Tumlaumu Nyoka au Adam na Eva?

Tumlaumu Nyoka au Adam na Eva?

Siyo kila jambo ni mpango wa Mwenyezi Mungu!
Mipango mingi mibaya ni mipango yetu sisi binadamu.
Usiniambie kuwa matendo yako yote tangu uamkapo hadi ulalapo ni mipango ya Mwenyezi Mungu.
Nitatoa mfano:
Miongo kadhaa iliyopita wakati nikiwa sekondari (maeneo ya kanda ya ziwa), mjukuu wa mama mwenye nyumba alifariki dunia. Msiba ulikuwa pale pale nyumbani tulipokuwa tumepanga mimi na kaka yangu.
Ni wazi kuwa kilichofanya aage dunia kilijulikana pale mtaani. Marehemu (binti) alikuwa mtu wa kujirusha sana na mwisho wake alibeba mimba. Ili kikwepa aibu na mambo mengine aliamua kumeza vidonge ili afanye abortion.
Mauti yalimkuta baada ya kuchukua uamuzi wa kuondoa maisha ya kiumbe kisichokuwa na hatia.
Pale msibani niliona kitu cha ajabu!
Wale wazee wenye kutia ina kwenye ndevu, walifika msibani kwa ajili ya kumpa pole mama mwenye nyumba juu ya msiba wa mjukuu wake. Kauli ya "Pole, hiyo ni kazi ya Mungu", ilitawala pale msibani.
Je ni kweli kuwa ile ilikuwa ni kazi ya Mwenyezi Mungu?

Mwenyezi Mungu ana mipango mizuri kwa wale wamchao - Romans 8:28.

Aisee
 
Katika uongo mkubwa wa hizi Dini, ni Huo wa Adam Na eva. Hiv ni lini watanzania mtapata akili? Binadamu wote duniani hatujatokana Na binadamu wawili walioishi miaka 6000 iliyopita...hata miaka 50,000 iliyopita binadamu walikuwepo juu ya USO wa dunia
 
McQueen, umeniacha hoi, Ina maana ni hadithi za sungura? Mbona watu wengi duniani wanaamini hivyo? Wamelogwa? Ndio maana ninasema dini ni miradi ya wajanja!angalia sasa wametuloga na kuamini vitu vya kitoto. Nikuulize kaswali kadogo, "hivi ufufuko ni kweli?".
 
Back
Top Bottom