Tumalize utata: Chama Vs Moloko

Tumalize utata: Chama Vs Moloko

Ukitaka kujua uwezo wa Chama kawaulize Nkana AS Vita, Horoya na Vipers, pia kawailize mabeki wao na kipa wao kitu gani aliwafanyia, pia uje uulize makipa na mabeki wa ligi kuu ni jinsi gani mwamba huwa anawatambaliza kama walevi wa chibuku.
 
Habari wanajukwaa,

Leo naona tumalize utata wa nani zaidi kati ya viungo hawa wawili. Wote ni viungo wazuri, ila mmoja ana uwezo zaidi anapokuwa kulia na mwingine anapokuwa upande wa kushoto.

Kitakwimu za ufungaji wa magoli tofauti si kubwa sana katika idadi ya magoli. Ukija katika uwezo wa kumiliki mipira na kudrive Moloko ana uwezo binafsi wa kuwapita mabeki na si kutegemea kuwekewa mipira ya kupenya kama ilivyo kwa mwenzake.

Je, unawazungumziaje wachezaji hawa?
Sijui kuna uhusiano gani kati ya kutokuwa na akili na mashabiki wa Yanga? Sijui kwakweli
 
Hivi wanaosema Sema Chama anakuwa mbaya team ikizidiwa, na mzuri team ikiwa inamiliki mpira, wanawaza nini ? Hivi nichezaji gani anakuwaga bora team ikiwa imezidiwa? Juzi tu Argentina ilifungwa na na Saudia na Messi akiwa ndani.

Tunachoangalia ni overall performance ya mchezaji katika team. Chama ameamua mechi nyingi sana muhimu kwa Simba ukianza ya Nkana, Al alhy, AS Vita na ya juzi ya Horoya. Amekuwa bora siku zote, killer pass nyingi sana, statistics zake za ndani ya ligi yetu na nje kwa maana ya mashindano ya caf yanambeba Chama, So far ndy top scorer kwa hii Champions league. Tatizo mnapenda kujadili mambo kwa ushabiki kuliko uhalisia, na mnajadili bila ya kuwa na takwimu.
Usiingie kwwnye mtego wa mtoa mada, huyo anataka ubishani usiokuwa na maana. Unamshindanishaje Chama na Moloko? Yaani ni sawa na usema Nyerere na Mwigulu nani zaidi?
 
Mwamba huyu hapa tena
5c3f8fe84d794a9c869adbf447b4ae83_336578062_129856996548603_7353580363190724626_n.jpg
IMG_20230321_200558.jpg
 
Back
Top Bottom