Uchaguzi 2020 Tume ya Taifa ya Uchaguzi yawataja wabunge 18 waliopita bila kupingwa. Wamo Nape, Kigwangala, January, Kabudi, Mnyeti...

Kama vyama vya upinzani kesho havitatoa tamko nitawaona hamna kitu. Hii tume ya kiboya kweli siku watu wakichoka wataenda barabarani wao..
.
Semeni kitu basi kesho. nimeandaa begi na mikate ya kutosha na maji ya kutosha tutalala barabarani. Kuna watu hii nchi kama yao vile
 
Sasa lile povu lilikua linawatoka tume juzi lilikua la nini? Hatuna tume ya uchaguzi nchi hii bali tume ya uchafuzi ya chama tawala ccm!
 
Lowassa pamoja na uzito wake wa kushindwa kujieleza jukwaani aliweza kupata kura nyingi kumzidi Magufuli.

Baada ya tume kupindua matokeo ndipo jamaa yenu akatangazwa mshindi,mwaka huu mnalo.
Yaani unafananisha kupendwa kwa Lowassa na Upunzani wa mwaka huu.

Kati ya wanasiasa waliowahi kuwa na mvuto kwa watanzania basi ni Lowassa , Nyerere na JK.

Hata wasiposema neno wakajisimamia tu. Sema Mwalimu aka wa outsmart wote alikuwa mwanafalsafa na mwalimu haswa.
 
Mbona wanadai wabunge 50 sijui wa chadema na act 47 wamekatwa alafu orodha ina majina 18 tu. Kwahiyo kuna majimbo yatakosa wawakilishi au Mimi ndio kichwa changu kizito
 
Unasubiri kuambiwa?
[emoji881] [emoji881] Hauko serious
 
Tanzania is the union between Tanganyika and Zimbabwe and the union was in the year 11961... nakumbuka miaka hio cjui ilikuwa.south afrika?
 
Dah hii ni hatar sana,inamaana wagombea wa ccm wajua zaid kujaza fomu ya uchaguzi kuliko vyama vingine? Hii hujuma hata mpumbavu anajua tu kuwa kunamchezo umechezwa
 
Sie chadema hatuta andamana, lakin cha moto mtakiona ccm.
 
Morogoro kunani?! Majimbo matano ni mengi sana kuachiwa kirahisi hivi.
Wengine wameuza mkuu wapinzani ni kituko sana wanateuluwa halafu wanaachwa yatima kwa hiyo akitokea mtu wa kumpa japo 5m si bora a uchukue alale mbele
 
Mkoa karibia mzima wa morogoro Kuna kupita bila kupingwa. Mkoa huu wenyeji wake wanatakiwa kufanyiwa utafiti wa uwezo wao wa kufikiri,elimu zao, maendeleo Yao,uchumi wao na namna wanavyoowana na ikiwezekana dini zao.kuna tatizo morogoro
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…