Tumejiaandaje kupokea wakimbizi toka Kenya?

connections

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2013
Posts
2,190
Reaction score
3,039
1. Yanayoendelea Kenya mmeyasikia/kuyaona kwenye vyombo vya habari. Kimbilio lao Kuu ni Tanzania. Tofauti na Majirani wengine kwao ni Njaa (Ethiopia, Uganda), vita (Somalia, Sudan).

2. Maandamano mapya yametangazwa huko. Na kiukweli naona balaa zito linawasubiri. Tumejipangaje majirani?
 
Maandamano mapya ni lini?
 
Wewe unaangalia Kenya. Wewe hujioni? Hapa huoni kuwa panafukuta? Njaa ikizidi hamna wa kumsimamisha
 
Sisi
Wewe unaangalia Kenya. Wewe hujioni? Hapa huoni kuwa panafukuta? Njaa ikizidi hamna wa kumsimamisha
Sisi ni MABOLIZOZO hakuna kitu tutafanya zaidi ya uKEYBOARD WARRIOR... ma tukianza tu. Tunagawanywa kwa kauli ya kulinda amani mpaka kwa viongozi wa dini watatumika, hapo tunapungua, vikiokotwa viroba kadhaa vya miili tunapungua tena, kisha tunaletewa skendo DIAMOND ana mimba ya P. Diddy, hapo kwisha habari yetu... 😂🤣
 
Tuwape pongezi tu wakenya Kwa kuamua kudai haki zao bila woga.Siku zote umma ikiamua hakuna Cha polisi Wala mwanajeshi anayeweza kuushinda umma.Viongozi wa Ccm kama wanajielewa wayafanyie kazi madai ya generation z maana maovu ya watawala ya Kenya yanafanana na ya Tanzania.mfano wake wa viongozi kulipwa mafao makubwa kama vile na wao waligombea urais,Kenya hili wamelipinga Gen z Hadi limefutwa lakini Tz lilipendekezwa na mke wa kikwete na spika kupiga makofi na kupitisha huo uhuni,kingine ajira kutolewa Kwa upendelea,huduma mbovu za kijamii Huku viongozi na watoto wao wakiishi maisha ya kifahari Kwa magari ya milioni mia sita na saa za mkononi za milioni miambili kama saa ya Samia Huku wanafunzi wanakaa chini ya mwembe wananyeshewa mvua wakiwa wanasoma na madudu mengine mengi tu ya kipumbavu yanayofanywa na Hawa ccm.msipobadilika ninyi wahuni ipo siku generation z ya Tanzania itakuwa ni moto wa kuotea mbali
 
Nyinyi mtaandamana mitandaoni, tu mtaanzia, barabara ya titwa, na ` kueelekea mitaa fecibuku na Insta, na kumalizia maandamano viwanja vya JF
Bado njaa haijakolea. Sasa hivi una milo miwili au mmoja. Itafika hakuna mlo hata mmoja. Mwanao na mke wamekaa wanamuangalia hapo wewe mwenyewe wala hutaamrisha utaamka mwenyewe kwenda mtaani hata risasi huwezi kuisikia. Njaa bado kwa sasa.
 
Hamna wakimbizi, maandamano sio vita. Kwankenya hairp tokea
 
bandits wameshagawanyika hawana nguvu sana, hawana uelekeo, wamepoteza lengo hata wanachokidai sasa hakieleweki na hakiwezekani na hakuna kitu watafanya zaidi ya kukanyagana, kuumizana na kuuana wenyewe 🐒
 
Uwoga wako ndiyo umasikini wako we kimbia wanakuja kumrithi mumeo.
 
Hayatuhusu
Hiyo ni kazi ya Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi
UNHCR ,

Kwanza maandamano sio vita hawawezi watu kukimbia bali watakaa ndani wasioandamana na kufunga milango ya nyumba zao !!

Maandamano sio Vita !🙌!
 
hakuna kitu kama icho kitatokea.
 
Yametangazwa na nani?; hao ni wahuni wako facebook tena nje ya nchi hasa wakina Miguna miguna ndio wanafanya hizo siasa. Maandamano ya awali ndio yalio ungwa mkono na raia wa Kenya, Ila now Raia wengi sana wanakubaliana na mabadiliko yanayo fanywa na Ruto.

Jikiteni kujadili ya kwenu.Mama yenu na timu yake wanaishi maisha ya anasa kwa kodi zenu na nyie mko busy na kushadahia kenya
 
Gen Z inatumika tu sasa hivi, kinachoendelea hivi sasa ni siasa, ukabila very soon utaibuka.
Ikashafika hiyo level Mungiki watakuwa activated, hapo ndiyo mtaona maana halisi ya blue flames
 
Wakenya wanajitambua ndiyo sababu Ruto aliwapongeza GenZ huku msiojitambua mnawaona wakorofi, hakuna atakae ikimbia Kenya labda mabwege toka Tanzania, acha kubeti na kusikiliza uchambuzi wa mpira unaowatia ujinga vijana wa Tanzania fuatilia kinachoendelea Kenya kupitia redio na Tv za Kenya, hakuna anayekamatwa wala kuteswa.
 
Yale Maandamano hayana nguvu tena ,na kwa sasa yakifanyika ni yanafanyika Nairobi tu sasa hii haina maana tena, Ruto mjanja alisha kata nguvu na Raia wengi wanakubaliana na anacho fanya Ruto kwa sasa. Sisi tuanze na huyu wetu ambaye ameziba masikio
 
Nyinyi mtaandamana mitandaoni, tu mtaanzia, barabara ya titwa, na ` kueelekea mitaa fecibuku na Insta, na kumalizia maandamano viwanja vya JF
Ahahahahaha! Umeua Mkuu! Kwahiyo Kenya Wana Gen. Z huku Tanzania tuna Gen. Mitandao! Ahahahahaha!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…