Tumekosea wapi ? Na nini kifanyike baada ya mvua hizi?

Tumekosea wapi ? Na nini kifanyike baada ya mvua hizi?

jozee jose

Member
Joined
Sep 22, 2022
Posts
52
Reaction score
120
Tangu January Hadi katikati ya mwezi huu( April) tumekuwa tukisikia na kushuhudia mvua kubwa zikinyesha Kwa baadhi ya mikoa nchini Tanzania.

Kwa mtazamo wangu haya ni matokeo ya ubinafsi wetu juu ya mazingira yanayotuzunguka.

Wiki Moja iliyopita niliongea na mdau mmoja ambaye Yuko mkoani Mbeya alielezea janga la maporomoko ya matope(mud flow) kuwa ni jambo ambalo halikuwahi kuwepo kabla pia amesema mvua zimekiwa kubwa mno hajawahi kuziona tangu 1999, Akaeleza sababu kuu ya maporomoko ya matope kutoka mlima kawetere ni ukataji wa miti ovyo, Kwenye hili alitia mkazo kuwa hakuna Sheria Wala hatua madhubuti ambazo anasimamia katika kuyatunza mazingira hayo.

Athari zilizotokea ni kama watu wamekosa makazi, miundo mbinu kama Barabara na mitaro imeharibika pamoja na mazao ya kilimo kama mahindi na maharagwe.

Ni nini tukitarajie baada ya mvua hizi?

Kuongezeka Kwa uhitaji hasa Kwa bidhaa ya chakula hili litapelekea vitu kupanda bei na ugumu wa maisha kuongezeka. Sasa ni nani alaumiwe?
 
Kuhusu ukataji miti ovyo, hili ni janga la kitaifa ambalo linachochewa na viongozi wetu wababaishaji na waliokosa maarifa.

Niko mahali ambako raia wamevamia milima na kufyeka miti ili kupata mashamba. Serikali ilikuwa ikiwakamata wahalifu kisha kuwatoza faini na kuwaachilia. Ukawa mtindo, watu wanafyeka huku wakijiandaa kulipa faini kisha kuachiliwa. Mtindo huo ndiyo umefanya milima yote imefyekwa na serikali imekosa cha kufanya. Matokeo yake ni makorongo kujaa maji kutokea milimani, maji yanayoharibu makazi na mashamba.

Viongozi wanachowaza ni kulipwa faini kisha kunyamaa kimya.
Ubinafsi na ujinga vinatumaliza.
 
wakati mwingine ni adhabu kwa watu wa eneo fulani kufanya dhambi ya mob ndio maana wanaadhibiwa kwa pamoja. Unakuta watu wa eneo fulani walimwaga damu isiyo na hatia, kuna ushirikina mwingi, ni wakaidi kwa Mungu wasio na shukrani inabidi wapigwe kwa tauni ili washike adabu wakae sawa
 
Tatizo la kutokuwa na mipango miji thabiti.
Maeneo yaliyopimwa ni machache,
Maeneo yaliyopimwa hayaheshimiwi.

Mipango miji sio agenda ya viongozi,wala kupanda miti kuhifadhi mazingira sio kitu kinachowaumizi kichwa viongozi.

Bei ya gesi wameacha imepanda sana,na hivyo kuchochea ukataji miti kwa ajili ya kupata mkaa,na hivyo kuathiri mazingira na tabia nchi.
Nini kifanyike?Jibu ni kuwa upimaji ufanyike jamii ihamasishwe kuheshimu na kutunza mazingira.
 
Mbona hapa bado kabisa haziajaanza?

Zitaendelea kunyesha kubwa zaidi hadi mwishoni mwa mwezi wa nane.

Tanesco wamepata tena kichaka cha kujisitiria kwa muda.😂😂😂
 
Kuhusu ukataji miti ovyo, hili ni janga la kitaifa ambalo linachochewa na viongozi wetu wababaishaji na waliokosa maarifa.

Niko mahali ambako raia wamevamia milima na kufyeka miti ili kupata mashamba. Serikali ilikuwa ikiwakamata wahalifu kisha kuwatoza faini na kuwaachilia. Ukawa mtindo, watu wanafyeka huku wakijiandaa kulipa faini kisha kuachiliwa. Mtindo huo ndiyo umefanya milima yote imefyekwa na serikali imekosa cha kufanya. Matokeo yake ni makorongo kujaa maji kutokea milimani, maji yanayoharibu makazi na mashamba.

Viongozi wanachowaza ni kulipwa faini kisha kunyamaa kimya.
Ubinafsi na ujinga vinatumaliza.
Nakubali kwa💯
 
Back
Top Bottom