Tumeshinda lakini tunaogopa

Yaani hali ngumu haswa, bora Feitoto aje kuikomboa Yanga maana tokea aondoke Yanga inaporomoko tu

Unazilinganisha timu wakati moja ipo Klabu bingwa na nyingine ipo shirikisho? 😂
 
Tafsiri ya umoja siyo kujidanganya kwamba hatuna matatizo wakati uhalisia ni kwamba tunayo.
Kama Simba hii unayosema ina matatizo hiyo inatinga robo Fainali nikumbudhe ni simba ipi nzuri uliwahi kuiona ikicheza nusu fainali ya Caf champions league ama Confederation
 
Kazi kwenye manyokanyoka sisi ndo tunasepaa..
 
Labda utusaidie wewe uliyesema timu ni nzuri kwa kuwa tuna shots nyingi
Mazembe na uto mmetolewa Champions league na hao tunaowapiga nje ndani afu mnapanua midomo tu eti mpira mbovu. Ulishaangalia mpira wa Al Hilal ya Ibenge aliyewatoa? Unavutia? Leo kacheze wewe uvutie na ushinde goli tano tuone
 
Mazembe na uto mmetolewa Champions league na hao tunaowapiga nje ndani afu mnapanua midomo tu eti mpira mbovu. Ulishaangalia mpira wa Al Hilal ya Ibenge aliyewatoa? Unavutia? Leo kacheze wewe uvutie na ushinde goli tano tuone
Sio kweli, Ni jina la timu ndio ile ile ila ubora wa timu ni tofauti na Vipers iliyomtoa Tp Mazembe. Vipers hii imecheza michezo zaidi ya saba na hawana goli hata moja.
 
Tafsiri ya umoja siyo kujidanganya kwamba hatuna matatizo wakati uhalisia ni kwamba tunayo.
Tunayo sana jana watu tunatazama mpira tunaombea uishe tu, wachezaji wanapoteza mipira ovyo tu yaani ili mradi ilikuwa presha tu
 
Mshika kibendera nae kachemka lile ni goli hamna offside pale.
Ile ni mbeleko ya wazi.
Baada ya kuona vile niliamua kuacha kuangalia mchezo wenyewe, na kwenda zangu bar kula vichungu.
 
Sio kweli, Ni jina la timu ndio ile ile ila ubora wa timu ni tofauti na Vipers iliyomtoa Tp Mazembe. Vipers hii imecheza michezo zaidi ya saba na hawana goli hata moja.
Vipers ilomtoa Mazembe mchezaji gani kaondoka? Bobos na Cesar hawakushiriki Champions league. Leta visingizio vingine. Na hiyo michezo saba mnayohesabiana ni pamoja na Raja,Horoya na Simba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…