Tumbushane sheria ambazo unahisi watungaji wenyewe wanazivunja

dvj nasmiletz

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2018
Posts
2,079
Reaction score
2,254
Kiukweli kuna sheria /taratibu zingine kuzifuata ni mtihani sana..yaani inakubidi tu uivunje ili vingine viendelee...

Kuna siku nipo class form 1..shule yetu kuanzia getini yamejaa mabango tu SPEAK ENGLISH ONLY
Sasa haja imenibana hatari nimevumilia karibu dk 20 nikashindwa na ticha hatoki class..kiingeleza cha kuombea ruhusa sijui..nikasimama mpaka kwa ticha

"ticha naomba ruhusa kwenda kujisaidia!?"

Ticha anakomaa tu ENGLISH PLIIZ

bembeleza,bembeleza aaah wap Ticha anazuga anielew eti ENGLISH PLEASE

Nikaona ujinga wakati huo haja ishaanza msafara taraatibu...

Nikarudia mara ya mwisho "TEACHER nisaidie nimebanwa!!

akasema tena "HEY ENGLISH PLEEASE!!

Sasa ile anamalizia pleasee mi tayari nipo chooni ndo namalizia kulock mlango..

Baada ya kujisaidia nikatulia humo km dk 5 hivi nawazia adhabu ya kuchimba visiki 12 peke yangu..

Dah..nikarudi darasani nina hofu kibao.ile naingia nakuta darasa zima wanavunja mbavu balaa..hadi teacher mwenyewe anakufa kucheka hatari...afu akasema "nyambafu ungekunya hapahapa!!"

Nikamjibu "Please english and you"!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…