Uchaguzi 2020 Tume imekataza Viongozi wa Dini kuwa waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2020. Chaguzi zote tangu 1995 viongozi wa Dini walishirikishwa

na mimi nashangaa....
 
..kwasababu hawana vyama/upande bila shaka watakuwa waangalizi wa uchaguzi wanaoaminika zaidi.
Hawatakiwi kabisa wengine wameharibiwa na uvyama akina Bagonza Wana upamde wa Chadema wakina Gwajima wanavaa Hadi nguo za CCM na kadi za vyama mifukoni

Angalia akina Askofu Bandekile au akina shehe katimba au Ponda hawajifichi misimamo Yao ya kivyama

Kuna Hadi padri Kanisa Katoliki anagombea ubunge kupitia CCM kuchukua Fomu hiyo.ni chaos wameanza kuwa na pande hivyo hawako neutral Tena!

Serikali inawarudisha kwenye msitari inawarudisha kwenye msitari sababu wao wenyewe wameshindwa kujiweka kwenye msitari

Serikali imefanya la maana wabakie tu kwenye shughuli zao za kidini tu
 

..mbona Tume imeng'ang'ani kuweka MAKADA WA CCM kuwa wasimamizi wa Uchaguzi?
 
Ni vizuri watu tuwe na uelewa wa Sheria ya Uchaguzi na nani mwenye haki kisheria kuwa mwangalizi (observer) kwenye uchaguzi wetu as opposed to msimamizi (administrator) wa uchaguzi. Sasa sema NEC na Sheria zinazungumzia nini - wasimamizi au waangalizi?
 

..Nazungumzia waangalizi / observers.

..kwa mara ya kwanza tangu tuingie ktk mfumo wa vyama vingi viongozi wa dini hawataruhusiwa kuwa waangalizi wa uchaguzi.
 
Kazi ya viongozi wa dini Sio kusimamia chaguzi za serikali Wala vyama
sawa ccm imeona aibu kufanya madhambi yao mbele ya watumishi wa Mungu,hawana hiyana.kama uchaguzi ni wa huru na haki c ndo hao watumishi watakuja kusema
 
..Nazungumzia waangalizi / observers.

..kwa mara ya kwanza tangu tuingie ktk mfumo wa vyama vingi viongozi wa dini hawataruhusiwa kuwa waangalizi wa uchaguzi.
Kwa uzoefu wangu wa kuwa mwangalizi wa uchaguzi kuanzia ule wa 2000 hadi uke wa 2015, sijawahi kuona viongozi wa dini kama vile wachungaji, maaskofu, mashehe au hata maimamu wakiwa waangalizi wa uchaguzi au hata taasisi zao za dini, sijawahi kuziona. Sana sana watu binafsi kutoka hizo taasisi ndio huwa wanashirikishwa kama wataalam au wasomi kutoka hizo taasisi na hivyo kuwa kama observer kwenye hizi chaguzi. Ngoja tuone hili lina maana gani mwaka huu wa 2020.
 

..hii taarifa nimeisikia toka kwa Katibu wa TEC.

..ningeweza kuleta video clip kama ushahidi lakini sikuwa na muda.

..tusubiri tuone nini kitatokea, lakini mimi nilidhani kuwa na observers wengi zaidi, wa kutoka taasisi mbalimbali, kungeongeza credibility ya chaguzi zetu.
 
Nchi ambayo ni secular haitakiwi kuingiza dini kwenye siasa.
 
Sawa JokaKuu ngoja tusikilizie ingawa mimi najua zoezi hili ni very expensive na linahitaji credible and competent operators ndio maana hata hao waangalizi kutoka EU au UN huwa wachache na huwa wanatumia operators wa humu humu ndani.
 
Alafu leo kuna dhehebu la walamba viatu fulani limetoa Eti tuzo kwa magufuli. Hii nchi ina machizi na wapuuzi wengi sana kwa kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…