Tumeingiliwa! na nadhani nchi imeshauzwa

Tumeingiliwa! na nadhani nchi imeshauzwa

Why now!? Walikuwa wapi miaka yote 46 tangu tupate uhuru? Hawakuijua Tanzania miaka hiyo iliyopita sasa ndio wamesikia kwamba kuna kanchi kanaitwa Tanzania na ghafla tu wakajenga interest kubwa na nchi yetu!? Tuwaogope kabisa hawa urafiki wao ni wa undumila kuwili na historia juu ya urafiki wao ipo ya kutosha kabisa. Wanafukuzwa na wajapan kila kukicha lakini hawana mpango wa kuondoka. Wakiingia kwetu basi itakuwa ni balaa tupu maana tutakuwa hatuna uhuru wa kuamua lolote bila wao kulikubali au watajenga uadui na sisi.

Sasa hivi hakuna nchi hata moja ya kiafrika iliyowakubalia kujenga kituo chao cha kijeshi katika Afrika, sasa inaelekea wameitarget Tanzania ili wajenge kituo hicho. Pia kupatikana kwa uranium nchini kwetu na uwezekano wa kupatikana mafuta kumewafanya hawa jamaa wenye tamaa kubwa ya rasilimali hizo kufanya kila njia kuhakikisha rasilimali hizo ndani ya nchi yetu zinakuwa chini ya control yao. Kumbuka hawa Wairaq walikuwa ni rafiki zao wakubwa sana, mara tu walipokataa kuwasikiliza basi wakawa maadui.

Jeshi letu limefundishwa na Watanzania wenyewe na limeweza kupambana na nduli na kumtwanga vizuri sana pia linasaidia kulinda amani katika nchi mbali mbali duniani hivyo tuna jeshi zuri tu ambalo halihitaji mafunzo toka kwa hawa mandumila kuwili

Fungua macho uone history ya urafiki wa Marekani siku zote si urafiki wa kweli ndio maana negative attributes zao ni kubwa mno kuliko positive attributes hata katika nchi wanazoziita ni marafiki kama UK, France, Germany etc. Kama umesikia Hillary katika kampeni zake anasema kwamba kama akishinda basi Clinton atakuwu ambassador wa kujenga upya reputation ya marekani iliyobomoka all over the World. Open your eyes bro.



Ndugu yangu weeeee,

Hujui kuwa sasa kwa jirani zetu hapo mlango wa pili kunawaka moto? Huyu jamaa ni mjanja sana. Anakimbizia watoto wake kwetu. Na sisi tusipokuwa makini tutajuta majuto ya shetani jehanamu
 
Waacheni waje waweke hiyo kambi, ukishakubali kuolewa unatakiwa ustahamili mengi..
 
Kishoka, is it confirmed that Tanzania will be a base for AFRICOM? i would really like to know this. It is very interesting to know where our government stand on this!

..it is not confirmed,it is suspected!

..sitashangaa wakipenda iwe hapa! this is the most stable country in the region,halafu hii region ni strategic.
 
Jiandaeni dada zenu kubakwa na wanajeshi wakimaekani kama wanavyofanya huko japan... na jinsi wanawake wakibongo walivyo na tamaa. Mbaya zaidi huyu muungwana anawa sevu majamaa uhuru wetu kama waiter wa rose garden. Siunajua inabidi ngozi nyeusi ndio zikafe Somalia na kwengineko in their secret war.TUMEKWISHA.. welcome to the AMERICAN EMPIRE...

..hivi hawa wakina dada si ndio wanaotembea na nyembe kwenye pochi?ukileta mzaha wanakuchorachora? nadhani kwa hawa itabidi watembee na visu vidogo!
 

Ingekuwa vema sana kama Marekani ingeweka makao makuu ya Africa Command yao Tanzania. Ingetusaidia kwa namna nyingi mno. Ingekuza utalii na mawasiliano ya aina mbali mbali, na hata kungeweza kuweko direct flights kati ya New York na Dar.
Hamjasema kwa nini mnaogopa Marekani. Si maadui wetu. Wanaweza kuwa mapatna wazuri sana.

..ila,inabidi tutumie nafasi hiyo kwa ustadi hasa,bila hivyo tutachanganyikiwa tu.

..nchi kama taiwan,singapore,south korea na japan,hata quatar na saudia zimeendelea kwa kiasi fulani kutokana na presence ya either states au uk.
 
TEKNOLOJIA YA NINI WAKATI WATU WANANJAA

KWANZA TUSHIBE NA TUWE NA CHAJKULA CHA KUTOSHA KISHA MAMBO MENGINE BAADAE

..kwani kilimo hakitumii tekenolojia? na katika dunia ya leo huwezi pata chakula cha kutosha bila kutumia tekenolojia!

..vitu kama umwagiliaji,madawa,mbegu mpya,resechi ya magonjwa,n.k

..we have to look at positive side of things!
 
m16.jpg

..duh,uswazi wanavumilia kichizi nowdays,yani hilo lisingefika kote huko! unamwona jamaa anavyolitolea macho? hapo kulikuwa na ffu nini?
 
Waacheni waje waweke hiyo kambi, ukishakubali kuolewa unatakiwa ustahamili mengi..

Ukimkataa shetani mkatae kwa mambo yake yote na hila zake zote.

Mie siewaelewi kabisaaaaaa
Leo hapo Bush akitoa scholarship za kwenda kusoma huko US nyie ndio mtakua wa kwanza na watoto wenu.
akitangaza kuwajengea barabara wala hamudiriki kunyanyua midomo kupinga msaada huo.
Yeye akiomba kujenga kitu midomo juuuuuuuuuuuuuuuuuuu

Watanzania wezangu HAKUNA BIASHARA YA NAMNA HIYO POPOTE DUNIANI
Hata baba yako alipokupeleka shule alisema ni kwa ajiri yako lakini ukweli pia alitegemea faida kutoka kwako kwa wewe kukupeleka shule.
Hapa kinachotakiwa ni watu kujipanga na ku rob hizo chansisi za kuwepo hao wa marekani HUU NI UTANDAWAZI MTU ANA WEZA JENGA ISHI MAHALI POPOTE.

Sasa inanza kujengeka tabia ya kua ni halali kwa muafrika kuendesha biashara na kuishi ulaya ama marekani lakini mzungu kuja kufanya biashara afrika ni mwizi anaibia maliasili zetu , TOO MUCH TOO MUCH. Tuweni washindani na sio roho mbaya na wivu usiona na misingi
 
..huyo fisadi njonjo na mzee bomani wamekuwa marafiki toka lini? au ndio mambo ya dina?!

njonjo na bomani ni marafiki sana ..kuna kipindi wote walikuwa ma attorney general...pia njonjo ni GOD FATHER wa mmoja wa watoto wa bomani....kwa namna njonjo alivyomshauri kenyatta wakatokomea na mandege na mali za east africa ns umojs ukavunjika ..it tells me ufisadi na usaliti nchi hii umeanza zamani.....[/B]
kupitia njonjo ...mmoja wa vijana wa bomani..amepewa u DIRECTOR - KENYA COMMERCIAL BANK[TANZANIA]...njonjo anazo hisa nyingi kwenye bank hiyo...inayomilikiwa na serikali ya kenya na wananchi kupitia soko la hisa la nairobi....
 
Mkamap,
Mkuu hata sikuelewi kabisa...
Nitajaribu njia tofauti na hiyo... Watanzania wengi wanalia na kuomba tukome kuchukua mikopo ya IMF kuwa ndiyo inayozidi kutulemaza na sisi kuendelea kuwa taifa tegemezi. Haya ni mawazo ambayo kama kweli serikali yetu itapitisha kutakuwepo hakuna tena kupokea msaada kama huo, hivyo mikakati mingi inayojengwa na fedha hizo haitakuwepo ama itajengwa kwa njia nyingine.
Kwa hiyo hili swala la Marekani linaweza kutopokelewa ikiwa serikali yetu itakubali kufanya yanayopendekezwa hapa na hakuna mahala panaposema kama ujenzi wa kambi hautakuwepo Tanzania basi nasi tutapoteza misaada mingine.. Hivi vitu havihusiani kabisa, zipo nchi zinazopeleka wanafunzi ama kupokea misaada toka Marekani zaidi yetu na hawana kambi.
Nambie nchi iliyofanikiwa zaidi kwa sababu ya kambi ya Marekani kama sio sifa za wao wenyewe kujikosha kuwa Japan ilipata maendeleo kwa sababu ya kambi zao hali inafahamika kabisa kuwa Japan na Ujarumani hawa walikuwa mbele yao kimaendeleo kabla ya vita kuu..Ujerumani na Japan walikuwa mbele vibaya sana na pengine vita ndio pekee iliyowarudisha nyuma wakati ule..leo hii wanakuja haraka sio kwa sababu ya Marekani... wana elimu na uwezo wa kutosha kabisa kuwa taifa kubwa bila Marekani na hakuna Mmarekani anayeweza kwambia wamekifanya nini hasa nchi hizo kuwaendeleza.
Kama waliweza mwanzoni kuwa mbele watashindwa nini leo hii wategemee misaada ya Marekani. Lakini tukumbuke tu kwamba Wajarumani na Wajapan wote wanataka kambi hizo zifungwe lakini Marekani amekataa kutokana na mikataba iliyowafunga jamaa na inawaruhusu Marekani kuwepo nchi hizo....And they can do nothing!

Kifupi fungeni ndoa hizo na chupi tutazivua tubakie na upande wa Khanga lakini swala la kuja jenga kwa baba mkwe kibanda chako mwenyewe, hiyo sii tamaduni yetu hata kidogo..
 
Wajameni, Bongo kuna dhahabu, almasi, gas, mafuta, platinum and %&^%%^"!£""!??@!!! mwataka sababu gani zaidi ya hapo???? It is obvious joji bush anawakilisha future interest za USA hapa!!!

TZ lazima itapendwa sana na kusifiwa sanaaaa!!! Tutalindwa sanaaa!!! security system yetu lazma ipokee order toka washington!! ndio wafanyavyo kuwaiti, saudia etc...!! watachukua madini na kiasi fulani uhuru wetu!

Hiyo ni upande mmoja, upande wa pili hawa jamaa wanajua kula na vipofu, tutapewa misaada, tutalindwa na kwa hakika tutafaidika!!! Kama wazee wa kijiweni wanavyosema ukitaka vya bure shika ukuta!!!!

Acheni waje jamani, wao watafaidika nasi vilevile. watatupatia na hao wajomba machotara pia!!!
 
It is clear our nation is reliant upon big foreign oil. More and more of our imports come from overseas. George W. Bush

What else!!!!
 
Mkamap,
Mkuu hata sikuelewi kabisa...
Nitajaribu njia tofauti na hiyo... Watanzania wengi wanalia na kuomba tukome kuchukua mikopo ya IMF kuwa ndiyo inayozidi kutulemaza na sisi kuendelea kuwa taifa tegemezi. Haya ni mawazo ambayo kama kweli serikali yetu itapitisha kutakuwepo hakuna tena kupokea msaada kama huo, hivyo mikakati mingi inayojengwa na fedha hizo haitakuwepo ama itajengwa kwa njia nyingine.
Kwa hiyo hili swala la Marekani linaweza kutopokelewa ikiwa serikali yetu itakubali kufanya yanayopendekezwa hapa na hakuna mahala panaposema kama ujenzi wa kambi hautakuwepo Tanzania basi nasi tutapoteza misaada mingine.. Hivi vitu havihusiani kabisa, zipo nchi zinazopeleka wanafunzi ama kupokea misaada toka Marekani zaidi yetu na hawana kambi.
Nambie nchi iliyofanikiwa zaidi kwa sababu ya kambi ya Marekani kama sio sifa za wao wenyewe kujikosha kuwa Japan ilipata maendeleo kwa sababu ya kambi zao hali inafahamika kabisa kuwa Japan na Ujarumani hawa walikuwa mbele yao kimaendeleo kabla ya vita kuu..Ujerumani na Japan walikuwa mbele vibaya sana na pengine vita ndio pekee iliyowarudisha nyuma wakati ule..leo hii wanakuja haraka sio kwa sababu ya Marekani... wana elimu na uwezo wa kutosha kabisa kuwa taifa kubwa bila Marekani na hakuna Mmarekani anayeweza kwambia wamekifanya nini hasa nchi hizo kuwaendeleza.
Kama waliweza mwanzoni kuwa mbele watashindwa nini leo hii wategemee misaada ya Marekani. Lakini tukumbuke tu kwamba Wajarumani na Wajapan wote wanataka kambi hizo zifungwe lakini Marekani amekataa kutokana na mikataba iliyowafunga jamaa na inawaruhusu Marekani kuwepo nchi hizo....And they can do nothing!

Kifupi fungeni ndoa hizo na chupi tutazivua tubakie na upande wa Khanga lakini swala la kuja jenga kwa baba mkwe kibanda chako mwenyewe, hiyo sii tamaduni yetu hata kidogo..

Mkuu soma tena unielewe
Hoja yangu ni kua hakuna mtu anayetoa msaaada bila yeye kunafufaika ,kwa namna nyingine msaada ni takrima
Hivyo ukitaka kuepukana na adha hiyo pia ulitakiwa kukataa na mambo yake mazuri yotee.
Mfano mtu akipata scholarship kwenda marekani watu wanafurahia anakwenda kujifunza elimu bora na kwanini mwanajeshi akipata hiyo kitu kama scholaship ya kujifunza zaidi ili aive zaidi ktk taaluma yake ya kijeshi watu wanaanza kuhoji?? Hapo hatutendi haki.
Tusifanye mambo kinafiki nafiki hao wanaosema kukataa misaada ya IMF ni wanafiki wakubwa, huwezi kataa msaada wakati njia mbadala huna.
Mugabe naye walimuchochea hivyo hivyo kataa waingereza na misaada yao fukuza hawa wazungu ktk mashamba yetu LAKINI leo ndio hao hao wanaomwita Mugabe ndio kawafikasha hapo wazimbabwe kwa maamuzi yake.
Mkubwa uchumi wetu na hali yetu tuliyonayo hatuna jinsi ila ni kujipanga vizuri ukichukua huo mkopo wa masharti na uwekeze vyema na utakapopata matunda thabiti ndio ujitutumue vinginevyo utau bure watanzania.
 
Mkamp..si kweli ikiwa tunakataa hili basi tukatae kila kitu umeonawapi?

Pia si kweli eti wanajeshi wakitaka kujifunza eti tunaleta longolongo...it seems huu mjadala mzima hujauelewa. Hakuna anaekataa mwanajeshi kujifunza.

Serikali yetu haipo serious ktk mambo ya elimu na hizo unazozisikia eti scholarship ni elim ndogo ambayo watu tunakuja kuwa watumiaji wa Teknologia.

Uingereza wana chuo cha Military, huwezi amini..Tanzania hupeleka mwanafunzi 1 kwa mwaka au baada ya miaka kadhaa. Hio misaasa unayoisikia si misaada, ni mikopo. ambayo tunakuwa na DENI kubwa. Matokeo yake mafisadi pesa kama hizo za kulipia madeni wanazitafuna.
Ilivyo Huko IMF,WB kuna mafisadi kibao tu..ili usamehewe deni lako, wao huwa wanaaangalia nani anadaiwa sana, wanakuja kuzungumza na viongozi wetu wakuu, wanawaambia sie tutawapigieni debe IMF,WB msamehewe deni..lkn tunahitaji 10% yetu. na hapo ndipo viongozi wetu wanapoweka 10% ..kula kwenda mbele.

Mabadiliko HALISI yatakuja endapo sie tutaanza kuwa serious ktk ELIMU na sio KUENEA KWA BAA KILA KONA. Unaonaje leo hii kila ilipo BAA IWEKWE LIBRARY...kila KONA..m telling you within 5 years hatutakuwa hapa tulipo.
 
Mkamap,

Nitakuuliza swali dogo sana.
Umezungumzia maswala ya mtu kumpeleka mwanawe Marekani kusoma, kwani hatuwezi kuwa na vyuo hapahapa nyumbani?.. Mwanajeshi kwenda America, hatuwezi kuwa na vyuo hapa hapa nyumbani... Kinachotakiwa ni mawazo yanayotazama mbele na sio kuwa watumwa. Nchi zilizoendelea hazipeleki wanajeshi wao nje kusoma kwani mazingira ni tofauti kinachotakiwa ni vifaa ambayo vinanunuliwa...
Nchi zote zilizoendelea hazipeleki watu nje kusoma ati kwa mabadilishano ya biashara...China wana jeshi lao na yawezekana hakuna hata mtu mmoja aliyekwenda mafunzo Amerika ama nchi ya nje..Ni ufinyu wetu kufikiria kuwa kila bora linatokana na misaada ambayo haiwezi kutusaidia kitu in a field at long run.
Ujio wa Bush hauhusiani kabisa na hizo scholarship kwani shule yoyote ile ni fedha yako...
Swala la IMF hilo ni mada nyingine kabisa na naweza pingana na wewe kwani hakuna hata nchi moja unayoweza nambia imepata hizo njia mbadala kutokana na IMF...
Toka wameingia IMF nchini ni zaidi ya Umri wa Utawala wa Nyerere, njia zipi zimekamilika?..reli ya Uhuru mbaya kuliko hata wakati ule, viwanja vya ndege ni kama alivyoviacha mwalimu, njia za mawasiliano bado wawekeshaji wote wanategemea vifaa vya taifa - Mwenge....Bandari ndio wala usiseme. Anachokuja kusaidia (promote) ati Maleria na Ukimwi, ambao ni mradi wa mkewe kawekesha ktk madawa ya kuzia maradhi hayo. Ukitaka kuondoa Maleria fukia mashimo yenye maji machafu na sio kuongeza hesabu ya vidonge.
Unafiki nadhani upo serikalini ambao wanafahamu kabisa kuwa misaada hii haitusaidii kitu lakini bado wanaichukua..Na kwa mfano wako Unafiki ni yule mwanafunzi anayesoma Marekani hali akijua kabisa elimu anayopewa na chuo hicho ni mbovu kuliko ya UDSM ama Tumaini.
 
Mkamap,

Nitakuuliza swali dogo sana.
Umezungumzia maswala ya mtu kumpeleka mwanawe Marekani kusoma, kwani hatuwezi kuwa na vyuo hapahapa nyumbani?.. Mwanajeshi kwenda America, hatuwezi kuwa na vyuo hapa hapa nyumbani... Kinachotakiwa ni mawazo yanayotazama mbele na sio kuwa watumwa. Nchi zilizoendelea hazipeleki wanajeshi wao nje kusoma kwani mazingira ni tofauti kinachotakiwa ni vifaa ambayo vinanunuliwa...
Nchi zote zilizoendelea hazipeleki watu nje kusoma ati kwa mabadilishano ya biashara...China wana jeshi lao na yawezekana hakuna hata mtu mmoja aliyekwenda mafunzo Amerika ama nchi ya nje..Ni ufinyu wetu kufikiria kuwa kila bora linatokana na misaada ambayo haiwezi kutusaidia kitu in a field at long run.
Ujio wa Bush hauhusiani kabisa na hizo scholarship kwani shule yoyote ile ni fedha yako...
Swala la IMF hilo ni mada nyingine kabisa na naweza pingana na wewe kwani hakuna hata nchi moja unayoweza nambia imepata hizo njia mbadala kutokana na IMF...
Toka wameingia IMF nchini ni zaidi ya Umri wa Utawala wa Nyerere, njia zipi zimekamilika?..reli ya Uhuru mbaya kuliko hata wakati ule, viwanja vya ndege ni kama alivyoviacha mwalimu, njia za mawasiliano bado wawekeshaji wote wanategemea vifaa vya taifa - Mwenge....Bandari ndio wala usiseme. Anachokuja kusaidia (promote) ati Maleria na Ukimwi, ambao ni mradi wa mkewe kawekesha ktk madawa ya kuzia maradhi hayo. Ukitaka kuondoa Maleria fukia mashimo yenye maji machafu na sio kuongeza hesabu ya vidonge.
Unafiki nadhani upo serikalini ambao wanafahamu kabisa kuwa misaada hii haitusaidii kitu lakini bado wanaichukua..Na kwa mfano wako Unafiki ni yule mwanafunzi anayesoma Marekani hali akijua kabisa elimu anayopewa na chuo hicho ni mbovu kuliko ya UDSM ama Tumaini.

Mkuu nielewe
Mie nimesema hakuna mtu dunia hii anayekupa msaada harafu akakuachia hivihivi ,hawa wazungu ktk nchi zao wenyewe kunamasikini wanaookota chakula ktk majalala hawana pa kulala sasa cha kujiuliza yani asipende mwezake mweupe aje utujengee sisi ???
Ndio nikasema tukitaka kuondokana na adha hii lazima tukatae misaada yao yote hakuna msaada mwema kutoka kwa mzungu/mwarabu.

Na ili kuikataa misaada hiyo lazima tuwe tumejipanga vya kutosha vinginevyo tutaishia kama Zimbabwe.Naona watu tuwe tunaelewa nini maana ya mfano.
mie nipo kinyume na hii misaada pia nipo kinyume na mtu anayepanda kupokea na yeye asitake kutoa.
 
Back
Top Bottom