KERO Tumepata huduma mbovu JKCI upande wa VIP, baadhi ya Watumishi wanahudumia Watu kwa kujuana

KERO Tumepata huduma mbovu JKCI upande wa VIP, baadhi ya Watumishi wanahudumia Watu kwa kujuana

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Moja kati ya jambo ambalo limekuwa likipigiwa kelele ni kuhusu ubora wa huduma za Watoa huduma katika taasisi na Mamlaka mbalimbali za Serikali, inaonekana ni kama sehemu ambayo Watu wengi hawajali sana kuhusu ‘customer care’.

Nilifika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kupatiwa huduma tena nikiwa na mwenzangu tukaelekea upande wa VIP tukiamini tutapata huduma nzuri na kwa haraka licha ya kuwa gharama zitakuwa kubwa.

Tulipofika hapo tukasajiliwa pekee kisha tukajulishwa madaktari hawapo tunatakiwa kuwasubiri, hiyo ilikuwa ni asubuhi mapema tu muda wa kazi.

Mgojwa ambaye nilikuwa naye hakuwa katika hali nzuri, tulilazimka kumfikisha hapo akiwa katika kiti cha kusukuma wagonjwa, ajabu tukaambiwa tunatakiwa kusubiri Daktari kwa masaa mawili.

Wahudumu tuliowakuta wa VIP wanahuduma Watu kwa mazoea sana, majibu mabaya, hata unapojaribu kuwaambia wakupe maelekezo kwa usahihi wanajibu kama vile tunaomba msaada.

Hali ya mgonjwa wetu ikawa inazidi kuwa mbaya tukiwa palepwale, tukawa tunajiuliza kama sisi VIP tunapata huduma ya aina hiyo, wale wanaolipa kawaida hali ipoje?

Alipofika Daktari na kuona hali ya mgonjwa ilivyo akasangaa kwanini hatujapata huduma wakati wazi Mgonjwa anaonekana yuko vibaya, ikabidi Daktari aanze kulazimisha vitu viende kwa haraka na kutusaidia kuhakikisha tunapata huduma ikiwemo vipimo.

Kibaya zaidi wakati sisi tunafika kuna wagonjwa wengine tuliwakuta hapo wanasubiri, hivyo mpaka Daktari anafika tayari walikuwa wamekaa kwa muda wa Saa tatu wakisubiri huduma.

Huduma zinatolewa kimafungu, ni kama vile watu wanapewa huduma kwa kujuana, na ukumbuke kuwa hapo ni VIP, inavyoonekana yaani kama hujiongezi wewe mwenyewe hupati huduma kwa wakati.

Kiufupi hakuna mawasiliano mazuri kati ya Wahudumu wa hapa na wagonjwa, wahudumu wanahudumia kwa mazoea au watu maarufu, wasio na connection ni tatizo.

Yaani ni tatizo kubwa sana sana, na huruma pia. Kuna mama nilimuona anajigeuza tu yupo hoi, nilipomuuliza akasema ameambiwa Daktari yupo kwenye kikao, awe na Subira, hivi for 3 hours kweli? Kikaoni tu wakati afya za watu zipo tete?

Kingine kibaya, tulipofika hapo upande wa VIP kulikuwa na mhudumu mmoja ambaye muda mwingi yuko bize na mambo yake, kule kwenye registration walikuwepo wawili.

Tulichobaini kuwa kuna ubaguzi ni kuwa kuna Wagonjwa ambao wanapewa Nurse kabisa wa kushughulikia kila kitu then wengine wanajishughulikia wenyewe kushuka chini kuuliza wapi niende na vitu vingine.

Pia Wahudumu wa JKCI tuliowakuta wako too defensive, yaani hawataki wagonjwa wahoji au kuuliza, ukiwauliza wanakuwa wakali na kukuona wewe ni mkorofi.
Mimi veterani wa miaka mitano hapo sasa nikumegee.
Tangu mheshimiwa sana Peter Kisenge akabidhiwe kitengo huduma zimezorota kiasi cha kutisha.
Unafika saa kumi ya usiku Toka nje ya Jiji kutamani update matibabu haraka uwahi usafiri wa kurudi utakaa sii chini ya saa nne kumaliza registration,kumuona Daktari na saa mbili zingine kutoka pharmacy ambapo kwenye computer zao wanacheza games, na Mungu akusaidiwe usiwe na vipimo au kubadilishiwa Daktari
Peter Kisenge mara yupo Zambia mara Comorro,au Kawe siku hayupo kwenye camps alizobuni mikoani kupima BP kitu local docs wanachoweza.
Sasa siku hizi katangaza Wasanii watatibiwa BURE 😡
 
Mimi veterani wa miaka mitano hapo sasa nikumegee.
Tangu mheshimiwa sana Peter Kisenge akabidhiwe kitengo huduma zimezorota kiasi cha kutisha.
Unafika saa kumi ya usiku Toka nje ya Jiji kutamani update matibabu haraka uwahi usafiri wa kurudi utakaa sii chini ya saa nne kumaliza registration,kumuona Daktari na saa mbili zingine kutoka pharmacy ambapo kwenye computer zao wanacheza games, na Mungu akusaidiwe usiwe na vipimo au kubadilishiwa Daktari
Peter Kisenge mara yupo Zambia mara Comorro,au Kawe siku hayupo kwenye camps alizobuni mikoani kupima BP kitu local docs wanachoweza.
Sasa siku hizi katangaza Wasanii watatibiwa BURE 😡
Shida ni nyomi, unafika saa 10 alfajir unakuta we ni mtu wa 70. Hii ya kujiandikisha inasaidia kupunguza upendeleo kwenye kupata huduma.


Hii ya kwenda mikoani imekaa kisiasa zaidi mkuu ama kujitangaza
 
Kabisa vitu vingine vinauma sana. Mtu kang'atwa na joka, sumu inasambaa mwilini kwanini husimpe huduma kwanza halafu mkawadai.
Hizo taaluma wamezipataje? Wanamatumizi mazuri ya ubongo kweli?? Utu huko wapi???
Kama ni hospital ya serikali,dawa na vifaa tiba siyo vyako,unaogopa hasara gani?!
 
Muhimbili yote hilo tatizo lioo sana haswa watu wa dini fulani wanapenda sana hio michongo mchongo anaonaga wanavyo kuwa busy kuhudumiana haswa wakija wale wenye rangi kidogo
Ni kama unaisema Agha khan...Yan akija wa upande wao...anapitiliza moja kwa moja kwa Dr...we utashinda hata siku nzima
 
Ni kama unaisema Agha khan...Yan akija wa upande wao...anapitiliza moja kwa moja kwa Dr...we utashinda hata siku nzima
Nimeona sana pia. Nilienda kwa Dr. Jumaa kutairi mtoto, alikuja mmama muhindi wa kariakoo eti wamempitisha Dr alimuuliza Namba akaanza kujibebisha, Dr. Alimtoa ndani na mwanae wakasubirie zamu yao
 
Nimeona sana pia. Nilienda kwa Dr. Jumaa kutairi mtoto, alikuja mmama muhindi wa kariakoo eti wamempitisha Dr alimuuliza Namba akaanza kujibebisha, Dr. Alimtia nadhani na mwanae wakasubirie zamu yao
Kuna haja kubwa sanaa somo la customer care likawa sehem ya mtaala wetu...Kenya wanatupigia gap hapa kwa huduma zao...wabongo tunaendekeza sanaa tamaa na kukosa weledi kazini
 
Back
Top Bottom