Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi ya uenguaji, somo la Jaffo haliwafai?

Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi ya uenguaji, somo la Jaffo haliwafai?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana heshima kwenu na moja kwa moja kwenye mada.

Ni kweli kuwa hatukuwahi kuwa na sakata la kuengua enguana kwenye chaguzi chaguzi hizi tokea tupate uhuru. Pia, ni kweli kuwa engua enguaji ya kwanza ilishuhudiwa kwa mara ya kwanza kwenye chaguzi za tawala za serikali za mitaa zinazoendeshwa chini ya tamisemi. Hizi ilikuwa ni katika chaguzi hizo ndani ya awamu ya 5.

Kwenye hali ya kufanana kama iliyopo sasa, wagombea uchaguzi wa upinzani kwa mamia na maelfu walienguliwa hali hakukuwa na mgombea hata mmoja aliyeenguliwa kutoka chama tawala yaani chama baba lao.

Kimsingi ilikuwa mithili ya kuilazimisha timu moja kuweka mpira kwapani kabla ya muda kwisha. Ndicho kilichotokea, hatimaye upinzani kuamua kuweka mpira kwapani!

Kwa hakika uchaguzi ule uliipaka sana nchi yetu hii pendwa matope machoni mwa jumuiya ya kimataifa. Katika angalau kuokoa jahazi, waziri wetu makini, mtalaamu wetu mahiri wa kupiga nyungu, alitangaza kuondolewa kwa pingamizi zote na bila masharti yoyote ili kuwarejesha wagombea wote kwenye sanduku. Hii ikiwa ni kwa ajili ya kulinda mustakabala mwema wa nchi yetu.

Kongole kwako Selemani Jaffo japo hatua yako ilikuja kwa kuchelewa mno.

Halipo somo kwa tume ya uchaguzi kuhusiana na hili ikizingatiwa kuwa labda yawezekana hatutaki kuona kuwa tupo njia panda?

Kwa nini kujiweka katika hatari tusiyoijua au kujitumbukiza bure kwenye tafrani ambayo mwenye kutaka kutwambia hatima yake kwa hakika atakuwa ni mwongo wa wazi?

Walisema waungwana "usipoziba ufa, utajenga ukuta."

Chonde chonde tungali nayo nafasi ya kurekebisha mambo vilivyo kabla ya kuchelewa mno.

Nafasi ya kuuziba ufa ingalipo japo haitadumu sana.

Waungwana wanasisitiza: "chelewa chelewa utakuta mwana si wako."

Ninawasilisha.
 
Jaffo aliikana kauli yake kesho yake baada ya kufokewa na uchaguzi ukaharibika. Baada ya uchaguzi Mwenye nchi akatoa kongole kwa ushindi wa kishindo na mapaka sasa mitaa, vitongoji na vijiji vyote nchini vipo chini ya CCM.
 
Jaffo aliikana kauli yake kesho yake baada ya kufokewa na uchaguzi ukaharibika.Baada ya uchaguzi Mwenye nchi akatoa kongole kwa ushindi wa kishindo na mapaka sasa mitaa,vitongoji na vijiji vyote nchini vipo chini ya CCM

Mkuu hakiki facts zako. Zangu zinanielekeza kuwa jitihada za kuwasihi upinzani kurejea ulingoni hazikufua dafu baada ya kuwa mzengwe wa kuwa engua ulikwisha pita.
 
Mkuu hakiki facts zako. Zangu zinanielekeza kuwa jitihada za kuwasihi upinzani kurejea ulingoni hazikufua dafu baada ya kuwa mzengwe wa kuwa engua ulikwisha pita.
Hapakuwa a good will na ndio maana baada ya pale Mkuu alikisifu Chama chake kwa ushindi wa kishindo.Hata huu wa sasa ilitakiwa ushindi wa kishindo lakini "disco limeingia morani"kavuruga mipango yote na inabidi plan B itumike.
 
Hapakuwa a good will na ndio maana baada ya pale Mkuu alikisifu Chama chake kwa ushindi wa kishindo.Hata huu wa sasa ilitakiwa ushindi wa kishindo lakini "disco limeingia morani"kavuruga mipango yote na inabidi plan B itumike.
Hahaha na kwa jicho la hali ya juu watu wanaiangalia hiyo plan B nayo itakuwaje. " Morani kachachamaa na disco ndo linanoga"😂😂
 
Hapakuwa a good will na ndio maana baada ya pale Mkuu alikisifu Chama chake kwa ushindi wa kishindo.Hata huu wa sasa ilitakiwa ushindi wa kishindo lakini "disco limeingia morani"kavuruga mipango yote na inabidi plan B itumike.

Nadhani enguaji ilikuwa kumpendezesha zaidi jiwe. Hawakutegemea upinzani watasusa jumla.

Upinzani walipokaza kuwauma iliwauma. Ninaamini jitihada za kuwarejesha wote zilikuwa za dhati ili kuzima vilio vya tume huru vilivyo pata uhalali zaidi.

Hata hivyo, upinzani kususa moja kwa moja iliwagharimu ndiyo sababu ya zile kauli - hata iweje kwenye hizi chaguzi, hakuna kumsusia fisi bucha tena: "tutabanana hapa hapa!"
 
jiwe ndio kaleta engua engua aondoke na engua engua zake.

Hatukuwahi kuwa na sakata la kuengua enguana tangia tupate uhuru.

Kitu kimoja chenye kushabihiana na jiwe ni engua engua.

Uko sahihi mkuu. Kutoka kwa jiwe kutaondoka na engua engua.
 
Hahaha na kwa jicho la hali ya juu watu wanaiangalia hiyo plan B nayo itakuwaje. " Morani kachachamaa na disco ndo linanoga"😂😂

Haipo nzuri kwake kuliko kukwiba kura. Hii ni kote. Huku na kule kwa bwana Maalim.

Kwenye kuzilinda panatakiwa waraka mzito kuliko wa bwana Roberto wa kule Amsterdam.
 
Back
Top Bottom