia pabaya.
Kwa maana nitafute fundi mwingine nitengenezee kwake huku nikiendelea kupambana na huyu wa mwanzo. Changamoto iliyojitokeza tena ikawa kwa muda ule wauza uniform wengine wana kazi zingine nyingi na bei zao zimeshaenda juu. Gharama za nauli nenda rudi Ars - Nrb nazo zikawa zinanipiga kama ngoma.
Hadi kuja kufanikiwa kupeleka nguo angalau kwa 70% tayari kiuchumi nilishayumba hivyo marejesho yakawa yanasuasua. Ninachokumbuka ule mkopo niliotakiwa niwe nimemaliza kulipa kabla hata ya August nilimaliza December kwa mafaini kibao huku nikiwa nimefilisika. Wale maafisa mikopo walijua kuniwashia moto.
Pamoja na yote hayo nilijipanga upya na baada ya miaka kama mitatu nilirudi tena benki na kuchukua mkopo. Ninamshukuru Mungu kwamba ninakopesheka na ninaendelea kuchukua mkopo. Somo kubwa ni kwamba usichukue mkopo kuanzisha biashara.
NimechekaMithali 22:7
"Tajiri humtawala maskini, Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye".
Nikasema nisome biblia inifariji ndo nikakutana na huo mstari. πππππ
Una marafiki wazuri.Kifupi nikopa NMB 10ml nialipa marjesho kama 6 biashara ikaanza kuyumba.aisee nilihangaika huku na huko nyumba isiuzwe bila mafanikio.mwisho niliongea na marafiki zangu wanimlizie deni then mambo yakiwa mazuri niwarejeshee wao badala ya benk,hivyo nilipigwa tough kama 4ml nikaokoa nyumba yangu..sasa deni limehamia kwa washkaji ndo mziki upo hapo.Mungu nisaidie
Tatizo nyie watu hamtaki kutoa connection na mie niingize vijisenti mbili tatumzabzab anataka awe mkopeshaji wa hiyo mikopo ya chupi mkononi ππππππ
Vipi unataka mkopo mie riba yangu 20% unalipa mwisho wa mweziDuh bora ingekuwa unalipa zote kwa mwezi
Ndio inapanswa mtu uwe na marafiki wa namna hiyoUna marafiki wazuri.
Hahaaa.. Wanasema gari yako dhamana yako.. watu wanatembezwa kwa miguu sanaDah! Nakumbuka mwaka flani niliwahi kuchukua mkopo kwa hawa jamaa ambao Bond unaweka gari.. aisee sitakaa nisahau, Jamaa wanajua kudai na marejesho yao ni tofauti na makubaliano ya Awali. Ukishindwa kurudisha ndani ya mwezi tu wanakuja kuchukua gari lako ambalo wanakuwa wameshabadilisha Jina.
Aisee hata uwe na shida kiasi gani ndugu yangu usikae ukaenda kwa wale jamaa wa Mkopo kwa dhamana ya Gari
Vile umechukua zako jiko la mkaa..ghafla yanakuja majiko ya gesi..Ilifana [emoji23][emoji23][emoji23]
Hapana mzabVipi unataka mkopo mie riba yangu 20% unalipa mwisho wa mwezi
π€£π€£π€£π€£On the otherside of the story: Kwa wakopeshaji, Kuna shost anaishi huko uswahilini kazi yake kukopesha wamama. Sasa kuna muda anaumwa sana ukimuuliza anasema wakopaji wanamloga asahau madeni π π π π π
Akaanza kwenda kwa mganga na yeye kujiweka fit, Mwisho ameolewa na mganga siku hizi na biashara yake ya kukopesha anaendelea nayo.
Mkopo unalipiwaga bima,ata ukiacha haina madharaVip unataka uache kaz ukimbie na mkopo? [emoji3]
Me nahisi huu mkopo bi mkubwa wangu atakuwa kakopa si bure mana anaomba ela balaa sio kawaida yaan mfn mwezi uliopita kaniomba ela ya bill ya dawasco mara 3hii mikopo kausha damu balaa sana mam yangu alichukua pesa kidogotu kama laki tatu hivi kila siku analipa 5 elfu amekauka apa na mkopo hauishi anafanya kulipa faini tu mkopo upo pale pale Ni huzuni kwa kweli nimeuza mpaka kitanda kumsaidia
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]mazaa alikua akichukua mikopo kwa wale SEDA.. asee mambo yakaenda kombo akawa anawatoroka maana anajua siku zao za doria..
Wakaja kwa kushtukiza kwetu ni badland kule gari unaacha road upite chocho kadhaa ndo ufike..
Braza alikua anajua ile gari ya alivyoiona chap mbiombio akaja kumshtua maza, chap akazama uvunguni..
Wakafika cha kwanza..mama yuko wapi ? Braza kwaambia amesafiri kuna msiba kijjini alikua anajibu kwa wasiwasi..
Mmoja wao akanichukua nlikua ndo niko Darasa la kwanza haoo hadi dukani...Mangi mpe mtoto mzuri biskuti ilikia zile za choclate 500/=nakumbuka..
Woii nikachoma maza yupo uvunguni kule.. [emoji23][emoji23][emoji23] wakaenda kumchomoa, hela hamna wakasomba mazaga hapo sebleni
Ile kipigo nlipata walivyoondoka biskuti ilitokea puani...
Ubaya wanakopa kwa kausha damu si chini ya wawili mtiti ndio huazia hapo.Me nahisi huu mkopo bi mkubwa wangu atakuwa kakopa si bure mana anaomba ela balaa sio kawaida yaan mfn mwezi uliopita kaniomba ela ya bill ya dawasco mara 3
Nikampa tu ila nikahisi kitu
Hii mikopo inawaathili sana wakinamama
Ha ha yan faida unajipangia mwenyewe [emoji3][emoji3]Kuanzia mwaka huu nimeamua kuchukua mkopo wa biashara badala ya kazini. Hapa nina kipengele cha 10m Nmb nimeshafanya marejesho mawili.
Kilichonivutia ni riba yaani nimeona kwenye mkopo wa biashara 10m nalipa 11,300,000/= kwa mwaka. Kwa mwezi 946,000/=. Wakati mkopo wa kazi muda mrefu na riba inakuwa kubwa.
Ninachofanya kazini nimeweka backup kama nitafeli huku basi nitazama kwa mkopo wa kazi kurefund. Lakini piashara ninayofanya ni ya fedha kwa hiyo fedha zote ninazo cash ninachowarudishia ni faida tu. Kinachonipa matumaini ni kuwa kwa vile cash zao zote zipo kama nitaona nafeli nazirudisha, sokomoko itakuwa kama zitaibwa au changamoto zingine unexpected.
Nashukuru Mungu 10m zao zinanipa at least 2.3m monthly profit nawapa rejesho na kuongeza mtaji. Kwa hiyo bado sina neno baya juu ya mkopo cha msingi nipo highly disciplined and very cautious, hata wife ananikubali katika heshima juu ya that why hajasita kuweka saini za mkopo na kuacha hati ya banda letu. Niombeeni nitoboe mwakani nivute 20m[emoji1787][emoji1787]
Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app