Tuliowahi kuwa na chawa tukutane hapa

Hahahaaa, ila huo utaratibu ulikuwa mzuri sana. Vipi lakini, na wewe walikukoa mkuu?

Members only, kama huna chawa ilikuwa hauhusiki kwenye huo mchezo.

Sema mama alikuwa anatunyoa sana kwa mikasi, halafu mimi nilikuwa napenda kufuga rasta kama Alpha Blond, kwa hiyo mama akawa ananiambia nikiona chawa tu nakunyoa.
 
Ha ha ha boarding tulikuwa tunaita Balloon, ile aina ya gari na ubaya wa hawa jamaa huwa wanavizia umetulia mbele za watu halafu ndo wanajitokeza
 
Khooooo kichefuchefu [emoji125]‍♀️[emoji125]‍♀️[emoji125]‍♀️[emoji125]‍♀️
 
Duh unanikumbusha tosa boys hiyo
 
Nimesikia baridi sana,nakumbuka wahindi niliosomanao dah aisee.
Waliniambia pia wako chawa wa mavuzi,nilipokuwa Delhi.
 
Hap wadudu walinitafuna sana nikiwa Kigonsera Sec. Nashukuru Mungu sasa ninakaz na inanisaidia kujiweka nadhifu
 
Ila kinachonishangaza ni kuwa hawa jamaa ukiwa mchafu tu wanakuibukia! Hivi huwa wanatoka wapi?
 
Nimesikia baridi sana,nakumbuka wahindi niliosomanao dah aisee.
Waliniambia pia wako chawa wa mavuzi,nilipokuwa Delhi.
Nasikia wapo wanaoitwa "maku" chawa! Sijui wakoje?
 
kunguni ni noma yule msela anajua kula na kipofu ....akiona unafurukuta tu anatuliza ball yaani anakuwa ameshajua kuwa amekupa vitu hivyo anasubiria tena upate usingizi ili aendeleze mechi
 
kunguni ni noma yule msela anajua kula na kipofu ....akiona unafurukuta tu anatuliza ball yaani anakuwa ameshajua kuwa amekupa vitu hivyo anasubiria tena upate usingizi ili aendeleze mechi
[emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
sio chawa za ukubwani chawa za utotoni, haikumaanisha uchafu la hasha ilikuwa ni hali ya kawaida iliyowatokea watoto wengi tulio ishi vijijini. na je Kunguni kitandani na mvua ikinyesha nyumba ina vuja visehem sehem sasa ikivuja kitandani ndio mnahama kabisa na je kulalia godoro la sufi kwenye kitanda kilicho sukwa cha miti au ulienda kwa babu yako akakuachia kitanda mjukuu yeye akatandika majani chini ili ninyi mlale. wote wa mjini hawana experience hii umeme ukikatika wanalalamika ni kweli walizaliwa nao na wakakua nao sisi huwa hatuhangaiki wakikata tunaona kawaida kwanza ndio tunaona matumizi yanapungua sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…