Tuma salamu kwa Mdau mmoja kwenye huu uzi kuadhimisha siku ya Radio duniani

Tuma salamu kwa Mdau mmoja kwenye huu uzi kuadhimisha siku ya Radio duniani

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Kila mwaka Februari 13 ni maadhimisho ya Siku ya Redio Duniani. Siku hii huadhimisha umuhimu wa redio katika kuhabarisha jamii, kukuza uhuru wa kujieleza, na kuwa msaada muhimu wakati wa majanga na matatizo.

Lengo la Siku ya Redio Duniani ni kuhamasisha watu kuhusu umuhimu wa redio. Ingawa leo hii dunia inatawaliwa na televisheni na simu za mkononi, redio bado ni moja ya vyombo vya mawasiliano vinavyoheshimika, rafiki wa kusafiri, na jukwaa la sauti za jamii kupitia redio za kijamii.

Pia redio bado ni chanzo cha taarifa kinachoheshimiwa na ina mchango mkubwa wakati wa dharura. Inachukua jukumu muhimu katika kukabiliana na masuala ya kimataifa kama mabadiliko ya tabia nchi na inatoa jukwaa kwa mitazamo isiyosikika mara nyingi.

Mada ya Siku ya Redio Duniani 2025 ni "Redio na Mabadiliko ya Tabia Nchi." Lengo la dhima hii ni kuhamsisha watangazaji katika vituo vya redio katika uandishi wao wa habari kuhusu suala hili muhimu ambalo limekuwa janga kubwa duniani
 
Back
Top Bottom