Binafsi naona kama tumezalisha kizazi cha vijana wa hovyo sana wanaoshabikia mpira kwa sasa. Sijui ni kwa nini hawa jamaa wanaoshabikia Simba wana uelewa na iq ndogo sana. Toka enzi na enzi miamba hii miwili haiwezi yote kuwa kwenye peak mara moja. Ni lazima mmoja awe chini na mwingine juu. Miaka 4 mfululizo, Simba ilikuwa juu na mbele ya Yanga ila Investment ya GSM imeiinua yanga sasa wakati Mo anasua sua upande wa pili. Hawa upande wa pili hawakubali ukweli sasa kila siku ni kusingizia uchawi, bahasha na marefa kuipendelea Yanga. Miaka 4 iliyopita Yanga hawakuwa wanalalamika wala singizia kuwa simba inahonga wala kuloga. Wao walikubali na kuumia kuwa simba ni tishio.
Kiukweli hauwezi fananisha simba na Yanga kwa sasa hata ukiweka mzania wa mchezaji mmoja mmoja utaona hilo ila Barba na Ahmed wanawaaminisha Yanga haiwezi shinda bila kuhonga au kuloga. Pathetic