Tume ya Haki Jinai: Rais asipoidhinisha Adhabu ya Kifo baada ya Miaka 3, Mfungwa apewe Kifungo cha Maisha

Tume ya Haki Jinai: Rais asipoidhinisha Adhabu ya Kifo baada ya Miaka 3, Mfungwa apewe Kifungo cha Maisha

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu Othman Chande amependekeza kuwa endapo itapita miaka 3 bila Rais kutoa Idhini katika Adhabu ya Kifo, Wafungwa wenye Hukumu hiyo waweze kubadilishiwa adhabu kuwa Kifungo cha Maisha.

Hata hivyo, Tume imesema kuna malalamiko kuhusu Adhabu ya Kifungo cha Maisha kuwa hakitoi nafasi ya Mfungwa kujirekebisha. Hivyo kuna mapendekezo kuwa Kifungo cha Maisha kipewa muda maalumu.

Kuhusu adhabu Kifo amesema Tume imebaini kuna maoni ya Kufutwa adhabu hiyo kwasababu ni ya kikatili na isiyozingatia Haki za Binadamu pamoja, kutotekelezeka kwa muda wa miaka 28 na kuwatia hofu Wafungwa.
 
In my opinion Kifo sio adhabu ni inevitablity na wote tutakufa...; Kwahio hawa watu waliokosa kwa manufaa ya jamii iliyobaki wafungwe maisha yao yote na kupewa suluba ya kazi ngumu na wanachozalisha kije kufidia jamii as a whole ya sisi waliotukosea kitaa...

Yaani kama kuna kazi hatarishi za maisha hawa ndio waende huko; au kuna sayansi tunahitaji specimen na hatuna uhakika kama itafanya kazi hawa ndio wawe guinea pigs (Its the price they have to pay kwa kosa walioitendea jamii) Huku kujidanganya kwamba nimemkomoa mtu kwa kumuua ni kama wewe unamcheka mzee eti amezeeka wakati eventually na wewe ndipo unapoelekea
 
Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu Othman Chande amependekeza kuwa endapo itapita miaka 3 bila Rais kutoa Idhini katika Adhabu ya Kifo, Wafungwa wenye Hukumu hiyo waweze kubadilishiwa adhabu kuwa Kifungo cha Maisha.

Hata hivyo, Tume imesema kuna malalamiko kuhusu Adhabu ya Kifungo cha Maisha kuwa hakitoi nafasi ya Mfungwa kujirekebisha. Hivyo kuna mapendekezo kuwa Kifungo cha Maisha kipewa muda maalumu.

Kuhusu adhabu Kifo amesema Tume imebaini kuna maoni ya Kufutwa adhabu hiyo kwasababu ni ya kikatili na isiyozingatia Haki za Binadamu pamoja, kutotekelezeka kwa muda wa miaka 28 na kuwatia hofu Wafungwa.
Asipoidhiniaha si atakuwa amevunja katiba aliyoapa kuielinda
 
Inabidi swala la kunyonga liondolewe kwa Rais, liachwe kwa Majaji wa Mahakama kuu maana kama wanatoa hizo adhabu basi wao ndo watekeleze
 
Futa hii death sentence ,haileti tija yeyote, hii adhabu imejionyesha haipunguzi watu kuua, a long sentence in jail ndio njia sahihi, hapa nchini tuna 30 yrs in jail kwa rapists, lakini bado kuna matukio mengi ya rape, hii adhabu haipunguzi matukio haya kutokea hapa nchini, we need to go to drawing board, peleka jela bila kupewa parolee
 
Wauwaji waachie huru tuje kuwashughulikia uraiani
Jitu limeuwa tena kwa kuskusudia lijambazi au limeuwa kisa lipate mirathi au mapenzi halafu mnalihukumu kifo ambacho hakipo

Leta huku tumalizane kijeshi
 
Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu Othman Chande amependekeza kuwa endapo itapita miaka 3 bila Rais kutoa Idhini katika Adhabu ya Kifo, Wafungwa wenye Hukumu hiyo waweze kubadilishiwa adhabu kuwa Kifungo cha Maisha.

Hata hivyo, Tume imesema kuna malalamiko kuhusu Adhabu ya Kifungo cha Maisha kuwa hakitoi nafasi ya Mfungwa kujirekebisha. Hivyo kuna mapendekezo kuwa Kifungo cha Maisha kipewa muda maalumu.

Kuhusu adhabu Kifo amesema Tume imebaini kuna maoni ya Kufutwa adhabu hiyo kwasababu ni ya kikatili na isiyozingatia Haki za Binadamu pamoja, kutotekelezeka kwa muda wa miaka 28 na kuwatia hofu Wafungwa.
Kamwe siungi mkono kabisa kuondolewa kwa adhabu ya kifo hapa Tanzania na hata katika nchi zingine zote kabisa, hususani nchi za Afrika. Sikubaliani kabisa na Hoja hii ya kufuta adhabu ya kifo.
Wapo baadhi ya Wahalifu wanastahili kupewa adhabu ya kifo, na pia wanastahili kunyongwa hadi kufa.
Matahalani, kwa hapa Tanzania kuna Askari Polisi wengi Sana wamekuwa wakifanya vitendo vya uhalifu wa kupora Mali za raia na kisha raia hao wamekuwa wakiuawa makusudi ili kupoteza Ushahidi, watu wengi pia wamekuwa wakiuawa kwa makusudi wakiwa mikononi mwa Askari Polisi au wakiwa kwenye Vituo vya Polisi, na Wauaji wamekuwa hawachukuliwi hatua zozote zile Kali za kuwapa fundisho juu ya uhalifu wao huo. Askari Polisi wamekuwa wakihusika katika uhalifu kama huo kwa kuwa Wana uhakika kuwa na wao hawatauwa badala yake wanahamisika zaidi na zaidi kuendelea kuua watuhumiwa. Mimi binafsi naamini kwa dhati kabisa kwamba Endapo kama Rais wa nchi hii angesaini Hati ya Kifo dhidi ya OCD Christopher Bageni, yule Askari Polisi aliyewaua kikatili wale Wafflanyabiashara wa madini kutoka huko Mahenge Morogoro, Basi Polisi wangeogopa kufanya matukio mengine ya uporaji na mauaji dhidi ya Wananchi.

Aidha, Endapo kama OCD Christopher Bageni angenyongwa hadi kufa Basi lile tukio la mauaji la Bw. Hamza Mohamed pale Selander Bridge Dsm kamwe lisingeweza kutokea, na hata yule Mfanyabiashara kijana wa madini kule Mtwara pia asingeweza kuuawa na wale Askari Polisi walioongozwa na OC-CID Kalanje.

Mwisho:
Namshauri Rais SSH akubali kusaini Hati ya Kifo ili aliyekuwa OCD Christopher Bageni aweze kunyongwa hadi kufa, kwa sababu Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani tayari zimeshatoa idhini na baraka zote kabisa kwamba mtu huyo anastahili kunyongwa hadi kufa. Huku mitaani kuna chuki kubwa sana dhidi ya hao Watu.
Endapo kama Rais anaona labda pengine kutokana na Imani yake ya kidini hawezi kusaini Hati za Kifo ili Watu hao wanyongwe, Basi namshauri AKASIMISHE MADARAKA hayo kwa Watu wengine walio chini yake ili waweze kutekeleza jukumu hilo kwa niaba yake.

Inakera Sana kwa kweli kuendelea kuwaona Watu wauaji ambao waliua wenzao kwa makusudi Halafu wao bado wanaachwa waendelee kufaidi maisha, Kamwe jambo hili halikubaliki hata kidogo.
 
Back
Top Bottom