Tumia pesa zako vizuri, kumbuka unavyokuwaga kama mgonjwa ukiwa huna pesa

Jitahidi uwe na mfumo mzuri wa kutumia pesa unayoipata, mfano unaweza kufanya hivi;
20% ya pesa yako iweke kwa ajiri ya dharula yaani akiba. Hii hata kama haukupata dharula endelea kuiacha kama akiba, itakusaidia mbeleni huko.
50% ya pesa yako iwe ya matumizi ya lazima, mf; usafiri, chakula, kodi, afya, etc.
30% ya pesa yako iwe ya matumizi yasiyo ya lazima, mf; kuchangia harusi, vinywaji, mambo ya fashion kama nguo, yaani hata usipofanya hayo matumizi hauwezi kupata madhara.

Hii itakusaidia, ingawa wengi wetu tukipata pesa ndo tunajua hapo hapo tuitumiaje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…